1
Uislamu ni nini? Unaweza kutoa maelezo ya kina kuhusu Uislamu?
UISLAMU NI NINI?
Maana ya Neno Uislamu Kilugha
Kilugha, Uislamu unamaanisha kujisalimisha, kunyenyekea na kutii. Dini hii ndio inaitwa Uislamu kwa sababu ni dini yenye msingi wa kusalimu amri za Allah na kuzitii.
Maana Yake Kiistilahi
Ni njia ya maisha, mfumo wenye misingi ya imani na matendo ya kuwafanya watu wapate furaha kamili duniani na ahera, iliyotumwa na Allah na kufikishiwa watu kupitia kwa mitume. Uislamu ni sheria ya kiungu inayowaongoza watu wenye akili kuelekea mambo mazuri kulingana na hiari zao.
Yaliyomo katika Uislamu
Maana ya Uislamu ni kujisalimisha: kujisalimsha kwenye amri na makatazo ya Allah. Uislamu hautakuwepo bila ya kujisalimisha kwenye hukumu za Allah. (Angalia al-An'am, 162 na an-Nisa, 65) Mwanadamu ni mja aliyeumbwa na Allah.
Kwa kuwa Allah amekizingira kila kitu kwa elimu Yake na kwa kuwa Yeye ana hekima, sharti la utumwa ni kujisalimisha Kwake. Sheria za uhai humshurutisha mwanadamu kujisalimisha kwa Allah kwa sababu Allah ndiye anayezijua zaidi sheria hizo na anamjua zaidi mwanadamu.
Ulimwengu na kila kilichomo ndani mwake hutii sheria za Muumbaji huyo. Kwa hivyo, dini ya ulimwengu wote ni Uislamu. Jua, mwezi na nyota, vyote hivyo vinafuata Uislamu. Kwa kuwa Uislamu unamaanisha kumtii Allah na kujisalimisha Kwake, tunaona kwamba viumbe vyote hivyo vinamtii Allah bila ya kuasi. Yaani, tunashuhudia kwamba vinajisalimisha na kwamba vyote vinafuata Uislamu.
“Je, wanataka dini isiyo kuwa ya Mwenyezi Mungu, na hali kila kilichomo mbinguni na katika ardhi kimesilimu kwa kumtii Yeye kikipenda kisipende, na kwake Yeye watarejeshwa?" (Aal-i Imran, 3/83)
Katika aya hiyo hapo juu, kujisalimisha kwa viumbe angani na ardhini kumetolewa kama mfano na mwanadamu ameambiwa yafuatayo: "Ewe Mwanadamu! Jisalimishe kama wao." Kama Ali (ra) anavyosema, "Uislamu ni utii na kujisalimisha." Mtu asiyejisalimisha kwa Allah hazingatiwi kuwa ni Muislamu. Mtu huzingatiwa kuwa ni mtumwa wa yule anayejisalimisha kwake. Uislamu ni alama na taswira ya imani. Je kujisalimisha bila ya imani, yaani, Uislamu bila ya imani unawezekana? Hata ikiwezekana, haikubaliki. Munafikuna (wanafiki) ni watu wanaojisalimisha bila ya imani. Leo, watu wanaojitambulisha kuwa ni Waislamu huku hawaamini kuwa ni lazima, hao hawajapokea hukumu za Allah kwa moyo na wanafuata itikadi (dini) zingine wanaingia katika kundi hili. Uislamu (kujisalimisha) thabiti, ni lazima kujisalimisha katika Sharia'ah ya Allah bila kusita, kikamilifu na bila ya masharti yoyote.
Kama mtu atajisalimisha kwa Allah kwa hiari yake mwenyewe, na akaishi kama Muislamu kwa kuuchagua Uislamu, ataishi kwa amani na kwa kutangamana na ulimwengu tangu alipojisalimisha kwa yule yule ambaye ulimwengu umejisalimisha kwake. Basi, mtu wa namna hiyo anakuwa mwakilishi wa Allah juu ya ardhi.
UISLAMU NI NINI?
Haiwezekani kufafanua maana ya dini ya Uislamu kwa kifupi bali kwa urefu. Maana yake pana inaweza kufanyika tu kwa ufafanuzi wa Quran na Sunnah kwa sababu yaliyo katika Uislamu na mipaka yake yanabainishwa na Quran na Sunnah. Uislamu unaweza kufundishwa kutoka katika Quran na Sunnah. Allah ameifanya dini hii kuwa kamilifu na pana kwenye vipengele vyote. Hakuna jambo lisilokuwa na ufafanuzi katika Uislamu. Imebainishwa iwapo jambo ni halali, haramu, makruh (lenye kuchukiwa), sunnah, au wajibu; hukumu ya kila tendo au imani imebainishwa. Katka Uislamu kuna hukumu mahususi kuhusu imani, ibada, siasa, masuala ya kijamii, uchumi, vita, amani, sheria na yote yenye kumhusu mwanadamu; au, msingi wa mujtahid kufanya hukumu ni Quran na Sunnah. Allah anaeleza rasilimali hii ya Quran kama ifuatavyo:
“Na tumekuteremshia Kitabu hiki kinacho bainisha kila kitu." (an-Nahl, 16/89 na pia angalia Yusuf, 111)
Wanazuoni ambao ni Mujtahid huwa wanahukumu masuala ambayo hukumu zake hazikufafanuliwa waziwazi katika Quran na Sunnah kwa kuegemeza maamuzi yao juu ya Quran na Sunnah.
Mtume (s.a.w) aliufafanua Uislamu kwa njia nyingi. Mmojawapo ni huu ufuatao:
"Uislamu umejengwa juu ya kanuni tano: Kushuhudia kuwa hakuna mwenye haki ya kuabudiwa isipokuwa Allah na kwamba Muhammad (s.a.w) ni Mjumbe Wake, kuswali, kulip zaka, kufanya Hajj na kufunga katika Mwezi wa Ramadhani." (Bukhari, Iman 1; Muislamu, Iman 22; Nasai, Iman 13; Tirmidhi Iman 3)
Hadithi hiyo hapo juu inaeleza kuwa Uislamu una misingi mitano. Tunachotakiwa kuzingatia ni ukweli kuwa misingi hiyo mitano ndiyo nguzo za Uislamu isipokuwa zenyewe peke yake haziundi Uislamu wote. Hatuwezi kusema kuwa nyumba huwa na msingi tu; halikadhalika, si sahihi kusema kuwa Uislamu una kanuni tano tu. Mwenye kusoma Quran ataona kuwa maadili, uchumu, masuala ya kijamii, amani, vita, wema, uovu n.k. ni mambo yaliyotajwa pamoja na kanuni hizo tano katika Quran. Uislamu una msingi na jengo. Msingi una kanuni hizo tano. Jengo lina hukumu zingine za Uislamu zinazohusu maisha ya kibinadamu. Wajibu wa Muislamu ni kuujua Uislamu wote kwa ujumla na kuutekeleza wote kwa ujumla.
Chini ya nuru ya hadithi maarufu hapo juu, tunaweza kugawanya misingi ya Uislamu katika makundi mawili: imani, iliyoelezwa kifupi kwa maneno ya shahada na amali njema, zilizotajwa kama amali nne kutokana na umuhimu. Uislamu ni imani inayoanzia katika kalima ash-shahada (maneno ya shahada) na kanuni za imani. Uislamu ni ibada inayojitokeza pamoja na swala, zakah, saumu na hajj. Hizo zinaitwa kanuni au misingi ya Uislamu. Sehemu zilizosalia za Uislamu ni jengo lililowekwa juu ya misingi hiyo. Mambo yanayounda jengo hilo ni mifumo ya kimaisha ya Uislamu: mfumo wa kisiasa, mfumo wa kiuchumi, mfumo wa kijeshi, mfumo wa kijamii,mfumo wa elimu, n.k. Uislamu pia una vibali ili kuhakikisha mamlaka yake. (Vibali vinamaanisha kwamba ni nguvu ya kuhakikisha kuwa sheria na amri za kimaadili zinatekelezwa; inamaanisha desturi zinazohusu ushurutishaji). Vibali hivyo ni jihad, kuamrisha wema na kukataza uovu, adhabu asilia na adhabu za kiungu anazotoa Allah duniani na ahera. Hivyo, Uislamu ni imani, ibada, mifumo ya kimaisha na vibali.
UISLAMU NI NINI?
Maana ya Uislamu ni hali ya mtu kujisalimisha kwa Allah kwa nafsi yake ya ndani na ya nje, kwa moyo na mwili, akili na dhamiri, matakwa na chuki, hisia na nia. Maana ya Uislamu ni kuokoa moyo wa mtu, akili, mwili, nafsi ya ndani na ya nje dhidi ya vyote isipokuwa Allah. Uislamu ni mfumo wa ujumla, mpango wa vitendo vya kibinadamu wenye kuamuru kwa njia ya sheria na ufunuo unaohusu vipengele vyote vya maisha na uliotangazwa na kufikishwa na Mtume. Wenye kuutii mpango huu watapata malipo na wasiotii wataadhibiwa. Uislamu ni ukamilifu wa hukumu zilizoshushwa na Allah, itikadi, ibada, maadili, muamalat (miamala) na yote yaliyo katika Quran na Sunnah.
Kinyume cha Uislamu ni Jahiliyya (ujinga). (Jahiliyya ni jina linalokusanya namna zote za ukafiri kama ndio imani na mtindo wa kimaisha. Maana yake ni ukafiri.) Ujinga ni dhahiri kabisa uko kinyume cha kila sehemu ya Uislamu. Kama Swahaba Umar anavyoeleza, "Wanapojitokeza wasiojua Uislamu na Ujinga, mafundo ya Uislamu hufunguka moja baada ya jingine." Uislamu ni kinyume cha Ujinga katika vipengele vyote kwa sababu kila sehemu ya Uislamu ni kazi ya ujuzi wa Allah inayokizingira kila kitu. Kila rai na mwenendo ulio kinyume na Yeye ni Ujinga kabisa kwa sababu ni kazi ya elimu ya mwanadamu yenye mipaka. Aidha, fikra na matakwa ya mwanadamu vinaweza kumwelemea na kuifanya wema uonekane kama uovu na shari kama vile ni heri.
"Je, wao wanataka hukumu za Kijahiliya? Na nani aliye mwema zaidi katika kuhukumu kuliko Mwenyezi Mungu kwa watu wenye yakini?” (al-Maida, 5/50)
Baadhi ya watu wanapoona uzuri na ukomavu katika matendo, mtindo wa kimaisha au baadhi ya mifumo ya baadhi ya watu wanaofuata njia ya Ujinga, wanakuwa na mashaka. Hayo ni kwa sababu jambo la Kiislamu wakati mwingine linaweza kuwepo kwa watu wenye mfumo wa Ujinga, pia. Jambo hilo la Kiislamu linaonekana zuri huko, pia. Mjinga hutwaa mfumo huo kwa sababu hajui ukweli wa Uislamu. Kama angejua ukweli, basi angefahamu kuwa tendo jema lisilo na ukamilifu aliloliona katika Ujinga ni la Uislamu na litageukia upande wa chanzo chake na asili.
Kuna Uislamu na Ujinga katika imani mbalimbali. Upo Uislamu na Ujinga katika maadili, siasa, mafunzo, vita, amani na masuala ya kijamii. Upo Uislamu na Ujinga katika masuala yote yanayomhusu mwanadamu, katika sheria na kanuni zote. Ujinga katika imani na ibada ndio ujinga wa hatari zaidi. Kwa hivyo, Allah anawasamehe watu wanaofanya baadhi ya matendo ya ujinga wakiwa na imani thabiti isipokuwa Hasamehe watu ambao imani yao na ibada zao ni za Ujinga hata kama wana maadili kamili ya Kiislamu.
"Hakika Mwenyezi Mungu hasamehe kushirikishwa, na husamehe yaliyo duni ya hilo kwa amtakaye.” (an-Nisa, 4/48)
Allah ameuleta Uislamu ukiwa kamili. Mtu anayeuchukua wote ni Muislamu. Mtu anayeuchukua baadhi yake na akaacha sehemu yake nyingine anachanganya Uislamu na Ujinga.
“Kisha nyinyi kwa nyinyi mnauwana, na mnawatoa baadhi yenu majumbani kwao, mkisaidiana kwa dhambi na uadui. Na wakikujieni mateka mnawakomboa, na hali kuwatoa mmekatazwa. Je! Mnaamini baadhi ya Kitabu na mnakataa baadhi yake? Basi hana malipo mwenye kutenda hayo miongoni mwenu ila hizaya katika maisha ya duniani, na Siku ya Kiyama watapelekwa kwenye adhabu kali kabisa. Na Mwenyezi Mungu si mwenye kughafilika na yale mnayo yatenda.” (al-Baqara, 2/85)
Ni lazima kila Muislamu atakasike dhidi ya desturi na kanuni zote za Ujinga na kuuchukua Uislamu wote.
Lengo la dini ya Uislamu
Hukumu zilizowekwa na Uislamu zinalenga furaha ya watu. Wenye kutenda kwa kufuata hukumu hizo watapata furaha kamili duniani na ahera. Uislamu unamfanya mtu apate furaha kwa kuboresha moyo wake, fikra na matendo. Kwa kuwa furaha ya jamii hutegemea furaha ya mtu mmoja mmoja, furaha ya mtu mmoja mmoja inamaanisha furaha ya jamii. Uislamu umeweka baadhi ya hukumu ili kufikia lengo hili. Zinaitwa hukumu za Shari'ah.
Hukumu za Dini ya Uislamu
Hukumu za dini ya Uislamu zimegawanyika katika makundi manne.
a) Imani (Hukumu zinazohusu imani): Ni hukumu zinazohusu masuala ambayo mwanadamu anahitaji kukubali au kukataa katika dini ya Uislamu. Hukumu hizi humfundisha mwanadamu anachotakiwa kukubali na kukataa. Kwa kuamini kanuni za imani, mwanadamu anachukua chakula chake cha kiroho, anatakasa moyo wake dhidi ya imani potovu na anapata thamani yake halisi.
b) Vitendo: Vitendo ni mambo anayoyafanya mwanadamu. Ni vitendo vinavyotakiwa kufanywa au kutokufanywa. Hukumu zenye kueleza amali gani zifanyike chini ya hali zipi na namna amali hizo kuwa ni amali zenye kufaa huitwa amali za kivitendo; mathalani, kuswali, kutoa zakah, kufanya jihad, kutafuta elimu.
c) Maadili: Hizi ni hukumu zenye kufafanua hali na vitendo, mitizamo na uhusiano wa Kiislamu na wa kibinadamu. Ni hukumu zenye kuhusu kuyapendezesha maadili na kuelimisha dhamira; mathalani, kutokutukana au kudanganya, mtu kutaka vitu ambavyo hutaka kwa ajili ya nafsi yake, kwa ajili ya wengine pia.
d) sheria [Muamalat (Miamala), Uqubat (Adhabu)]: Hizi ni hukumu zilizo nje ya masuala kama ya imani, maadili na vitendo binafsi na vyenye kuhusu kuongoza dola, utawala wa jamii, masuala ya kiuchumi, ndoa, talaka, mirathi, mambo ya kibiashara na kisiasa; kwa kifupi, ni hukumu zote zenye kuamua sheria na kanuni za dola ya Kiislamu.
Uislamu si sehemu tu ya maisha ya mwanadamu bali ni wote kikamilifu pamoja na vipengele vyake vyote. Uislamu umeyazingira na kuyaainisha masaa ishirini na nne ya mwanadamu na masuala mengine yote tangu kuzaliwa mpaka kufa. Uislamu ndio maisha yote ya mwanadamu. Ni wote kikamilifu pamoja na imani yake, ibada na sheria. Hauwezi kugawanywa au kuambatanishwa na kitu kingine. Haukubali kupunguzwa au kuongezwa, na ushirikina. Ni mfumo kamilifu uliokamilishwa na Allah.
Sifa Bainifu za Ujumla za Uislamu
1) Uungu: (Ni wa Mola Mlezi; hali ya kuwa mungu) Uislamu ni dini ya kweli na ya kiungu. Uislamu unategemea ufunuo. Malengo na madhumuni yake ni ya kiungu. Radhi za Allah ndiyo malengo ya msingi ya Muislamu. Chanzo na mtindo wa Uislamu ni wa kiungu, pia.
2) Ubinadamu: (Kutangamana na hali ya kibinadamu) Quran ilishushwa kwa watu, na mitume waliteuliwa kutoka miongoni mwa watu. Uislamu unampa umuhimu mkubwa mwanadamu na akili ya kibinadamu; na umeweka hukumu. Kwa mujibu wa Uislamu, mwanadamu aliumbwa juu ya ardhi kwa namna bora kabisa na kama mwakilishi; alifanywa kiumbe wa kipekee mwenye sifa muhimu ya kiroho; na ulimwengu umetiishwa kwake. Uislamu hauyapuuzi makundi yoyote yenye uwezo na nguvu. Unawaongoza wote hao kwenda kwenye kutengemaa, kazi na maendeleo. Kwa kushughulikia mizigo anayomudu kuibeba, mwanadamu anaendelea katika njia yake kwa amani, usalama na utulivu. Majukumu hayo yanatangamana na hulka ya mwanadamu. Yanaunganishwa na uthabiti wa moyo na dhamiri ya mwanadamu. Uislamu unalenga katika kustawisha hulka yake. Hukumu zote za Uislamu zimeelekezwa kwenye furaha ya duniani na ahera..
3) Upana na kuenea: Uislamu ni wa milele wa kuwepo daima, mpana wa kuwajumuisha watu wote na wa kina kirefu cha kujumuisha mambo ya duniani na nje dunia. Ujumbe na hukumu zake ni zinauhusu ulimwengu wote na wanadamu. Uislamu unapanga hatua zote za maisha ya mwanadamu, tokea kuzaliwa mpaka kufa na nyanja zote za kimaisha. Mafunzo ya Uislamu pia ni mapana. Upana huo hudhihirika katika imani, ibada, tafakuri, maadili na fadhila, na utaratibu na sheria.
4) Wastani na usawa: Uislamu ni dini yenye nguvu za kimsingi kama vile usawa, kati upole, haki na wastani. Ni njia ya kuepuka ubadhirifu na upungufu. Uislamu hauna mambo ya msimamo mkali. Haumwachi mwanadamu apotee na kukandamizwa. Uwezo wa mwanadamu hautoshi kuweka mfumo wa usawa. Tunaweza kuona kirahisi vipengele vya wastani (haki na usawa) katika imani, ibada, maadili na utungaji sheria. Kuna mizani kati ya dunia na ahera, maada na roho, tajiri na masikini. Uislamu huweka kwa usawa ndani na nje ya mwanadamu, roho na mwili, mtu mmoja mmoja na jamii, wanawake na wanaume, familia na taifa. Uislamu unapambanua haki zao kwa kila mmoja kwa usawa na utangamano.
5) Uwazi: Kanuni za imani na fikra za Uislamu ziko wazi na bayana. Ni nyepesi kuzifahamu, kueleza na kukubali. Hazikataliwi na akili na mantiki.
6) Dini Safi: Ni dini isiyoweza kuvurugwa kwa kuwa hairuhusu uchambuzi na usanisi (uunganishaji), kupunguzwa na kuongezwa na kwa kuwa chanzo chake ni kamili na kisichobadilika. Haiingiliwi na ushirikina. Ni dini pekee ya kweli iliyokamilishwa na kukubaliwa na Allah.
7) Upwekeshaji (Tawhid): Uislamu kimsingi ni dini ya upwekeshaji. Katika Uislamu ndiko kwenye kumwamini Allah kwa usahihi. Katika Islam, sifa za Allah haziwezi kuhusishwa na watu na viumbe wengine. Uislamu unasisitiza kuwa Allah hafanani na yeyote. Watu na viumbe wengine hawawezi kufanywa miungu. Haiwezekani kumwabudu yeyote mwingine isipokuwa Allah.
8) Kuwakubali Mitume wote: Muislamu anawaamini mitume wote waliotumwa na Allah. Hambagui yeyote miongoni mwao. Anawakubali kuwa ni wajumbe na waja wa Allah kwa kutokuwafanya miungu na kutokuwapa sifa za Allah wasizozistahiki.
9) Mamlaka ni ya Allah: Allah ndiye mwenye maamuzi, sheria na kanuni na kuweka sheria. Uislamu umejenga jamii ambapo hukumu, utawala, amri na mamlaka ni ya Allah na ambapo hakuna wenye kudhulumu, kudhulumiwa na watumwa wa watumwa.
10) Chanzo kamili: Chanzo kikuu cha Uislamu ni Quran. Quran ni kitabu ambacho hakitageuzwa-geuzwa mpaka Siku ya Kiama. Nakala zote za Quran duniani ni sawasawa.
11) Kutangamana na ulimwengu: Ulimwengu na kila kilichomo huzingatiwa kuwa kinafuata Uislamu kwa kuwa kinajisalimisha kwa Allah na kumtii. Mwenye kuupokea Uislamu na kujisalimisha, anatii kanuni zilezile katika kutangamana na ulimwengu. Hivyo, jitihata na nguvu za mwanadamu huunganika na nyezo za ulimwengu. Uislamu haumfanyi mwanadamu ashindane na kupigana na nguvu za asili ulimwenguni.
12) Uislamu unajenga jamii moja (umma): Uislamu unajenga jamii (umma) yenye utangamano na uaminifu na kutenda kwa mshikamano. Nguvu za msingi za jamii hii, inayounganishwa na kifungo cha imani na isiyobagua mbari, rangi, nchi na matabaka ni undugu, mshikamano, usawa, haki, kunasihiana ukweli na subira, kueneza heri na kupambana na shari. Ni jamii bora yenye maadili ambapo desturi mbaya kama vile uzinifu, ukahaba, wizi, dhuluma na riba vimeondshwa, ambapo matakwa yaliyovuka mipaka wa mwanadamu kwa ajili ya kula, kunywa, makazi na ngono umezuiwa. Makafiri hutazamwa kama ni umma mmoja; halikadhalika, Waislamu wote ni umma mmoja ambapo wao kwa wao huangaliana kama ndugu.
13) Wepesi na bishara: Uislamu humwangalia yeyote mwenye kutamka kalima ash-shahada na kuishi nayo maishani kuwa ni Muislamu pasi na kujali kuwa hapo nyuma alikuwa vipi. Uislamu umejikita juu ya kanuni ya usawa na haki. Haumruhusu yeyote kushurutishwa kuwa Muislamu. Unalenga katika kuenea kwa kuzishinda nyoyo. Hukumu zake ni nyepesi zinazoweza kutekelezeka. Mengi mepesi yamewekwa kuhusu ibada kwa kuzingatia ustahamilivu wa mtu (Mengi mepesi kuhusu ibada yameelezwa kuuchukua uthabiti wa mtu kwenda kwenye umakini). Majukumu magumu hayajaamrishwa na Uislamu. Kwa rehema ya Uislamu, ruhusa na bishara ni nyingi. Uislamu unaangalia mahitaji ya kiroho na kimwili ya binadamu kwa ustahamilivu na kuzitafutia ufumbuzi mwepesi na rahisi. Hata hivyo, wote wenye kupuuza kumwabudu na kumtii Allah licha ya wepesi wote huo kwa sababu ya uvivu na kuipenda sana dunia wanaonywa juu ya adhabu ya Allah.
14) Uislamu unaipa umuhimu the akili na elimu: Uislamu ni dini ya ufunuo lakini unaipa umuhimu akili. Uislamu pia unaipa umuhimu mkubwa sayansi na na elimu, kwa kueleza kuwa elimu ni faradhi kwa Waislamu wote; unayapa umuhimu masuala kama kazi, mafunzo na fikra. Isisahaulike kuwa Uislamu si dini ya kufikirika bali ya kiakili.
15) Haki za kibinadamu: Uislamu, ambao unajali haki za kibinadamu kwa namna ambayo hawataweza kuiona katika mfumo (dini) wowote mwingine, unalinda haki zifuatazo za mwanadamu:
a. Usalama wa dini: Uislamu unalinda haki ya dini na uhuru wa kuitekeleza dini.
b. Usalama nafsi: Uislamu unahakikisha haki ya kuishi.
c. Usalama wa akili: Uislamu, unaoamuru sayansi na tafakuri, unakataza vyenye kudhuru akili kama vile ulevi na madawa; unachukua kila hatua ili kulinda akili dhidi ya namna zote za kuchanganyikiwa.
d. Usalama wa kizazi: Unachukua hatua zote za lazima ili kuhakikisha adabu na heshima na makuzi ya kizazi chenye afya.
e. Usalama mali: Uislamu unaziba njia zinazoelekea kwenye uhalifu kama vile wizi ili kuhifadhi mali; zaidi ya hayo, humpa mwanadamu haki na fursa ya kuwa na njia za kutosha za kutafuta riziki.
Kwa ujumla, Uislamu unatoa dhamana kwa heshima, adabu, uhuru, dini, uhai, utafutaji riziki na kazi ya kila mtu.
Kuhusu suala la haki za binadamu, Uislamu bado upo katika kiwango cha juu sana ambacho hakiwezi kufikiwa. Unahimiza kanuni za undugu wa wanadamu. Uislamu unakataa ubaguzi wa kimbari na kutambua ubora wa mtu isipokuwa kwa taqwa (uchamungu). Amri za Uislamu, makatazo, hukumu, ibada, ufahamu wa adhabu, n.k vinahakikisha usawa. Kiasi hiki kikubwa cha usawa hakipo katika mifumo mingine hata kwa nadharia. Uislamu haujaacha kutilia maanani dhuluma kwa ajili ya usawa. Hauruhusu unyanyasaji wa kijinsia kwa kutoona tofauti za kijinsia kwa kisingizio cha usawa wa wanawake na wanaume na kuvuka mipaka kutakakopelekea kwenye kuwanyonya na kuwakandamiza watu. Kuhusu suala la haki za kibinadamu, Uislamu bado upo katika kiwango cha juu sana ambacho hakijawahi kufikiwa. Unahimiza kanuni za undugu wa wanadamu. Uislamu unakataa ubaguzi wa kimbari na kutambua ubora wa mtu isipokuwa kwa taqwa. Amri za Uislamu, makatazo, hukumu, ibada, ufahamu wa adhabu, n.k vinahakikisha usawa. Usawa wa kiasi hiki haupo katika mifumo mingine hata kwa nadharia. Uislamu haujaacha kutilia maanani dhuluma kwa ajili ya usawa. Haupuuzi tofauti za kijinsia kwa kisingizio cha usawa wa wanawake na wanaume na kuruka mipaka kutakakopelekea kwenye kuwanyonya na kuwakandamiza watu.
Uhusiano wa Uislamu na Shari'ah za Mitume Waliotangulia
a) Uislamu ni jina la dini zote zilizoshushwa kupitia kwa mitume wote. (angalia al-Baqara, 130 - 133). Utu uliletwa duniani na mtume (Adam). Allah aliwatuma mitume kuleta shari'ah (sheria) tofauti zilizoegemea mazingira ya wakati huo na mahitaji ya wanadamu; hata hivyo, imani ilikuwa ileile kwa mitume wote.
b) Dini zilizofikishwa na mitume waliotangulia zilipelekwa kwa baadhi ya mataifa. Dini aliyotumwa Mtume Muhammad (s.a.w) ni ya wote. Yaani, Allah aliileta ulimwenguni kote na kwa watu wote; ni njia ya maisha itakayokuwa halali mpaka Siku ya Kiama.
c) Dini ya Uislamu, aliyofikisha Nabii Muhammad (s.a.w), ilifuta hukumu (shari'ah) za dini zilizofikishwa na mitume waliotangulia. Yaani, iliyo hai kwa sasa ni shari'ah ya Nabii Muhammad (s.a.w).
d) Dini ya Uislamu inathibitisha vitabu vyote na mitume wote waliotumwa na Allah kabla ya Nabii Muhammad (s.a.w).
Baadhi ya Aya Zinazoeleza Uislamu
“Bila ya shaka Dini mbele ya Mwenyezi Mungu ni Uislamu.” (Aal-i Imran, 3/19)
“Na anaye tafuta dini isiyo kuwa Uislamu haitakubaliwa kwake. Naye Akhera atakuwa katika wenye kukhasiri.” (Aal-i Imran, 3/85)
“Na mwenye kuuelekeza uso wake kwa Mwenyezi Mungu, naye akawa anafanya wema, basi huyo hakika amekwisha kamata fundo lilio madhubuti. Na mwisho wa mambo yote ni kwa Mwenyezi Mungu.” (Luqman, 31/22)
“…Leo nimekukamiliishieni Dini yenu, na nimekutimizieni neema yangu, na nimekupendeleeni UISLAMU uwe ndiyo Dini....” (Al-Maida, 5/3)
Misingi ya Islam
Misingi (nguzo) za Uislamu ni mitano: Kushuhudia kuwa hakuna mwenye haki ya kuabudiwa isipokuwa Allah na kwamba Muhammad (s.a.w) ni Mjumbe Wake, kuswali, kulipa, kufanya Hajj na kufunga wakati wa mwezi wa Ramadhani.
Katika hadithi ambayo Mtume anafafanua Uislamu, inayojulikana kama hadithi ya Jibril, tuliyoitaja mwanzoni na inayoeleza kuwa Uislamu umejengwa juu ya nguzo tano (ambazo wajinga kimakosa huziita masharti ya Uislamu), nguzo hizo tano zimeorodheshwa. Tutashughulikia kanuni za msingi za imani tunazoziita kalima ash-shahada au kalima at-tawhid kwa kina tutakapoeleza suala la upwekeshaji (tawhid). Hapa, tutataja kwa kifupi kanuni (nguzo) zinazoeleza kama mifano ya kifani kutokana na umuhimu wa aina hizi za ibada na tunazoweza humo humo kueleza matendo hayo mema pamoja na ibada nyengine kama hizo zinazohusiana na imani. Namna ya kuzifanya ibada hizi imeelezwa kwa kirefu katika vitabu vya maswali na majibu na katika somo la fiqh.
Ni nini amali njema (amal salih)? Amali njema ni vitendo anavyovipenda Allah. Amali njema ina sifa mbili: Ya kwanza ni kuafikiana na shari'ah ya Uislamu; ya pili ni nia iwe kwa ajili ya Allah na kulenga kumwabudu. Kama amali haina sifa hizo mbili, haizingatiwi kuwa ni amali njema kwa Allah. Amali hiyo haina faida wala malipo. Mola wetu Mlezi anasema ifuatavyo:
“…Mwenye kutaraji kukutana na Mola wake Mlezi basi naatende vitendo vyema, wala asimshirikishe yeyote katika ibada ya Mola wake Mlezi..” (al-Kahf, 18/110)
Nafasi ya amali njema katika Uislamu ni muhimu sana kwa sababu vitendo hivyo ni matunda ya kumwamini Allah na akhera. Maana ya kalima ash-shahada (tawhid) inadhirika kwa kufanya matendo mema na kuendelea kufanya hivyo. Tunapokumbuka kuwa maana ya Uislamu ni kujisalimisha na utii, na kwamba kujisalimisha huko kunamaanisha kutii na kujisalimisha kwenye amri za Allah, inadhihirika wazi kuwa Uislamu hauwezi kuwa bila ya vitendo, utii na ibada. Aya nyingi zinasifu amali njema kutokana na umuhimu wake katika Uislamu. Baadhi ya aya hizo huzitazama kama ziko karibu na imani; baadhi hutaja malipo yake na nyingine hutaja manufaa yake katika akhera.
“Naapa kwa Zama! Hakika binaadamu bila ya shaka yumo katika khasara, Ila wale walio amini, na wakatenda mema, na wakausiana kwa haki, na wakausiana kusubiri...” (al-Asr, 103/1-3)
Kuhusu baadhi ya aya zingine, angalia al-Maida, 9 ; ar-Ra’d, 29 ;an-Nahl, 97 ; al-Kahf, 30; Maryam, 76; al-Ankabut, 7, 9.
Ni lazima kuufata Uislamu ili amali iweze kukubaliwa. Kwa hivyo, Allah anataja imani na amali njema kwa pamoja. Kama mtu atafanya jema lenye kufikiana na shari'ah ya Uislamu na kwa ajili ya Allah, jambo hilo litakataliwa na Allah isipokuwa akiukubali na kuufuata Uislamu wote kikamilifu. Amali hiyo haitakuwa na malipo. (angalia Aal-i İmran, 3/85)
Kuna namna nyingi za amali njema. Hayo ni mambo yote anayoamuru Allah, ambayo ama yanahusu ibada au miamala. Muislamu anapofanya jema kwa lengo la kumtii Mola wake Mlezi, anajisalimisha kwenye shari'ah na atakuwa anatafuta radhi za Allah, hapo atakuwa mtu wa amali njema.
Kwanza kabisa, matendo mema (kwa mtazamo finyu) ni matendo ya ibada. Vitendo vikuu vya ibada swala za kila siku, hajj na zakah. Hiyo ni misingi ya Uislamu. Hairuhusiwi hata kidogo kupuuza au kutweza umuhimu wake. Kwa hivyo, imeelezwa waziwazi katika hadithi mashuhuri zenye kuufafanua Uislamu.
Umuhimu wa ibada katika Uislamu ni mkubwa. Ibada huratibu uhusiano wa mtu na Mola wake Mlezi na kuonesha kumtumikia kwake Allah. Ibada ni haki maalumu ya Allah kutoka kwa waja Wake. Ni lazima kuchunga ibada na kuwaita watu wengine kwenye kanuni za imani na kisha ibada. Ibada isipokamilika, imani ya mtu haiwezi kuimarika na haitatulia moyoni mwake. Zaidi ya hivyo, leo hii, kwa vile mamlaka ya ukafiri yamefika kila mahali, imani ya watu wanaotekeleza ibada kivivu na kuacha baadhi ya ibada hususani swala za kila siku ni jambo la hatari. Yaani, ni vigumu sana mtu kundelea kuwa muumini bila ya kuswali na kufanya ibada nyengine. Ibada ni kama vile maji kwa samaki na hewa kwa mwaadamu.
Miongoni mwa ibada hizo, swala za kila siku zina umuhimu maalumu katika sharti la imani. Uislamu unaeleza swala kama sifa inayotofautisha kati ya Muislamu na kafiri. Hairuhusiwi kupuuza swala hata safarini, vitani, au mtu anapougua. Ni tabia ya wanafiki kuacha swala na kupuuza unapowadia wakati wa kuswali. Mtu anaporejea kwa Mola wake Mlezi, jambo la kwanza atakaloulizwa ni swala. Swala ni ibada ambayo mara kwa mara humkumbusha mtu kuhusu utumishi wake kwa Allah na maana ya kalima at-tawhid. Swala humzuia mtu kufanya vitendo vyote vibaya, uzinifu na uovu. Baadhi ya aya za Quran zinazohusu umuhimu wa swala ni hizi zifuatazo: ar-Rum, 31; al-Baqara, 1-3, 153 na 238; an-Nisa, 103; 142; al-Ankabut, 45...
Muislamu huitwa kwenye swala kwa tamko “Allahu Akbar”; anaanza swala kwa maneno hayo; anayakariri wakati anaposwali kwa sababu Allah ni mkubwa kuliko kila aliye mkubwa na Yuko juu kuliko kila mfalme mwenye nguvu. Kama mtu atasikamana na Allah, ambaye ni mkubwa na mwenye nguvu kuliko kila kitu, hatamwogopa yeyote. Ataacha kuwaabudu wengine.
Saumu, hajj, zakah na ibada zote zingine huimarisha imani, hutakasa roho ya uovu na kumfanya mtu amng’ang’anie Mola wake Mlezi. Katika saumu, mtu hutanguliza kumpenda Allah kuliko mahitaji ya mwili wake. Humfanya Muislamu awe mnyoofu, kuthubutu na matakwa na subira. Zakah ni ibada kwa upande wa mali inayomwezesha Muislamu kutakasika dhidi ya ugonjwa wa ubahili. Shukrani kwa nia ya zakah, anaifahamu vyema kuwa Allah ndiye mmiliki halisi wa mali na kwamba yeye amepewa dhamana tu ya mali hiyo. Zakah inamaanisha kutanguliza radhi na kumpenda Allah kuliko kupenda mali. Inamaanisha mtu kutenga fungu la mali yake na kuwapa masikini katika jamii na kwa hivyo kuchangia ustawi wa kijamii. Hajj ni mafunzo ya kivitendo kwa Muislamu. Tunaona kuwa Muislamu anatumikia kwa vitendo na waziwazi kwa njia ya ibada ya hajj. Maamrisho kama vile kutafuta elimu, kufanya jihad, kuamrisha wema, kukataza uovu, kuwa na subira na tawakkul, kuwa na taqwa, kumpenda Allah na kuhofu adhabu Zake ni katika matedo mema yanayosisitizwa sana katika Quran.
Kufikisha ujumbe wa Uislamu
Uislamu lazima ufikishwe kwa kila mmoja kadiri mwanadamu anavyokuwepo. Lengo halisi la kulingania na kufikisha ni kuwaokoa watu dhidi ya kuwa watumwa wa watu wengine na kuwafanya wamwelekee Allah peke yake, ambaye ni Mmoja. Lazima kila mara kuwe na watu wenye kutekeleza wajibu huo.
“Na uwe kutokana na nyinyi umma unao lingania kheri na unao amrisha mema na unakataza maovu. Na hao ndio walio fanikiwa.” (Aal-i Imran, 3/104)
Aya hiyo inathibitisha wajibu huu. Uislamu lazima ufikishwe kwa kila mtu lakini hususani kwa wenye kutenda matendo ya kijuujuu kama Waislamu kwa sababu wanaouona kama Uislamu si Uislamu halisi. Hali hii lazima ibadilishwe kabisa na waoneshewe ukweli.
Lengo mojawapo la kuwaita watu kwenye Uislamu ni kuunusuru usihodhiwe na watu wasiomfikishia yeyote na kumjulisha kila mmoja kuhusu Uislamu. Hakuna anayeweza kuuhodhi Uislamu. Hakuna anayeweza kuwa na amri juu ya ibada na kuwataabisha Waislamu kuifanya. Wenye kufanya hivyo, ikiwa wanaifanya kwa niaba ya Uislamu au ya Ujinga, wanamvunjia heshima Allah kwa sababu Allah anataka viondoshwe vikwazo vyote vyenye kuwazuia watu kumfikia. Zaidi ya hivyo, Amefaradhisha kufanya jihad dhidi ya vizuizi hivyo ili watu wajue, wajifundishe na waupokee Uislamu, ulio msafi na wenye kufahamika kirahisi, wenye kutangamana nao. Kuwanusuru watu dhidi ya utawala na uonevu wa watu wengine, dhidi ya mabwanyenye, wenye mamlaka, wahenga, mababa, mabwana na desturi wanazozing’ang’ania, na kuwawezesha kuufikia Uislamu, ambao ni mfumo na utukufu wa Allah, katika namna zote za maisha... Hivi ndivyo Uislamu ulivyo; mitume wote walitumwa kwa ajili ya hilo.
Kuupa Mamlaka Uislamu Maishani
Kanuni ambayo ni msingi mkuu wa Uislamu katika historia nzima ya mwanadamu ni ya “La ilaha illallah”. Yaani, kanuni ya kuuweka uungu, ubwana, utawala na mamlaka kwa Allah peke yake. Kanuni hii inapasa idhihirike kwa njia ya imani moyoni, ibada katika hisia, na vitendo na sheria na mfumo maishani. Kama mtu hashuhudii kuwa hakuna mwenye haki ya kuabudiwa isipokuwa Allah kwa njia inayofaa, huzingatiwa kuwa anamkosea heshima Allah na Uislamu.
Kanuni hii hutumika kikamilifu pindi mwanadamu anapomgeukia Allah kikamilifu katika maisha yake. Hivyo, mwanadamu anatazama hukumu za Allah katika mambo yote na hatua zote za maisha yake; anapokea na kutanguliza amri za Allah kuliko rai zake mwenyewe.
Mtu mwenye kutoa khabari na kuwafikishia watu hukumu za Allah ni Mjumbe wa Allah (s.a.w). Kanuni hii ndio inayounda sehemu ya pili ya kalima ash-shahada.
“Muhammad ni Mjumbe wa Mwenyezi Mungu.” (al-Fath, 48/29)
Hii ni sehemu ya pili ya kanuni ya msingi inayoegemewa na Uislamu. Kanuni hii itakapotekelezwa kikamilifu katika vipengele vyote vya kimaisha, mfumo kamili utaajitokeza. Huo ni mfumo anaouridhia Allah.
Lengo la Uislamu ni kuondoa Ujinga. Ni lazima kuweka wafanyakazi wapya tendaji wa kuweza kuutambua. Hili ni kundi la watu wanaofuata mbinu ya Kiislamu katika mtindo wao wa kimaisha, hali ya akili, mfumo wa kijamii, kiwango cha hukumu na njia, kwa kifupi, kila kitu. Ni hao tu ndio wanaoweza kuujenga tena umma wa Kiislamu na kustahiki kuwa ndio wanaotambulishwa na aya zifuatazo:
“Nyinyi mmekuwa bora ya umma walio tolewa watu, kwa kuwa mnaamrisha mema na mnakataza maovu, na mnamuamini Mwenyezi Mungu.” (Aal-i Imran, 3/110)
“Na vivyo hivyo tumekufanyeni muwe Umma wa wasitani, ili muwe mashahidi juu ya watu, na Mtume awe ni shahidi juu yenu...” (al-Baqara, 2/143)
2
Ni zipi nguzo za Uislamu?
Dini ya Uislamu imejengwa juu ya nguzo tano. Nazo ni: saumu, salah (kuswali), Hajj (kuhiji Makka), Zakat (Kutoa zaka), kushuhudia Upweke (tauhidi ya) wa Allah na utume wa Mtume Muhammad (Shahadah).
Nguzo mojawapo ya Uislamu ni kufunga katika Mwezi wa Ramadhani. Kwa njia ya saumu, Waislamu wanajikinga dhidi ya kutawaliwa na nafsi yenye uovu kwa kuitia nidhamu na kuitakasa. Na hapo inakuja hisia ya kuwahurumia masikini katika nyoyo zao kwa kuhisi maumivu yao ya kuwa na njaa.
Nguzo nyingine ya Uislamu ni kuswali. Inamaanisha kusimama mbele ya Allah mara tano kwa siku kwa mtu kujifahamu udhaifu wake na upungufu kwa kuinama na kusujudu na kuonesha utumwa Kwake. Swala za faradhi ni ibada ya wote na shukrani ya wote. Kila Muislamu ni lazima atekeleze. Mtume Muhammad (s.a.w) aliamuru: Swala ni nguzo ya dini (Tirmidhi, Iman-8)
Nguzo nyingine ya Uislamu ni Hajj (Kwenda Hija katika mji mtakatifu wa Makka). Wameamrishwa Waislamu wenye uwezo wa mali na wa kiafya kulingana na sheria ya Kiislamu, kwenda Hajj angalau mara moja maishani katika msimu mahususi uliopangwa na sheria (Shariah) ya Kiislamu. Mojawapo ya hekima za ibada hii, ambayo ni ya lazima, ni Waislamu wa dunia nzimakuweza kukutana na kudhihirisha kuwa watu wote wako sawa mbele ya Allah (SWT) pasi na kujali utaifa, lugha, rangi ya ngozi, na hadhi ya kijamii.
Nguzo nyingine ya Uislamu ni kutoa zaka (Zakah), ambayo ni nguzo ya mwisho ya Uislamu. Allah Mtukuka amewafaradhishia Waislamu matajiri, kwa ajili ya Allah, kwa kuwapa, Waislamu masikini kiasi (2.5 %) katika mali zao, kilichopangwa na Uislamu. Mali hii, ambayo tajiri humpa masikini, huitwa Zakah. Kwa mujibu wa sheria ya Kiislamu, hii ni haki ya maskini. Uislamu unawahimiza Waislamu kuwasaidia masikini hata kwa njia isiyokuwa ya Zakah pia. Nazo huitwa sadaqah (sadaka).
Ili kuweza kuwa Muislamu, ni lazima mtu atamke kalima ash-shahada. Maana ya kalima ash-shahada ni kama ifuatavyo "Ninashuhudia kuwa hakuna mwenye haki ya kuabudiwa isipokuwa Allah na kwamba Nabii Muhammad ni mja Wake na mjumbe Wake."
Sehemu ya kwanza ya shahada inaeleza kuwepo kwa Allah na upweke (tauhidi Wake na kuwa Hana washirika au washindani. Sehemu ya pili inaeleza kuwa Nabii Muhammad (s.a.w) ni mja wa Allah na kwamba aliteuliwa na Allah kuwafikishia watu Misingi ya imani na nguzo za Uislamu.
3
Kwa nini Uislamu ni dini ya kweli?
“Bila ya shaka Dini mbele ya Mwenyezi Mungu ni Uislamu. Na walio pewa Kitabu hawakukhitalifiana ila baada ya kuwajia ujuzi, kwa sababu ya uhasidi ulio kuwa baina yao. Na anaye zikataa Ishara za Mwenyezi Mungu basi hakika Mwenyezi Mungu ni Mwepesi wa kuhisabu.” Qur’an, Familia ya Imran (Aal-i Imran); 19 (3: 19)
Dini inamaanisha “malipo kwa mtindo wa malipo au adhabu” na inaeleza uhusiano kati ya mfuasi na kiongozi mwenye madaraka. Kama neno lenyewe lilivyo, umetolewa ufafanuzi kadhaa wa neno dini. Zipo tofauti za kimsingi kati ya fafanuzi zinazotolewa na wanasayansi wa Kimagharibi (Ulaya) na wanazuoni Waislamu. Bado, kuna tofauti za kimsingi kati ya rai za pande zote mbili kuhusu chanzo cha dini na njia yake ya kimsingi ya kutokea.
Kwa mujibu wa rai ya Kiislamu, dini inamaanisha ukamilifu wa kanuni unaomwongoza mwanadamu ili aweze kuishi kulingana na lengo aliloumbiwa na ili atambue lengo hilo katika nidhamu mahusussi. Dini ni msingi unaorekebisha uhusiano unaozingatia amri tukufu na utawala wa upande mmoja na utii na ufuasi wa upande wa pili, isipokuwa inafahamika kutokana na aya ambayo kwa mujibu wa Qur’an, thamani ya dini na kujitolea kumewekwa ili kuzingatie utii wa hiari. Kwa maneno mengine, kwa mujibu wa ufahamu wa Kiislamu, dini ni msingi unaoelekeza watu wenye kufahamu waelekee kwenye mema (kwa vitendo) na furaha kwa matakwa yao, na sheria ya kiungu inayorekebisha vitendo vya watu kwa kuzingatia uchaguzi wao.
Aya hiyo ndio sehemu ya kwanza ambayo neno Uislamu limetajwa katika Qur’an Tukufu. Maana ya Uislamu katika kamusi ni “kuwa mwaminifu, kutii, kujisalimisha na kuwa katika mwelekeo na amani”. Kama neno, Uislamu linamaanisha “kukubali kuwepo kwa mambo yote aliyotangaza Mtume Muhammad (s.a.w) kwa niaba ya dini na kuwa katika utii unaoidhihirisha hayo”. Jina la dini ya kweli aliyotumwa Mtume ni Uislamu. Bado, katika lugha ya Kiarabu, Uislamu ni hali isiyo na kikomo inayoonesha kuitii dini hiyo. Mtu anayefuata dini ya Uislamu ametajwa kuwa ni Muslam katika lugha ya Kiarabu na kama musalman katika lugha ya Kiajemi. Katika lugha ya Kituruki, maneno Islamiyet na Muslumanlik hutumika kwa ajili ya dini hiyo na neno musluman hutumika kwa mtu anayefuata dini hiyo.
Kuna uhusiano mkubwa kati ya maana ya neno Uislamu kwenye kamusi. Kwa mujibu wa ufahamu wa Kiislamu, dini ni sheria inayoeneza muwafaka kwa kuzuia kutoafikiana na ukinzani kati ya viumbe wenye matakwa na akili. Dini inaeleza muwafaka si miongoni mwa watu tu isipokuwa pia kati ya watu na Allah. Kwa njia hii, ukubalifu kati ya matakwa ya Muumba na matakwa ya viumbe huenezwa.
Kwa kuwa dini zote za kimbinguni zina msingi wa kumpwekesha Allah, dini ya Uislamu aliyoijulisha Mtume Muhammad na dini zingine zilizotangazwa na mitume wengine kimsingi zinalingana. Hata hivyo, kwa mujibu wa baadhi ya wanazuoni wa Kiislamu, maneno kama vile dini ya Uislamu na jamii ya Kiislamu yanaweza tu kutumika kwa ajili ya dini aliyotummwa Mtume Muhammad na wafuasi wake. Ingawa Uislamu unaafikiana na dini za kweli zilizotangulia, dini hiyo ina baadhi ya sifa mahususi na baadhi ya maamrisho mahususi ya kipekee kwa jamii inayoifuata. Kwa mujibu wa kundi jingine la wanazuoni, pia inawezekana kwa dini zilizotangulia za mbinguni kuweza kuitwa Uislamu. Wanaeleza kuwa, katika Qur’an Tukufu kuna aya kadhaa zenye kuunga mkono rai hiyo: maneno ya majibu ya mitume wa Yesu kuwa “Shuhudia kuwa sisi ni Waislamu”, maelezo kuhusu Ibrahim kuwa “Alikuwa Muislamu hanif” na tena kutoa nafasi ya sifa ya ujumla kama vile “Amekupeni jina ‘Waislamu’ hapo kabla na hata sasa” ni mifano ya hilo. Kulingana na mtu kuwa na mitazamo kinzani, maelezo kama hayo yanawahusu Mitume.
Kwa mtazamo wetu, katika vitabu vitukufu isipokuwa Qur’an Tukufu, neno dini halikutajwa kwa ajili ya wafuasi wa vitabu hivyo na kama tutaona maneno kama vile Uyahudi na Ukristo yalitokea baadaye na yakatumiwa kwa ajili ya wafuasi wao baadaye, maana ya maneno “Bila ya shaka Dini mbele ya Mwenyezi Mungu ni Uislamu” yanaweza kufahamika kirahisi. Ingawa dini ilitangazwa na Mtume Muhammad ina kanuni mahususi, huku Qur’an ikithibitisha kwa msisitizo tamko la mitume waliotangulia linaloonesha kuwa walchotangaza kimsingi lilikuwa katika Uislamu; hata hivyo, kwa mujibu wa hekima ya kiungu, njia kamilifu zaidi ya imani hiyo inaweza tu kufikiwa kwa kutumwa Mtume Muhammad.
Kwa hali hiyo,njia pekee ya kuweza kupata radhi za Mtukuka Allah ni kuamini yote Anayoyasema. Kutokana na hayo, kwa kuanzia katika uhalisia, ingawa majina ya dini hizo zingine yanaweza kuwa yalitajwa ili kueleza itikadi fulani, muwafaka wa watafutaji ndani ya mipaka ya Allah Mtukuka unathibitisha lengo la msingi na haliepukiki kwa wakati uliotakiwa kwa ajili ya matamko ya Kiungu ili kuingiza fikra hiyo katika akili na dhamiri ya wanadamu. Wanazuoni wa Kiislamu wameeleza ufahamu huo kama “jamii tiifu” na “jamii iliyolinganiwa”; neno la kwanza hapo linaeleza watu wanaoendea matakwa yao ya utii kwenye yale haswa yaliyotangazwa na kudhihirishwa na Mtume Muhammad; na la pili linaeleza kundi linalowezekana kuwa hivyo ambalo bado halijafikia kiwango hicho isipokuwa katika kipindi cha tafakuri kilichotajwa hapo. Kwa hivyo,kwa kulinganisha na majina kama vile “Uyahudi” na “Ukristo”, baadhi ya waandishi wa Kimagharibi wanaouita Uislamu kwa kulifinya ina kuwa ni “Umuhammadi” halifai kwa sababu liko mbali na ukweli na pia lina sifa ya kuzuia mawasiliano pamoja na yaliyotajwa hapo juu.
Kuifahamu aya kwa njia hiyo katika nukta ya lengo kuu haikinzani na fikra kuwa kilammoja aliyeishi katika wakati wowote au mahali popote na akaacha kumshirikisha Allah na kuweza kujielekeza katika imani hiyo anaweza kuitwa “Muislami” kwa mujibu wa ufahamu wa Qur’an’. Kwa hakika, katika aya kadhaa, inaweza kuonekana kuwa vigezo hivyo vimezingatia kukokoka watu katika ahera.
Kwa maana pana, Uislamu (kuwa Muislamu) unaeeza utii moyo, ulimi na tabia. Utii muhimu zaidi na wa thamani kubwa kati ya hayo ni wa moyo. Katika Qur’an, kunaonekana kuwa neno Uislamu pia linatumika kwa ajili ya utii ambao haujafikiakiwango cha imani.
Maneno “Waliopewa vitabu” limefahamika kwa ujumla kuhusiana na yaliyomokwenye maneno “Watu wa Kitabu”. Neno elimu limeelezwa kama “ufunuo na shuhuda waziwazi”. Katika aya, matamshi ya watu wa Vitabu wanaoangukia katika ridhaa baada tu ya elimu kuja ni kwa ajili ya kuonesha kuwa walijulishwa kiasi cha kutosha kuhusu matamshi ya Kiungu na ingawa hawana udhuru kwa hilo, wanaangukia katika vurugu na kugombana kwa sababu ya makosa yao na kwa kufikiria manufaa yao na tamaa za kibinadamu. Kwa kuanzia na “Kwa sababu ya dhuluma miongoni mwao”, baadhi ya maelezo yalitolewa na watu yaliyodokezwa hapa yalikuwa yanawahusisha Wayahudi au Wakristo au makundi yote mawili. Nuru ya elimu ya kihistoria, hapa, inaweza kusemwa kuwa badala ya kusonga mbele katika njia ya amani na ustaarabu kwa kutumia ufunuo mwongofu uliowekewa, jamii, zilizoambiwa kwa ufunuo wa kiungu, huku akili ya kawaida ikiwekwa mbali kwa sababu ya matakwa ya kibinafsi na hususani kutenganisha katika makundi ya kidini kwa kuzingatia kuwa matakwa yao kinzani yamekosolewa. Licha ya onyo hilo, kukariri kosa hilohilo kwa wanaoamini Qur’an kumesababisha kizuizi muhimu katika kutimiza Mpango wa kufikisha ujumbe wa Kiungu kwa wanadamu kwa njia bora zaidi na kuchukua nafasi wanayostahiki katika the mashindano ya ustaarabu.
4
Inaweza kuthibitishwa kuwa Uisilamu ni dini ya upendo, amani na uvumilivu? Unaweza kutoa mifano ya hayo?
Neno Uisilamu linamaanisha amani kwa Kiarabu. Uisilamu ni dini iliyoteremshwa ili kumwakilisha mtu pamoja na maisha yaliyojaa utulivu na amani ambayo yana huruma isiyo na mwisho ya Allah iko waziwazi. Allah anawaita watu kuja katika maadili ya Uisilamu kuwa ndio kigezo ambacho huruma, uvumilivu na amani vinaweza kufanyiwa kazi. Yafuatay yanaelezwa katika aya 208 ya sura al-Baqara:
“Enyi mlio amini! Ingieni katika Uislamu kwa ukamilifu, wala msifuate nyayo za She’tani; hakika yeye kwenu ni adui aliye wazi.”
Kama inavyoonekana katika aya, Allah anaeleza kuwa usalama wa watu unaweza kuhakikishwa tu kupitia kuukubali Uisilamu na kutekeleza kwa vitendo maadili ya Quran.
Allah anailaani fitina
Allah anawaamuru watu kujiepusha kufanya amali mbovu na kuwakataza na ukafiri, madhambi, uasi, dhuluma, ukandamizaji, mauaji na umwagaji damu. Wale wasiotii amri hii ya Allah wanatambuliwa kuwa ni wale wanaofuata nyayo za Shetani kama aya inavyoeleza; wanajitwalia waziwazi mwelekeo ambao Allah ameuharamisha. Zipo aya nyingi zinazohusiana na suala hilo katika Quran. Mbili kati ya hizo ni hizi zifuatazo:
“Na wale wanao vunja ahadi ya Mwenyezi Mungu baada ya kuzifunga, na wanakata aliyo amrisha Mwenyezi Mungu yaungwe, na wanafanya fisadi katika nchi: hao ndio watakao pata laana, na watapata Nyumba mbaya.” (ar-Rad, 13/25)
“Na utafute, kwa aliyo kupa Mwenyezi Mungu, makaazi ya Akhera. Wala usisahau fungu lako la dunia. Nawe fanya wema kama Mwenyezi Mungu alivyo kufanyia wema wewe. Wala usitafute kufanya ufisadi katika ardhi. Hakika Mwenyezi Mungu hawapendi mafisadi.” (al-Qasas, 28/77)
Kama inavyoonekanwa, Allah anakataza aina zote za matendo yanayohusiana na fitina, ikiwemo kutishia na matumizi ya nguvu na kuwalaani wale wote wanaotenda matendo ya namna hiyo. Mwisilamu ni mtu anaeipamba na kuiboresha dunia.
Uisilamu unaulinda uhuru wa kutafakari na uvumulivu
Uisilamu, ambayo ni dini inayoeleza na kuhakikisha waziwazi uhuru wa kutafakari na maisha, imetoa maamrisho yanayozuia na kukataza kuwekana roho juu, migogoro kati ya watu, kusemana na hata kuwadhania watu vibaya.
Sio tu kutishia na matumizi ya nguvu, Uisilamu unakataza kuweka hata shinikizo dogo kwenye fikra za watu.
“Hapana kulazimisha katika Dini. Kwani Uwongofu umekwisha pambanuka na upotofu.” (al-Baqara, 2/256)
“Wewe si mwenye kuwatawalia.” (al-Ghashiya, 88/22)
Ni kinyume na maumbile na uhalisia wa Uislamu kuwateza nguvu watu ili waamini katika dini au kufanya ibada. Kwa kuwa, Uisilamu umeweka utashi huru na ridhaa makini kuwa ndio sharti la imani. Bila ya shaka, Waisilamu wanaweza kuonya na kuhamasishana hivyo wanaweza kutekeleza kwa vitendo sifa za kimaadili zilizofafanuliwa ndani ya Quran. Hata hivyo, hawawezi kutezana nguvu kuhusiana na hilo. Sio sawa kupendekeza vipaumbele fulani vya kidunia ili kumfanya mtu fulani afanye ibada.
Fikiria kuhusu kigezo cha jumuia kilicho kinyume cha mtindo wa hilo. Mathalani, jaalia kuwa watu wanatezwa nguvu kuabudu. Jumuia ya namna hiyo iko kinyume kabisa na Uisilamu. Kwa kuwa, imani na ibada vinakuwa na thamani vinapotekelezwa kwa ajili ya Allah. Ikiwa mfumo wa utawala utawalazimisha watu kuamini na kuabudu, watu watakuwa ni washika dini kwa sababu ya kuuogopa mfumo-tawala. Kilichokuwa na thamani kwa upande wa dini ni kutekeleza dini kwa vitendo kwa ajili ya Allah katika mazingira huru kabisa.
Allah ameharamisha kuua watu wasio na hatia
Kwa mujibu wa Quran, kumuua mtu asiye na hatia ni moja ya madhambi makubwa mno:
“…aliye muuwa mtu bila ya yeye kuuwa, au kufanya uchafuzi katika nchi, basi ni kama amewauwa watu wote. Na mwenye kumuokoa mtu na mauti ni kama amewaokoa watu wote. Na hakika waliwajia Mitume wetu na hoja zilizo wazi. Kisha wengi katika wao baada ya haya wakawa waharibifu katika nchi.” (al-Maida, 5/32)
“Na wale wasio mwomba mungu mwengine pamoja na Mwenyezi Mungu, wala hawaui nafsi aliyoiharamisha Mwenyezi Mungu isipo kuwa kwa haki, wala hawazini – na atakaye fanya hayo atapata madhara,” (al-Furqan, 25/68)
Kama inavyoonekanwa katika aya hapo juu, wale wanaoua watu wasiokuwa na hatia wanaonywa na adhabu kali. Allah anaeleza kuwa kumuua mtu mmoja ni uhalifu mkubwa mno kama kuua watu wote. Haiwezekani kwa mtu anayetii mipaka iliyowekwa na Allah kumdhuru hata mmoja achilia mbali kuua maelfu ya watu wasio na hatia. Wale wanaodhani kwamba wanaweza kuikwepa haki na kunusurika nayo hawatoweza kukwepa kisasi mbele ya Allah. Kwa hivyo, waumini wanaojua kwamba watalipiziwa mbele ya Allah baada ya kifo wanatenda mambo kwa uangalifu mno ili kutii mipaka iliyowekwa na Allah.
Allah anawaamuru waumini kuwa na huruma
Maadili ya Mwisilamu yanafafanuliwa kama ifuatavyo katika aya:
“Tena awe miongoni mwa walio amini na wakausiana kusubiri na wakausiana kuhurumiana. Hao ndio watu wa kheri wa kuliani.” (al-Balad, 90/17-18)
Moja ya sifa muhimu mno za maadili yaliyoteremshwa na Allah kwa waja Wake ili wapate wokovu Siku ya Kiama, rehema Zake na Pepo ni “kuamrishana subira”.
Uisilamu, unaoelezwa katika Quran, una muundo wa kisasa, wenye kuelimisha na wa kimaendeleo. Mwisilamu wa kweli anayo haiba ya amani, uvumilivu, kidemokrasia, kitamaduni, utambuzi/usomi, uaminifu, jicho la sanaa na sayansi na ustaarabu.
Mwisilamu aliyelelewa na maadili ya juu yaliyotajwa na Quran anatangamana na kila mtu kwa upendo unaotumainiwa na Uisilamu. Anaonesha heshimwa kwa fikra za aina zote, anathamini uzuri wa kisanaa na sanaa, na anaonesha kuwafikiana, sifa za kujumuika pamoja na uwastani. Jumuia zilizoundwa na watu kwa mfumo huo zitakuwa na maendeleo zaidi ya ustaarabu na maadili ya juu kuliko zile za dola za kisasa zinazofuatana na furaha, amani, haki, usalama, wingi wa neema na usitawi.
Allah anaamrisha uvumilivu na subira
Nadharia ya “kusamehe na kuvumilia” iliyotajwa na ibara “shikamana na kusamehe” katika aya 199 ya sura al-Araf katika Quran inaunda moja ya kanuni za kimsingi za dini ya Uisilamu.
Ikirejelewa historia ya Uisilamu, itaonekana waziwazi kuwa ni namna gani sifa hizi muhimu za maadili ya Quran zinatekelezwa kwa vitendo. Waisilamu wanaondosha matendo maovu katika kila pahala wanapopafikia na kuweka uwastani wa uhuru na uvumilivu. Wanawawezesha watu wanaotofautiana kidini, kilugha na kitamaduni kuishi pamoja chini ya paa moja la amani na utulivu; pia wanawafanya wale wanaowatii kunufaika na elimu kubwa, utajiri, na ubwana. Kwa hakika, moja ya sababu muhimu za kwa nini Ufalme wa Uthmaniya, ulienea kwenye eneo kubwa la kijiografia, uliokuwepo kwa karne kadhaa ni kuufanyia kazi uwastani wa uvumilivu na kufahamu kuwa umetambulishwa na Uisilamu. Mara zote Waisilamu wamekuwa ndio wenye huruma zaidi na waadilifu katika vipindi vyao. Matapo mengine ya kikabila yaliyoishi katika umbo hili la mchanganyiko wa kimataifa wametekeleza dini zao kwa uhuru na walikuwa na nyenzo zote za kutekeleza dini zao na tamaduni.
Pindi uvumilivu, waliokuwa nao Waisilamu katika namna yake halisi, utatekelezwa kwa namna ambayo Uisilamu unaamuru, utaleta amani na utulivu kwa dunia nzima. Kwa hakika, yafuatayo yameelezwa katika Quran.
“Mema na maovu hayalingani. Pinga uovu kwa lilio jema zaidi. Hapo yule ambaye baina yako naye pana uadui atakuwa kama rafiki jamaa wa kukuonea uchungu. (Fussilat, 41/34)
Aya ya hapo juu inavutia mazingatio kwa sifa hii.
Yote yanaonesha kuwa sifa za kimaadili ambazo Uisilamu umewashauri watu ni za wema utakaoleta amani, utulivu na haki kwa dunia. Ushenzi, unaoitwa “ugaidi wa Kiisilamu”, ulioweko kwenye agenda ya dunia, ni kazi iliyofanywa na washabiki wajinga ambao wako mbali kabisa-kabisa na maadili ya Quran na wahalifu ambao hawana mahusiano kabisa na dini ya Uisilamu. Utatuzi wa kielimu wa kutumika dhidi ya watu hawa na makundi yanayofanya ushenzi chini ya kusingizio cha Uisilamu ni kuwafundisha watu kuhusu maadili halisi ya kweli ya Uisilamu.
Kwa maneno mengine, dini ya Uisilamu na maadili ya Quran hayaungi mkono ugaidi na magaidi; kinyume chake, yataiokoa ardhi kutokana na matatizo ya ugaidi.
Dini ya Amani na Mtume wa Upendo
Mitume ni watu walioteuliwa kuifanya dunia kuwa ni ardhi ya ustawi na amani. Wameletwa ili kufikisha dini ya Uisilamu, ikimaanisha, “amani na usitawi” kwa utu. Mtume ameeleza yafuatayo katika hadithi:
“Sisi mitume ni ndugu wa baba mmoja, dini yetu ni moja.” (Bukhari, Anbiya, 48)
Allah anaeleza yafuatayo katika Quran:
“Bila ya shaka Dini mbele ya Mwenyezi Mungu ni Uislamu.” (Aal-i Imran, 3/19)
Anatuhabarisha kuwa mitume wote waliteremshwa ili wawajuvye watu kuhusu dini hii na kwamba mitume wameonesha mifano ya mwanzo kwa watu.
Usilamu unamaanisha kuwa ni amani na usitawi. Mwisilamu maana yake ni mtu mwenye kupata amani na usitawi na mwenye lengo la amani na usitawi. Moja ya majina ya Allah ni “Salam” (Amani). Kwa mujibu wa hayo, yeye ndiye chanzo cha amani na usitawi. Mwisilamu anaejisalimisha Kwake ni mtu anaepata amani na utulivu katika ulimwengu wake wa ndani kwa kushikamana na chanzo cha amani na usitawi na kisha ni mwenye kutaka kufikisha amani hii kwa ulimwengu wa nje. Kwa hakika, Mwisilamu mwema anajaribu kujiweka mbali na aina zote za mkanganyiko, migogoro na hisia zenye kuidhuru amani ya ndani hata kama anaishi katika mazingira yasiyopendeza kabisa. Kwa hivyo, Mwisilamu anaeikusudia “Daru’s Salam’ (ardhi ya amani na usitawi), Pepo, amechaguliwa kuifanya dunia kuwa ni ardhi ya amani. Labda ni kwa sababu hii, mtu wa kwanza aliyeingizwa Peponi kabla ya kuja duniani; kwanza, aliumbwa aishi Peponi na aliandaliwa kwa utamaduni wa Peponi; kisha, akaletwa duniani. Vile kutumwa duniani, binadamu ana mapenzi na Pepo; anajaribu kujenga duniani kwanza na anaota angalau kuipata huko ahera.
Vivyo hivyo, jina jengine la Mwisilamu ni mumin (muumini), linalomaanisha kuwa na usalama na uaminifu. Mumin pia ni jina la Allah. Kwa hivyo, muumini maana yake ni mtu anayemwamini Allah, ambaye ndiye chanzo cha usalama na uaminifu, anayeshikamana Naye, ambaye ni mwenye kufungamana na amani ya dunia yake ya ndani na anayechukua uwastani huu wa usalama aliyoujenga katika dunia yake ya ndani kuupeleka katika dunia ya nje. Kwa hivyo, uwepo wa waumini ni jambo zuri kwa kila mtu. Kwa hakika, yafuatayo yanaelezwa ndani ya Quran huku kukitajwa jumuia ya Uisilamu:
“Nyinyi mmekuwa bora ya umma walio tolewa watu, kwa kuwa mnaamrisha mema na mnakataza maovu, na mnamuamini Mwenyezi Mungu…” (Aal-i Imran, 3/110)
Jina jengine la Allah ambaye ni mmiliki wa dini ya Uisilamu ni Wadud (Hud 11/90). Wadud ni nomino inayomaanisha yule anayependa mno au yule anayependwa sana. Ndio, Allah ndio chanzo cha mapenzi. Ameumba mapenzi na akayaweka ndani mwetu pale Alipoyapuliza ndani mwetu kutokana na roho Yake. Kama Ibn Arabi anavyoeleza,
“tumetokana na asili ya mapenzi; tumeumbwa nje ya mapenzi; tukayaelekea mapenzi na kuyapa moyo wetu.” (Ibnu'l-Arabi 1998, 38)
Kwa hakika, yafuatayo yanaelezwa katika aya:
“Hakika Mola wangu Mlezi ni Mwenye kurehemu na Mwenye upendo.” (Hud, 11/90)
Allah, aliye mzuri katika namna zote na anapenda mazuri, ameyaingiza mapenzi katika maumbile ya binadamu, akatuma mitume, waliojawa na upendo, ili upendo uonekana dhahiri katika maneno na mtazamo; pia ametuma vitabu vilivyo na kanuni zinazowawezesha watu kupenda na kupendwa. Hatimaye, alimtuma Bwana Muhammad (s.a.w.) na kuwageuza watu walioshambuliana kikatili kuwa watu wanaopendana na kuwapendelea wengine zaidi ya wao wenyewe. Aya mbili zifuatazo zinahusiana na suala hilo:
“Na shikamaneni kwa Kamba ya Mwenyezi Mungu nyote pamoja, wala msifarikiane. Na kumbukeni neema ya Mwenyezi Mungu iliyo juu yenu: vile mlivyo kuwa nyinyi kwa nyinyi maadui naye akaziunganisha nyoyo zenu; kwa neema yake mkawa ndugu. Na mlikuwa ukingoni mwa shimo la Moto, naye akakuokoeni nalo. Namna hivi Mwenyezi Mungu anakubainishieni Ishara zake ili mpate kuongoka.” (Aal-i Imran, 3/103)
“Na walio na maskani zao na Imani yao kabla yao, wanawapenda walio hamia kwao, wala hawaoni choyo katika vifua vyao kwa walivyo pewa (Wahajiri), bali wanawapendelea kuliko nafsi zao, ingawa wao wenyewe ni wahitaji. Na mwenye kuepushwa uchoyo wa nafsi yake, basi hao ndio wenye kufanikiwa.” (al-Hashr, 59/9)
Kwa mujibu wa Uisilamu, ushindi mkubwa ni amani. Kwa hakika, kinachomaanishwa na ushindi wa wazi katika aya ya mwanzo ya sura ya al-Fath “Hakika tumekufungulia Ushindi wa dhaahiri” ni Mkataba wa Amani wa Hudaybiyah (Tabari, 26:67-68; Ibn Kathir, 4:183) kwa mujibu wa wanazuoni wengi. Kulingana na kipengele muhimu mno cha mkataba huu, uliotiwa saini na makundi mawili yaliyokuwa ukingoni kuingia vitani, Waisilamu na washirikina wa Makkah wasingepigana kwa muda wa miaka kumi. Kwa mkataba huu, uliotiwa saini baada ya mapigano ya Badr, Uhud na Khandaq mnamo mwaka wa 6 wa Kuhama, Mtume (s.a.w.) aliondosha kikwazo cha vita vilivyouepusha Uisilamu, dini ya uaminifu na amani, kutoenea; kwa namna fulani, kikwazo kati ya watu na mapendefu yao na kuutafuta ukweli kiliondoshwa.
Bwana Muhammad (s.a.w.), Nembo ya Upendo na Uaminifu
Bwana Mtume (s.a.w.) alifanya kazi kwa ajili ya wema wa jumuiya, ambayo uwepo wake ni manufaa kwa utu, na alifariki baada ya kuiunda jumuia hiyo. Kwa hakika, alipokuwa hai, Wayahudi wa Khaybar haikuwasaidia kusema, “Pepo imejengwa duniani na Waisilamu” kutokana na yeye kusimamisha haki na usawa. Mtume (s.a.w.) ameonesha na kuweka mfano bora zaidi kupitia mfumo wa maisha yake.
“Hakika nyinyi mnayo ruwaza njema kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu na Siku ya Mwisho, na akamkumbuka Mwenyezi Mungu sana.” (al-Ahzab, 33/21)
Kwa hakika, alithaminiwa na kila mtu wakati wa uhai wake wa miaka-arubaini kabla ya utume mjini Makkah na aliitwa ‘Muhammadu’l-Amin’ (Muhammad Mwaminifu). Uaminifu huu na hadhi hii vilimsababishia/ulimsababisha Bibi Khadijah (r.a.) kumteua kuwa ni kaimu wake katika biashara ya kimataifa; alichaguliwa kuwa ni mwamuzi katika tukio la kuliweka Jiwe Jeusi kwenye Kaaba na alikuwa ni mjumbe wa kuheshimika katika jamii iliyoitwa Hilf al-Fudhul (Umoja wa Waadilifu), ulioanzishwa mjini Makkah ili kupambana dhidi ya dhuluma mjini humo. Uaminifu wake katika ubia wa biashara kabla ya kupewa utume umevutia umakini wa kila mtu. Maisha yake kabla ya utume ni kipindi cha miaka arubaini, ambao ni muda zaidi ya nusu ya maisha yake ya miaka sitini-na-tatu. Katika kipindi hicho, kabla hajapokea ufunuo kutoka kwa Allah, aliishi akiwa safi na mwaminifu ilhali watu wengine wamenyimwa uaminifu. Kwa hivyo, ukamilifu wake wa kimaadili kabla ya utume ni muhimu mno kwa watu wa leo ambao wangetumia sifa hasi/mbaya kuwa ndio kisingizio cha kutomwamini yeye. Yafuatayo yanaelezwa katika aya za Quran zikifafanua kuwa alikuwa ni mtu aliyejulikanwa kwa maadili yake ya juu katika jumuia aliyoishi: “Au hawakumjua Mtume wao, ndio maana wanamkataa?” (al-Mu'minun, 23/69)
“Sema: Mwenyezi Mungu angeli taka nisingeli kusomeeni, wala nisingeli kujuvyeni. Kwani nalikwisha kaa nanyi umri mzima kabla yake! Basi, je! Hamzingatii?” (Yunus, 10/16)
Nimeishi miongoni mwenu kwa miaka arubaini kabla ya kuwa mtume. Mnajua usahihi wangu, uaminifu, kuaminika na kutojua kusoma wala kuandika. Sijawahipo kumwasi Allah nilipokuwa kijana. Iweje mniombe nifanye kitu kama hicho sasa? (Qurtubi, 8:321) Moja ya aya za Quran zinataja sifa zake nzuri kama ifuatavyo:
“Na kwa hakika wewe una malipo yasiyo katika.” (al-Qalam, 68/3)
Aya hii ya sura al-Qalam, iliyoteremshwa kuwa ni sura ya tatu baada ya sura za al-Fatiha na al-Alaq, waziwazi zinathibitisha uaminifu alionao kwa sababu aya za Quran zilizozungukia maisha yake yote bado zilikuwa hazijateremshwa kwa wakati huo. Alikuwa na maadili adhimu na ya juu. Baadaye, Bibi Aisha, mkewe, aliifanyia muhtasari haiba yake ya kimaadili, iliyokuwa ilishapevuka zaidi na kamilifu kwa Quran kama ifuatavyo:
“Maadili yake ni maadili ya Quran.” (I. Hanbal, Musnad, 6:188)
Wakati wa sherehe ya arusi ya Mtume na Bibi Khadijah, Abu Talib, ami yake alimtambulisha mtoto wa nduguye, aliyekuwa na umri wa miaka ishirini-na-tano, kama ifuatavyo: “Kwa kweli, Muhammad ni kijana asiyekuwa na mfano na hawezi kuzingatiwa kuwa ni sawa na kijana yeyote wa Kikuraish. Hivyo, amekuwa ni kijana wa kipekee kwa heshima yake, utukufu wake, wema na weledi.” (I. Hisham, 1/201)
Bibi Khadijah (r.a.) alimwambia Mtume (s.a.w.), mumewe, yafutatayo wakati alipotaharuki mno pale alipopokea ufunuo wa mwanzo:
“Tulia; usiwe na wasiwasi. Naapa kwa Allah kuwa Allah hatokufedhehesha au kukuaibisha. Kwa kuwa, unawatunza ndugu zako. Daima unasema ukweli. Katu hukuwa mbadhirifu. Wewe ni mkunjufu na unawasaidia wanyonge. Unapenda kuwakirimu wageni. Unawasaidia watu walio katika matatizo na waliodhulumiwa.” (ibid, 1:253)
Wema alionao pia umetajwa na maadui zake. Kisra wa Roma alimuuliza Abu Sufyan, ambaye bado hakuwa muumini wakati huo, aliyekuwepo kwa Kisra kama ni balozi, akiuliza kuhusu sifa za Mtume (s.a.w.) na mazungumzo yafutayo yalitokea kati yao:
- Je umewahi kumsikia akisema uongo?
- Hapana, hatujawahi kusikia uongo wowote kutoka kwake.
- Mtu asiyedanganya watu hawezi kuongopa kuhusu Allah.
Jafar b. Abi Talib, aliyehamia Ethiopia, ameeleza yafuatayo mbele ya Najjash:
“Ewe Najjash! Allah ametuletea mtume miongoni mwetu; tumeshamjua kwa miaka arubaini kuwa ni mwaminifu, mtukufu na ni mtu wa kuaminika…” (Ibn Kathir, Tafsir, 2:411)
Mtume (s.a.w.) alikwenda Taif ili kuwafikishia watu wanaoishi huko ujumbe wa Uisilamu na kuwaomba wamuunge mkono alipofurushwa kwa shinikizo kubwa la washirikina na makafiri katika miaka yake kumi ya utume. Alikaa huko kwa miaka kumi na kutembelea nyumba moja baada ya nyengine akiwahubiria kuhusu Uisilamu. Hata hivyo, walimfanya kituko na kumfukuza. Walimrushia mawe na rafiki yake, Zayd mpaka miguu yao ikaroa damu walipokuwa wakiondoka. Alikimbilia kwenye bustani na huko akaomba dua ifuatayo:
“Ewe Allah! Nakulalamikia udhaifu wangu, ukosefu wa nyenzo na mateso niliyofanyiwa na watu. Ewe Mwingi wa Rehema kuliko wote. Ewe Mola Mlezi wa wanyonge na Mola wangu Mlezi pia. Umeniaminisha kwa nani? Kwa watu nisiowazoea ambao wamenipokea kiuadui? Au kwa adui ambaye umemtunuku madaraka juu ya mambo yangu? Kwa kuwa hujanikasirikia, basi sijali. Hisani yako ni tulizo kubwa mno kwangu. Narejea kwako kwenye nuru ya Uso Wako ambao giza la aina zote linatoweka na jambo lolote la dunia hii na baadaye limepangiliwa vyema, isijekuwa hasira Zako au kutokuridhika Kwako kuniangukie mimi. Ninatamani radhi zako mpaka uridhike. Nguvu zote ni zako.” (Köksal, 5/66-71)
Wakati huo huo, malaika alifika na kumwambia Mtume angewaangamiza kama angetaka. Bwana Mtume (s.a.w.) akajibu yafuatayo:
“Hapana. Sitaki waangamizwe. Kinyume chake, natarajia vizazi vyao vitamwabudu Allah na hawatomshirikisha Yeye na kitu chochote.” (Köksal, 5/76)
Jino lake lilipovunjwa katika vita vya Uhud, watu waliomzunguka wakamwomba awalaani washirikina. Akasema,
“Sikuletwa kuja kuwalaani watu. Ewe Mola Mlezi! Waongoe watu wa kabila langu kwa sababu hawaelewi.” (Bukhari, Anbiya, 37)
Kwa kifupi, alikuwa na upendo kwa watu wote; alijitolea maisha yake yote ili kuwaokoa watu; alikuwa mtume wa upendo na huruma. Kwa mujibu wake yeye, kumwongoa mtu mmoja, yaani, kumfanya asilimu, ni bora zaidi kuliko dunia na vilivyomo ndani yake.
Makkah ilikombolewa katika mwaka wa nane wa Hijria. Watu wa Makkah, waliomfukuza Mtume (s.a.w.) na waumini kutoka nje ya mji wao, waliowadhulumu na kuwatesa na walioushambulia mji wa Madinah mara kadhaa baada ya kuhamia huko, walilazimika kujisalimisha kwenye jeshi lililoingia Makkah chini ya amri ya Bwana Mtume (s.a.w.). Ilhali watu wa Makkah wanasubiria kwa wasiwasi na woga, Bwana Mtume (s.a.w.), aliyeonesha upendo, huruma na uvumilivu wa kiwango cha juu, aliwahutubia ifuatavyo:
“Leo hii hamtolaumiwa: Allah atakusameheni, kwani yeye ni Mwingi wa Rehema kwa wale wenye huruma. Ondokeni. Mko huru!” (Köksal, 15/288-289)
Ni muhimu mno kwetu kujua majina na sifa za Mjumbe wa Allah ambazo zimetajwa katika aya za Quran na hadithi ili tumjue vilivyo.
Ni mtume wa huruma (Rasulu'r-Rahma, Nabiyyu'l-Marhama). Hakuletwa kwa kundi fulani maalumu bali ni rehema kwa viumbe wote.
Yeye ni mbashiri wa habari njema na mwonyaji (al-Mubashshir, al-Bashir; al-Mundhir, an-Nadhir).
Yeye ni ukweli ulio dhahiri (al-Haqqu'l-Mubin).
Yeye ni kishikizo cha kuaminika (al-Urwatu'l-Wuthqa).
Yeye ni njia iliyonyooka (as-Siratu'l-Mustaqim).
Yeye ni nyota yenye kupenya mwangaza (an-Najmu'th-Thaqib).
Yeye ni taa inayoangaza nuru (an-Nur, as-Siraju'l-Munir).
Yeye ndiye anayelingania kwa Allah (Dai ilallah).
Yeye ndiye mwombezi ambaye uombezi wake ndio unaokubalika (ash-Shafi', al-Mushaffa').
Yeye ndiye mboreshaji (al-Muslih).
Yeye ndiye kipenzi na rafiki wa Allah (Habibullah, Khalilurrahman).
Yeye ndiye mwenye ushahidi mzuri na hoja (Sahibu'l-Hujja wa'l-Burhan).
Yeye ni mtu wa pekee aliyeteuliwa na Allah (al-Mustafa, al-Mujtaba, al-Mukhtar).
Amesifika; yeye ndiye anayestahiki kusifiwa (Muhammad, Ahmad, Mahmud, Hamid).
Yeye ni Muhammad mwaminifu (Muhammadu'l-Amin).
Yeye ndiye mtume wa mwisho (Khatamu'n-Nabiyyin) (Qadi Iyad, 189-195).
Inawezekana kumjua mtu huyu aliyejawa na upendo, aliyeteuliwa kuwa ni nembo ya uaminifu na wa kuchukuliwa kuwa ndio kigezo si kwa kingine isipokuwa kwa kumjua, kuwa kama yeye na kumpenda. Hichi ndicho kinachokusudiwa kwa kumwelewa yeye. Kwa hakika, alisisitiza ukweli huu kwa kusema,
“Mtu anayeifuata sunnah yangu ni katika mimi; na mwenye kuipuuza sio katika mimi.” (Ma'mar ibn Rashid, 11/291)
Kwa ujumla, kumfahamu na kumpenda Mtume (s.a.w.) kunawezekana tu kupitia kumjua yeye vizuri katika namna zote, kumfuata yeye, kumtaja sana, kuheshimu manufaa ya kilimwengu aliyoyatambulisha, kupenda alichokipenda na kujiweka mbali na asichokipenda, na kuwa na maadili ya Quran, ambayo ndio maadili yake.
Sura za Upendo kutoka katika Maisha ya Mtume
Sasa, tunataka kuonesha baadhi ya sura za upendo kutoka kwenye maisha ya Mjumbe wa Allah:
1. Kumpenda Allah: Mjumbe wa Allah (s.a.w.) alikuwa makini kwamba muda wote alikuwa chini ya uchunguzi wa Allah. Alijaribu kutimiza wajibu wake wa kumhudumia yeye. Lengo lake kuhusiana na hili lilikuwa ni “Kuwa mja anaeshukuru” (Bukhari, "Munafiqun," 79) Mtume (s.a.w.) alikuwa ni mtu aliyemjua Allah kwa namna bora zaidi. Mara zote alikuwa akiwasiliana Naye. Lengo lake la pekee lilikuwa ni kupata radhi Zake. Kifo kilimaanisha kumfikia Yeye. Kwa hakika, mapenzi ya Allah na kupenda kwa ajili ya Allah ndio maudhui makuu katika maneno yake mengi. Isitoshe, ukweli kwamba amejawa na upendo uliounganishwa na uhusiano wake na kuwasiliana na Allah.
2. Kupenda Watoto:Mtume (s.a.w.) aliwabeba watoto mapajani mwake, aliwabusu na kuwabimbabimba. (Bukhari, "Adab", 22) Pale mtu mmoja aliposema kuwa anao watoto kumi lakini hajawahi kumbusu hata mmoja wao, Mtume akasema, “Mtu asiyeonesha huruma hatohurumiwa. Nitafanyaje kama Allah ameondosha huruma moyoni mwako?” (ibid). Aliwajali watoto na vijana; aliwaheshimu na kuwathamini. Vijana walikuwa na nafasi muhimu na ya kipekee kati ya wale waliomwamini yeye. Aliwazawadia vijana fanisi kwa kuwateua kuwa makomandoo wa majeshi kulikowahusisha Maswahaba watukufu. Kwenye vikosi vya Tabuk, alimpa Zayd b. Thabit bendera ya Wana wa Najjar, ambaye alikuwa na miaka ishiri tu; Alimteua Bwana Ali, aliyekuwa na umri wa miaka ishirini-na-moja, kuwa ni mbeba bendera katika Vita vya Badr; alimteua Usama b. Zayd, aliyekuwa na umri wa miaka kumi na nane kuwa ni komando wa jeshi lililokuwa na wanajeshi elfu arobaini lililotumwa dhidi ya Wana wa Qudaa; alimteua Muadh b. Jabal, aliyekuwa na umri wa miaka ishirini-na-moja, kuwa ni kadhi wa Yemen. (Doğuştan Günümüze…, 1:391-392)
3. Kuipenda Familia yake na Jamaa: Alikuwa ni kiongozi wa familia aliyeipenda familia yake. Hakuepuka kuisaidia. Alikuwa akikata-kata nyama, akikata-kata mbogamboga za mung’unye, na kupika. Aliitunza zaidi familia yake kuzingatia wajibu wao kwa Allah kuliko kitu kingine chochote. Kwa kuwa, alipokea amri ifuatayo kutoka kwa Allah:
“Na waamrishe watu wako kusali, na uendelee mwenyewe kwa hayo. Sisi hatukuombi wewe riziki, bali Sisi ndio tunakuruzuku. Na mwisho mwema ni kwa mchamngu.” (Ta-Ha, 20/132)
Alianza kuwalingania watu wake kwanza kwa sababu Allah alimwamuru ifuatavyo:
“Na uwaonye jamaa zako walio karibu nawe.” (ash-Shuara, 26/214)
Daima aliendeleza mahusiano yake na jamaa zake na kuwaomba wafanye hivyo, pia. Mara zote alisisitiza kuwapenda wazazi wawili, aliwahamasisha watu kuwapenda mama zao walezi na kaka zao walezi na marafiki wa baba zao; aliwajali na kuonesha mfano mzuri kabisa.
4. Kuwapenda Marafiki: Mtume (s.a.w.) aliwanyanyua hadhi watu walioishi katika giza la Jahiliyyah hadi kwenye cheo cha watu bora katika historia ya binadamu kwa kuvumilia aina zote za matatizo na ugumu. Aliwasamehe watu waliomtesa kipindi cha nyuma na kuwatukuza.
“Hakika amekwisha kujieni Mtume kutokana na nyinyi wenyewe; yanamhuzunisha yanayo kutaabisheni; anakuhangaikieni sana. Kwa Waumini ni mpole na mwenye huruma.” (at-Tawba, 9/128)
“Na wainamishie bawa lako (la huruma) Waumini.” (al-Hijr, 15/88)
“Na watwae kwa upole wanao kufuata miongoni mwa Waumini...” (ash-Shuara, 26/215)
5. Kuupenda ummah: Alijitolea maisha yake kwa ummah wake; atasema, “Ummah wangu! Umman wangu! Ewe Allah! Nautaka ummah wangu!” ahera wakati mitume wengine watashughulishwa na matatizo yao wenyewe. (Abu Awana, Musnad, 1:158)
6. Kupenda Utu: Yeye ni mtume aliyeletwa kuwa ni rehema kwa viumbe wote (al-Anbiya 21/107). Alimlingania kila mtu kuja katika Uisilamu haijalishi walikuwa wabaya kiasi gani. Alikuwa ni mtume ambaye hakuacha kujitoa muhanga kwa namna yoyote ili kuwaokoa watu. Alizuru majumba, masoko, miji, na alienda safari za mbali katika maeneo mengi chini ya mazingira magumu kabisa. Aliwatendea vyema majirani zake bila ya kujali imani zao. Alipinga kuua watu bila ya haki, kuwatesa na kuwafanya watumwa. Alikataza kuua watu kwa kuwatesa hata katika vita; aliwaamuru wanajeshi wake kutokuwagusa wale ambao hawakushiriki katika vita na wale waliosema tumeukubali Uisilamu. Idadi ya watu waliokufa vitani wakati wa zama zake ilikuwa ni kiasi cha watu mia nne tu.
Upendo na huruma ya Mtume (s.a.w.) ilikuwa na asili ya kiungu:
“Basi ni kwa sababu ya rehema itokayo kwa Mwenyezi Mungu ndio umekuwa laini kwao. Na lau ungeli kuwa mkali, mwenye moyo mgumu, bila ya shaka wangeli kukimbia. Basi wasamehe, na waombee maghfira, na shauriana nao katika mambo. Na ukisha kata shauri basi mtegemee Mwenyezi Mungu. Hakika Mwenyezi Mungu huwapenda wanao mtegemea.” (Aal-i Imran, 3/159)
7. Upendo wake kwa viumbe wengine na mazingira: Tunaona kwamba aliwapa umuhimu viumbe wengine wasiokuwa binadamu, kwa wanyama na mimea na kwamba alifanya kadri awezavyo kuweka mazingira safi.
“Wahurumieni waliopo ardhini ili waliowepo mbinguni wakuhurumieni nyinyi” (Tirmidhi, Birr, 16)
Kwa kuitamka hadithi ya hapo juu, Mtume ameashiria kuhurumiwa ni kuonesha huruma kwa viumbe vyote ardhini. Alieleza kuwa mwanamke aliyempa mbwa maji alisamehewa na yule aliyemuua paka kwa kumtesa alizivuta hasira za Allah. Alipomwona mtu akimkama mbuzi, alisema:
“Unapokama yawache baadhi ya maziwa kwa mtoto wa mbuzi.” (Majmua'z-Zawaid, 8:196)
Alipoulizwa, “je kuna thawabu mtu anazipata kwa kuwafanyia hisani wanyama?, akasema, “Ndio, kuna thawabu kwa kila hisani iliyofanywa kwa kiumbe chochote.” (Bukhari, Shurb, 9) Aliwaamuru watu kutia makali kisu wanapochinja mnyama na sio kuwanyanyasa wanyama wanapowachinja. (Muslim, "Sayd". 57)
Wakati mmoja, alipanda miti ya mitende mia tano (I. Hanbal, 5:354) na kueleza yafuatayo kuhusiana na hilo:
“Kama Mwisilamu atapanda mti kisha wanadamu, wanyama wa nyumbani, wanyamapori au ndege wakala matunda yake, kile walichokila kitazingatiwa kuwa ni sadaka kwa yule aliyeupanda mti ule.” (Muslim, Musaqat, 10)
“Kama unao mche wa mti, basi uatike hata kiama kinapokaribia sana kufika, uatike.” (Bukhari, al-Adabu'l-Mufrad, 168)
Alipomwona mtu anaupiga mti ili kondoo wake wale majani yake, aliingilia kati na kusema
“Taratibu! Kama unataka majani yaanguke, utikise mti; wala usiupige.” (Usdu'l-Ghaba, 3:276)
Allah ameitangaza Makkah kuwa ni eneo lililohifadhiwa (haram) na Mtume (s.a.w.) ameitangaza Madina na Taif kuwa ni maeneo yaliyohifadhiwa. (Bayraktar, 5:223-227)
“Ardhi yote imefanywa ni msikiti kwa ajili yangu; udongo wake ni safi na kufanya vitu kuwa safi.”
Zipo hadithi nyingi zinazoeleza upendo wa Mtume (s.a.w.) kwa Makkah, Madinah, Mlima wa Uhud na sehemu nyenginezo. Pia alipendezwa na viumbe wa mbinguni na kuthamini kupaa kwao na kuratibu nyakati kuwa ndio fursa ya kuomba.
Kumpenda Mtume
Mapenzi ni hisia ambazo zimejikita katika moyo na kudhihirika kwa maneno na ishara. Kumpenda mtu fulani maana yake ni kumpa vitu kwa ajili ya kipenzi. Mapenzi ni tendo la kutoa. Kumpenda Mtume (s.a.w.) ni kuuratibu moyo wa mtu kwa ajili yake, kujitolea muhanga na mtu kutoa mali na maisha kwa ajili yake ikibidi kufanya hivyo. Hili litatokea kwa kumjua tu yeye, kumfuata, kupenda alichokipenda na aliowapenda, kuonesha heshima kwa Quran na sunnah zake, ambazo amezikabidhi kwetu, kuzitunza na kutomtangulia kwenye suala lolote.
Hakuna mapenzi bila ya elimu. Kwa hivyo, hatuwezi kumpenda sawasawa isipokuwa tumjue yeye kikweli. Sio sahihi kuweka mpaka wa kumpenda yeye kwa kuwa na jina lake, kulitaja jina lake kwa heshima, vitu vyake binafsi alivyonavyo (masalio/kumbukumbu). Inamaanisha kuwa makini na ukweli kwamba kumpenda yeye kunamaanisha kulitaja jina lake mara kwa mara kwa heshima, kwamba tunamtaja pale tunapotamka kalima at-tawhid, salawat, tunaposoma na kusikiliza adhan, tunapotamka maombi ya Allahumma salli wa barik “Maamkizi ya Allah, rehema na baraka ziwe juu yako, ewe Mtume!”
Ni lazima kupenda ili kupendwa. Ili kustahiki upendo, kupenda na kupendwa kunawezekana tu kupitia kuwa na mahusiano na Allah ambaye ndio chanzo cha mapenzi.
“Hakika walio amini na wakatenda mema Arrahmani Mwingi wa Rehema atawajaalia mapenzi…” (Maryam, 19/96)
Chanzo cha mapenzi ni Allah, ambaye pia anaitwa al-Wadud (Mwenye Upendo wa Dhati).
“Sema: Ikiwa nyinyi mnampenda Mwenyezi Mungu basi nifuateni mimi, Mwenyezi Mungu atakupendeni na atakufutieni madhambi yenu. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kufuta madhambi na Mwenye kurehemu. Sema: Mt’iini Mwenyezi Mungu na Mtume. Na wakigeuka basi Mwenyezi Mungu hawapendi makafiri.” (Aal-i Imran, 3/31-32)
Marejeo:
Asım Köksal, İslâm Tarihi; Bukhari, al-Adabu'l-Mufrad; Doğuştan Günümüze İslâm Tarihi; Abu Awana, Musnad; Ibn Hisham, as-Siratu'n-Nabawiyya; Ibnu'l-Arabi, İlâhî Aşk, (Kilichofasiriwa na Mahmut Kanık), İstanbul, 1998; Qadi Iyad, Kitabu'sh-Shifa; Ma'mar b. Rashid, al-Jami'; Mehmet Bayraktar, "Asr-ı Saadette Çevre Bilinci", Bütün Yönleriyle Asr-ı Saadet'te İslâm; Muhammed Hamidullah, Hz. Peygamberin Savaşları; Munawi, Faydu'l-Qadir; Tabari, Tafsir; Ibn Kathir, Tafsir; Razi, Tafsir; Qurtubi, Tafsir.
5
Kama Uislamu ni dini ya kweli, kwa nini ni kuna watu wengi wanaoukataa na ambao ni watu wa dini zingine duniani? Nani anayewazuia watu kuwa Waislamu?
Awali ya yote, tusisahau kuwa huenda idadi ya Waislamu ni ya kwanza kwa wingi au angalau ya pili. Kama ingekuwa dini ya kweli inategemea idadi ya wafuasi wake, dini za Ukristo na Uislamu ni za kweli. Mmoja kati ya watu watatu duniani ni Muislamu kwa sasa. Wingi huu wa idadi ni dalili ya ukweli muhimu.
Katika historia nzima, hakuna dini iliyoweza kuwafanya watu wote duniani waifuate. Kama nukta hii itapozingatiwa, italazimu kuamini kuwa hakuna dini ya kweli. Fikra hii si sahihi hata kidogo.
Wale wasiokubali dini ya Uislamu wamegawanyika katika makundi matatu:
Kundi la kwanza: Hawaukubali Uislamu bila ya ushahidi wowote wenye kuupinga. Huko kunaitwa kukataa bila ya kukubali. Yaani, hao ni watu wasiojihangaisha kutaka kujua kama Uislamu ni sahihi au laa, wanaopendelea starehe zao tu, wasiotaka kuukataa Uislamu kwa kuegemea ushahidi wowote au wasiofikiria kutumia juhudi zozote za kukubali Uislamu kwa ushahidi wowote. Watu wengi wasioukubali Uislamu ni kama hao. Hawataki kuacha starehe zao kwa kuukubali Uislamu, unaolenga kuadabisha maisha ya watu kwa kuwabebesha mizigo na majukumu. Kundi hili, lililotofautiana na Uislamu, likokatika ujinga kabisa.
Kundi la pili: Ni watu wenye mzio wa kuuchukia Uislamu bila ya sababu, wasiosikia ushahidi wowote unaoupendelea Uislamu na wanaozingatia kila dalili dhaifu kuwa ni ushahidi ulio kinyume na Uislamu. Hao ni wachache na hawakumudu na kamwe hawataweza kuukataa ukweli wa Uislamu kupitia ushahidi wa kisayansi au wa kimantiki bila ya chuki. Kinyume chake, wengi wasio Waislamu wameukubali Uislamu kupitia sayansi na mantiki katika historia yote. Hata leo, maelfu ya watu, miongoni mwa ambao kuna mamia ya wanasayansi na wahudumu a kanisa, ambao waliuwa Wakristo, ambayo ni dini inayodai kuwa ya wote, wamesilimu na kuendelea kusilimu.
Kwa mujibu wa Nursi, kuna vizuizi vinavyozuia Uislamu, ambayo dini ya wote na inayofanya masuala yake yote yakubaliwe na Akili, dhidi ya kuenea duniani kote. Orodha yake ni kama ifuatavyo:
1. Ujinga wa wageni/wasio-Waislamu. Hata watu wa Kitabu hawakuweza kutofautisha kati ya rangi nyeupe na nyeusi kwa sababu walikuwa wajinga sana.
2. Wanaishi maisha yasiyo ya ustaarabu. Kwa hivyo, walishindwa kabisa kufahamu uzuri wa ustaarabu wa Kiislamu.
3. Hususani watu wa Kitabu, walionekana kung’ang’ania sana dini yao. Ung’ang’anizi huo kiliwazuia kuuona ukweli wa Uislamu.
4. Utawala na udikteta wa wahudumu wa kanisa na viongozi wa kidini. Udikteta huu haukuwaruhusu watu kuwa na uhuru wa kuhoji na kufanya uamuzi.
5. Watu waliwatii na kuwafuata wahudumu wa kanisa na viongozi wa kidini bila ufahamu. Ukweli kuwa Akili za watu zilinyakuliwa na hazikuwaruhusu watu kufikri uwezekano kuwa ukweli ungeweza kuwa mwingine.
6. Mtu mmoja mmoja na utawala wa kijamii na mamlaka waliyo nayo Waislamu. Udikteta huu umeharibu mazuri ya Uislamu na ustaarabu wa Quran kimamlaka na kusababisha mandhari yaliyoonekana kutowafurahisha wageni.
7. Maovu mengi miongoni mwa Waislamu yaliyoanzia kwenye vitendo vilivyokuwa kinyume na Uislamu. Maovu haya yasiyo ya Uislamu yaliharibu mvuto wa jua la Uislamu na kuzuia jua hilo angavu kama mawingu mazito lisizifikie Akili. Vizuizi hivyo viwili vilianza kupotea kwa kuibuka fikra ya uhuru miongoni mwa wanadamu, na Matakwa ya kutafuta ukweli.
8. Kizuizi cha nane kilikuwa kuwepo kwa hadaa kuwa kulikuwa na mabishano katika baadhi ya masuala katika Quran na yaliyothibitishwa na sayansi. Kutokana na hadaa hii, wanasayansi wengi walijitenga na Uislamu, wakifanya kosa kubwa sana.
Kwa mujibu wa Nursi, kikwazo cha kwanza, cha pili na cha tatu vimevunjwa kwa neema ya elimu na ustaarabu, na vimeanza kupotea.
Kikwazo cha nne na cha tano vimeanza kutoweka kwa kuwa fikra ya uhuru na hali ya kutafiti na kutafuta ukweli imejitokeza miongoni mwa watu.
Kikwazo cha sita na cha saba vitatoweka kama udikteta utaondoshwa na upande mbaya wa uovu utaonekana. Ukweli kuwa nguvu ya kimamlaka inayoshikiliwa na mtu mmoja mmoja imeanza kuporomoka inaashiria kuwa udikteta wa kutisha wa makundi makubwa katika jamii na wa kamati pia utaporomoka katika kipindi cha miaka thelathini au arobaini. Na ghadhabu kubwa katika bidii ya Kiislamu, pamoja ma ukweli wa matokeo mabaya ya uovu unadhihirika wazi kuwa vikwazo hivyo viwili vinakaribia kuporomoka; kwa kiasi, vimeanza kuwa hivyo. Inshaallah, vitatoweka kabisa hapo baadaye.
Kikwazo cha nane kinaelekea kwenye kutokomea kwani inadhihirika kuwa hakuna ubishani kati ya ukweli wa Quran uliofahamika kwa usahihi na uvumbuzi uliofahamika vyema wa kisayansi. Hapo nyuma, wanasayansi na wanafalsafa waliupinga Uislamu kwa sababu hawakujua vyema kuhusu uhakika wa Uislamu. Hali hiyo imebadilika kabisa kwa sasa.
“Katika Muhtasari wa Miujiza ya Quran, Risale-i Nur inaonesha nuru za hali ya kimiujiza ya miujiza iliyopo chini ya aya zote zinazoshambuliwa na sayansi, na inadhihirisha ukweli mtukufu, usioweza kufikiwa na sayansi, katika sentensi hizo na ibara za Quran tukufu kuwa lengo la wanasayansi wanalodhani kuwa linaonesha ukosoaji; inamlazimisha hata mwanafalsafa mbishi sana kujisalimisha. Ni ushahidi unaojidhihirisha wenyewe, yeyote anayetaka anaweza kuona.”
“Wakati ujao utakuwa mzuri kwa Uislamu peke yake. Na mtawalawake atakuwa mambo ya kweli ya Quran na imani… Sisi, Waislamu, ambao ni wanafunzi wa Quran, tunafuata ushahidi; tunaendea mambo ya ukweli wa imani kwa njia yay mantiki, ingawa, na nyoyoni mwetu. Hatuachi ushahidi unaopendelea utii usio na fikra na uigaji wa mhudumu wa kansa kama wanavyofanya baadhi ya wafuasi wa dini zingine. Kwa hivyo, siku za baadaye, pindi akili, sayansi na teknolojia itakapoenea, kwa hakika, huo utakuwa wakati Qur'an itakapopanda juu, inayoegemea shuhuda za kimantiki na kuiachia akili ithibitishe.” [Hutbe-i Şamiye (Hotuba ya Damaskas)]
6
Ni yapi masharti ya msingi ambayo dini ya Uislamu inayomshurutisha mtu?
Ili kuweza kufahamu umuhimu unaopewa haki za kibinaadamu katika Uislamu, ni lazima tuangalie hali ya dunia kabla ya Uislamu.
1. Dola zote za duniani zilikuwa zikitawaliwa na tawala za kifalme. Mfalme, mtawala au dola ilikuwa na mamlaka kamili juu ya watu aliowatawala. Aliweza kumnyonga yeyote kwa matakwa yake na hakuwajibika kwa yeyote.
2. Watu waligawanyika katika matabaka. Watu waliomzungua mfalme, ndugu zake na waheshimiwa walikuwa katika daraja la upendeleo. Kwa upande mwingine, kulikuwa na watu wengi waliotwezwa na ambao haki zao zilikiukwa, hao waliunda tabaka jingine. Kulikuwa na tofauti kubwa baina ya matabaka.
3. Utumwa ulitumika katika hali ya unyama mkubwa. Heshima ya mwanadamu ilikandamizwa.
4. Watu walikuwa wakitendewa kulingana na mbari zao na rangi, ubora wa ukoo ulizingatiwa kuwa ndio kigezo pekee. Watu hawakuthaminiwa kwa akili zao, elimu, uwezo, maadili na wema.
5. Hakukuwa na haki za msingi na uhuru. Haki za msingi kama vile uhuru wa dini na dhamiri, haki ya kumiliki mali, uhuru wa kupata makazi, uhuru wa fikra haukumhusu raia wa kawaida. Watu walikuwa wakidhulumiwa na kuteswa kutokana na imani zao na fikra.
6. Kanuni za msingi za sheria zilikandamizwa chini ya miguu. Haikuwezekana hata kufikiria dhana za sheria za msingi kama vile usawa mbele ya sheria, utawala wa sheria, haki ya kutoingiliwa (faragha) na uhalali wa adhabu. Hakukuwa na mahakama huru na isiyopendelea. Matakwa binafsi na amri ziliiweka kando sheria; watu waliotenda uhalifu uliofanana waliadhibiwa adhabu tofauti kwa kuzingatia matabaka yao.
Dunia ilipokuwa hatika hali hii, dini ya Uislamu ilikuja na kufanikisha mapinduzi makubwa katika historia ya mwanadamu.
Ikiangaliwa kwa macho yasiyo na upendeleo, itaonekana kuwa malengo makuu ya kibinadamu yanayoamuliwa sasa yalishaamuliwa katika Quran na katika Sunnah za Mtume Mtukufu kwa karne nyingi kabla ya matamko ya haki za kibinaadamu kutolewa katika ulimwengu wa Magharibi.
Kwa hakika, kanuni zinazohusu haki za kibinadamu zilizomo katika hotuba (Hotuba ya Kuaga) aliyohutubu Mtukufu Mtume (s.a.w) wakati wa Hajj ya Kuaga ni mfano wa wazi juu ya hilo.
Hotuba hiyo iliyosomwa katika hadhara ya Waislamu zaidi ya 100.000 mnamo mwaka 632 BK; yaani, miaka 1157 kabla ya Tamko la Haki za Mwanadamu na Raia kutolewa mwaka 1789, linalozingatiwa kuwa ni waraka wa kwanza wa kimaandishi unaohusu haki za kibinaadamu.
Kanuni hizo mpya zilizowekwa na Uislamu kuhusu haki za kibinaadamu zilikuwa ni zenye kuvutia mno juu ya kupigania haki za kibinaadamu huko Magharibi.
Mwanadamu ana thamani zaidi ya kipekee kuliko viumbe wengine. Thamani hiyo huongezeka anapomwamini Allah na kutii amri Zake. Hivyo, mwanadamu anakuwa mgeni mheshimiwa zaidi ulimwenguni. Mwanadamu anapata thamani ya utu anapozaliwa au hata kabla yake, kwa kuumbika kwake katika mji wa mimba, na anakuwa nayo katika maisha yake yote.
Thamani inayoanzia tokea kuwa mwanadamu inamwenea kila mmoja. Huruma hii imemzingira kila mmoja, mwanamume au mwanamke, mzee au kijana, mweusi au mweupe, mnyonge au mwenye nguvu, masikini au tajiri pasi na kujali dini, taifa, mbari na rangi zao.
Hivyo dini ya Uislamu inahifadhi damu ya kila mmoja isimwagwe, heshima isivunjwe, mali isiporwe, nyumba isiingiliwe bila ya ruhusa, ukoo usivunjwe na dhamiri kutokandamizwa. Inahakikisha heshima na hadhi ya kibinadamu.
Haki za msingi na uhuru ulioleta utu kutokana na Uislamu ni kama ifuatavyo:
1. Uislamu umemaliza ubaguzi wa kimbari na rangi. Watu wote wanatokana na Adam. Haiwezekani mtu kujichagulia mbari na rangi. Ni kudura ya Allah. Ni makosa makubwa na madhara makubwa kwa Uislamu na utu kuwabagua watu kwa rangi na mbari na kudharau baadhi ya mbari na rangi na kuwatazama wengine kuwa ni bora.
Allah anaeleza katika Quran kuwa amewaumba watu kutokana na mwanamume mmoja na mwanamke mmoja, na akawafanya mataifa na makabila wanapoongezeka ili waweze kujuana. (al-Hujurat, 13)
Kama ilivyoonekana, sababu ya watu kutofautiana kwa mbari na rangi ni kujuana na kusaidiana wala si kudai kuwa ni bora.
Tukio litakaloangazia ufahamu huu wa Uislamu ni kama ifuatavyo:
Swahaba Abu Dharr, siku moja alimkasirikia Bilal al-Habashi na akamtukana kwa kumwita, “mtoto wa mwanamke mweusi”. Abu Dharr alimdharau kwa sababu ya rangi ya mama yake. Mtume (s.a.w) alipoambiwa hayo, Mtume alikasirika na akamwambia Abu Dharr kama ifuatavyo:
— Ewe Abu Dharr! Umemshutumu Bilal kwa sababu ya rangi ya mama yake? Inamaanisha kuwa bado una fikra za Jahiliyya!"
Abu Dharr, ambaye alitamka maneno hayo kutokana na kushikwa na ghadhabu za ghafla bila ya kukusudia, alisikitikia sana alichofanya na akatubu. Alianza kulia, akalala chini na kuweka uso wake chini; kisha, akasema,
“Sitainua uso wangu kutoka ardhini isipokuwa mpaka Bilal aje kunikanyaga shavuni.” Akakariri kumwomba msamaha Bilal.
2. Uislamu umekomesha jambo la kujifaharisha kwa koo na mababu. Katika mkutano ambao Maswahaba walikuwepo, Sa'd bin Abi Waqqas aliwaomba baadhi ya Maswahaba mashuhuri wawaorodheshe wahenga wao. Wakati huo huo, aliwaorodhesha wahenga wake tokea mwanzo mpaka mwisho. Salman al-Farisi (Mwirani) pia alikuwepo hapo. Hakuwa na wahenga wa kujifaharisha nao kama wa-Qurayshi. Hakuwajua wahenga wake kwa kina, pia.
Sa'd bin Abi Waqqas alipomwomba awaorodheshe wahenga wake, hakupendezwa na ombi hilo na akasema, “Mimi ni Salman; mwana wa Uislamu. Siwajui wahenga wangu kama mlivyo nyinyi. Ninajua jambo moja tu. Allah amenitukuza kupitia Uislamu.”
Swahaba Umar pia aliudhiwa na jambo hilo lisilo la lazima la Sa’d lililoleta hisia za Jahiliyya. Alilipenda sana jibu hili lenye maana kubwa la Salman; akasema, “Mimi ni Umar; mwana wa Uislamu.” Hivyo, alitoa jibu sawa na la Salman.
Mtume (s.a.w) aliposikia habari za tukio hilo, alilipenda sana jibu la Salman. Akasema, “Salman ni katika mimi; anatoka katika familia yangu.”
Mtume aliwaozesha mabinti wa familia mashuhuri za wa-Quraysh kwa baadhi ya watumwa waliopewa uhuru miongoni mwa Maswahaba; hivyo, aliondosha fikra za Jahiliyya zilizoegemea ubora wa koo.
3. Uislamu umewapa watu haki ya kuangalia na kuwakagua watawala wao. Unalenga kumaliza vitendo vya kidikteta, uonevu, dhuluma na uhalifu.
Swahaba Abu Bakr alipoteuliwa kuwa Halifa, aliwahutubia watu kama ifuatavyo:
"Enyi watu! Nimeteuliwa kuwa ni kiongozi wenu ingawa mimi si mbora zaidi baina yenu. Kama nitatekeleza jukumu langu kulingana na Uislamu, nitiini. Kama nitaiacha njia sahihi, nionyeni."
Siku moja, wakati wa Ukhalifa wake, Swahaba Umar aliwauliza Waislamu msikitini, "Mtafanyaje kama nitaiacha njia sahihi? Wakasema, "Tutakusahihisha kwa mapanga yetu." Swahaba Umar akafurahi baada ya kusikia jibu hilo.
4. Uhuru wa fikra na dhamiri. Uhuru wa fikra na dhamiri ni haki muhimu zaidi baada ya haki ya kuishi. Kumnyima mtu haki hii kunamaanisha kumtoa katika utu wake na kumshusha mpaka katika kiwango cha wanyama. Kwa hiyo, Uislamu hauruhusu kukandamizwa fikra na dhamiri. Huku kukiwa na kanuni, “kusiwe na kulazimishana katika dini”, Uislamu haukuzingatii huko kufaa kuwafanya watu wakubali kanuni za imani kwa nguvu.
5. Uislamu umeshughulikia desturi ya utumwa kwa uangalifu sana na kulipa hilo ngazi ya kisheria.
Dini ya Uislamu ilipokuja, utumwa ulikuwa umeenea kote duniani pamoja na vitendo vyake viovu sana na vya kinyama. Uislamu kwa kawaida haukutarajiwa kuukomesha mfumo huo kikamilifu, ambao ulienea duniani kote. Kwa hivyo, haukukomesha utumwa kisiasa kali na kwa ghafla lakini ulirekebisha sana masharti na kuupa hali ya utu na ustaarabu zaidi. Licha ya hayo, Uislamu uliongeza na kurahisisha njia za uhuru na kuingiza kanuni ambazo zingekomesha utumwa kwa njia isiyo dhahiri.
6. Uhuru wa Mali. Kupenda vitu na tamaa ili kupata mali ni miongoni mwa hisia kadhaa ambazo Allah alimpa mwanadamu. Hili limeelezwa wazi katika Quran.
Uislamu umempa kila mtu haki ya mali na kuwaandalia namna ya kutimiza haja hii kihalali. Haki iliyowekwa na Uislamu kwa kila mmoja kuweza kumiliki mali kamwe haiwezi kuingiliwa bila ya idhini ya mwenyewe.
7. Usawa wa Kisheria. Uislamu unawatazama watu wote kwa usawa mbele ya sheria kama yalivyo meno ya kitana. Hauruhusu upendeleo unaozingatia hali ya kijamii na koo za watu.
Katika Uislamu, utawala wa sheria na sheria hiyo kuwa juu ni lazima. Mkuu wa dola na watu wa kawaida hutendewa sawa. Mhalifu kwa hakika huadhibiwa hata kama ni mkuu wa dola.
Kesi ya Fatih Sultan Mehmet na msanifu majengo wa Kigiriki, Swahaba Ali na Myahudi, Salahaddin al-Ayyubi na Mwarmenia katika hadhara ya makadhi ni mifano yenye kuvutia sana kuhusu jambo hili.
Katika siku ya ushindi wa Makkah, mwanamke mmoja kutoka familia mashuhuri ya kabila la Makhzum aliiba na kukamatwa nacho. Alipaswa kuadhibiwa. Hata hivyo, kwa kuwa alikuwa ni wa familia mashuhuri, hawakutaka familia hiyo kuaibika; kwa hivyo, walitaka mwanamke huyo asamehewe. Wangelifanyaje hilo? Wangemweleza nini Mtume kuhusu hilo? Hatimaye, waliamua kumtuma Usama, ambaye Mtume alimpenda sana, kwenda kwa Mtume. Usama alikwenda mbele ya Mtume na kumweleza suala hilo. Akamwomba Mtume amsamehe mwanamke mwenye hatia. Mtume alikasirika sana. Akatoka na kutoa hotuba ifuatayo ya kihistoria: “Enyi watu! Mnajua sababu za umma za kabla yenu kuangamizwa? Mtu wa hadhi ya juu alipotenda uhalifu, wao, walimwachilia. Mtu wa kawaida alipotenda kosa, kwa hasira walimtaka mtu huyo aadhibiwe. Ukandamizaji huu ulisababisha kuangamizwa kwao. Naapa kwa Allah, kama Fatima, binti wa Muhammad, angeiba, ningemwadhibu bila ya kusita.
Hapo, adhabu ilitimizwa.
Maneno yaliyo katika hotuba ya Swahaba Abu Bakr alipoteuliwa kuwa Khalifa hayana kifani.
"Walio dhaifu miongoni mwenu ndio wenye nguvu zaidi machoni mwangu mpaka wapate haki zao; wenye nguvu ni dhaifu sana machoni mwangu mpaka nichukue haki za wengine kutoka kwao."
8. Kutoingiliwa na Uhalali wa Adhabu. Katika Uislamu, hakuna adhabu bila ya sheria, na haiwezekani kumwadhibu mwingine badala ya mhalifu.
Kanuni ya kutoingiliwa na uhalali wa adhabu imeelezwa kama ifuatavyo katika sura al-Anam: "Na kila nafsi haichumii ila nafsi yake. Na habebi mwenye kubeba mzigo wa mwenziwe." (Aya: 164)
9. Uhuru na Uadilifu wa Mahakama. Katika Uislamu, mahakama, ambazo ni taasisi za haki, zimeepushwa na kila namna ya msukuko kutoka nje, chuki binafsi na kinyongo, na matendo ya kidikteta; mahakimu hawaruhusiwi kupoteza uadilifu wao. Katika mahakama za Kiislamu, wakuu wa dola wameshitakiwa sambamba na raia wa kawaida; walikuwa wakiadhibiwa ikiwa walikutwa na hatia.
10. Kinga ya Makazi na Kutoingiliwa. Katika Uislamu, hakuna mwenye haki ya kumwingilia mtu na kuingia katika makazi yake bila ya idhini. Katika Uislamu kumekatazwa kupeleleza mambo ya faragha ya watu.
11. Uhuru wa Kusafiri. Uislamu unazingatia kuwa safari humsaidia mtu kujifunza mambo na kupona maradhi. Kwa hiyo, watu wanahamasishwa kusafiri.
12. Haki ya kuishi na kuhakikisha ulinzi wa uhai, mali na heshima. Hili limeelezwa vyema na Mjumbe wa Allah katika Hotuba ya Kuaga:
"Enyi Watu!, kama mnavyoutazama mwezi huu, siku hii, na mji huu, Makkah, kuwa ni mtukufu, basi utazameni uhai, mali na heshima ya kila Muislamu kuwa ni dhamana takatifu. Hayo yamehifadhiwa dhidi ya namna zote za ukiukwaji."
13. Hifadhi ya Kijamii. Dini ya Uislamu inamlinda mtu ili asipate tabu na asidhuriwe kwa uzee, ugonjwa, majanga, na ajali; unamhakikishia maisha mema ya baadaye wa masikini kwa njia za hifadhi ya kijamii ilizoziweka. Uislamu unawahimiza watu kufanya kazi kwanza ili waweze kujitunza wenyewe kifedha. Kwa kuongezea, umeweka hifadhi ya kipekee katika familia na baina ya majirani na shukrani ziende kwenye taratibu kadhaa ilizoziweka. Taratibu hizo zote za hifadhi zisipotosheleza, dola yenyewe inahakikisha hifadhi ya kila mmoja. Utaratibu wa zakah na taasisi zingine ndizo hifadhi za uhakika za kijamii.
14. Uhuru wa kazi, mishahara, haki na usawa. Kufanya kazi na kufanya juhudi kunatambuliwa na kuhimizwa katika Uislamu. Hakupendezi kuombaomba na kuwa ni mzigo kwa wengine. Kufanya kazi ili kupata riziki kwa njia halali kunazingatiwa kuwa ni ibada kama mtu huyo atakamilisha majukumu yake ya faradhi. Aya inayosema "Mtu huyo hatakuwa na kingine isipokuwa kile anachokipigania" inaonesha umuhimu ambao Uislamu umeweka kwenye bidii na kazi.
Kwa kuhakikisha uhuru wa kazi — kwa sharti kuwa imepatikana kihalali —, Uislamu unapanga mahusiano baina ya waajiriwa na mwajiri katika njia bora kabisa.
Kanuni ya "Mlipe mfanyakazi mshahara wake kabla jasho lake halijakauka" inahakikisha haki ya mfanyakazi katika njia kamilifu.
Kama ilivyo kanuni, mfanyakazi atajitaidi kufanya kikamilifu kazi aliyopewa na kwa namna bora zaidi na kustahiki mshahara anaoupata.
15. Ulinzi wa Watoto. Uislamu unawatunza watoto tangu kuzaliwa kwao, unawasaidia wazazi katika matumizi yao ya chakula na mavazi na unatenga mali kwa ajili yao kutoka hazina. Leo, dola zote tajiri huwapa ruzuku wazazi kwa ajili ya watoto. Mjumbe wa Allah alilisisitiza jeshi lake kutowaua wanawake na hususani watoto wakati wa vita.
16. Elimu ya Msingi ni Lazima na Bure. Hadithi inayosema, "Kutafuta elimu ni faradhi kwa kila Muislamu, mwanamume na mwanamke" inaweka elimu ya lazima. Mtaala wa elimu ya msingi umeandaliwa kwa uangalifu katika Uislamu.
Pamoja na, elimu ya kidini, elimu ya kimaadili na ya kujua kusoma na kuandika, elimu ya ufundi imejumuishwa katika elimu ya msingi. Uislamu unaona kuwa ni lazima mtoto ajifundishe elimu ya ufundi pamoja na elimu ya dini.
7
Sharia ni nini, Sharia imeishi vipi, je, Sharia inafaa katika karne hii?
Uislamu umetanguliza rai zake kuhusu utaratibu wa kiutawala kama ulivyofanya kwenye masuala mengine. Uislamu umeweka kanuni kadhaa kwa ajili ya usimamizi wa dola. Dola inatakiwa iongozwe kwa kuzingatia kanuni kama vile haki, sheria, kutokiuka haki za binadamu, kutotumia vibaya uongozi wa dola, n.k.
Sharia ni jina la hukumu za ujumla na sheria zilizoletwa na Uislamu. Inajumuisha uongozi wa dola, pia.
Lazima tufikishe na tuishi maisha ya Uislamu wa kweli na ukweli unaokubaliana na Uislamu. Kwa hivyo, baadhi ya matumizi yenye kufanyika kwa jina la Uislamu lakini hayakubaliani na Uislamu yana madhara kwa Uislamu na Waislamu.
Unakutana na mtu. Anasema kuwa anaswali na anafunga. Unaendelea kuzungumza na unagundua kuwa mtu huyo anayetekeleza amri hizo mbili muhimu zaidi anapinga Sharia na unapatwa na mshangao.
Unakutana na mtu mwingine. Anaitetea Sharia kwa shauku kubwa. Unapoingia kwa kina katika maisha yake ya ndani na ufanyaji ibada, unagundua kwamba hana hata 1% ya shauku yake anayoionesha katika kutumia sheria ya adhabu ya Kiislamu kwenye ibada yake. Unapatwa na mshangao tena.
Unakuwa na rai inayofanana kuhusu watu hao wawili: Hawaijui Sharia!
Nini sharia na isiyo sharia?
Sharia inamaanisha “dini”, “amri ya Allah”, “amri na makatazo ya Allah”.
Mtu anapaswa kujua maana ya dhana pindi anapoikataa au kuikubali. Kuiunga mkono au kuipinga ni jambo jingine.
Dhana mojawapo inayojadiliwa zaidi ni Sharia. Watu wengi wana kiwewe kuhusu jambo hilo. Kila mmoja anaizungumzia, haijalishi kama wanajua maana yake au hapana.
Kwanza, hebu tuangalie kamusi inayozingatiwa kuwa ni kamusi muhimu zaidi katika lugha yetu, “Qamus” ya Shamsuddin Sami:
Sharia inafafanuliwa kuwa ni, “sheria ya Allah inayotegemea amri na makatazo ya Allah, na kanuni za aya, hadithi na ijma (muafaka) wa ummah.”
Mambo mawili yanavuta hisia katika ufafanuzi huo. Moja ni ukweli kuwa Sharia ni “amri na makatazo ya Allah”. Jingine ni kuwa, sheria hizo za Allah zinategemea juu ya “aya, hadith, na ijma ya ummah.”
Ömer Nasuhi Bilmen anaeleza neno hilo katika kazi yake ya uhakika: “Hukuk-u İslamiyye ve Istılahat-ı Fıkhiyye Kamusu” kama ifuatavyo kwa kirefu:
“Katika lugha ya dini, Sharia ni hukumu zote za kidini na za kidunia, sheria alizoziweka Allah Mtukuka kwa waja Wake. Kwa hivyo, Sharia ni usawe wa dini na inajumuisha kanuni za imani zinazoitwa sheria za msingi, na ibada, maadili na sheria za madai zinazoitwa hukumu za kinaganaga.”
“Sharia inamaanisha sheria ya Allah iliyofikishwa na Mtume kwa mujibu wa maana yake ya ujumla. Inapotamkwa ibara ‘sheria za Sharia’, ni muhimu kufahamu hukumu za sheria ya Allah. Na, kinachomaanishwa na hiyo ni hukumu ambazo zinategemea Quran, hadithi na ijma.”
Nukta kuu zifuatazo zimeorodheshwa kitaalamu katika ufafanuzi wa kinaganaga hapo juu:
1. Allah ameweka Sharia kwa ajili ya Waja Wake.
2. Sharia ni ukamilifu wa hukumu za kidini na kidunia.
3. Sharia ni kisawe cha neno “dini”.
4. Kuna hukumu zote kuhusu maadili, ibada na maisha ya kila siku pamoja na hukumu kuhusu kuamini dhana ya Sharia.
5. Kwa ujumla, sheria ya Allah iliyotambulishwa na kila Mtume inaitwa Sharia.
6. Kinachokusudiwa na Sharia ni dhahiri kuwa ni hukumu zinazotegemea Quran, hadithi na ijma.
Mfasiri (mufassir) mmojawapo wa zama zetu, Elmalılı Hamdi Efendi anaeleza Sharia kama ifuatavyo katika tafsiri yake adhimu iitwayo, “Hak Dini Kur'an Dili”:
“Katika kamusi, Sharia inamaanisha njia inayofuatwa ili kuteka maji mtoni au katika chanzo cha maji. Hutumika kisitiari kwa ajili ya sheria maalumu na njia nyoofu iliyowekwa na Allah kwa wanadamu ili kuwawezesha wafikie maisha ya milele na furaha halisi, inayomaanisha dini.”
There are also some important points that attract attention in that definition, too:
Pia kuna baadhi ya nukta muhimu zinazovutia kutokana na ufafanuzi huo, pia:
1. Allah ameweka Sharia na kuwawajibisha waja Wake.
2. Allah ameshusha Sharia ili Waja Wake wafikie maisha ya milele na furaha halisi.
3. Sharia ni jina la njia ya hukumu nyoofu na sheria mahususi.
4. Sharia inamaanisha dini.
Mwanazuoni mashuhuri mwenye fikra nyingi wa zama zetu, Badiuzzaman, anaeleza yafuatayo alipokuwa akifafanua Sharia:
“Sharia inamaanisha mambo mawili. La kwanza ni Sharia inayoratibu vitendo na hali za mtu, ambaye ni dunia ndogo, inayokuja kutoka katika sifa ya maneno. La pili ni Sharia kubwa ya kimaumbile inayoratibu utendaji na utulizano wa dunia, ambayo ni mtu mkubwa, inayotokana na sifa ya utashi, ambayo wakati mwingine kimakosa huitwa maumbile.”
Kuna nukta kadhaa muhimu katika ufafanuzi huo, pia. Badiuzzaman anaieleza Sharia kwa kuigawanya katika sehemu mbili na kufafanua dhana ya maumbile.
1. Sharia tunayoijua, inayoratibu vitendo na hali za mtu, ambaye ni “dunia ndogo”, inayotokana na sifa ya Allah ya kusema.
2. Sharia inayoratibu utendaji na utulizano wa dunia, ambayo ni “mtu mkubwa”.
3. Ni makosa kuziita sharia katika dunia yakinifu kuwa ni “maumbile” kwa sababu dhana hiyo haidokezi kuhusu Allah. Hata hivyo, Allah ndiye anayeweka na kutumia sheria za kimaumbile.
Maelezo hayo yanadokeza maana nyingine: Dunia hii imepangwa vizuri na kamilifu kwasababu viumbe wa ulimwenguni wanatii sheria za asili za Allah bila ya kuasi. Hakuna dosari hata chembe. Maana yake, kama wanadamu watatii sheria ya Allah bila ya kuasi, watafikia upatanifu walioukosa na furaha wanayoitafuta. Sababu ya kutokupatana na kutokutulia ni uasi na uchupaji mipaka. Ufunguo wa kupata amani duniani upo katika Uislamu kama ilivyo furaha ya ahera.
Kutokana na maelezo hayo yote, mtu anayesema, “Sharia” anasema, “kanuni za kidini”. Mwanadamu ni kiumbe huru.
Anaweza kukubali au kukataa.... “Hakuna kulazimishana katika dini.”
Sharia imeishi vipi?
Allah, ambaye ameipa mbegu uwezo wa kuwa mti na ambaye ameupangilia kuzaa maatunda, ameweka baadhi ya hali za utambuzi wake. Mkusanyiko wa hali hizo unaitwa Sharia ya kimaumbile. Mbegu hiyo inahitaji kupata udongo wake, kukutana na maji na kupata jua ili iwe mti.
Maumbile ya mwanadamu ni kama mbegu hiyo, mbegu inayoweza kuleta uhai Peponi. Sharia ni mkusanyiko wa sheria ambazo mwanadamu anahitajika kutii ili astahiki kuingia Peponi, ambapo ni mahali pa furaha ya maumbile ya mwanadamu.
Akili inaweza kumjua Allah kama itafikiria ndani ya mipaka aliyoiweka Allah. Ulimi unakuwa mteuliwa kwa ajili ya kutamka maneno matukufu katika ardhi hiyo ya milele kwa kusema maneno mema na ya manufaa. Mwili unastahiki kupata manufaa yanayotokana na neema za mali za ardhi hiyo ya furaha kwa sababu ya kujichosha kwake kwa ajili ya Allah.
Kutokana na hisia kama vile upendo, hofu na huruma kwenye jicho, sikio, mkono na mguu, kila kitu kinaboreka, kinanyanyuka na kwenda kwenye ulimwengu wa juu zaidi kama tu vitafanya kazi kulingana na amri za Allah. Sharia ni jina la njia ya kuuendea ukweli. Maana yake katika kamusi ni “njia iliyofuatwa ili kupata maji kutoka katika chanzo cha maji”.
Yunus, mshairi wa kisufi, ameeleza kwa muhtasari njia ya kumfikia Allah na kupata ukweli kama ifuatavyo katika shairi: Sharia na tariqah ni njia kwa ajili ya wanaoweza, tunda la ukweli limo ndani mwake.
Kikomo cha safari hakitaweza kufikiwa bila ya kutembea njiani. Madai ya kuufikia ukweli bila ya Sharia ni hadaa isiyo na lolote isipokuwa kuwavuruga wanaodai umakini wa mwenye kumiliki.
Tariqah ni alama ya ibada ya sunna (nafilah). Ni kitendo cha mafunzo yanayopaswa kufanyika ili kuweza kutembea kwa uimara katika njia ya Sharia na kuwa na nguvu zaidi dhidi ya nafsi na shetani. Ni njia ya mja kujisogeza karibu na Mola wake Mlezi. Inamsaidia mtu kuizoeza nafsi yake kwa ufanisi zaidi.
Kwa kifupi, ni muhimu kutii amri za Allah kwa usahihi na kuendeleza ibada za sunna ili kuufanya moyo wa mtu uwe thabiti na roho yake iwe na nguvu zaidi. Hebu tumsikilize imamu Rabbani:
“Ni Sharia kuuzuia ulimi usiseme uongo na useme ukweli. Kama mtu ataondosha fikra ya kuongopa kutoka moyoni mwake kwa kujibidiisha, ni tariqah; kama ataifanya bila ya shida yoyote, ni haqiqah (ukweli).”
Je, hatuyafahamu yafuatayo kutokana na mfano mzuri wa imamu huyo mashuhuri? Kusema ukweli muda wote. Ni maadili ya juu ambayo Allah ameridhika nayo, ambayo ni haqiqah. Mja kwanza anatakiwa atii amri ya Sharia, “usidanganye” ili kufikia haqiqah hiyo; auepushe ulimi wake mbali na dhambi hiyo. Kisha, anaanza kutibu roho yake ili hali ya kutaka kudanganya isijitokeze moyoni mwake. Anaanza kujitahidi kuitambua. Mwishowe, moyo unaanza kuchukia kusema uongo bila ya kuulazimisha au kufanya bidii. Kutokea hapo na kuendelea, uongo hautaukaribia moyo huo. Anapozungumza, kwa hakika atasema ukweli kirahisi. Mtu huyo anazingatiwa kuwa amefikia haqiqah ya kusema ukweli.
Inafahamika kutokana na kauli ya imamu mashuhuri kuwa inawezekana kupata mwisho mwema bila ya tariqah. Mtu anaweza kupata fursa ya kupata haqiqah moja kwa moja kutoka katika Sharia. Hata hivyo, ni hakika kuwa fursa hiyo haitaweza kuwepo bila ya Sharia.
Sitaki kufanya uchambuzi wa tasawwuf (usufi) hapa. Nimeandika sentensi kadhaa hapo juu ili kueleza kuwa haitakuwa timilifu kufahamu kanuni za Uislamu tu kuhusu sheria ya adhabu pindi dhana ya Sharia inapotajwa. Kutokuongopa pia ni Sharia. Mtu asiyedanganya, hasengenyi, haingilii mali, maisha na wake wa watu yuko katika njia ya Sharia na haqiqah. Kama mtu wa namna hiyo atapinga Sharia, atakuwa anajipinga mwenyewe.
Msingi wa dini umeegemea katika kuumbwa kwa mwanadamu. Kuwepo kwa ulimwengu wa viumbe visivyo hai. Kila chembe, nyota, hewa, udongo, maji, mwangaza, kwa kifupi, kila kitu kinategemea utashi enevu wa Allah. Vinashughulika kulingana na sheria ya Allah aliyoiweka. Kila kitu kinatii Amri Zake kulingana na utashi Wake. Ulimwengu wa malaika unatoa uoni mwingine wa ukweli. Viumbe hao, walioumbwa ili kufanya ibada, kumtukuza na kumsifu Allah, hawana utashi kama wanadamu walivyo. Wanatimiza amri zote za Allah.
Ama kuhusu mwanadamu, analeta mtazamo tofauti kabisa katika rangi ya maumbile. Kila seli na kiungo cha tunda la hisia la ulimwengu linalomtukuza Allah linadumu katika kumtukuza na kumwabudu Allah. Usimamizi wao haumtegemei mwanadamu. Yeye mwenyewe hawezi kulifanya ini lake lifanye kazi; hawezi kuifanya damu mwilini mwake izunguke kwa kufuata utashi. Sultani huchaguliwa katika nchi ya mwili ambaye humtii Allah pamoja na seli zake zote: Roho hupewa utashi kama Baraka kubwa na mtihani.
Mwanadamu ana hiari na utashi. Anaweza kuashiria upande wowote autakao kwa kidole; anaweza kugeuza uso wake upande wowote anaoutaka. Anaweza kutumia hisia zake zote alizonazo kadiri atakavyo. Anaweza kwenda popote anapotaka, kula chochote anachotaka na kuepuka chochote asichokipenda.
Utashi huo unakabiliwa na zawadi na mtihani, na hatimaye ni Peponi na Motoni.
Hivyo, Sharia ni mfululizo wa amri na makatazo yanayoamuru utashi wa binadamu kubakia ndani ya mipaka ya eneo analoliridhia Allah na yanayouonya utashi wa binadamu kujiepusha na eneo asiloliridhia Allah. Mja ameamrishwa ashikamane na kamba ya Allah.
Kuna maeneo mawili mbele ya utashi wa binadamu. Moja ni dunia, na jingine ni ahera. Hata hivyo, kuna sheria na kanuni zilizowekwa kwa ajili ya mambo yote ya kidunia. Kama mja atazitii, atazingatiwa kuwa ameabudu na ataendesha maisha yake ya kidunia kirahisi zaidi na kwa furaha.
Tunaona kuwa mijadala kuhusu Sharia kwa kawaida hufanyika katika kundi la pili. Kundi hilo la pili limegawanyika katika sehemu mbili: mahusiano ya kijamii na adhabu. Kitovu cha mijadala inayohusu Sharia ni sehemu ya mwisho. Kwa hakika kuna hukumu nyingi sana zilizowekwa na Uislamu kuhusiana na sheria ya adhabu. Hizo ni sehemu ya Sharia hiyo na ni muhimu kuziamini. Mtu asiyezitii atawajibika kama amri na hukumu zingine. Kutokutii amri hiyo kunamfanya mtu awe mwenye dhambi kama uasi huo una namna ya usugu na kumwasi Allah. Kama mtu huyo atakana na kukataa amri hiyo ya Allah, kuwa hukumu inayotokana na Quran na sheria, anakuwa kafiri. Hata hivyo, Uislamu si hukumu hizo pekee na dini haina amri hizo peke yake. Ili kushughulikia jambo hilo peke yake katika uwanja huo itakuwa tathmini potofu na ufahamu usio sahihi.
Hukumu za Kiislamu zimegawanyika katika makundi matatu makuu yafuatayo. La kwanza ni majukumu ya mtu kwa nafsi yake. La pili ni majukumu yake kwa familia yake. Na la tatu ni majukumu yake katika maisha ya kijamii. Kuna vigezo na hukumu ambazo Sharia imezileta kuhusu wao. Inazingatiwa kuwa ni ukafiri kuikataa yoyote ile na ni dhambi kutokuitii yoyote katika hizo. Hata hivyo, lenye kipaumbele ni majukumu ya mtu kwa nafsi yake. Na jukumu muhimu zaidi kuliko yote ni ibada. Kuna hukumu zinazohusu wajibu wa mtu kwa nafsi yake na familia yake katika vitabu vitukufu vyote. Ibada imeamrishwa kwao wote, na kuyaepuka madhambi kunazingatiwa kuwa ni lazima.
Kuna tofauti kadhaa katika umbo, muda na kiasi cha ibada lakini haiwezekani kuonesha dini isiyoamrisha ibada na maadili ya juu. Hata hivyo, kanuni za kijamii, hususani hukumu zinazohusu usimamizi wa dola zipo kikamilifu katika Uislamu, ambayo ni dini kamilifu na ya mwisho.
Tunapaswa kueleza hususani yafuatayo: Lengo la kuumbwa kwa mwanadamu lipo katika dini zote. Kusudio ni kueleza kama ifuatavyo katika aya iliyo katika Quran: “Sikuwaumba majini na wanadamu isipokuwa waniabudu”. Pia kuna baadhi ya amri na makatazo yanayozingatia utambuzi wa hali kadhaa. Mojawapo ni hukumu zinazohusu sheria ya adhabu. Hukumu hizo zinategemea mazingira. Waislamu wanaoishi Ujerumani, Uingereza, Ufaransa hawana uwezo wa kutumia amri hizo. Na hawawajibiki nazo.
Katika mijadala inayohusu jambo hilo, itakuwa ni uonevu kumwonesha muumini kama mtu asiyekubali baadhi ya amri za Uislamu na kumkosoa. Ni muhimu kuepuka tuhuma za namna hiyo zinazoharibu undugu wa Kiislamu na ambazo adhabu zake ni kali huko ahera.
Fikiria nchi ambayo watu wake ni masikini. Je, unaweza kuwatuhumu watu wa nchi hiyo kwa kutokutimiza wajibu wa zaka? Bila ya shaka hapana. Hali hiyo si sawa na ya Muislamu anayeamini sheria za adhabu ya Kiislamu lakini hawezi kuzitumia? Ni wajibu wa dola kuzitumia. Kwa hivyo, mtu mmoja hana jukumu lolote kuhusu jambo hilo.
Kanuni za msingi za Uislamu ni amri za Allah ambazo mtu anapaswa kutii bila ya kujali mahali alipo.
Hukumu zinazohusu usimamizi wa dola ni amri za Allah, pia; ni wajibu kwa kila muumini kuziamini lakini hana wajibu wa kuzitumia.
“Sharia inahusiana na maadili, ibada, ahera na inafaidisha 99%. Inahusiana na siasa 1%. Watawala wanapaswa waifikirie.” Badiüzzaman.
Ningependa kutaja vigawanyo vya hukumu za Kiislamu. Hukumu za Allah zimegawanyika katika sehemu mbili: baadhi yake ni hukumu zinazotumika kwa ajili ya Waislamu tu; zingine ni hukumu zinazotumika kwa kila mmoja anayeishi nchi ya Kiislamu. Sehemu ya pili ni hukumu na sheria zinazohusu mahusiano ya kijamii na adhabu. Kama asiye Mwislamu atalipa jizyah (kodi ya kichwa inayotozwa kutoka kwa ambao hawakusilimu, lakini wanataka kuishi chini ya himaya ya Uislamu), anakuwa chini ya hukumu zote zinazohusu mahusiano ya kijamii na adhabu kama raia wa nchi hiyo. Kama ataiba kitu, atakatwa mkono wake; kama atamkashifu mtu kuhusu uzinifu, ataadhibiwa. Baadhi ya watu wanatathmini jambo hilo kinyume na wanasema maneno yaliyovurugika yanayowafanya wawajibike kama vile, “haina maana kuswali na kufunga katika nchi ambayo sheria ya Kiislamu ya adhabu haitumiki”. Wanawatuhumu Waumini wanaowapinga kwa kutozingatia baadhi ya hukumu za Allah.
Kwa hakika, dai hilo linakuwa halali kwao. Wanafanya kosa kwa kupuuza hukumu zainazounda asilimia tisini na tisa ya Sharia na ambazo ni misingi ya dini na kwa kuzipa umuhimu zaidi hukumu na sheria za mahusiano kijamii na adhabu zinazotumika kwa kila mmoja, awe Muislamu au asiye Muislamu, na zinazohakikisha amani na furaha ya jamii.
Muumini anayesoma surat al-Fatiha katika kila rakaa ya swala na kumwomba Allah amwongoze kwenye “njia iliyonyooka” anapaswa awe makini. Kila namna ya msimamo mkali, iwe kwa kupuuza au kuzidisha, inamwondoa mtu kutoka katika njia iliyonyooka.
Je Sharia inafaa katika karne yetu?
Tutataja namna mbili za msimamo mkali kuhusu jambo hilo hapa. Huku baadhi ya watu wakidai kuwa haiwezekani kutawala kwa sheria za Uislamu katika karne hii, wengine wanamlaumu kila asiyetawala kwa sheria za Uislamu kwa ukafiri bila ya kuzingatia nia zao. Kundi moja linakichofanya ni kupuuza na jingine linachokifanya ni kuzidisha kiasi. Maana yake, yote mawili yana msimamo mkali; wamekengeuka kutoka katika njia iliyonyooka.
Tunataka tuanze kutaja kosa la kwanza. Kuna kanuni mashuhuri. “Kama jambo limeamuliwa, linakuwa limeamuliwa pamoja na namna ya kulifikia, vifaa na zana.” Tunapotaja mkono, vidole huukamilisha. Hutaweza kuufikiria mkono bila ya vidole. Hutaweza kunufaika kutokana na mkono bila ya vidole. Tunapotaja uso, hutaweza kutenganisha macho kutoka usoni. Uso bila ya macho ni kitu kisicho kamili. Huwezi kutenganisha weupe wa macho mbali na weusi wa macho, pia. Kidole ni sehemu inayokamilisha mkono; jicho ni ukamilisho wa sehemu ya uso na mboni ya jicho ni ukamilisho wa sehemu ya jicho. Sheria za Kiislamu ni kama hivyo pia. Lazima ziwe fikra kwa ukamilifu wake. Ni hapo ndipo inaweza kumboresha mtu mmoja na jamii na kuwaongoza kwenye amani na furaha.
Katika jamii ambapo misingi ya Uislamu inapuuzwa na maisha ya mtu mmoja mmoja na familia yanaegemea juu ya kanuni zilizo potovu, kutumia tu sheria zinazohusu maisha ya kijamii na adhabu hazitakuwa na manufaa yoyote. Pengine isiwezekane kutumia sheria hizo katika jamii ya aina hiyo. Hata kama itawezekana, watu wengi watazitii bila ya kuziamini na bila ya kutaka, kwa kuangukia katika unafiki. Mtu anaonekana kama Muislamu lakini anaishi kama adui wa Uislamu.
Ningependa kutoa mfano kuhusu ukweli kuwa Sharia lazima zitathminiwe kuwa ni kitu kamili. Katika Uislamu, riba ni haram, imekatazwa. Ni muhimu kuzingatia aya inayohusu riba pamoja na aya ifuatayo, “Waumini si vinginevyo bali ni ndugu”. Kisha, ukweli ufuatao utadhihirika: “Muumini anapomkopesha mali nduguye aliye katika haja muhimu na anayemwomba mkopo, hatataka arudishiwe na ziada. Hiyo haiendani na undugu.”
Katika jamii ambapo undugu wa Kiislamu umedhoofika, ambapo mtu anajaribu kumhadaa nduguye na ambapo mali ya dola inaporwa pasi na huruma, kama makatazo ya riba hayawezi kutumika, ni kosa la muundo potofu, si kosa la dawa au chakula.
Ama kuhusu dai la pili linalovuka mipaka ya unyoofu, si haki kumwita ni kafiri mtu asiyeutumia Uislamu kikamilifu na asiyetawala au hawezi kutawala kulingana na Uislamu. Imani ni kinyume cha ukafiri. Kama mtu anatoa hukumu kinyume na Uislamu au anatumia lililo kinyume na Uislamu, atakuwa ni kafiri kama tu atalifanya hilo kwa kuukataa Uislamu. Vinginevyo, dhambi yake au dhuluma inaweza kutajwa na si ukafiri wake. Kuna sharti la nia na utashi katika imani na ukafiri. Mtu anazingatiwa kuwa ni kafiri kama tu atasema, “hukumu za Kiislamu kuhusu jambo fulani ni kadhaa lakini halikubali na kulifanya”. Kama hana nia au utashi kama huo na kama hukumu yake potofu inakuja kutokana na ujinga wake au udhaifu wa utashi wake na kama anajua kuwa anachokifanya si sahihi, haiwezekani kumwita kafiri kwa mujibu wa hukumu ya Ahl Sunnah. Wakhawariji tu, ndio wanaoamuru kuwa mwenye kutenda madhambi makubwa anakuwa ni kafiri, na Mutazilah, wenye rai kuwa mtu wa aina hiyo yuko baina ya imani na ukafiri, wanaweza kudai hivyo. Wanazuoni wote wa Ahl Sunnah wanaafikiana kuwa Wakhawariji na Mutazilah wamekengeuka kutoka katika lililo sahihi.
Lazima tuwe makini sana. Tunaweza kukengeuka kutoka kwenye lililo sahihi na wakati huo huo tunadhania kuwa tunautetea Uislamu.
8
Ni zipi Sifa Bainifu za dini ya Uislamu?
Sifa kuu bainifu za Uislamu zenye kuubainisha na dini zingine ni kama ifuatavyo:
1- Uislamu unawahutubia watu wote na karne zote; kanuni zake zinatimiza mahitaji yote za kiutu.
Sifa hii ya Uislamu ya kuenea kote, nyakati zote na kwa wote imetajwa kama ifuatavyo katika Quran:
"Na hatukukutuma ila kwa watu wote, uwe mbashiri, na mwonyaji." (Saba', 28)
"Sema: Enyi watu! Hakika mimi ni Mtume kwenu nyinyi nyote, niliye tumwa na Mwenyezi." (al-A'raf, 158).
2- Uislamu ni dini ya wepesi na urahisi.
Katika Uislamu, watu hawatakiwi kufanya wasiyoyaweza au yale wanayotaabika kuyafanya.
Kanuni za wepesi na urahisi za Uislamu zimeelezwa kama ifuatavyo katika Quran:
"Mwenyezi Mungu haikalifishi nafsi yoyote ila kwa kadiri ya iwezavyo..." (al-Baqara, 286).
"Usitutwike tusiyo yaweza..." (al-Baqara, 286).
“Mwenyezi Mungu anakutakieni yaliyo mepesi wala hakutakieni yaliyo..." (al-Baqara, 185).
Wakati Quran inabainisha kuwa Uislamu ni dini ya wepesi na urahisi, Mtume anaeleza kanuni zifuatazo katika hadithi zake:
"Nimetumwa niwe rehema kwa viumbe wote. Sikutumwa kukuteseni wala kusababisha taabu..."
"Allah hakunituma kama mtu wa kusababisha taabu na shida au mtu wa kuwatakia hayo. Amenituma kuwa ni mwalimu na kurahisisha mambo..."
"Lililo bora katika dini yenu ni lililo jepesi zaidi. Bila ya shaka kuwa dini ni wepesi..."
"Jiepusheni na niliyoyakataza na fanyeni niliyokuamrisheni kadiri muwezavyo. Mataifa ya kabla yenu yaliangamizwa kwa sababu ya wingi wa matatizo yao na kuwapinga mitume wao."
"Fanyeni amali njema kadiri muwezavyo. Allah hatachoka kukulipeni mpaka mchoke kuabudu."
"Rahisheni mambo; msiyafanye magumu. Toeni habari njema; msiwaogopeshe watu."
Bi. Aisha alisimulia kitendo cha Mjumbe wa Allah (s.a.w) kuhusu hilo kama ifuatavyo:
"Pindi Mjumbe wa Allah (s.a.w) alipopewa hiari ya kuchagua kati ya mambo mawili, alichagua lililokuwa jepesi zaidi isipokuwa la dhambi. Kama jambo hilo lilikuwa dhambi, bila ya shaka aliliepuka zaidi kuliko watu wote."
Hadithis hapo juu inaonesha amri zilizo nyepesi kutekeleza zilizomo katika Uislamu. Wepesi huu ni nafasi kubwa katika kudhihirisha kuwa ni dini ya wote na itaendelea kuwepo mpaka Siku ya Kiama.
Baadhi ya mifano kutoka katika nyendo za Uislamu zinaonesha kuwa dini hiyo ni nyepesi:
Katika dini yetu, ni lazima kuchukua udhu kwa kutumia maji. Hata hivyo, yanapokosekana maji au kunapokuwa na hatari ya kuugua kwa sababu maji ni ya baridi sana, tayammum hufanywa kwa udongo. Udongo huchukua nafasi ya maji.
- Dini yetu huwapa manufaa wasafiri na kuwaruhusu kuswali swala za rak'ah 4 kuwa rak'ah 2 kutokana na baadhi ya sababu kama vile uchovu, kukosa muda, n.k.
- Ni faradhi kusimama wima wakati wa kuswali. Hata hivyo, wasioweza kusimama wanaweza kuswali wakiwa wamekaa kitako.
- Inaweza kuwa vigumu kwa wagonjwa na wasafiri kufunga kufunga katika mwezi wa Ramadhani. Kwa hivyo, dini yetu inaweka uhuru wa kufunga au kula. Si dhambi kama hawatafunga. Wanaweza kufunga watakapopona au kurejea kutoka safarini.
- Kama kuna hatari kama vile magonjwa ya mlipuko, vita, n.k, Waislamu wanaofanya hajj wanaweza kuahirisha hajj zao mpaka hatari iishe.
3- Hukumu zote za Uislamu ni za weledi. Hakuna chenye kutofautiana na mantiki katika Uislamu.
Mali muhimu zaidi ya mwanadamu inayomtofautisha na viumbe wengine ni akili. Mwanadamu hufikiria mambo mengine, hubainisha heri na shari na huchagua kati ya haki na batili akilini mwake.
Kwa hivyo, akili na watu wenye hekima wametajwa takribani katika aya 70 katika Quran. Ibara "Je hawasikii?", "Je hawaelewi?" yametumika mara nyingi.
Kuwa na akili timamu ni lazima ili kuweza kuwajibika katika dini yetu; kwa hivyo, wasio na akili timamu hawawajibishwi.
Watu wasiomwamini Mtume (s.a.w) walimwambia, "Tuoneshe baadhi ya miujiza ili tumwamini Allah na kukukubali wewe kuwa ni mtume", Allah hakuyapenda waliyoyasema na akawataka watizame adhi na mbingu na kuzitafakari ili waamini kuwepo Kwake badala ya kutaka kuona miujiza. Jambo hilo limeelezwa katika Quran kama ifuatavyo:
"Hakika katika kuumbwa kwa mbingu na ardhi, na kukhitalifiana usiku na mchana, na marikebu ambazo hupita baharini kwa viwafaavyo watu, na maji anayo yateremsha Mwenyezi Mungu kutoka mbinguni, na kwa hayo akaihuisha ardhi baada ya kufa kwake, na akaeneza humo kila aina ya wanyama; na katika mabadiliko ya pepo, na mawingu yanayo amrishwa kupita baina ya mbingu na ardhi, bila shaka zimo Ishara kwa watu wanao zingatia." (al-Baqara, 164)
Anas, mmojawapo kati ya Maswahaba mashuhuri, alimsifu mtu mbele ya Mjumbe wa Allah (s.a.w) huku akimtaja. Mjumbe wa Allah akamuuliza Anas:
- Akili yake iko vipi?
Anas akasema:
- Ewe Mjumbe wa Allah! Ibada yake, maadili na fadhila ni nzuri. Mjumbe wa Allah akauliza tena:
- Akili yake iko vipi? Anas akasema:
- Ewe Mjumbe wa Allah! Sisi tunataja ibadayake, ihsani isipokuwa wewe unauliza akili yake. Hapo, Mjumbe wa Allah alisema:
- Mfanya ibada mpumbavu anaeza kuhadaiwa na Shetani kirahisi na kutenda madhambi zaidi kuliko anayefanya dhambi kutokana na ujinga wake. Watu wanaweza kumkaribia Allah kwa mujibu wa akili zao.
Hadithi hiyo hapo juu, iliyosimuliwa katika "Adabu'd-Dunya wa'd-Din" cha Mawardi ni mfano mzuri sana na tukio lililokera linaonesha umuhimu wa akili katika Uislamu.
Baadhi ya hadithi zingine zinazohusu akili ni kama ifuatavyo:
"Mtu asiye na akili hana dini."
"Allah hampendi muumini asiyetafakari."
"Kama akili ya mtu si timamu, dini yake haitakuwa timamu..."
"Pepo ina daraja 100. Daraja 99 ni kwa ajili ya wenye akili timamu; daraja 1 ni kwa ajili ya wengine..."
"Ewe Ali! Watu wanapojikurubisha kwa Allah kwa amali mbalimbali njema, wewe jikurubishe kwa akili yako."
"Allah hakuumba kitu chochote chenye thamani kubwa na utukufu zaidi kuliko akili."
4- Uislamu ulikomesha na kuondoa tofauti za kimatabaka, dhuluma na upendeleo uliokuwepo katika kila enzi na kuweka kanuni zilizoondoa tofauti zilizozingatia asili.
Yafuatayo yameelezwa katika Quran:
“Enyi watu! Hakika Sisi tumekuumbeni kutokana na mwanamume na mwanamke." (al-Hujurat, 13).
Mtume amesema yafuatayo:
"Watu ni wana wa Adam. Allah alimuumba Adam kutokana na mavumbi ya ardhi." Hivyo, Uislamu unaeleza kuwa watu wote wanatokana na baba mmoja na mama mmoja na kwamba kwa kuangalia asili hakuna atakayedai kuwa mbora kuliko wengine.
5- Uislamu unawatazama watu kuwa wanalingana kama vile meno ya kitana katika mbele ya sheria. Uislamu hauzipi umuhimu tofauti za kimbari, rangi na lugha; unaeleza kuwa kinachomfanya mwanadamu kuwa na thamani na kumfanya mbora kwa watu wengine ni uchamungu moyoni mwake na kiwango cha imani yake. Mtume anaeleza yafuatayo kuhusu jambo hilo:
"Enyi watu! Msisahau kuwa Mola wenu Mlezi ni mmoja (huyo huyo) na kuwa baba yenu ni mmoja. Mwarabu si mbora kwa asiye Mwarabu, asiye Mwarabu si mbora kwa Mwarabu, mweupe si mbora kwa mweusi na mweusi si mbora kwa mweupe kwa chochote isipokuwa taqwa (kumhofu Allah)."
Hivyo, dini yetu inamtazama kila mtu kwa usawa mbele ya sheria; haiupi umuhimu ubora wa kidunia na vyeo vya muda mfupi; inazingatia moyo wa mwanadamu badala ya mwonekano wake.
Uyahudi huzipa umuhimu starehe za kimwili na kunufaika kwa njia ya mali. Unawahamasisha wafuasi wake wazipe umuhimu tamaa za kidunia. Dini ya Ukristo na Uhindu huyapa umuhimu Maendeleo ya roho, kwa kudhoofisha Matakwa ya roho kwa kutia maumivu juu ya Mwili na kupuuzia maisha ya kidunia. Hata hivyo, Uislamu umeweka usawa kati ya the roho na Mwili, dunia na ahera. Unayapa usawa yote mawili; unalenga katika kutimiza mahitaji ya yote mawili kilakimoja kivyake.
Aya ifuatayo ya Quran inaeleza uwiano kati ya dunia na ahera katika Uislamu kwa namna bora kabisa: “Mola wetu Mlezi, tupe mema duniani na Akhera."
Islam hauipi umuhimu dunia kwa kuleta hasara ya ahera au (kuipa umuhimu) ahera kwa hasara ya dunia.
Uislamu unaeleza kuwa ahera itapatikana humu duniani na kuwataka watu waitumikie dunia kama vile hawatakufa na kuitumikia ahera kama vile watakufa kesho.
6- Hakuna tabaka la wahudumu wa kidini katika Uislamu. Kila mtu anapaswa ajifundishe dini yake kadiri anavyoweza. Katika Uislamu, hakuna tabaka la watu maalumu wenye kupendelewa linalofanya kazi kama kiunganishi kati ya mja na Muumba kwa ajili ya ibada na kuwafanya watu watubu madhambi yao.
7- Uislamu ni dini ya maadili na fadhila na inalinda sayansi, elimu na ukweli kikamilifu.
9
Je inaweza kuthibitishwa kupitia ushahidi wa Quran kuwa Uisilamu sio dini ya ugaidi bali ni kinyume chake inakataza gaidi, vurugu na fitina?
Quran imekemea vikali ugaidi na kuzielezea vurugu na fitina kuwa ni mambo maovu mno.
Uisilamu umekataza aina zote za ugaidi, dhuluma, na usaliti na kupinga aina zote za vurugu na tabia mbaya. Uisilamu haujibu uovu kwa uovu. Dini ya Uisilamu imeletwa na Allah Mtukufu ili kusimamisha haki, kuvunja udikteta na dhuluma za kiholela za uovu wa kikatili na kuifanya dhamiri ya mtu kuchemka. Hivyo, Uisilamu uko makini mno kuhusu hilo. Quran unayazingatia mauaji ya mtu asiye na hatia kuwa ni mauaji mabaya kabisa yaliyofanywa dhidi ya watu wote.
Allah Mtukufu anatangaza “… aliye muuwa mtu bila ya yeye kuuwa, au kufanya uchafuzi katika nchi, basi ni kama amewauwa watu wote. Na mwenye kumuokoa mtu na mauti ni kama amewaokoa watu wote… (al-Maidah, 32) Quran pia inalaani aina zote za fitina. Quran inatutanabahisha juu ya vichochezi na kueneza fitina ya wale wanaoanzisha mfarakano, wanaosababisha uhasama katika maisha ya jamii, na kueneza uhasama akiwa katika madaraka, na pia inaonesha bayana kitisho cha kueneza ufisadi, na uzito wa uhasama: “Na anapo tawala hufanya juhudi katika nchi kwa kufisidi humo na kuteketeza mimea na viumbe. Na Mwenyezi Mungu hapendi ufisadi.” (al-Baqarah, 205)
Quran imekataza fitina, katika sura al-Baqarah, 217, Allah Mtukufu anatangaza: “Na fitina ni mbaya zaidi kuliko kuuwa.” (Al-Baqarah, 217)
Ndani ya nafsi ya Mwisilamu, anayezitumia aya hizi za Quran kwa kiwango kikubwa, mnakuwa hamna uadui, chuki na ukatili. Umo undugu fulani hata kati ya adui yake mkubwa. Mwisilamu anaukubali ukweli, ambao, “tunamvumilia kiumbe kwa sababu tu ya Muumbaji.” Mwisilamu ni mtetezi wa upendo. Hana muda wa uhasama. Katika Quran Tukufu, Allah Mtukufu amewazindua waumini wajiepushe na madhara ya sehemu za ibada, kwa kuashiria kuwa sehemu za ibada zimehifadhiwa dhidi ya watu fulani kutokana na uingiliaji kati wa watu wengine: “… Na lau kuwa Mwenyezi Mungu hawakingi watu kwa watu, basi hapana shaka zingeli vunjwa nyumba za wat’awa, na makanisa, na masinagogi, na misikiti, ambamo ndani yake jina la Mwenyezi Mungu linatajwa kwa wingi.” (al-Hajj, 40)
Mtume Muhammad ni mtume wa huruma na upendo. Katika Quran Tukufu, Allah Mtukufu anaeleza: “Nasi hatukukutuma ila uwe ni Rehema kwa walimwengu wote.” (al-Anbiya, 107) Mtume (S.A.W.) ameonesha maadili yote mema kwa namna bora zaidi katika maisha yake na kuinasihi jumuia yake kujiepusha na fitina. Aliwaamuru kujiweka mbali na fitina kwa uzito usio na kifani na kwa umakini:
Jihadharini na fitina! Kwa kuwa, wakati ule ule, ulimi ni kama pigo la upanga. (Ibn Majah, Fitan, 24)
“Hapa pana uhakika kuwa kutatokea fitina, mfarakano na mgogoro. Itakapotokea hali hii, nenda Uhud na upanga wako. Upige jiwe kubwa mpaka livunjike vipande vipande. Kisha bakia nyumbani kwako. (Usitoke nje) hadi utakapokufikia mkono wa dhambi au kifo kikufikie nyumbani kwako.” (Ibn Majah, Fitan, 24) Ni kabla ya Siku ya Kiama, kutakuwa na fitina kama vipande vya usiku wa giza. Wakati wa fitina hiyo, mtu ataamka asubuhi hali ya kuwa ni muumini, lakini ataishia kuwa kafiri ifikapo usiku; ikifika usiku atakuwa muumini lakini ikifika asubuhi atakuwa kafiri. Wakati wa fitina hiyo, mwenye kukaa atakuwa bora zaidi ya mwenye kusimama wima. Hivyo vunjeni pinde zenu, vurugeni mishale yenu na mapanga yenu yapigeni kwenye mawe. Kama itaingia ndani ya nyumba ya mmoja wenu, uwe yule mbora zaidi kati ya wana wawili wa Adam (kuwa utakayeuliwa sio muuaji). (Abu Dawud, Fitan 2, Tirmidhi, Fitan 33)
10
Je, njia fanisi zaidi ya kueneza Uislamu ni vita au tabligh (kulingania)?
Ni muhimu kujibu maswali "Mtume ni nani?", "Wajibu wake ni upi?" Ili kuweza kutathmini dhana ya jihad kwa usahihi. Huku akiwafanya watu wote waende katika ulimwengu wa ahera, Allah Mtukuka aliwatuma mitume ili wawaongoze watu katika safari yao ya kuwapeleka Peponi au Motoni. Wajibu mkuu wa wajumbe hao wa Allah ni kuwafanya watu wamjue Allah, kuwafundisha ibada, halali na haramu, na kuwafundisha namna ya kumshukuru Allah kwa neema Zake zisizo na ukomo.
Mtume Muhammad (s.a.w), ambaye ni Mtume wa zama za mwisho, alitimiza wajibu huu kikamilifu; aliwajulisha watu kuhusu Allah huko Makkah, aliwafundisha amri Zake na makatazo na aliwaambia kuwa kuabudu masanamu ni kumshirikisha Allah. Alivumilia namna zote za mateso na ukatili wa watu waliopinga ujumbe wake kwa miaka kumi na mitatu na kisha alihamia Madinah kwa kufuata amri na idhini ya Allah; aliendelea na wajibu wake huko. Washirikina waliotaka kumzuia asitekeleze wajibu huu wa juu kabisa waliendelea kumsumbua huko Madinah pia lakini hawakuweza kuuzuia Uislamu kufuatwa na watu wa huko.
Kitu muhimu sana cha Mtume (s.a.w) wa zama za mwisho kilichotajwa katika vitabu vyote vya mbinguni ni kwamba yeye ni “sahib-us sayf” (mmiliki wa upanga); yaani, pamoja na uongofu wa kiroho, anaruhisiwa kupigana (anapozuiwa kufikisha ujumbe wake). Baadhi ya mitume waliotangulia, kama vile Nabii Dawud na Nabii Suleiman, waliendesha jihad zao kwa mapanga pindi ilipolazimu.
Historia inapochunguzwa bila upendeleo, itaonekana kuwa jambo kubwa lililofanya Uislamu uvutie nyoyo na ari halikuwa vita bali kufikisha ujumbe, yaani, kuwaambia watu kuhusu uhalisia wa Uislamu na kuwaonesha mazuri ya Uislamu. Wanahistoria wanakubali kuwa makundi mawili ya watu yalikuwa na mchango mkubwa zaidi katika kuenea kwa Uislamu. La kwanza ni wanazuoni na walimu waliojitolea maisha yao kwa kufundisha Uislamu na wakahamia nchi za mbali sana ili kufanya hivyo. Kundi la pili ni wafanyabiashara waliokwenda katika baadhi ya nchi ili kufanya biashara na wakawaonesha watu wa huko mazuri ya Uislamu.
Aya zifuatazo zinaonesha waziwazi kuwa Uislamu umeenea kwa njia ya kufikisha ujumbe na wito wala si kwa njia ya upanga:
“Hapana kulazimisha katika Dini. Kwani Uwongofu umekwisha pambanuka na upotofu.” (surat al-Baqara, 256)
“Basi kumbusha! Hakika wewe ni Mkumbushaji. Wewe si mwenye kuwatawalia.” (al-Ghashiya, 21-22)
Kuna shuhuda nyingi zinazoonesha kuwa Uislamu umeenea kwa njia ya kufikisha ujumbe wake. Tutataja baadhi yake: Mtume (s.a.w) alipoanza kufikisha ujumbe wa Uislamu katika mji wa Makkah, hakuwa na mali au nguvu. Ingawa washirikina wote wa hapo walimfanyia uadui, alizishinda nyoyo za watu kwa kufikisha ujumbe na ushawishi. Watu wengi, kuanzia Abubakr mpaka Umar, walisilimu kama hivyo na wakamtamkia kila mmoja kuwa Uislamu ulikuwa ni nguvu isiyoshindika. Kama Maswahaba wangetaka, wangewaua washirikina wote wa Quraysh, wa kwanza Abu Jahl, kwa ghafla moja. Hata hivyo, hawakufanya hayo. Waliendelea kufikisha ujumbe wa Uislamu kwa kustahamili mateso na taabu za aina zote; hawakutumia kitisho na vurugu.
Waislamu waliohamia Madinah kabla ya Mtume waliwaingiza watu wengi katika Uislamu huko kwa kufikisha ujumbe wa Uislamu na kuwalingania Uislamu. Hivyo, misingi ya Uislamu iliwekwa kwa njia ya kufikisha ujumbe kote Makkah na Madinah.
Katika miaka iliyofuata, Uislamu uliimarika Madinah. Washirikina wa Makka waliwakubali Waisilamu kuwa wana nguvu na wakasaini nao mkataba huko Hudaybiya. Kipindi cha mkataba kilikuwa ni miaka kumi lakini kilidumu kwa miaka miwili na kikavunjwa na washirikina wa Makka. Hata hivyo, idadi ya watu waliosilimu katika kipindi cha miaka hiyo miwili ilikuwa ni zaidi ya idadi ya watu walioufuata Uislamu katika kipindi cha miaka ishirini tangu Uislamu ulipoibuka.
Katika karne zilizofuatia, Wa-Mogul waliumaliza ukhalifa wa ukoo wa Abbas; wakachoma na kuharibu rasilimali za Kiislamu. Hata hivyo, baada ya muda, walianza kusilimu kwa hiari yao wenyewe. Ni ukweli wa kihistoria kuwa panga halikuwa na lolote katika kusilimu kwa Wa-Mogul.
Kuenea kwa Uislamu katika maeneo ya Indonesia, Malaysia na Africa kulifanyika kwa njia ya ufikishaji ujumbe na si kwa njia ya upanga.
Baada ya kuiangalia historia hiyo kwa kifupi, hebu tuangalie hali ya leo: Waislamu wamepoteza uwezo wao wa kimali katika karne iliyopita lakini Uislamu umeendelea kuenea na kuendelea kiroho. Watu wengi waliosilimu katika nchi za Ulaya kwa kuanzia na Ujerumani na Uingereza, na katika Amerika ni wanasayansi; wengi wao wamesilimu baada ya kuuchunguza tu, bila ya hata kufikishiwa ujumbe wa Uislamu.
11
Ni thamani zipi za msingi ambazo dini ya Uislamu inaamuru zihifadhiwe?
Kuna haki nyingi ambazo Uislamu unawapa watu. Tunaweza kuorodhesha thamani nyingi zinazozingatiwa kuwa ni haki za msingi kama ifuatavyo: Uhai, dini, akili, mali na kizazi.
1- Haki ya Kuishi:
Dini ya Uislamu unamzingatia mtu kuwa ni kiumbe bora zaidi na unachukulia kuwa kulinda haki za kibinadamu ni katika kanuni za msingi. Imeelezwa katika Quran kuwa kumuua mtu bila ya haki ni kosa kubwa sana kama kuwaua watu wote na kuwa kuhifadhi uhai wa mtu ni kitendo cha thamani ya juu sana kama vile kuwahifadhi watu wote.
Mtume (s.a.w) aliwahutubia Waislamu wote kama ifuatavyo katika Hajj ya Kuaga: "Kama mnavyouchukulia mwezi huu, siku hii, mji huu kuwa ni Tukufu, basi chukulieni kuwa uhai na mali ya kila Muislamu kuwa ni dhamana tukufu " (Bukhari, "Ilm", 37, "Hajj", 132, Muslim, "Hajj, 147), kwa kueleza kuwa haki ya kuishi ya kibinadamu si yenye kuguswa. Katika hadithi nyingine, yameelezwa yafuatayo: "Epukeni mambo saba yenye kuangamiza. Mojawapo ni kumuua mtu, ambako kumeharamishwa na Allah isipokuwa kwasababu za haki." (Bukhari, "Wasaya", 23; "Tib", 48; "Hudud", 44; Muslim, "Iman", 144; Abu Dawud, "Wasaya", 10).
Kuwaua watu kama vile wanawake, watoto, wazee na viongozi wa dini kumeharamishwa hata katika wakati wa vita. Kumuua mtu na hata kujiua kumeharamishwa na kunazingatiwa kuwa ni katika madhambi makubwa.
2- Haki ya dini:
Kila mtu ana uhuru wa kuchagua dini. “Hapana kulazimisha katika dini.” (al-Baqara, 2/256), “Nyinyi mna dini yenu, nami nina Dini yangu...” (al-Kafirun, 109/6). Jambo hili limesisitizwa katika aya hizo hapo juu. Wasio Waislamu wanaoishi katika mamlaka ya dola ya Kiislamu wamepewa haki ya kutekeleza dini zao wenyewe.
3- Akili:
Akili ndio sifa bora zaidi ya mwanadamu kwa sababu dhamana za Allah ni shukurani zinazokubaliwa na akili na mwanadamu anaweza kupata radhi na kuridhika kwa Allah, hilo ni la kushukuru. Chanzo na mzizi wa elimu ni akili. Uhusiano kati ya elimu na akili ni kama uhusiano kati ya tunda na mti, mwangaza na jua, kuona na jicho. Akili ndiyo inayombainisha mwanadamu na viumbe wengine hai na wasio hai ulimwenguni na kumfanya awe bora zaidi.
Maonyo katika Quran yaliyosababisha watu kufikiri kama vile “Fikiri!”, “Je hamfikiri?”, “Je, hawafikiri”, “Angalia!”, “Je, hawaoni?”, “Pateni onyo, Enyi wenye macho!” inaonesha umuhimu unaopewa akili.
Badiuzzaman Said Nursi anaeleza akili kuwa ni muhtasari wa hali ya dhamiri iliyochujwa kutokana na hisia, kitu cha thamani kubwa kwa mwanadamu, hali ya nuru, ufunguo wa kufungulia hazina za ulimwengu, kifaa kinachoangalia majina na sifa za Allah yanayojidhihirisha duniani, mtafiti anayetafutia ufumbuzi mafumbo ulimwenguni, mwongozo wa kiungu unaomwandaa mtu kupata furaha ya maisha ya milele, zawadi ya thamani kubwa inayotenda kazi juu ya ushahidi na kumwonesha mtu malengo makubwa na ya matunda ya kudumu, na kitu cha msingi kilichoachanishwa na mada na kinahusiana na mada katika utendaji wake.
Dini ya Uislamu imeharamisha ulevi, unaolewesha watu, ili kuuhifadhi msingi huo muhimu na umeweka adhabu juu ya wenye kukiuka uharamishwaji huo. Katika sheria ya Kiislamu, vitu vyote vyenye kumduwaza mtu na kumwondolea uwezo wake wa kufikiri na kuwa na mantiki huzingatiwa kuwa ni haramu pamoja na vinywaji vyenye kulewesha.
4- Mali:
Dini ya Uislamu inahakikisha haki ya kupata mali. Uislamu unamtaka mtu aishi maisha yenye kufaa heshima ya binadaamu. Uislamu haupingani na mali. Uislamu hautaki mali kuwa ni nguvu inayomilikiwa na sehemu ya jamii; unataka mali ienee baina ya watu.
Dini yetu inazingatia kuua kuwa ni katika madhambi makubwa; halikadhalika unauzingatia wizi na unyang’anyi kuwa ni dhambi kubwa na unaweka adhabu kali sana kama vile kukatwa mkono wa mwizi katika kesi ya wizi.
5- Kizazi:
Desturi ya ndoa ni lazima kwa ajili ya kudumisha na kuendeleza kizazi cha binadamu. Kudumu na kustawi kwa kizazi cha biadamu kunawezekana tu kupitia kuanzishwa kwa familia, ambayo inaunda jamii ambayo ni muhimu sana katika jamii. Desturi ya ndoa imeegemea juu ya mkataba wa ndoa unaounda msingi wa jumuiya ya Kiislamu.
Katika kulipa umuhimu jambo la kuiimarisha jamii ya Kiislamu, dini ya Uislamu imetumia na imehimiza kuwa na watoto na kuongeza idadi ya watu. Kwa hakika, Mtume Mtukufu (s.a.w) amesema, "Oeni wanawake wapenzi na wenye kuzaa kwa sababu nitajifaharisha kwa wingi wenu katika hadhara ya ummah zingine katika Siku ya Kiama." (Ahmad b. Hanbal, I, 412).
Nabii Zakariyya (s.a.w) alimwomba Allah dua ifuatayo ili kuendeleza kizazi chake: "Na hakika mimi nawakhofia jamaa zangu baada yangu: na mke wangu ni tasa. Basi nipe mrithi kutoka kwako. Atakaye nirithi mimi na aurithi ukoo wa Yaaqub. Ewe Mola wangu Mlezi! Na umjaalie awe mwenye kuridhisha! " (Maryam 19/5-6)
Katika Uislamu, kuwa na watoto na kuendeleza kizazi huzingatiwa kuwa ni ibada. Kutokana na umuhimu wake, kumdhuru mtoto katika mji wa mimba, kuharibu mimba na kutoa mimba huzingatiwa kuwa ni kuua. Kumeharamishwa kuua kijusi ambacho viungo vyake vimeshadhihirika. Mjumbe wa Allah (s.a.w) alipopokea ahadi ya utii kutoka kwa wanawake, aliamuru “kutowaua watoto wao kwa njia yoyote” kama ni sharti. Sharti hili ni muhimu sana. Mtoto yuko chini ya udhibiti wa mama yake kabla hajazaliwa. Hata hivyo, baada ya kuzaliwa, baba, sio mama, ndiye anayewajibika. Kisha, sharti la “kutowaua watoto wao kwa njia yoyote” linahusiana na kijusi katika mji wa mimba.
"Ewe Nabii! Watakapo kujia wanawake Waumini wanakuahidi ya kwamba hawatamshirikisha Mwenyezi Mungu na chochote, wala hawataiba, wala hawatazini, wala hawatawauwa watoto wao, wala hawataleta uzushi wanao uzua tu wenyewe baina ya mikono yao na miguu yao, wala hawatakuasi katika jambo jema, basi peana nao ahadi, na uwatakie maghfira kwa Mwenyezi Mungu..." (al-Mumtahina, 60/12).
12
Nini unafikiria kuhusu msiba wa tarehe 11 Septemba na jaribio la tukio hilo la kuyahusisha mashambulizi mengine ya kigaidi duniani na dini ya Uisilamu?
Mwisilamu hawezi kuwa gaidi; gaidi hawezi kuwa Mwisilamu wa kweli
Uisilamu ni dini ya uvumilivu; Uisilamu unazingatia kuwa kiumbe ni chenye thamani mno; unazingatia uvunjaji wa sheria na mashambulizi dhidi ya watu wasio na hatia ni madhambi makubwa. Kwa hakika, aya ya Quran tuliyoitaja inatangaza kwa kupaza sauti:
‘Aliye muuwa mtu bila ya yeye kuuwa, au kufanya uchafuzi katika nchi, basi ni kama amewauwa watu wote. Na mwenye kumuokoa mtu na mauti ni kama amewaokoa watu wote. Na hakika waliwajia Mitume wetu na hoja zilizo wazi. Kisha wengi katika wao baada ya haya wakawa waharibifu katika nchi.’ (5: 32).
Kwa kweli, Mwisilamu huhudumia maisha tu na sio kifo. Kwa hivyo, lazima tusisahau kanuni mbili kuu za sheria zilizowekwa na Uisilamu:
Ya kwanza: Aya ya Quran: ‘Na habebi mwenye kubeba mzigo wa mwenziwe’ (6: 164). Yaani, mtu mwengine hawezi kuadhibiwa kwa sababu ya mtenda mauaji. Katika sheria, uhalifu na adhabu ni vitu binafsi.
Ya pili: mtu huzingatiwa kuwa hana hatia hadi itakapothibitishwa kuwa ni mkosa. Yaani, hakuna anayeweza kushitakiwa isipokuwa tu ithibitike kuwa ni mwenye hatia. Haizingatiwi kuwa ni haki kumwadhibu mtu bila ya ushahidi. Mtu anazingatiwa hana hatia isipokuwa ithibitishwe kuwa ni mkosa. Yafuatayo yanaripotiwa kutoka kwa Bwana Mtume: ‘Muumini anaweza kujilinda yeye mwenyewe katika muktadha wa dini isipokuwa akiua mtu asiye na hatia kinyume na sheria.’
Kilugha, Uisilamu unamaanisha amani. Hili linaonesha kuwa amani ya kweli ya kiwiliwili na akili inawezekana tu kupitia kumtii Allah na kujisalimisha Kwake. Mwisilamu anakuwa Mwisilamu kamili ikiwa tu anaishi katika amani na maelewano katika jumuia. Maisha ya kumtii Allah na kumwabudu Yeye yataupelekea moyo kukinai na amani ya kweli itafikiwa katika jumuia. ( 13:28-29).
Mitume wote wa Allah waliwafikishia watu ukweli walipowalingania kuja kwenye njia sahihi. Ni muhimu hapa kukumbuka hadithi ya Mtume ifuatayo: ‘ vipo vitu vitatu ambavyo ndio vipengele vya msingi kuhusiana na imani: kuwasaidia watu hata kama mtu ana hali ngumu ya kiuchumi; kuomba amani kwa watu kwa shauku; kuwatendea watu haki kama yeye mwenyewe anavyotaka atendewe kwa haki.
Bwana Mtume pia amesema:
Watu ni kama kundi la mifugo; kila mmoja wa kundi hili anapaswa awe kama mlinzi na mchungaji wa wengine na anapaswa abebe jukumu la kundi zima la mifugo.’
‘Ishini pamoja, shikamaneni, msizozane; rahisishianeni; msitiliane uzito na msifanyiane ugumu.’
‘Mtu anayelala usiku tumbo lake likiwa limeshiba ilhali majirani zake wana njaa basi huyo sio muumini wa kweli.’
‘Mwisilamu ni mtu anayemwabudu Allah na hayadhuru maisha ma mali za wengine.’
Kwa kifupi, Uisilamu haubezi mtu mmojammoja au jumuia. Kwa hakika, una lengo la kuleta maelewano na uwiano kati yao. Ujumbe wa Uisilamu ni kwa watu wote. Kwa mujibu wa Uisilamu, Allah ndiye Mlezi na Muidhinishaji wa Dunia. (1:1). Bwana Mtume ni mjumbe aliyetumwa kwa watu wote. ‘Sema: Enyi watu! Hakika mimi ni Mtume kwenu nyinyi nyote, niliye tumwa na Mwenyezi Mungu’ (7:158). ‘Nasi hatukukutuma ila uwe ni Rehema kwa walimwengu wote.” (21: 107).
Katika Uisilamu, watu wote huzingatiwa kuwa ni sawa bila ya kujali rangi zao, lugha, mbari au nchi. Hatuwezi kukataa, katika zama zilizoitwa zama za mapambazuko leo, kuwa bado vipo vikwazo, ubaguzi na kutendewa tofauti kati ya watu kutokana na sababu tulizozitaja. Uisilamu umetokomeza ubaguzi wa namna zote na upendeleo, na kutangaza duniani kuwa kila mmoja ni sawa kutokana na ukweli kuwa wote ni viumbe wa Allah. Uisilamu una mashiko ya kikweli ya kimataifa; unakataa upendeleo unaogemea rangi, koo, mbari, damu na eneo. Tunakemea aina zote za mashambulizi dhidi ya wanadamu. Tunasikitika kutokana na aina zote za uvunjwaji wa sheria unaowalenga watu wasio na hatia. Uisilamu unakataza mauaji ya kutisha ya watu wengi ambapo watu wasio na hatia huuliwa pamoja na madhalimu. Kwa mujibu wa Uisilamu, hakuna atakaebebeshwa jukumu kutokana na makosa ya wengine.
Uisilamu hauruhusu kuuliwa watu wasio na hatia na wasio na hifadhi. Kama mauaji hayo ya watu wengi yamefanywa na baadhi ya Waisilamu mmoja mmoja kuwa ndio dai la kibaguzi la vyombo vya habari, tutawatangaza madhalimu wote kuwa ni wahalifu na watenda dhambi kwa niaba ya Uisilamu. Tunataka kutilia mkazo kuwa ni muhimu mno kuwaadhibu madhalimu kwa adhabu kali bila ya kumbagua yeyote kwa upande wa kidini, mbari na jinsia.
Tunapokabiliana na matukio hayo, lazima tusisahau kuhusu ukweli kuwa dola mbalimbali na mtu mmoja mmoja: Kama ukiwa ndani ya meli au nyumba na mkiwa na watu tisa wasiokuwa na hatia na mmoja ni muuaji yuko nanyi, mtajua tu ni namna gani mtu huyo anayetaka kuizamisha meli au kuiteketeza nyumba kwa moto alivyo katili. Utapiga mayowe ili kumfanya kila mtu asikie ukatili wake. Hata kama mtu asiye na hatia ni mmoja tu na tisa waliobaki ni wauaji, tena itakuwa ni kinyume na haki kuizamisha meli hiyo au kuiteketeza nyumba hiyo kwa moto. Ni hivyo hivyo kwa matukio ya aina hii, pia. Tunakemea matendo haya ya damu na yasiyo na huruma na tunataka kumkumbusha kila mtu kuwa ni hatari mno kufanya matendo hayo hayo.
13
Je, Uislamu dini ya vita?
Vita havipendezi lakini utu haukuweza kuondoa vita katika historia nzima. Katika Quran, mapambano ya watoto wawili wa Adam yametajwa. Mmoja hakuwa na hatia na mwingine ni mgomvi. Yule mgomvi akamuua yule ambaye hakuwa na hatia. (Angalia sura al-Maida, 27-31). Jina la yule ambaye hakuwa na hatia ni Habil; na jina la mgomvi ni Qabil.
Qabil alipomuua ndugu yake, damu ya binadamu ilimwagwa kwa mara ya kwanza duniani. Hata hivyo, damu hii ilizidi kadiri wakati ulivyosogea na ikaenea duniani kote. Habil na Qabil ni wawakilishi wa watu wasio na hatia na wagomvi. Madam watu kama Qabil wapo duniani, watu kama Habil watakuwa na haki ya kujilinda.
Hivyo, Uislamu unaruhusu vita kwa kuzingatia masharti kadhaa ili kuzuia udhalimu wa wakandamizaji na kuhakikisha kuwa amani inaenea kote. Mathalani, tuangalie aya ifuatayo:
“Wameruhusiwa kupigana wale wanao pigwa vita kwa sababu wamedhulumiwa - na kwa yakini Mwenyezi Mungu ni Muweza wa kuwasaidia.” (al-Hajj, 39)
Aya hii inamwambia Mtume na Maswahaba wake ambao ndio walio katika daraja la kwanza katika Uislamu. Walifanyiwa dhuluma na mateso yaliyosababisha kifo kwa baadhi yao katika mji wa Makkah. Baadhi yao walikwenda Abyssinia kwa kufuata ushauri wa Mtume. Baadaye wengine walihamia Madinah. Takriban kila mara walisikia habari kama zifuatazo: “Watu wa Makka wanashambulia; Watu wa Makka wameshambuliwa.” Waislamu waliruhusiwa kupigana walipokuwa katika hali hizo.
Yafuatayo yameelezwa katika aya nyingine zinazohusu vita:
“Na piganeni katika Njia ya Mwenyezi Mungu na wale wanao kupigeni, wala msianze uadui. Kwani Mwenyezi Mungu hawapendi waanzao uadui.” (al-Baqara, 190)
Masuala yafuatayo yametajwa katika aya hiyo:
1- “Piganeni na wale wanaokupigeni.” Yaani, msipigane na wale wasiokupigeni. Kwa hakika, Mtume aliwaamuru makamanda wake wasiwaue watoto, wanawake, wazee na waliojitenga kwa kukaa katika mahekalu.
2- Vita lazima viwe “fi sabilillah”, yaani “katika njia ya Allah.’ Huenda wengine wakapigana ili kuvamia nchi mpya na kupata rasilimali za malighafi, n.k. Hata hivyo, Muislamu anaweza kupigana kwa ajili ya njia ya Allah tu. Yaani, anapambana ili kuzuia ukatili, uovu na vurugu duniani.
3- Hairuhusiwi kuvuka mipaka wakati wa vita au baadaye. Uislamu unawaamuru Waislamu kuua kwa namna nzuri wanapolazimika kufanya hivyo. Mathalani, Uislamu unakataza kuua kwa kutesa na kukata masikio, pua, n.k.
Yafuatayo yameelezwa katika aya nyingine:
“Na mna nini msipigane katika Njia ya Mwenyezi Mungu na ya wale wanao onewa, wanaume na wanawake na watoto, ambao husema: Mola Mlezi wetu! Tutoe katika mji huu ambao watu wake ni madhaalimu, na tujaalie tuwe na mlinzi anaye toka kwako, na tujaalie tuwe na wa kutunusuru anaye toka kwako’’ (an-Nisa,75)
Katika aya hii, Waislamu wanashauriwa kupigana kama wanakandamizwa katika mji au kama wanazuiwa kutekeleza imani yao. Mwishoni mwa vita, Waislamu wanakuwa huru dhidi ya uonevu na wanapata uhuru wa dini na dhamiri; watu wa nchi hiyo wanakuwa huru kusilimu ama laa.
Tunaweza kusema yafuatayo katika kuhitimisha:
Kilicho muhimu katika Uislamu ni amani si vita. Hata hivyo, watu wanapokandamizwa au dola inaposhambulia dola nyingine, vita vitakuwepo. Uislamu unaruhusu vita katika hali hizo. Uislamu haukuanzisha vita katika wakati ambao havikuwepo duniani. Wanaouzingatia Uislamu kuwa ni dini ya vita waangalie historia yao wenyewe, wataona kuwa kulikuwa na vita takribani katika kila kipindi cha historia yao. Kwa hiyo, kuwepo kwa hukumu za vita katika Uislamu si upungufu kwa Uislamu bali ni ukamilifu. Katika hukumu zilizotajwa katika aya na hadithi, uhalisia kama vita ambavyo haviepukiki ulibadilishwa na kuwa ustaarabu na utu kutoka ubedui na unyama.
14
Je, Uislamu ni dini ya kimantiki?
Hukumu na kanuni za dini ya Uislamu zinafaa kwa umbo la mwanadamu na mantiki yake. Tathmini hii ni sahihi. Isipokuwa kwa sehemu ndogo ya kanuni ambazo ni “ta'abbudi” (zinahitaji utii bila ya kuhitaji kujua mantiki yake), kanuni zote katika Uislamu ni "ma'qul al-mana" (zinafahamika kiakili na kimantiki).
Ukweli kuwa amri na makatazo ya Uislamu yanawafaa watu waliobaleghe na wenye akili timamu na hawawajibishwi watu wasio na akili timamu unaonesha kuwa Uislamu huipa umuhimu akili na kuiambia akili na pia inaonesha kuwa Uislamu ni “dini ya mantiki”.
Kwa mfano, desturi ya zaka katika Uislamu ni mpango uliowekwa kwa matajiri kuwasaidia masikini na kuweka usawa wa kijamii, kuzuia migogoro baina ya masikini na matajiri na kuigeuza migogoro hiyo kuwa suluhu, mapenzi-heshima na huondoa dhuluma inayochochea chuki baina ya matabaka katika jamii. Kazi hii ya zaka inaweza kufahamika kirahisi na pia ni ya kiakili sana.
Kwa kuongezea, sharti la kwanza katika kusilimu ni kumwamini Allah na kuamini mitume Wake. Imani iko moyoni. Moyo una nafasi ya kutosha ya kuwa na hisia, msukumo, hadithi na akili kuhusu Allah. Ni ishara dhahiri ya ukweli huu kuwa mtu asiye na akili timamu hawajibiki kuwa na imani.
Mtindo wa Qur’an umejaa shuhuda za kimantiki zinazotakiwa kwa ajili ya kuthibitishwa na akili ya mtu. Humo kila mara kuna shuhuda na mifano ya kimantiki inapoeleza kuwepo kwa Allah, kwamba Nabii Muhammad (s.a.w) ni mtume wa kweli, kwamba Qur’an ni neno la Allah, na kuhusu kuwepo kwa ufufuo baada ya kufa.
Kwa kweli, kama amri au adhabu yoyote ya Allah haitoshelezi mantiki ya mwanadamu, basi haitaweza kusemwa kuwa hapa lipo jaribio lisilo na upendeleo. Kama mtu anamwajibisha mwanafunzi wa shule ya awali kwa maswali ya sayansi yanayofaa kwa ajili ya shahada za chuo kikuu au za udaktari wa falsafa, basi mtu huyo atakuwa ameonewa. Ndio sababu, mara zote akili na fikra za kibinadamu zinatiliwa mkazo katika Qur’an na kuna maneno kama ifuatavyo: “Je hamfahamu? Je hamfikiri?”
Pili, maneno “Uislamu ni dini ya mantiki” hutilia mkazo falsafa ya mtu anayeziegemeza fikra zake kwenye sababu na mantiki yake yeye mwenyewe. Hayo si sahihi. Kwa mujibu wa mtu huyo, “Fikra za akili zilizo bora hufanana”, kwa hivyo mambo asiyoweza kuyafahamu hayako sahihi. Kwa hiyo, kile ambacho Uislamu unacho na kile unachokipinga katika mtazamo wake kinakuwa si sahihi.
Ni kwasababu Uislamu ni dini ya mantiki. Kisichokuwa na mantiki hakina nafasi katika dini.
Watu wa namna hii wenye falsafa kama hii hawawezi kufahamu dhana ya “mantiki” kwa sababu mantiki yenyewe peke yake haiwezi kushika kila kitu bila ya hali za nje; kinyume chake, inajaribu kwenda katika mwelekeo wa elimu na fikra alizopewa hapo kabla. Ni uthibitisho bora kabisa wa ukweli huu kuwa mtu mwenye akili ya juu sana lakini ambaye si lazima awe msomi hawezi kufahamu na kufanya mambo anayoyafanya mhandisi, daktari au mufti ambaye si hodari.
Nukta muhimu zaidi ya kuitaja hapa ni hii: Haifai kwa baadhi ya watu wasiofahamu jambo fulani kusema jambo hilo “halina mantiki.” Wengi wetu hatujui kuhusu fizikia, kemia, unajimu, hisabati, n.k. na hatuyafahamu hayo lakini hakuna anayesema kuwa hayo hayana mantiki kwasababu watu wengine hawayafahamu. Akili peke yake haiwezi kugundua kila kitu. Kama ingewezekana, kusingekuwa na haja ya mitume. Kila jambo lina uwanja wa kitaaluma unaoweza kufahamika kwa wataalamu peke yao. Wataalamu hao wanaweza kufahamu kwa urahisi masuala ambayo watu wengine hawawezi kuyafahamu. Halikadhalika, ukweli kuwa baadhi ya watu hawawezi kufahamu ukweli wa Quran haimaanishi kuwa ukweli huo si wa kiakili na usio na mantiki.
Nukta nyingine muhimu ni hii: Kuwepo kwa baadhi ya mambo yanayoitwa ta’abbudi na kwamba hayawezi kufahamika kwa akili kunahusu kujaribiwa mwanadamu. Kanuni za imani ni za kisayansi na zimeegemea mantiki. Kanuni chache za Uislamu zipo ili kuijaribu imani na kujisalimisha sio kuiridhisha akili. Kuna haja ya kuwepo baadhi ya mambo ambayo akili haiwezi kuyafahamu kwa urahisi ili idhihirike kama mtu anaamini akilini mwake tu au anaamini na anajisalimisha kwenye Uislamu.
Kwa kuhitimisha, mtu anayesema, “Kwa kuwa Quran ni neno la Allah, kila kilichomo ndani mwake ni sahihi – hata kama akili yangu haiwezi kufahamu “anafaulu jaribio. Anayesitasita na huku akisema, “Jambo kadha katika Quran halina mantiki; akili yangu haiwezi kulifahamu” anafeli jaribio kwa sababu ama si mnyoofu au ni mjinga sana.
Mathalani, ukweli kuwa swala ya subuhi ina rak'ah mbili lakini swala ya adhuhuri ina rak'ah nne haihusiani na akili. Hata hivyo, masuala kama vile kuharamishwa kwa nyama ya nguruwe na ulevi kunaweza kuelezwa na sayansi na mantiki. Mambo ya kimantiki ni zaidi kuliko mambo ya ta’abbudi.
15
Kwa nini Allah amefanya dini nne za lazima? Je isingekuwa sawa kama ungepelekwa Uislamu tu?
Kila kitu ni bora katika mazingira kilipokuwepo. Hata hivyo, kwa ujumla kuna jambo ambalo ni bora zaidi na zuri zaidi ya mambo yote.
Kwa mfano, katika Qur’an tukufu, kumeelezwa kuwa mwanadamu aliumbwa kwa udongo bora mwusi. Kwa ulinganifu, vitu vingine viliumbwa kwa dosari? Hapana. Hivyo pia ni viumbe vizuri sana katika mazingira yao wenyewe.
Kwa mfano, jua ni zuri mno katika mazingira yake lenyewe. Kwa maneno mengine, hakuna watu ambao wangeweza kuishi kama Jua lisingekuwepo. Hata hivyo, mwanadamu ni Mzuri sana kwa ujumla, na Jua ni Zuri sana kwa upande wa kuwepokwake, na kwa upande wa Kazi linayofanya. Tunaweza kutoa mifano mingine zaidi. Kondoo, ardhi, miti ya matunda, malaika, n.k. vyote ni viumbe wazuri sana na wakamilifu kabisa katika mazingira yao wenyewe.
Kwa hali hiyo, ukweli kuwa mwanadamu ni mkamilifu zaidi haimaanishi kuwa viumbe wengine si wakamilifu na kuwa wameumbwa wakiwa na kasoro.
Hakuna kondoo wengine walio wakamilifu kuliko wale kondoo waliopo wanaweza kufikiriwa. Hakuna ngamia wengine zadi walio wazuri zaidi kuliko ngamia hao au hakuna jua zuri zaidi kuliko Jua linavyoweza kufikirika. Kwa namna hiyo hiyo, vitabu vitukufu vilivyoshushwa vilikuwa vikamilifu zaidi vilivyopelekwa katika nyakati hizo.
Kumfundisha mwanafunzi mwanafunzi wa shule ya msingi jedwali la kuzidisha namba si ziada wala upungugufu. Hata hivyo, si jedwali lakuzidisha namba bali mada za masomo ya juu hufundishwa mwanafunzi wa chuo kikuu. Halikadhalika, vitabu vitukufu vilivyotumwa kabla ya Qur’an vilikuwa bora sana katika wakati wao na kuvituma katika wakati huo kulifaa na si upungufu. Kwa mtazamo huo, kila mtume na kila ufunuo waliopelekewa ni bora na ulifaa sana kwa wakati wake.
Hata hivyo, kwa maneno mengine, Qur’an ilishushwa pindi watu wote walipokuwa katika kiwango sawa na cha wanafunzi wa chuo kikuu ambao wanaweza kuchukua masomo yao kutoka katika kitabu kimoja na kutokakwa mtume mmoja.
Kwa kutazama kuwa sayansi nyingi zilizosonga mbali hufundishwa katika vyuo vikuu, je tunaweza kusema sayansi inayofundishwa katika chuo kikuu inapaswa wafundishwe watoto wa shule za msingi? Wanadamu pia kama taasisi ya elimu. Kila kipindi ni kama idara za shule na wahadhiri wa idara hizo ni Mitume.
Kwakuwa tangu wakati wa Adam (amani iwe juu yake), wanadamu wamefikia mpaka katika kiwango cha chuo kikuu na wamepata uwezo wa kuchukua mafunzo kamili ya dini ya Uislamu. Kwa hivyo, dini kamilifu zaidi ilibakishwa kuwa ndio ya mwisho. Umuhimu wa hisabati pia upo hata katika shule ya msingi. Hata hivyo, somo hilo hufundishwa kulingana na kiwango cha wanafunzi wa shule ya msingi na mwalimu hafundishi kila anachokijua bali hufundisha mada wanazoweza kuelewa.
Vivyo hivyo, mitume wengine waliwafundisha watu kulingana na viwango vyao na wakawaelimisha. Mwishowe, walipofikia kiwango cha kuweza kufundishwa katika vipengele vyote, dini ya Uislamu na Mtume mtukufu (s.a.w) aliletwa.
-Kwa nini Allah aliachilia Injili na Taurati kugeuzwa-geuzwa na Akailinda Qur’an? Kwa nini Allah aliachilia maneno Yake kubadilishwa hapo kabla?
1. Kumtegemea Allah juu ya yale tusiyojua sababu (busara) zake kunadhihirisha ukamilifu wa imani yetu na uaminifu wetu kwa dini yetu.
2. Viumbe alivyoviumba Allah duniani havilingani. Yeye huviambatanisha baadhi kwa kuwepo sababu na kuumba baadhi yao bila ya sbabu au maana. Kwa mfano, ingawa kila mtu anatokana na mama na baba, alimuumba Adam (s.a.w) bila ya mama na baba, Isa (s.a.w) bila ya baba na Hawa bila ya mama. Inamaanisha kuwa wakati mwingine huwa Anatenda nje ya sheria za ujumla.
Aidha, kwa mujibu wa sheria, moto huunguza, Mwezi haupasuki katika vipande viwili, miti haitembei na fimbo hazigeuki nyoka. Hata hivyo, kwa amri na utashi wake Allah, Ibrahim (s.a.w) hakuunguzwa na moto, Mwezi ulipasuka vipande viwili, mti ulitembea kwa amri ya Mtume (s.a.w) na fimbo ya Musa (s.a.w) iligeuka nyoka.
Aidha, wakati baadhi ya mitume walikuja na wakauliwa na kaumu walizotumwa kwao, Allah aliwahifadhi baadhi ya mitume Wake kama vile Musa, Ibrahim na Muhammad (s.a.w).
Hali sawa na hiyo inaweza kuwa ilijitokeza kuhusu vitabu. Allah, ambaye aliachilia vitabu vingine vibadilishwe, alizuia Qur’an Tukufu kutobadilishwa kwa ukarimu Wake mahususi. Kwa sababu hiyo, Ameashiria kuwa Qur’an iko chini ya Hifadhi Yake binafsi. Allah, aliyemhifadhi Ibrahim (s.a.w) asiungue katika moto, pia ameihifadhi Qur’an kubadilishwa.
Roho zetu na mashetani haziwezi kuuliza kwa nini Hakuzuia mitume Wake wengine wasiuliwe lakini akamhifadhi Ibrahim; haziwezi kutoa rai zao juu ya jambo hilo, pia.
3. Kama Adam asingetolewa Peponi, watu wengi wasingeongezeka. Mbegu hutoka ghalani na kufika mashambani ili zigeuke kuwa miti; halikadhalika, watu wameshuka katika shamba laDunia kutoka ghala la Pepo ili waweze kuongezeka kama miti.
Halikadhalika, kama vitabu vingine visingebadilishwa, basi, ufunuo wa Qur’an usingekuwepo. Vilipaswa kubadilishwa ili ije fursa ya kuja ufunuo Qur’an. Hata hivyo, wale tu waliovibadilisha ndio wanaowajibika na ubadilishwaji huo.
4. Hadhi ya Mtume (s.a.w) miongoni mwa mitume wengine iko dhahiri. Alitumwa ili iwe rehema kwa ulimwengu wote na utume wake haufungamani na wakati au kipindi fulani isipokuwa ni wa nyakati zote na vipindi vyote. Na ametumwa kwa watu na majini. Mitume wengine hawana sifa hizo.
Kwa hivyo, Kitabu cha mtume (s.a.w) ni cha nyakati zote na sehemu zote. Kama kitabu hicho kisingekuwa na muhuri kuwa hakibadilishiki, watu wangekibadilisha. Muhuri huo umekihifadhi.
5. Hakuna anayweza kufanya chochote tofauti na anavyotaka. Hayo, Ameyaonesha kwa kuiifadhi Qur’an.
16
Nini kifanyike ili kuujua na kuutekeleza vyema Uislamu?
Mtu anapaswa ategemeze maisha yake ya kidini juu ya Sunnah ya Mtume, si katika akili yake na mantiki. Maana yake, anapaswa ajue namna Mtume alivyotekeleza dini na alichounasihi ummah wake.
Je Uislamu ni dini ya kinadharia tu bila ya kutekelezwa kivitendo? Inapaswa utafute majibu ya maswali haya hapo juu na ujaribu kuutekeleza Uislamu kwa kujisalimisha kwa Allah. Kunaweza kuwepo tofauti kadhaa katika maisha ya mtu katika hatua fulani za maisha kutokana na athari za umri wake.
Tunapotaja Uislamu, jambo la kwanza linalokuja akilini ni Quran na maisha ya Mtume. Allah alishusha kitabu chenye amri na makatazo na Mtume aliyetekeleza yaliyomo ndani ya kitabu hicho. Basi, njia ya kuwa Muislamu mzuri ni kutii Quran na Mtume (s.a.w). Kumfanya Mtume, ambaye ni Quran hai, kama mfano ni jambo analolipenda sana Allah. Kwa hakika, Allah anaeleza yafuatayo katika Quran: “Sema: Ikiwa nyinyi mnampenda Mwenyezi Mungu basi nifuateni mimi, Mwenyezi Mungu atakupendeni na atakufutieni madhambi yenu.'” (Aal-i Imran, 31)
Katika hadithi iliyosimuliwa na Abu Dawud, Mtume amesema, “Tahadhari! Katika wakati mfupi ujao, baadhi ya watu watasema Quran inatutosha. Hata hivyo, nimepewa elimu kiasi au mara mbili ya kiasi cha Quran.” Hivyo, akaeleza kuwa Quran haiwezi kufahamika kikamilifu bila ya Mtume.
Ama kuhusu amri ambazo wanazuoni wa Kiislamu wamezitoa kutoka katika Quran, tuna aya ifuatayo, ambayo iko waziwazi, kuhusu jambo hilo: “…Na lau kuwa wangelilipeleka kwa Mtume au kwa wenye mamlaka kati yao, wale wanao chunguza wangelilijua...” (an-Nisa, 83)
Kama inavyoweza kuonekana, tumeombwa tuwaendee wale waliopewa mamlaka baada ya Mtume. Kuwepo kwa madhhab manne ndio ufafanuzi wa aya hiyo.
Kwa kuhitimisha, njia ya kujifunza vyema Uislamu na kuutekeleza ni kulingana na Quran, Sunnah na hukumu zilizotolewa na wanazuoni wa Kiislamu kutokana na vyanzo hivyo viwili.
Ama kuhusu kutafiti dini zingine na rai zilizo kinyume na Uislamu, ni muhimu kwetu kujifunza sana dini yetu na kwa usahihi kwanza. Inafaa kutafiti vitu vizuri jaani katika maeneo ya jirani nasi kabla hatujajenga misingi na kuta za jengo letu kwa uimara?
Msinielewe vibaya; sitaki kusema kuwa hakuna jema huko bali kama tunataka kupita katika chumba chenye sumu, tunahitajika kuvaa kichuja hewa madhubuti. Vinginevyo, tutadhurika na sumu. Kama tunataka kutafiti baadhi ya mambo yanayodhuru dini na yenye sumu, tunahitaji kichuja hewa kizuri kitakachozuia gesi za namna zote, maana yake, tunahitaji imani nzuri na ya kweli ya kidini ili rai hizo zisitudhuru.
Ndiyo, njia pekee ya kumpata Allah na ukweli ni kuiamini Quran na kutenda kulingana nayo kwa sababu Quran ni kitabu kitukufu kilichoteremshwa na Allah ili kuwaongoza wanadamu kwenye kheri na ukweli. Quran ndiyo itakayomwonesha mwanadamu furaha kamili ya kidunia na ya ulimwengu mwengine na itakayoitengeneza hulka ya mwanadamu. Inamwita mwanadamu kwenye imani na upwekeshaji, ibada na utumishi, undugu na upendo. Inaweka vigezo bora kabisa kuhusu imani na amali njema. Uislamu umejengwa kwa kuegemea juu ya vigezo vya Quran. Hakuna ukweli nje ya kanuni imara na adhimu za Uislamu na hakuna haja ya kutafuta. Chochote ambacho Quran inakiona chema na kukisadikisha ni kweli; chochote inachokiona kibaya na kukikataa ni batili. Uislamu, uliowekwa na Quran, unazikataa imani potofu za zamani, ushirikina, fedheha na umalaya. Kisha, Waislamu wote wanahitajika kutathmini mambo halisi matukufu yanayohusiana na itikadi, ibada, maadili, halali, haramu, kumtaja Allah, fikra na upendo unaotegemea Quran.
Aya za Quran zina nguvu ya kutosha kumshawishi kila mmoja. Watu wa kawaida wanapenda uwazi wa mtindo wake; wasomi na wanasayansi wanavutiwa na ufasaha wake na balagha yake. “Bila ya shaka, katika kumkumbuka Allah nyoyo hupata kuridhika.” Watu wenye fikra nyingi wa ngazi zote hutosheleza haja yao kwa ajili ya imani kwa Quran na wanakomaa kwa kuifuata.
Quran imemhimiza mwanadamu atafakari na imempa vigezo kwa ajili ya hili. Watu wameweza kusoma kitabu cha ulimwengu kupitia vigezo ilivyofundisha, wamevumbua ukweli mwingi uliojificha ndani mwake na wamempata Muumbaji na Mola wao. Ni nuru ya Allah iliyowekwa akilini ili kumulika gizani na katika njia za maisha zenye dhoruba. Jua linaangazia dunia yakinifu na Quran imeteremshwa ili kuangazia dunia ya kiroho.
Yafuatayo yameelezwa katika Quran: “Hakika hii Qur'ani inaongoa kwenye ya yaliyo nyooka kabisa.” (al-Isra, 9)
Ni muhimu kufuata sheria za sayansi ili kufanikiwa katika sayansi hiyo; halikadhalika, ni muhimu kukubali kanuni za Quran na Sunnah ili kuupata ukweli.
Ndiyo, mwanadamu anaweza kujua nafsi na sifa za Allah Mtukuka kwa njia ya uongofu wa Quran na Sunnah tu. Anaweza kufahamu anapotoka na anapokwenda, ana jukumu gani duniani, maumbile na uhalisi wa dunia nyengine, na kitakachokubaliwa na kukataliwa huko kwa kupitia njia hizo mbili. Atajifunza aina ya amali, vitendo na mitazamo itakayovutia radhi za Allah Mtukuka na amali zipi, vitendo na mitazamo itakayovutia ghadhabu Zake, kipi ni kweli na kipi si sahihi, kipi ni kosa na kipi ni sawa kutoka katika kitabu cha Allah na Mtume Wake. Kila Muislamu ana wajibu wa kutambua dunia yake ya imani na kuabudu chini ya uongofu wa viwili hivyo halisi.
Pia atajifundisha kutokana na misingi hiyo miwili, Quran na Sunnah, jinsi atakavyoingia katika wigo wa Uislamu na kuamini kanuni mahususi na jinsi atakavyodumu katika wigo wa Uislamu (kwa kutenda amali fulani na kuacha amali fulani). Kwa kuwa vigezo vya Waislamu wote ni Quran na Sunnah, Muislamu anatakiwa kutathmini rai zote za kibinadamu, madai, imani na itikadi zinazoegemea juu ya Quran na hadithi, ambazo ni tafsiri ya Quran.
Mosi, Quran inatufundisha kanuni za imani, "kumwamini Allah, kadhalika na kuwaamini malaika, vitabu vya kiungu, mitume, akhera, qadar (kwamba Allah ameumba kila kitu, iwe kheri au shari). Mtu anakuwa muumini pindi tu anapoamini ukweli wa imani kama ulivyoelezwa katika Quran.
Quran imefundisha Uislamu ambao una maamrisho na makatazo yote ya Allah, kwa waumini. Muumini anapotii hayo mamrisho na makatazo, anakuwa ni Muislamu kamili.
17
Je Uislamu, Agano la Kale na Agano Jipya vimeathiriwa na Wasumeria?
Kwa kweli, suala kwamba baadhi ya habari na mambo mazuri yaliyopo leo katika umma au utamaduni yapo pia katika mojawapo ya dini za kweli haioneshi kuwa dini hiyo iliathiriwa na utamaduni huo; badala yake, inaonesha kuwa chanzo chake pia kilikuwa ni ufunuo. Wakati muda ukiendelea mbele, uhusiano wake na ufunuo ulisahaulika na kutazamwa kuwa ni utamaduni wa umma huo kwa sababu Allah aliwatuma mamia kwa maelfu ya mitume kwenda kwa wanaadamu. Mtu wa kwanza pia ni mtume wa kwanza. Kuwa baadhi ya habari zilizoelezwa na dini pia zipo katika utamaduni zinaonesha kuwa zilitokana na ufunuo. Hata hivyo, ufunuo ulisahaulika kadiri wakati ulivyosonga mbele na ilidhaniwa kuwa ilitokana na utamaduni au mtu.
Habari ya Nabii Musa (s.a.w) kuwekwa katika kikapu imetajwa katika aya nyingi. Kisa cha maisha ya Nabii Musa (s.a.w) kinaposomwa, itaonekana waziwazi. Mitume wengi waliishi katika Mashariki ya Kati; kwa hiyo, baadhi ya vidokezi vya habari njema vya dini za Mwenyezi Mungu vinaweza kuwepo katika utamaduni wa ki-Sumeria. Inamaanisha kuwa baadhi ya mitume walioishi kabla ya Musa (s.a.w) walitoa habari njema kuwa angekuja. Kwa hakika, habari njema kuhusu Mtume wetu (s.a.w) upo katika vitabu vitakatifu vilivyotumwa kabla yake.
Baadhi ya watu wasio na imani hutumia maandiko kwa namna hiyo ili kuikana dini. Hata hivyo, Quran inatuambia kuwa hakuna umma ulioachwa bila ya mtume, mwonyaji au mwongozaji. Matukio sawa na hayo katika historia ya dunia yanathibitisha habari hii ya Quran.
Inajulikana kuwa Waarabu wa Zama za Jahiliyya walikuwa na dalili za dini ya Hanif ya Nabii Ibrahim zilizosalia tokea maelfu ya miaka iliyopita. Kuwepo kwa Kaaba, Waarabu wakiizingatia kuwa ni tukufu na walikuwa wakiizunguka, kulingana kwa vitendo vya ibada zao kunazua kusema kuwa hayo yameingizwa kutoka katika dini zingine; kuwepo kwa sheria zenye kufaa heshima ya mwanaadamu au kuwepo kwa maandiko ya kale kuhusu habari za kale ni ushahidi wa kuwepo dini, lakini hayo ni mambo ya kihistoria yaliyopinduliwa na wayakinifu na wakanamungu wanaotumia uyakinifu wa Dajjal.
Ikiwa baadhi ya visa kama cha Nabii Ayyub (s.a.w) – kama vilikuwa ni kweli – vilisimuliwa katika zama za kabla hajaishi, vinaweza kuwa ubashiri mwema kumhusu yeye au vinaweza kuwa na maana ifuatayo:
Huenda wapo wengi waliopata majaribio makubwa kama Nabii Ayyub katika historia. Upambanuzi wa Quran unalenga katika kutoa mifano ya matukio ya kuenea kote na yanawakilisha maisha ya mashujaa wenye subira walioishi na watakaoishi kuwa ni mifano hai ili watu wapate mazingatio.
Kwa kuhitimisha, matukio yanayotajwa na Quran na wahusika katika matukio hayo kwa hakika ni matukio ya kihistoria. Hata hivyo, kunaweza kuwa na matukio mengine yenye kulingana nayo.
18
Unawezaje kueleza amani hiyo ambayo utu unaitafuta ipo katika Uislamu?
Katika kitabu chake Dhana za Baada ya Mambo ya Sasa, Prof. Dr. Ibrahim Ozdemir anaeleza kwa kifupi kuhusu matendo ya Kiislamu chini ya anwani ya undugu wa Kiislamu pamoja na Utu. Ninakuachieni hakikisho hili muhimu. Ni amani, ndiyo inayotafutwa na utu katika Islam?
Kwa mujibu wa Quran, mwanadamu ni kiumbe bora zaidi kuliko vyote. Yeye ni Khalifa (kiongozi wa umma wa Waislamu) wa Allah (swt) ardhini. Kwa sababu ya hilo, imeambatanishwa umuhimu mkubwa kwake na amepewa heshima. Kuua asiye na hatia kunazingatiwa kuwa ni kuwaua watu wote.
Mtume Muhammad (s.a.w) aliyaheshimu mazishi ya wasio-Waislamu, kwa hiyo hilo lilisisitiza jinsi kulivyo na umuhimu mkubwa wa kuwa mwanadamu kuliko kuwa katika dini yoyote. Dhana hii ina fungu kubwa kwa Waislamu kuwastahamilia watu wengine wa dini tofauti na kuwa na desturi ya kujadiliana nao.
Kwa upande mwingine, kwakuwa dhana ya Kiislamu kuhusu dini zingine inategemea hukumu za Quran, kamwe hawajawashurutisha watu kubadili dini chini ya kuyumba kwao. Inapaswa ionekane kuwa ni tokeo la kiasili la kanuni (la Quran), Hakuna kulazimishana katika dini. (Baqarah Surah, 2:256)
Hapo, watu waliokuwa katika eneo lililopigwa vita kamwe hawakukumbana na ushurutishaji, mbali na sharti la kulipa kodi maalumu (jizya); wameachwa huru kuchagua imani yao.
Baadhi ya kauli za Mitume (s.a.w) zimeleta nuru kuhusu suala la watawala wa Kiislamu. Nazo ni;
“Mwenye kuwadhuru raia Wasio-Waislamu raia katika dola ya Kiislamu ananidhuru mimi, na anayenidhuru mimi anamuudhi Allah." (Sahih Bukhari, Hadith)
"Mwenye kuwadhuru raia Wasio-Waislamu katika dola ya Kiislamu, mimi ni adui yake, na nitakuwa adui yake katika Siku ya Kiama." (Bukhari)
Kulazimishwa katika dini kulikatazwa tangu siku ya kwanza ya Uislamu kwa sababu tu ni kinyume na msingi wa dini. Imeelezwa waziwazi katika Quran Tukufu kuwa mpango wa Mtume Muhammad ni kufikisha maagizo ya Allah na uongofu na si kuwashurutisha kuwa Waislamu.
Utendaji wa Mtume Muhammad (s.a.w) kwa hakika umefanyika kulingana na kanuni za Quran. Kama inavyoeleweka, Mtume Muhammad (s.a.w) alianza kuishi pamoja na Wayahudi baada ya kuhama kutoka Makka kwenda Madina. Mtume (s.a.w) aliacha waraka (hati) ulioandikwa kuhusu mahusiano yake na Wayahudi. Mkusanyiko wa sheria zilizopangwa katika mfumo maalumu, ambazo Mtume Muhammad (s.a.w) aliziweka pamoja na vipaumbele vya kiraia vya Madina zinapaswa zikubalike kuwa ni katiba ya kwanza ya kimaandishi ambayo haikuwahi kufanywa hapo kabla na dola tawala.
Katika katiba hii ya kimaandishi, yenye ibara hamsini ilieleza kuwa Wayahudi wanaweza kuendelea na dini yao. Kwa kueleza hayo, Wayahudi na marafiki zao walikuwa wamepewa uhuru wa kidini.
Eneo la Najran lilikuwa katika upande wa kusini mwa Makka, palikuwa ndio kitovu cha Ukristo. Mtume Muhammad (s.a.w) pamoja na mkataba maarufu aliowekeana pamoja na Wakristo wa Najran aliwaekea uhuru wa kidini kujitawala. Juu ya hayo, haki za kinga ya maradhi ilitolewa kwa madhabahu yao na kwa viongozi wao wa kidini.
Kanuni hizi za msingi zilizoelezwa kwa uangalifu katika Quran na Sunnah (Vitendo adhimu vya Mitume), baadaye zikatumiwa na watawala wa Kiislamu. Kwa muktadha huu maagizo ya Abu Bakr (as) [Halifa wa kwanza (kiongozi wa umma wa Waislamu)] baada ya kifo cha Mtume Muhammad (s.a.w) aliyowapa makamanda wake watendaji na mkataba alioweka Omar (as) wakati wa ushindi wa Jerusalem unaakisi mtazamo huo huo. Juu ya hayo, Abu Bakr katika maagizo yake kwa mmoja wa makamanda wake, msikate mitende, miti yenye matunda, na msiue wanyama kama kondoo, ngamia, na mbuzi isipokuwa [mkimhitaji] kwa ajili ya chakula, kwa kuyapa umuhimu maskani ya kiasili hata katika nyakati za vita.
19
Kwa nini Uchaguliwe Uislamu?
Dini zote zina kanuni kuu za namna moja na zinasisitiza mambo ya namna moja. Kila Mtume aliyetumwa na Allah alikuja kuendeleza na kutimiza yale ya mtume aliyemtangulia, alikariri ujumbe wa mtangulizi/watangulizi wake, aliutimiza kulingana na hali na mazingira, alifafanua masuala yaliyohitaji ufafanuzi, alifanya upya mambo yaliyohitajika kufanywa upya na kuunganishwa na mambo yenye kufanana nayo katika upande wa nidhamu - katika kukubaliana na mazingira ya kipindi hicho na mahitaji ya kipindi hicho. Masuala haya ya upwekeshaji, utume, kufufuliwa baada ya mauti na ibada yalikuwa mambo ya msingi kwa mitume wote. Ndiyo, kanuni zilizotajwa hapo juu ziliunda msingi wa ujumbe wa mitume wote huku kukiwa na tofauti ndogondogo katika mtindo, maneno na mitazamo.
Ujumbe wa Quran ni muendelezo wa ufunuo ulioanzia kwa Nabii Adam (as), mtu wa kwanza na mtume wa kwanza. Hivyo, msingi wa dini zote hizo mbele ya Allah ni mmoja: Uislamu.
“Bila ya shaka Dini mbele ya Mwenyezi Mungu ni Uislamu (utii kwa Matakwa yake). ” (Aal-i Imran, 3/19)
Mitume waliotumwa katika enzi na mahali tofauti hawakupingana; Nabii Muhammad (s.a.w) pia, hakumkana yeyote katika wao.
“Mtume ameamini yaliyo teremshwa kwake kutoka kwa Mola Mlezi wake, na Waumini vile vile. Wote wamemuamini Mwenyezi Mungu, na Malaika wake, na Vitabu vyake na Mitume wake. Hatutafautishi baina ya yeyote katika Mitume wake, na (Waumini) husema: Tumesikia na tumet'ii. Tunakutaka maghfira Mola Mlezi wetu! Na marejeo ni kwako.." (al-Baqara, 2/285)
“Sema: Tumemuamini Mwenyezi Mungu, na tuliyo teremshiwa sisi, na aliyo teremshiwa Ibrahim, na Ismail, na Is-haak na Yaakub na wajukuu zao, na aliyo pewa Musa na Isa na Manabii wengine kutoka kwa Mola wao Mlezi. Hatubagui baina yao hata mmoja, na sisi ni wenye kusilimu kwake." (Aal-i Imran, 3/84)
Kwa upande wake, Nabii Muhammad (s.a.w) ni kama muendelezo na ukamilishaji wa mitume wote waliotangulia. Hata hivyo, kuna tofauti; yeye ni mtume wa mwisho; hakuna mtume atakayekuja baada yake; kwa hivyo, yeye ndiye aliyeleta Ujumbe wa Kiungu kwa wote.
Allah, aliyemuumba mwanadamu, anayemjua kwa kina na ndiye anayempa mahitaji yake, alipeleka ujumbe kwa watu katika kila enzi na kuishia kwa Nabii Muhammad (s.a.w). Hivyo, hakutakuwa na mitume baada yake; hakutakuwa na mabadiliko katika ufunuo; na watu watafuata ufunuo wa misho.
“…Leo nimekukamiliishieni Dini yenu, na nimekutimizieni neema yangu, na nimekupendeleeni UISLAMU uwe ndiyo Dini...” (al-Maida, 5/3)
“Na anaye tafuta dini isiyo kuwa Uislamu haitakubaliwa kwake. Naye Akhera atakuwa katika wenye kukhasiri…” (Aal-i Imran, 3/85)
“Muhammad si baba wa yeyote katika wanaume wenu, bali ni Mtume wa Mwenyezi Mungu na Mwisho wa Manabii, na Mwenyezi Mungu ni Mjuzi wa kila kitu.” (al-Ahzab, 33/40)
Dini ya Uislamu ina kanuni zote zinazomkamilisha mwanadamu kimwili na kiroho na zinazohakikisha furaha yake na uokovu. Uislamu humwongoza mtu na jamii wenye kuifuata kwenda kwenye furaha, kutoka katika uzuri na kwenye ukamilifu kutoka katika furaha. Uislamu unaipa umuhimu hifadhi ya maisha. Unawaadhibu vikali wale wanaojaribu kuvuruga amani katika jamii. Huamuru umoja, kusaidiana na mshikamano. Unalinda uhai wa kijamii dhidi ya vurugu na kitisho.
Dini ya Uislamu ina kanuni zote zinazomkamilisha mwanadamu kimwili na kiroho na zinazohakikisha furaha yake na uokovu. Uislamu humwongoza mtu na jamii wenye kuifuata kwenda kwenye furaha, kutoka katika uzuri na kwenye ukamilifu kutoka katika furaha. Uislamu unaipa umuhimu hifadhi ya maisha. Unawaadhibu vikali wale wanaojaribu kuvuruga amani katika jamii. Huamuru umoja, vipawa na mshikamano. Unalinda uhai wa kijamii life dhidi ya vurugu na hofu.
Uislamu unawapa watu maadili makubwa watu na huwanufaisha katika vipengele vyote. Masuala yake yote yana manufaa mengi sana, na huponya maradhi ya kimwili na kiroho. Dini ya Uislamu inazingatia elimu na busara; Hivyo, unawaelekeza watu wenye akili kwenye matendo mema na furaha kwa kuwafanya watumie utashi wao wenyewe. Huutazama ujinga kuwa ni adui mkubwa; huwapeleka watu kwenye tafakuri. Ni lazima kuzingatia hali ya dunia kabla na baada ya Enzi za Upeo wa Furaha ili kufahamu namna dini ya Uislamu ilivyokuwa ni rehema kubwa kwa utu.
Kabla ya Uislamu, dunia nzima ilikuwa katika ujinga na upotovu, kitisho na vurugu. Ushenzi huu na hofu iliyoathiri sana dunia pia iliikumba Rasi ya Uarabuni. Watu walikuwa wakijivuna kwa kuwazika mabinti zao. Waliamini ushirikina, waliabudu masanamu waliyoyatengeneza kwa mikono yao na kuyaomba msaada.
Katika kipindi cha giza, nuru ya Quran iliibuka kama jua kutoka katika pembe ya Rasi ya Uarabuni. Ilivunjavunja matabaka ya ukafiri na ukandamizaji. Iling’aza macho kwa ufunuo wa juu, ilisafisha roho kwa rehema na uongofu, ilichangamsha Akili na kuziongoza dhamiri. Iliondoa ushirikina na kuweka upweke (wa Allah) nyoyoni. Ilondoa uonevu na kuweka haki. Iliondoa chuki na uadui kutoka nyoyoni na kuweka mapenzi, huruma na upole nyoyoni.
Athari hii ya Quran sio finyu kwa kuishia katika Enzi za Upeo wa Furaha pekee. Taifa lolote lililopokea Uislamu na kuutekeleza baada ya hapo lilipata maendeleo katika sayansi, biashara, na kuwa ni mifano ya kuigwa na mataifa mengine. Mfano mzuri zaidi ni maendeleo ya ustaarabu wa Andalusia, wa-Seljuki na wa-Ottoman.
20
Je, kuna kanuni kama vile "Hakuna kuulizana katika dini" katika Uislamu? Kama ipo, inamaanisha nini?
Kuna namna mbili za amri za shari'ah:
1. Amri na makatazo yanayokuja moja kwa moja kutoka kwa Allah; tunaziita “taabbudi”, yaani, sababu (hekima) zake hazijulikani.
2. Sehemu ambayo sababu (hekima) zake zinapatikana katika amri za Allah na makatazo ya Allah; tunaziita “maqul al-mana”.
Tunaweza kuangalia swali lako katika sura tofauti. "Kwa nini swala ya asubuhi iwe na rak'ah nne na si kumi au ishirini?" (Rakaa nne ni mjumuiko wa rakaa mbili za faradhi, na mbili za sunna ) Jibu ni "kwasababu Allah ametuamrisha kufanya hivyo."
Swala ya adhuhuri ilipangwa na Allah iwe ya rak'ah 10 (Nne za faradhi na sita za sunna kabliya na baadiya). Kutafuta hekima yake hakutafanikiwa. Jawabu sahihi la swali hilo ni kwa sababu Allah ameamrisha hivyo. Hata hivyo, baadhi ya kanuni za shari'ah zinaweza kufafanuliwa kwa hekima, lakini hizo si sababu halisi. Sababu za uhakika ni amri za Allah na makatazo.
Mathalani, "Kwa nini Allah ameamrisha salah (swala)?" Mtu anaweza kuorodhesha hekima na madhumuni ya jambo hilo katika vitabu vikubwa-vikubwa. Mtu anaweza kujibu kwa nini tunafunga saumu kwa kutafuta hekima na sababu zake. Hata hivyo, sababu (hekima) na manufaa hayawezi kushika nafasi ya Amri za Allah. Mathalani, sababu mojawapo ya kufunga ni kuhisi namna watu wanavyoumizwa na njaa na kuwaendea kwa huruma.
Hivyo, mtu anaweza kusema “Ninaweza kuhisi njaa zaidi na kuzidisha huruma yangu na ninaweza kumsaidia masikini zaidi na zaidi.” Ingawa wakati wa imsak (muda wa kuanza kufunga) ni saa kumi alfajiri, kama mtu anakusudia kufunga saa tano usiku, lakini kama atafungua dakika 5 kabla ya iftar (kufuturu wakati wa magharibi), je, funga yake itakubaliwa? Hapana kwa hakika. Kuna wakati maalumu uliopangwa wa kufuturu. Na ingawa mtu anabakia na njaa kwa muda mrefu zaidi, funga yake haikubaliki. Hiyo inamaanisha kuwa, hekima ya kufunga inayotakiwa imetumika (kwa kubakia na njaa), lakini kwa sababu ya kufungua katika wakati asiouruhusu Allah, funga yake haikubaliwi.
Hivyo, tuziangalie amri zote na makatazo yote kwa namna hiyo. Hiyo inamaanisha kuwa, tunaitekeleza kwa sababu Allah ametuamrisha tufanye hivyo. Kwa hakika, zinaweza kuwepo sababu (hekima) zake, pia. Na sababu hizi zinaweza kutafutwa. Hiyo pia ni elimu na ibada. Hata hivyo, hekima na manufaa kwa hakika si sababu halisi, bali ni ufafanuzi.
21
Je, Uislamu ni dini ya hofu?
Kunaweza kuwepo baadhi ya dini potovu zinazoegemea hofu lakini si sahihi kusema kuwa msingi wa dini zote ni hofu. Hususani wanaoitizama dini ya Uislamu kuwa ni dini ya hofu, hawako sahihi. Quran inatoa habari njema na maonyo. Maonyo hayalengi katika kuwatisha watu; bali badala yake, yanalenga katika kuwalinda watu dhidi ya kufanya makosa. Kuwajulisha watu kuhusu hatari wanazoweza kuzikabili na yanalenga katika kuwaonya dhidi ya kuchukua hatua; hayalengi katika kuwatisha.
Uislamu hautaji Jahannamu tu, bali pia Pepo. Kabla ya kuja Uislamu, watu walikuwa wakiishi bila ya kuamini imani ya ufufuo; walikuwa wakiamini kuwa wangepotea baada ya kufa. Uislamu uliondosha imani hii na ukawapa waumini habari njema kuwa watakwenda Peponi. Kwa hakika, hadithi ifuatayo ya Mtume (s.a.w) ni mfano mzuri wa hayo:
"Rahisisheni, msifanye ugumu; toeni habari njema, msiifanye ngeni." (Bukhari, 3/72.)
Dini ya Uislamu ni msaada wa Muumbaji kwa wanadamu na elimu ya kuujua ukweli unaolenga katika kuwafanya wawe na furaha duniani na kupata wokovu katika akhera. Tunamjua Muumbaji wetu na sisi wenyewe tunashukuru kwa Uislamu; pia tunafahamu lengo la msingi la kuwepo na kupata amani na utulivu katika dunia yetu ya ndani na ya nje tunashukuru kwa hilo. Mitume wote tokea Nabii Adam mpaka Nabii Nuh, tokea Nabii Ibrahim mpaka Nabii Musa, tangu Nabii Isa mpaka Nabii Muhammad (s.a.w) walikuwa wajumbe na viongozi wa wito huu wa amani, mapenzi na wokovu.
22
Je Uislamu, uliokuja miaka 1400 iliyopita, unajibu maswali ya zama zetu na kutosheleza haja zake?
Lengo la Qur’an katika Mkusanyiko wa Risale-i Nur limejadiliwa katika nyanja mbili:
Kufundisha ukweli wa Uwanja wa Kimamlaka na maadili ya Uwanja wa utumishi (ibada). Tunaposema Uwanja wa Kimamlaka, tunamaanisha mtu, sifa, vitendo, na majina ya Allah (SWT). Qur’an imemtambulisha Allah (SWT) kwa wanadamu katika njia hii na ikawalinda dhidi ya kila namna ya ushirikina (imani potovu). Inapokuja kwenye uwanja wa utumishi, inamaanisha majukumu ya wanadamu kwa Allah (SWT). Alichoamrisha Allah (SWT) na kukataza ni nini? Vitendo gani na amali gani zinazomvutia radhi Zake na kinachosababisha ghadhabu Zake? Majibu ya maswali haya yamejibiwa vizuri sana katika Qur’an.
Katika nyanja zote mbili, akili ya binadamu haina hata neno moja la kusema. Katika nyanja zote mbili hakutakuwa na athari ya muda. Allah (SWT) bado ana nafsi Yake na sifa kama zilivyokuwa hapo tangu. Mkondo wa kibinadamu aliouweka Allah (SWT) unathibitisha yaleyale kama ilivyokuwa hapo tangu na tangu.
Hapa ni kweli kuwa katika zama za mitume waliotangulia, katika karne mbalimbali, kulifanyika njia tofauti kwenye mitazamo. Na mabadliko haya yamefikia kikomo pale mwanadamu anapokuwa amefikia mahali ambapo kila mmoja anaweza kujifunza kutoka kwa mtume mmoja na akapata nidhamu kutokana na Kitabu kimoja.
Mijadala au upingaji wa namna hii hufanyika zaidi kwenye njia zinazohusu mitazamo na maadili, bado kinyume cha njia hizo hakiwezi kupatikana. Pingamizi huletwa na watu waliozoea uharibifu; na kuona kuwa njia za Qur’an hazitafaa katika jamii yenye ufisadi wa namna hii, wanajaribu kuleta madai ya aina hii.
Ukweli haubadiliki kwa kufuata idadi ya watu. Ukweli uko pale pale. Umma unapaswa uutafute na kuufuata, sio kuuweka ukweli uwategemee wao.
Hebu tutoe mifano miwili. Qur’an imekataza pombe na riba. Si mwingine bali wenye waraibu ndio wanaoweza kudai kuwa mambo hayo ni mazuri na yana manufaa. Katika nchi au katika karne, kama watu wengi wanakunywa pombe au wanajihusisha na riba, hii isingemaanisha kuwa Qur’an haikusudii kuiambia nchi hiyo au karne hiyo. Badala yake, hiyo itamaanisha kuwa wao wako nje ya wanaoambiwa na Qur’an, kwamba wako nyuma sana na kwamba wamepotoka.
Njia nyingine ziko kama hivyo.
23
Je, Uislamu ni rai au mtindo wa kimaisha?
Uislamu ni dini pekee aliyoshusha Allah kwa mwanadamu tangu mwanzo wa uumbaji. Nuh, Ibrahim, Musa na Isa wote walifanya kazi ya kueneza dini hiyo hiyo moja. Mtume wetu, Muhammad (s.a.w), alifikisha ujumbe wa mwisho wa Allah kwa kuwa alikuwa ni mtume wa mwisho.
Uislamu ni dini yenye kutambulika kikamilifu. Uislamu unawakilisha mfumo wa kimaadili unaomwongoza mtu katika kila hatua yake.
Dini ambayo Allah aliwachagulia wanadamu kuwa inawafaa katika maisha yao ni dini ya Uislamu. Allah aliirahisisha sana dini Yake ili watu waitekeleze kwa vitendo.
Kumtumaini na kumtegemea Allah, ambaye ni mmiliki wa viumbe wote na matukio yote yanayofanyika ulimwenguni, na kumfanya Yeye rafiki, inamaanisha mwisho wa hofu zote za mtu, wasiwasi, matatizo na taabu. Huu ni urahisi mmojawapo muhimu na katika mazuri yaliyoletwa na dini ya Uislamu kwa anayetekeleza maadili ya Quran kwa vitendo. Kwa kuongezea, Allah aliwajulisha watu kuhusu amri Zake na hukumu Zake zote, zinazowafaa kwa umbile lao na ambazo si ngumu.
Allah anaeleza katika Quran kuwa maadili ya dini ni rahisi na kuwa mambo yatakuwa mepesi kwa wafuasi wa dini ya Allah kama ifuatavyo:
"Na tutakusahilishia yawe mepesi.." (al-A'la, 87/8)
"…Yeye amekuteueni. Wala hakuweka juu yenu mambo mazito katika Dini. Nayo ni mila ya baba yenu Ibrahim..." (al-Hajj 22/78)
Sambamba na aya za hapo juu, Mtume (s.a.w) amesema,
"Dini ni wepesi." (Bukhari, Iman: 29; Nasai, Iman: 28; Musnad, 5:69)
Hivyo, aliwaita watu kwenye kuitekeleza dini.
Ni kweli kuwa dini ya Uislamu ni namna bora ya maisha kwa ajili ya asili, amani na furaha ya mwanadamu na kuwa maisha yaliyoongozwa na maadili ya Quran ni maisha bora zaidi kwa mwanadamu.