FAQ katika kifungu cha Mwanamke

1 Ni zipi haki za wanawake katika Uislamu? Una majibu gani juu ya madai kuwa Uislamu unawashinikiza na kuwawekea vikwazo wanawake?

Katika nyakati za kabla ya Uislamu, wanawake hawakuwa wakitaamwa kuwa ni wanadamu. Dini ya Kiislamu imewainua wanawake mpaka katika hadhi wanayoistahiki. Uhuru haumaanishi kuweza kuishi kwa matakwa ya nafsi ya mtu au Shetani. Kinyume chake, unamaanisha kuishi kama anavyotaka Muumbaji. Kwani mtu asiyetii matakwa ya Allah anatii matakwa ya nafsi na Shetani.

Sasa tutaeleza haki za ujumla za wanawake kwa kifupi:

“Na mmoja wao akibashiriwa kwa msichana, uso wake unasawijika, naye kajaa chuki....” (an-Nahl, 16/58 )

Katika aya hiyo, Allah anaeleza jinsi watu wa Jahiliyyah walivyowatazama wanawake. Hata hivyo, Quran  imeeleza yafuatayo: 

“Anaumba apendavyo (na anapanga), anamtunukia amtakaye watoto wa kike, na anamtunukia amtakaye watoto wa kiume.” (ash-Shura, 42/49)

Mwnamke huzaliwa sawa na anavyozaliwa mwanamume; yeye pia ni mtoto kama alivyo wa kiume. Wazazi watawajibishwa ikiwa watawabagua kwa huruma na zawadi; pia watazingatiwa kuwa wamepuuza nasaha za Mtume na hawatapewa uombezi wa Mtume. Kwa kujua kuwa hisia za Jahiliyyah zitakuwa zinajirudiarudia, Mtume (s.a.w) alisisitiza umuhimu wa kuwaelimisha wasichana kama ifuatavyo:

“Baba anayewalea mabinti zake watatu au wawili atakuwa pamoja nami peponi, hata mtoto mmoja.” (Ibn Majah, Adab 3)  

Mtoto wa kike anapozaliwa, mnyama (aqiqa) huchinjwa kama ilivyo kwa mtoto wa kiume. Inatakiwa apewe jina zuri na aelimishwe na mama yake. Apewe elimu ya kijinsia kutoka kwa mama yake. Hakuna aya au hadithi inayohimiza sayansi na elimu huku ikiwabagua wanawake. Kinyume chake, Mtume (s.a.w) alinasihi elimu mahususi kwa wanawake na aliwaamuru wanaume kuhifadhi haki zao. Wanawake Mujtahid walikwezwa katika wakati wa uhai wake. (Mathalani, Aisha, mke wa Mjumbe wa Allah (s.a.w) ni mmoja wao.)

Mwanamke amenyanyuliwa bila ya ubaguzi wowote na anapofikia wakati wa kuolewa, ni haki yake na sunnah kumwona mtaradhia wake. Asipompenda mtaradhia, ana haki ya kumkataa; mkazo wa wazazi, walezi au mtaradhia wake hautabadili chochote.

Anapoamua kuolewa, anaweza kusisitiza apokee kiasi cha mahr anayotaka. Mahr ni haki yake ya kimaumbile na dhamana ya maisha aliyoiweka Allah. Anaweza kuitumia atakavyo madam ni halali. Anaweza kutumia mahr yake na mali zingine kwa kuitoa sadaka au biashara; anaweza kuanzisha makampuni, kununua hisa, n.k.; anaweza kupata pesa na kuitumia anavyotaka. Matumizi yote ya nyumbani na ya mwanamke yafanywe na mwanamume. Mwanamume hana haki ya kumwambia, “jinunulie mwenyewe mapambo yako, nguo na vipodozi”. Anapaswa ampe matumizi yake kulingana na kipato chake. Kama mwanamume hawezi kumtimizia matumizi baada ya ndoa, mwanamke akidai talaka itakubalika.

Mumewe hawezi kumdhalilisha; asisahau kuwa mkewe ni mwandani wake. Hawezi kumkasirikia na kumwacha peke yake nyumbani.

“Mwanamume bora ni yule anayewatendea vyema wanawake.” (angalia Bukhari, Nikah 43; Muslim, Fadhail 68)

Kutaniana na kujiburudisha kati ya wanandoa ni jukumu la mume.

Mwanamume asimpige mkewe isipokuwa pindi akiasi, kukiuka sheria. (angalia aya 34 ya sura an-Nisa na tafsiri yake kuhusu kuwapiga wanawake. Mathalani, angalia Ibn Kathir IV/257; Qurtubi VI/170,172,173; Elmalı IV/1351; Abu Dawud, Manasik 56; Ibn Majah, Manasik 84; Muslim, Hajj 147; Tirmidhi, Rada'11; Abu Dawud, Manasik 56; Halabi Saghir uk. 395; Halabi Kabir uk. 621; Canan, Terbiye uk. 391;) Mwanamume asimsumbue mkewe kwa kurejea ghafla kwa sababu ya wivu wake.

Katika hadithi, Mtume (s.a.w) amewakataza wanaume walio mbali na nyumba zao kwa muda mrefu wasirejee nyumbani usiku ghafla. Sababu mojawapo ni kumpa mwanamke muda wa kunyoa nywele za kwapani na za siri na kujipamba na kuchana nywele. Hadith inayohusu jambo hilo ni hii ifuatayo:

“Unaporejea nyumbani usiku, usimwendee moja kwa moja; mpe fursa ya kunyoa na kuchana nywele zake.” (Bukhari, Nikah 121,122; Muslim, Rada' 58, Imarah 181,182; Darimi, Nikah 32, Jihad 163; Musnad NI/298)

The scholars who explain the hadith state that coming home suddenly at home might mean that the man suspects of his wife.

Maulamaa wanaoifasiri hadithi hiyo wanasema kuwa kurejea nyumbani ghafla kunaweza kumaanisha kuwa mwanamume anamshuku mkewe.

Mume pia ana wajibu wa kumtosheleza mkewe. Mtume (s.a.w) alimfananisha mwanamume aliyemaliza upesi tendo la kujamiiana kuwa ni kama majogoo, yaani, kama wanyama. Pia aliwanasihi wanaume kutokuanza kujamiiana na wake zao bila ya kuwapapasa wanawake. (Kutoka katika Daylami, Ghazzali, Ihya N/52 (Tafsiri. N/129); angalia pia Suyuti, al Jamiu's-Saghir (pamoja na Fathu'I-Qadir) VI/323) kwani, mwanamume anaweza kuamshwa hisia zake kwa kutazama tu lakini mwanamke huwa tayari kujamiiana baada ya kupapaswa kwa muda mrefu. Mwanamume mzuri ni yule anayemudu kumwandaa mkewe kwa ajili ya kujamiiana na kumtosheleza kama anavyotosheka yeye. Waanaume wanaojijali wenyewe tu wakati wa kujamiiana wasisahau kuwa wanawadhulumu wanawake na wanastarehe kwa kuwatesa wake zao.

Mwanamke ana haki ya kudai talaka kutoka kwa mwanamume asiyeweza kujamiiana naye kwa mwaka mmoja baada ya ndoa.   

Mwanamke ana haki ya kukataa kujamiiana kabla ya kutanguliziwa mahr yake.

Matumizi ya mwanamke, kutunzwa na tiba zifanywe na mwanamume. Ikiwa mwanamke hawezi kuoka mkate, mumewe anunue mkate. ikiwa mwanamke anataka kujipamba, mwanamume alipie vifaa na manukato. Mume anunue gauni mbili au suti mbili kila mwaka, moja kwa ajili ya majira ya joto (kiangazi) na nyingine kwa ajili ya majira ya baridi (kusi). Ikitokea kutoelewana, sifa ya mavazi huamuliwa na mamlaka za mahali husika. Mwanamke anaweza kutaka matumizi pindi mumewe anapokwenda kuvinjari kwa siku asizokuwepo. Akitaka anaweza kudai kitanda kingine cha kulala pindi anapokuwa katika hedhi zake.

Anaweza kutaka mtumishi kulingana na hali ya mumewe. Mshahara wa mtumishi ulipwe na mume. Mwanamke hawajibiki kufanya kazi yoyote ya nyumbani isipokuwa zile ambazo kwa desturi hufanywa na wake katika eneo husika.  

Akitaka, anaweza kuafikiana na mumewe juu ya kiasi maalumu cha matumizi. Ikiwa kiasi hicho kitageuka kuwa hakitoshi, anaweza kutaka kiongezwe; kama mumewe hataafiki, anaweza kushitaki mahakamani.  

Ikiwa mwanamke hataki ndugu wa mumewe, mume anatakiwa kukodi au kununua nyumba nyingine kwa ajili yake. Sababu ya amri hiyo ni ukweli kuwa watamzuia kutaniana na kujamiiana na mumewe. Zaidi ya hayo, mwanamke ana haki ya kudai chumba kingine ikiwa ana watoto isipokuwa watoto wadogo wasiotambua mambo ya kujamiiana.

Mwanamke ana haki ya kuwatembelea wazazi wake mara moja kwa wiki; mume hawezi kulizuia hilo.

Mwanamke ana haki ya kufanya kazi katika biashara halali isiyoingilia haki za mumewe.

Ikiwa mwanamke anataka kwenda katika hamamu baada ya hedhi na uzazi, mumewe atalipia hamamu hilo, hata hivyo, ikiwa itajulikana kuwa mwanamke hajisitiri mwili wake inavyotakikana katika hamamu, hatapelekwa katika hamamu hilo.

Mume anatakiwa alipie matumizi ya mkewe aliyempa talaka rejea au isiyo rejea katika wakati wa iddah.

Mpaka sasa tumetaja mifano michache tu iliyomo katika vitabu vya fiqh kuhusu haki za wanawake juu ya wanaume. Huo si ushauri bali ni haki za kisheria zenye adhabu. Wanawake wakilazimishwa kufanya kazi na wakafanya kazi ngumu ambazo wanaume peke yao ndio wenye kuweza kuzifanya katika baadhi ya sehemu, si kosa la Uislamu bali ni kosa la wale wanaoishi kinyume na Uislamu.

Maulama wengi wa Kiislamu wanasema kuwa mwanamke ana haki ya kupiga kura kunapokuwa na uchaguzi. Kwani, hakuna ushahidi unaoeleza kuwa hawana haki hizo. Mbali na hayo, maana ya uchaguzi ni kutii. Mtume (s.a.w) alipokea utii kutoka kwa wanawake. (Angalia al-Mumtahina (60) aya 12 na maelezo yake) Rai ya kila mmoja wakiwemo wasichana wadogo iliulizwa kwa ajili ya halifa aliyetarajiwa kuteuliwa baada ya Hadhrat  Umar (ra). [angalia Muhammed Hamidullah, Islam Müesseselerine Giriş Ist.1981, uk. 112 (imechukuliwa kutoka kwa Ibn Kathir)]

Mwanamke anapofariki, sanda yake inunuliwe na mumewe.

(Kwa maelezo zaidi kuhusu vipengele vilivyoelezwa katika muhtasari wa hapo juu, angalia Ibn Abidin, Raddu'l-Mukhtar, Misri 1380 (1960) NI/571 n.k.. angalia pia sehemu zinazohusu nafaqa katika vitabu vyote vya fiqh, hususani Sarakhsi, Mabsut V/180, n.k..)

Kama inavyoonekana, mwanamke hana wasiwasi juu ya matumizi; yaani, ana dhamana kamili ya kijamii. Hizo zote ni haki za kisheria zinazotumika mahakamani pindi kunapokosekana maelewano. Katika Uislamu, mume na mke si maadui ambao kila mara hujaribu kupata haki za mwenzake. Wao ni nusu mbili zinazokamilisha kitu kizima, kusaidiana wao kwa wao; mathalani, Mtume (s.a.w) aliwasaidia wake zake kufanya kazi za nyumbani; Hadhrat  Ali (ra) na mkewe Fatima (ra) walifanya kazi kwa pamoja.

MWANAMKE KATIKA FAMILIA:

Uislamu unaeleza kuwa mwanaume na mwanamke waliumbwa kwa usawa:

“Enyi watu! Hakika Sisi tumekuumbeni kutokana na mwanamume na mwanamke...” (al-Hujurat, 49/13).

Uislamu pia unaeleza kutokufanya ubaguzi baina ya mwanamume na mwanamke na kuwa hakuna aliye mbora kwa mwenzake katika kuzaliwa, kufa na kuishi baada ya mauti. Kwani, mwanamume atasimama na kuhesabiwa peke yake mbele ya Allah. (Maryam, 19/93) Hali ya wanawake waumini wanaotenda amali njema na kutokuiacha njia ya Allah imeelezwa kama ifuatavyo: Mwenye kutenda mema, mwanamume au mwanamke, naye akawa ni Muumini, tutamhuisha maisha mema; na tutawapa ujira wao kwa bora ya waliyo kuwa wakiyatenda.” (an-Nahl, 16/97).

Tofauti kati ya mwanamume na mwanamke ipo katika viwiliwili vyao; inaelezwa kuwa wanawake ni viumbe dhaifu na laini. Kwa hiyo, tofauti zipo katika shughuli za maisha ya mtu mmoja mmoja na kijamii; inaonekana kwamba wanawake wamehifadhika hapo. Uislamu haukuwashusha wanawake kama ilivyokuwa katika imani za maisha ya Jahiliyya; pia haukuwafanya wanawake watawale kama ilivyo katika familia ambazo mkuu ni mama. Uislamu umeanzisha familia ya kuigwa ambapo kila mwanafamilia ana majukumu yake na hakuna dhuluma katika majukumu hayo. Uislamu umeweka mfano bora wa familia ulioanzisha enzi mpya, kuondosha mitazamo yote ambayo ingeweza kuwakandamiza wanawake katika familia na kuiharibu familia.

Uislamu unamwajibisha mwanamume kubeba majukumu ya mkuu wa familia.

Wanaume ni wasimamizi wa wanawake, kwa kufadhiliwa (nguvu) na Mwenyezi Mungu baadhi yao juu ya baadhi, na kwa mali yao wanayo yatoa...” (an-Nisa, 4/34)

Allah anaeleza yafuatayo katika aya nyingine kwa kumpa mwanamume wajibu wa kuwa mkuu wa familia:

“...Nao wanawake wanayo haki kwa Sharia kama ile haki iliyo juu yao. Na wanaume wana daraja zaidi kuliko wao. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye nguvu na Mwenye hikima.” (al-Baqara, 2/228)

Mwanamume anatakiwa akabili mahitaji ya familia na kuhifadhi familia dhidi ya athari zote za nje; ana majukumu muhimu sana. Mwanamume hawezi kuingilia mali binafsi ya mwanamke katika familia; hawezi kumtwisha mwanamke mzigo. Zaidi ya hayo, ikiwa mwanamke hataki kumtunza mwanaye, anaweza kumwomba mumewe aweke mtumishi; mwanamke hahitajiki kufanya kazi za nyumbani, pia. Hata hivyo, majukumu ya nyumbani kama hayo ni ishara ya taqwa ya wanawake; kwa hiyo, Mtume (s.a.w) anawahimiza hayo wanawake. Mwanamke anatakiwa kutii amri halali za mumewe. (Abu Dawud, Nikah, 40).

Muendelezo wa maisha ya familia ya Kiislamu unawezekana tu kwa kuhifadhiana hazi za kila mmoja.

“Mnazo haki juu ya wanawake na wanawake wana haki zao juu yenu.” (Tirmidhi, Rada, 11).

Maana ya kujisalimisha na kutii haki za kila mmoja kwa upande wa mwanamke ni kumtimizia mumewe majukumu ya halali.  

HAKI ZA MWANAMKE JUU YA MUMEWE:

Kwa kuwa mwanamume amewajibishwa kuleta chakula, anatakiwa akabili mahitaji yakinifu ya mwanamke na kulifanya hilo kiuhalali. (an-Nisa, 4/34). Mwanamume anatakiwa amtendee wema mwanamke na kulinda haki zake:

“... Na kaeni nao kwa wema, na ikiwa mmewachukia, basi huenda mkakichukia kitu, na Mwenyezi Mungu ametia kheri nyingi ndani yake. (an-Nisa, 4/19).

Uislamu unamkataza mwanamume kufanya ubadhirifu wa “mamlaka ya usimamizi na kuongoza familia”. Inamaanisha kuweka mpangilio katika familia. Kwa hiyo, mwanamume haruhusiwi kutumia fadhila hiyo kwa kumwonea mwanamke. Ni kwa kanuni hii tu ndipo mahusiano kati ya mwanamume na mwanamke yataweza kuendelea katika hali ya kawaida.

Uislamu unawapa wanawake fursa ndogo sana na katika mipaka halali, kutumia vipawa na ufanisi wao katika mambo ya mahusiano ya kijamii. Katika mfumo huu wa kijamii, Uislamu unawaruhusu wanawake kufanya kazi, kushiriki katika shughuli mbalimbali na kujifunza ili kuwasaidia Waislamu. (Bukhari, Ilm, 36; Ibrahim Jamal, Müslüman Kadının Fıkıh Kitabı, kilichotafsiriwa na Beşir Eryarsoy, İstanbul 1987, uk. 483, ff)

“Mwanamke ni kama ubavu. Kama utajaribu kuunyoosha, utauvunjika. Kama unataka kuwa na furaha, uache kama ulivyo.” (Bukhari, Nikah, 79).

“Mbora wenu ni yule anayemtendea mkewe vyema zaidi.” (Tirmidhi, Rada, 11; Ibn Majah, Nikah, 50).

Tunajifunza kutokana na hadithi hizo hapo juu kuwa Mtume (s.a.w) kila mara aliwaonya Waislamu kuhusu wanawake na kuwa aliwanasihi wanaume wawatendee wema. Wanawake wasipigwe; wapewe mawaidha. Hata hivyo, wakikaidi, wakawaasi waume wao, wakakaa na wanaume wasio mahram, wakufuja mali za wanaume na kufichua siri za familia, kwanza wakemewe; kisha, wakaripiwe vikali; kusipokuwepo mabadiliko, wanaweza kupigwa kidogo ili kuwaonya. (an-Nisa, 4/34). Kama kuwapiga kidogo hakusaidii, wasipigwe kwa nguvu.

HAKI ZA MUME JUU YA MKE:

“Wanaume ni wasimamizi wa wanawake, kwa kufadhiliwa (nguvu) na Mwenyezi Mungu baadhi yao juu ya baadhi, na kwa mali yao wanayo yatoa.(an-Nisa, 4/34).

Basi wanawake wema ni wale wenye kut'ii na wanao jilinda hata katika siri kwa kuwa Mwenyezi Mungu ameamrisha wajilinde...” (an-Nisa, 4/34).

Wanawake wawatii na kuwaheshimu waume wao ili waume wao wabebe vyema majukumu yao nyumbani. Mwanamke anatakiwa kumtii mumewe kwenye mambo ya halali. Mbali na hayo, kazi za nyumbani anazozifanya mwanamke na kuwatunza watoto zitazidisha taqwa ya mwanamke. Kwani, Uislamu haukuyawajibisha hayo kwa wanawake; umewahamasisha wanawake wayafanye hayo ili wapate radhi za Allah.

Wanaume ni bora kwa wanawake kwasababu ya kuwa na baadhi ya sifa za kimaumbile na uwezo wasiokuwa nao wanawake. Hata hivyo, haimaanishi kuwa wanaume ni bora kwa heshima na utukufu. (Mawdudi, Tafhimu'l Qur'an, I, İstanbul 1986, uk. 317, 318).

“Mwanamke akiswali swala tano za kila siku, akifunga katika mwezi wa Ramadhani, akihifadhi tupu yake na kumtii mumewe, milango ya Pepo itakuwa wazi kwa ajili yake.” (Bukhari, Misqat, II/202).

Hata hivyo, utii uliotajwa katika hadithi hiyo unahusu mambo yanayolingana na amri za Allah; ikiwa mume atataka jambo lililo kinyume na amri za Allah, mke hatakiwi kumtii. Kwani, kumtii Allah ni bora zaidi kuliko kumtii mume.

Kutoshelezeana kijinsia ni jambo muhimu katika familia; kwa hiyo, haifai kwa yeyote kati yao kupuuza hilo. Mwanamke anatakiwa aujue ukweli huo na amheshimu mumewe kuhusu jambo hilo. Uislamu unaeleza kuwa wanaume na wanawake wako sawa katika kuumbwa. Hakuna tofauti ya adhabu za kidunia katika usawa wa wanawake na wanaume. Adhabu za uhalifu unaofanyika dhidi ya wanaume na wanawake ziko sawa. Ukweli kuwa mwanamke hupokea nusu ya fungu katika mirathi ikilinganishwa na mwanamume si jambo la kudhalilisha au kutokuwepo usawa. Inapozingatiwa kuwa mume ana wajibu wa kumtunza mke, kuwa amtimizie mahitaji, kuwa wazazi wa mwanamke au mlezi wanatakiwa kumtunza na kukidhi mahitaji yake kabla ya kuolewa na kuwa mumewe ayafanye hayo baada ya ndoa, ltadhihirika alilokusudia Allah katika amri hiyo.   

Mwanamke hatakiwi kumpa mwanamume chochote kutoka katika mirathi aliyopata kama hataki kufanya hivyo. Hata hivyo, mwanamume anatakiwa kukidhi mahitaji yake. Kwa hivyo, inawezekana kwa mwanamke kupokea mirathi bali kutoitumia. (Ibrahim Jamal, sawa na rejea ya hapo juu uk. 485).

Allah amemuumba mwanamke awe mwenyeji wa nyumba. Mwanamume anawajibika kupata mali kwa ajili ya familia; mwanamke awajibika kutumia mali vyema kwa ajili ya kaya. Kwani, mwanamke ni mwenye kuchunga nyumba ya mumewe. Uislamu haumwajibishi mwanamke kwenye mambo mengine yoyote. Quran inamhimiza mwanamke kubakia nyumbani kwa aya ifuatayo:

“Na kaeni majumbani kwenu...” (al-Ahzab, 33/33)

Hata hivyo, katika baadhi ya hali, anaweza kutoka. Mathalani, kama hakutakuwepo mwanamume wa kuitunza kaya, ikiwa atahitajika kufanya kazi kwa sababu ya shida ya fedha, ikiwa mwanamume hawezi kupata mali ya kutosha, ikiwa mwanamume ni mgonjwa na hawezi kufanya kazi, n.k., mwanamke anaweza kutoka na kufanya kazi.

“Allah anawaruhusu wanawake kutoka ili kukidhi mahitaji yao.” (Bukhari-Muslim).

Hata hivyo, hali ya maisha ya leo ikizingatiwa, Mwanamke wa Kiislamu hawezi kujihifadhi dhidi ya macho ya wanaume waovu sokoni, mitaani na maisha ya kibiashara mbali na kwamba ni mwangalifu sana. Kwa hiyo, wanawake wajiepushe mitaani hata kama wana shida ya kifedha.

Uislamu unawapa wanawake majukumu ya nyumbani na unaondoa haja ya kufanya kazi. Uislamu utainusuru roho ya mwanamume aliyefanyiwa usaliti katika wakati wa vita na amani.

Rejea:

- Seyyid Kutub, İslâm Kapitalizm Çatışması, İstanbul 1988, uk. 129;
- Said Havva, Uislamu, Tafsiri na Said Şimşek, Ankara nd., uk. 197, ff;
- Mustafa Sibai, Kadının Yeri, İstanbul 1988, uk. 57 ff.;
- Abdullah Nasuh Ulvan, İslâmda Aile Eğitimi, I, uk. 221 ff.;
- Ömer Ferruh, İslâm Aile Hukuku Tafsiri na Yusuf Ziya Kavakcı, İstanbul 1976, uk. 228 ff;
- Hadhrat  Peygamber ve Aile Hayatı, Komisyon, İstanbul 1989, uk. 171 ff;
- M. Ali Haşimi, Kur'an ve Sünnette Müslüman Şahsiyeti, Tafsiri ya Resul Tosun, İstanbul 1988, uk. 63 ff.
 (Şamil İslam Ans, Kadın item)

2 Kwa nini fungu la mirathi wanalopewa wanawake katika Uislamu ni nusu ya wanalopewa wanaume? Ni utaratibu gani uliowekwa na Uislamu kuhusu fungu la wanawake katika mirathi na usawa?

Fungu la mwanamke katika Mirathi na Usawa

A. Hali ya kabla ya Uislamu

Sababu mojawapo ya watu kudai kuwa Uislamu unawaona wanaume ni bora kuliko wanawake na kuwa unakiuka usawa wa wanaume na wanawake ni ukweli kuwa mwanamke hupewa fungu moja lakini mwanamume hupewa mafungu mawili katika mirathi. Kwa hakika, kuwapa fungu moja kwa wanawake na mawili kwa wanaume hakuhusiani na jambo la wanaume kuwa bora kuliko wanawake. Kinyume chake, kwa kuwapa wanawake fungu kutoka katika mirathi, Uislamu umelinda haki za watoto wadogo na wanawake waliokuwa wakidhulumiwa na kuonewa na watu wa Jahiliyyah. Kiukweli, yafuatayo yameelezwa katika aya:

Wanaume wana sehemu katika wanayo yaacha wazazi na jamaa walio karibia. Na wanawake wanayo sehemu katika waliyo yaacha wazazi na jamaa walio karibia. Ikiwa kidogo au kingi.” (an-Nisa, 4/7)1

Katika jamii ya Waarabu wa Jahiliyyah, wanawake hawakuwa wakipewa fungu lolote katika mirathi. Zaidi ya hivyo, wanawake walirithiwa kama mali pindi waume wao walipofariki. Ni wale wanaume waliotumia silaha tu na kulinda nchi ndio waliokuwa na haki ya kurithi. Mali ya mwanamume aliyekufa iligawanywa miongoni mwa ndugu zake wa kiume walioweza kupigana. 2 Hata hivyo, mjini Madinah, watoto waliobaleghe waliweza kurithi mali za baba zao; watoto wadogo, mabinti na akina mama hawakurithi chochote kutoka kwa baba zao. 3

Mwenyezi Mungu anakuusieni juu ya watoto wenu: Fungu la mwanamume ni kama fungu la wanawake wawili.4

Kwa hiyo, ilipoteremshwa aya hiyo, washirikina hawakuipenda amri hiyo na wakasema,

“Mwanamke anapewa moja ya nne au moja ya nane; binti anapewa nusu ya fungu; watoto wadogo nao wanapewa mafungu. Lakini, hawawezi kuendesha farasi wala kupigana. Watoto wadogo pia wanapewa mirathi lakini watoto wadogo hawasaidii chochote katika vita.” 5

Kinachofahamika kutokana na mtizamo huo ni kwamba thamani ya mtu ilipimwa kwa mchango wake katika uchumi.

Fikra hizo ni za Waarabu wa Jahiliyyah, ambazo bado zimo nyoyoni mwa baadhi ya watu, dhidi ya utaratibu wa ugawaji alioufaradhisha Allah kwa msingi wa haki na sababu nyingi zenye hekima. Fikra za Jahiliyyah zilizomo akilini mwa baadhi ya watu wanaoishi leo haitofautiani sana na fikra za Waarabu wa Jahiliyyah. Sababu za kushuka aya hiyo zinadhihirisha waziwazi hali ya wanawake na watoto katika enzi za Jahiliyyah. Mke wa Sa’d b. Rabi, aliyekufa shahidi katika Vita vya Uhud, alikwenda mbele ya Mjumbe wa Allah pamoja na mabinti zake wawili. Akasema,

“Ewe Mjumbe wa Allah! Hawa ni mabinti wa Sa’d. Baba yao alikufa shahidi katika Uhud. Ami zao wamerithi mali yake na hawakuwaachia chochote mabinti hawa. Hata hivyo, mabinti hawa hawawezi kuolewa bila ya mali yoyote.”

Mjumbe wa Allah (s.a.w) alisikiliza malalamiko ya mwanamke huyo na akasema, “Allah ataleta amri Yake kuhusu jambo hili.” 6 Papo hapo, aya ya mirathi iliteremshwa. 7

Uislamu umewanusuru wanawake na watoto wasinyimwe mirathi; umewapa utu wa kijamii na wa kisheria pamoja na wanaume. Kwa hiyo, wale wanaodai kutetea haki za wanawake wasiukosoe Uislamu kwa kusema, “Uislamu unawapa wanawake nusu ya fungu”; badala yake wapokee na kukiri usawa na ubora wa Uislamu, unaowapa wanawake haki ya mirathi kwa njia ya mapinduzi makubwa. Kwa amri hii, Quran haikuondoa tofauti na dhuluma tu miongoni mwa watoto wadogo na wakubwa bali pia imeweka haki za mirathi kwa mama, binti, dada, bibi, mjukuu wa kike, n.k. kwa kuwataja mmoja mmoja kwa majina. Mafungu hayo, yaliyopangwa na Quran kuwa ni haki zisizobadilika, haziwezi kuondolewa na mpango wowote wa kisheria au kidesturi kama vile wosia. Hayo yamejumuishwa katika kundi la (nasiban mafrudan) “fungu lililopangwa” (an-Nisa, 4/7). Ibara hiyo ni ishara ya wazi kabisa kuwa amri hiyo iko dhahiri na yenye kufahamika na kuwa haiwezi kubadilishwa.

B. Aya Zinazohusu Mirathi ya Wanawake

Ni dhahiri kuwa mwanamke ana haki ya kurithi kama alivyo mwanamume katika Uislamu. Vipingamizi juu ya amri hiyo vinahusiana na ukweli kuwa mwanamke hupewa nusu ya fungu la mwanamume.

Awali ya yote, hebu tueleze kwamba umajumui kuwa Uislamu umeamuru mwanamke apewe nusu ya fungu katika mirathi unatokana na kutokuitathimini aya zinazohusu jambo hilo kwa makusudi. Aya hizo zinapotathiminiwa bila ya chuki zozote na kwa uangalifu, madai ayo yataonekana kuwa si kweli:

1. Kumpa mwanamke nusu ya fungu katika mirathi hakudumu katika hali zote; hutokea pale tu anaporithi pamoja na kaka yake (zake) wa baba mmoja na mama mmoja:

Mwenyezi Mungu anakuusieni juu ya watoto wenu: Fungu la mwanamume ni kama fungu la wanawake wawili. Na ikiwa wanawake zaidi ya wawili, basi watapata thuluthi mbili za alicho kiacha maiti. Lakini akiwa mtoto mwanamke ni mmoja, basi fungu lake ni nusu. (an-Nisa, 4/11) 8

Kwa hiyo, ni dhahiri kuwa kanuni ya kumpa mwanamke nusu ya anachopata mwanamume katika mirathi si kanuni inayojumuisha hali zote. Kwa hivyo, kudai kuwa mwanamke hupewa nusu ya anachopata mwanamume katika mirathi ni kanuni ya ujumla tu pasi na kujali hali ya mwanamke na yanakusudia kukwepa maana ya aya iliyotajwa hapo juu. 

2. Kama inavyodhihirika katika aya hiyo, fungu la mwanamke katika mirathi si nusu ya lile la mwanamume kama madai hayo yalivyodai. Ikiwa aliyefariki ameacha mabinti (angalau wawili) tu, theluthi mbili watapewa wao. Ikiwa aliyekufa amemwacha binti mmoja tu, atapata nusu ya mali yote. (an-Nisa, 4/11)

3. Ikiwa mtoto atafariki na kuacha mirathi na ana watoto, basi mama na baba kila mmoja atapewa moja ya sita ya mali. Ikiwa aliyefariki hakuacha watoto na wazazi ndio warithi, basi mwanamke atapata theluthi ya mali yote. Ikiwa aliyefariki ameacha ma-kaka, mama atapata moja ya sita ya mali yote.  (an-Nisa, 4/11) 9

4. Mume akifariki, mkewe atapewa robo ya mali. Mtu akifariki na kuacha watoto zaidi ya mmoja kwa mkewe mmoja au mke mwingine, au ikiwa mwanaye wa kiume ana watoto, mkewe atapata moja ya nane ya mirathi.

“…Na wake zenu watapata robo mlicho kiacha, ikiwa hamna mtoto. Mkiwa mna mtoto basi sehemu yao ni thumni...” (an-Nisa, 4/12) 10

Kama inavyoonekana, madai kuwa fungu la mwanamke kila mara ni nusu ya lile la mwanamume si kweli. Fungu hubadilika kutegemeana na warithi waliopo.

C. Kwanini Mafungu mawili kwa mwanamume na Fungu moja kwa mwanamke?

Kwa mujibu wa Quran, inaweza kuonekana dhuluma kwamba mwanamke anapata nusu ya fungu anaporithi pamoja na kaka yake pindi jambo hilo linapotazamwa kijuujuu lakini kwa hakika ni haki. Licha ya kuwa ni haki, itaonekana kuwa ni sahihi litakapotazamwa chini ya nuru ya uadilifu na haki.

1. Katika Uislamu, mirathi imegawanywa kwa kuzingatia mahitaji na wajibu wa watu. Matumizi ya mama, mke, binti na dada yanapaswa yatimizwe na baba, mume, mtoto wa kiume na kaka. Kwa ujumla, mwanamke hahitajiki kutoa matumizi kwa nduguze. 11 Mwanamume anatakiwa atoe matumizi kwa mkewe, binti, mama na dada katika hali zote. Mwanamume ni mlinzi rasmi wa familia yake na anawajibika kwa kila mwanafamilia. Kwa hiyo, kulingana na kanuni “Zawadi zinategemea majukumu”, mwanamume, ambaye ndiye anayewajibika kuwapa matumizi mkewe, mabinti, mama na inapolazimu kumpa dada yake, hupewa mara mbili ya fungu la dada yake, ambaye hana majukumu hayo.

2. Mwanamke ana mamlaka kamili ya kutumia mali yake apendavyo. Hata kama mwanamke ni tajiri, hahitajiki kutoa mali yoyote kwa ajili ya familia. 12 Kutokana na mtazamo huo, kama mwanamke na mwanamume wangepewa mafungu sawa, uwiano usingekuwa dhidi ya mwanamume kwa kuwa anahitajika kutoa matumizi kwa ajili ya familia; mwanamke hana wajibu huo. Badiuzzaman Said Nursi anaeleza yafuatayo kuhusu jambo hilo:

Aya “...Fungu la mwanamume ni kama fungu la wanawake wawili...” ni haki kabisa, pia ni huruma haswa. Ndiyo, ni haki, kutokana na wanaume wengi huelemewa kwa kumchukua mke na kumkimu. Ama kwa wanawake, wao hupata mume na kumtwisha mzigo wa maisha, na hilo hupunguza walichorithi.”13

3. Kama mwanamke hajaolewa, yeye ni mtu mmoja asiyewajibika kumtunza yeyote. Anapoolewa, mumewe anatakiwa amtolee matumizi yeye na wanawe kama ilivyoelezwa hapo juu. Mwanamke hana wajibu wa kuchuma mali. 14 Zaidi ya hayo, mwanamke anapata mahr kutoka kwa mumewe na atapata zawadi nyingi kama vile dhahabu, vyombo vya ndani, pesa n.k. kulingana na desturi. Mwanamke halazimiki kutumia mali aliyo nayo. 15 Akitaka, anaweza kuizidisha kwa kuwekeza. Kaka atatumia mirathi aliyopata kwa ajili ya gharama za ndoa, mahr na matumizi ya familia. Mbali na hayo, ikiwa dada ambaye hajaolewa hawezi kuishi kwa kutegemea mirathi aliyopokea, kaka anatakiwa amsaidie. 16 Kwa hiyo, jambo hili linapotazamwa kwa mtazamo huo, kumpa mwanamume fungu moja na mwanamke nusu ya fungu ni haki kabisa.   

Ni muhimu kuzingatia kuwa Uislamu unapendekeza muundo ambao wanawake watajitegemea kijamii lakini huru kiuchumi. Hilo ni muhimu ikiwa tunataka kufahamu mkazo wa Uislamu juu ya kupendana wote wawili, kuheshimiana, kuvumiliana na kuelewana miongoni mwa wanafamilia. Hata hivyo, haijalishi uhuru wa uchumi ulivyo bora, haimaanishi kuwa wanawake wanatakiwa watoe matumizi yao wenyewe na kuwa wanaweza kuishi kwa kujitegemea nje ya familia. Wajibu wa kiuchumi wa familia kila mara unamtegemea mwanamume. Kwa hakika, haki hii, wanayopewa wanawake, inaonesha umuhimu ambao dini yetu inawapa wanawake. 

4. Kaka anaweza kumpa dada yake fungu sawa au zaidi akitaka wakati wa kugawana mirathi. Hilo litatazamwa kuwa ni mchango au zawadi. Hakuna anayeweza kuzuia hilo.

5. Suala hilo pia lina sura ya kisaikolojia. Uislamu si wa wakati au enzi, nchi au taifa fulani tu. Unaenea vyote; unazingatia nyakati zote, jumuia zote na saikolojia zote za kibinadamu katika amri zake. Takribani katika jumuia zote, mabinti wamekuwa wakitazamwa kuwa ni “wasichana wenye kutoa mali ya nyumbani na kuwapelekea watu wengine”; hayo yapo hata leo. Kwa hakika, hata kama ataolewa, ana familia tofauti na ana watoto, bado atahitaji huruma na ulinzi wa wazazi wake na kaka zake. Huruma anayopata ina thamani kubwa kuliko mali anayopata kutoka katika familia yake. Katika hali hiyo, kumpa mtoto wa kiume na binti fungu lililofanana wakati wa kugawanya mirathi kunaweza kuiharibu huruma hiyo. Katika kulishughulikia hilo kwa mtazamo huo, Badiuzzaman Said Nursi anasema yafuatayo juu ya hayo:

“Pia ni rehema, kwani msichana mnyonge anahitaji sana ukarimu wa baba yake na kaka zake. Qur'an inaamuru kuwa apate ukarimu wa baba yake bila ya wasiwasi. Baba yake hamwangalii kwa wasiwasi kwa kumfikiria kuwa ni “mtoto mwenye madhara ambaye kwa sababu yake itaondoka mali yake na kwenda mikonomi mwa mgeni.” Wasiwasi na hasira havitangamani na ukarimu wake. Pia anapata ukarimu wa kaka yake na hifadhi bila ya ushindani na husuda. Hamfikirii “kama ni mshindani atakayeangamiza nusu ya familia na kuipa sehemu muhimu ya mali yetu kwa mtu mwingine.” Hawatakuwa na chuki na uhasama uliochanganyika na hisia zake za kumhurumia na kumhifadhi. Kwa hivyo, msichana, ambaye ni mlaini na mdhaifu kimaumbile, kijuu juu anaonekana amenyimwa sehemu ndogo, lakini badala yake anapata mali isiyokwisha kwa njia ya huruma ya wale walio karibu naye. Na kumpa zaidi ya anavyostahiki kwa dhana ya kumhurumia zaidi kuliko Rehema ya Kiungu, si ukarimu, bali ni makosa makubwa. Kwa hakika, ulafi wa kishenzi wa zama hizi, unaokumbusha udhalimu wa kuwazika watoto wachanga wa kike wakiwa hai katika zama za Ujinga kwa sababu ya husuda za kishenzi, huenda zikafungua njia za uovu wa kikatili. Ama kuhusu hilo, hukumu zote za Quran zinathibitisha hukumu hii, Nasi hatukukutuma ila uwe ni Rehema kwa walimwengu wote.(al-Anbiya, 21/107).” 17

Kwa tathmini hii, Badiuzzaman Said Nursi anashughulikia suala hilo kwa mtazamo wa kina.

Migogoro hutokea baina ya wengi kati ya ma-kaka na ma-dada kwa sababu wanaume na wanawake wanapokea mafungu sawa kutoka katika mirathi ya leo. Kaka hawezi kukubali pindi dada anapopata nusu ya mali ya baba yake na kuwapelekea watu wengine. Kwa sababu ya fikra hii ya Jahiliyyah, migogoro mingi ya mirathi hutokea baina ya makaka na madada katika nchi yetu. Leo, watu wengi huwashinikiza dada zao kuwataka wayaache mafungu yao kutoka katika mirathi au watosheke na kiasi kidogo. Madada kwa ujumla huachilia haki zao chini ya shinikizo. Wanawake hubembelezwa na kunyamazishwa katika mahakama haramu za kisheria za kifamilia. Kama tuonavyo katika vyombo vya habari, migogoro ya mirathi inaweza kubadilika na kuwa umwagaji damu usiokoma. Kutokutumia mpango wa ugawaji mirathi wa Allah na kutokutosheka na fungu lake mtu husababisha ukosefu mkubwa wa haki na dhuluma nyingi.

Kutokana na sababu tulizojaribu kuziorodhesha hapo juu, mwanamume hupewa fungu lake kutegemeana na kiwango cha majukumu yake ya kifedha; mwanamke, ambaye hana majukumu ya kifedha ama akiwa ni tajiri au masikini, daima huwepo chini ya dhamana ya kijamii hata akiwa hajaolewa, binti, mke, mama na mjane; yeye hupewa fungu kulingana na alivyo. 18 Ikiwa amri hii ya Allah, mwenye hekima zisizo na ukomo katika amri Zake, si ya haki, inamaaisha kuwa hakuna haki juu ya ardhi.

Kwa kuhitimisha, sheria ya mirathi, ambayo hushughulikiwa kama ni mwendelezo wa sheria ya familia katika Quran, ni jambo lililoelezwa kwa kina. Kuutazama usawa wa wanawake katika mirathi, ambao ni katika masuala ya kisasa zaidi hivi leo, kutokana na mtazamo wa usawa huunda tu msingi wa kosa lenyewe. Kwani, mafungu ya wanawake hutathminiwa tofauti katika hali tofauti tofauti. Hilo hushughulikiwa katika makundi tofauti kutegemeana na kama yeye ni mke, mama, dada pekee au mmojawapo kati ya dada wengi. Wenye kutetea usawa kamili katika kila jambo likiwemo hili husingizia kutoangalia kanuni za msingi zilizotajwa hapo juu. Kwa hiyo, mwanamke huyo hupewa nusu ya fungu la mwanamume katika baadhi ya hali katika mirathi halihusiani na dhana ya kuwa wanaume ni bora kuliko wanawake. Kama ingekuwa kama hivyo, tungepaswa tuseme kuwa watoto ni bora kuliko baba zao kwa kuwa wanapokea fungu kubwa kuliko baba zao. Yatakuwa ni madai ya kubezwa. Kinyume chake, utaratibu huu wa ugawaji unawiana moja kwa moja na majukumu ya mwanamke na mwanaume; unalenga kusambaza matumizi kwa urari na kuhakikisha yanakuwepo mapenzi na haki katika maisha ya kifamilia na ya kijamii.

Mbali na hayo, ukweli kuwa mambo ya lazima na wajibu wa mwanamke na mwanamume ni ya kimaamuzi hapa na kuwa watoto, wanaokaribia  kuanza maisha na watakaokabiliana na shida  za kifedha katika maisha kwa sababu ya kuhitaji mali zaidi kuliko wengine, wanapewa mafungu zaidi kuliko wazazi wao na kuwa wanaume hupewa kuzidishiwa kuliko wanawake kusudio ni kuhakikisha maisha ya kibinadamu katika familia, ambayo ni kitengo cha chini zaidi cha kijamii. Pia ni ishara ya hatua zilizochukuliwa ili kuunda tabaka la kati. 19

Marejeo

1. an-Nisa, 4/7.
2. angalia Tabari, Jamiu’l–Bayan 4/262, Misri, 1968; Razi, Tafsiru’l-Kabir 9/194, Beirut; Tahir b. Ashur, at–Tahrir wa’t-Tanwir 4/248, Tunus, nd; Ibn Kathir, Tafsirul-Qur’ani’l-Azim 2/161. Waarabu walikuwa wakisema, “Wale wasiopigana kwa mikuki, wasioweza kulinda nchi yao na wasioweza kupata ngawira hawawezi kurithi.” angalia rejea ya hapo juu; kuhusu desturi ya mirathi katika Enzi za Jahiliyyah, angalia Ali Osman Ateş, İslâm’a Göre Cahiliye ve Ehl-i Kitap Örf ve Adetleri uk. 379-388.
3. Hamidullah, Muhammad, İslâm Peygamberi 1/260, İrfan Yay. İst. 1980; Kwa ajili ya desturi ya mirathi katika Uyahudi, angalia Ali Osman Ateş, İslâm’a Göre Cahiliye ve Ehl-i Kitap Örf ve Adetleri uk. 372-380.
4. an-Nisa, 4/11.
5. Angalia Tabari, sawa na rejea ya hapo juu 4/275; Ibn Kathir, sawa na rejea ya hapo juu 2/197.
6. Abu Dawud, Faraid 4; Ibn Majah, Faraid 2.
7. Wahidi, Asbabu’n–Nuzul p.150; angalia Ibn Kathir, sawa na rejea ya hapo juu 2/196; Qurtubi, al-Jami’ li Ahkami’l-Qur’an 5/39; Razi, sawa na rejea ya hapo juu 9/203-204. Jambo lililompata Jabir b. Abdullah pia ni sababu miongoni mwa sababu za kushuka aya. Angalia Bukhari, Tafsiru’l-Qur’an 4; Tirmidhi, Faraidh 6; Tirmidhi, Tafsiru’l-Qur’an 5.
8. an-Nisa, 4/11.
9. an-Nisa, 4/11.
10. an-Nisa, 4/12. Jambo la kifani katika aya hiyo ni kuwa wanawake wanapewa haki ya madeni na wosia kama ilivyo kwa wanaume.Na fungu lenu ni nusu walicho acha wake zenu ikiwa hawana mtoto. Mwanamume au mwanamke anapofariki, madeni yake hulipwa, wosia wake hutimizwa halafu mirathi hugawanywa. Inamaanisha kuwa mwanamke ana namna zote za haki za kiraia na kijamii. Mwanamke anaweza kumiliki mali, anaacha mirathi, anapata mirathi, anatoa wosia, anatimiza wosia, anakopa na anakopesha. Yaani, Quran inampa mwanamke haki ya kumiliki mali na kutumia mali yake atakavyo; kwa hivyo, inampa mwanamke uhuru wa kuwa na mali binafsi. Angalia Süleyman Ateş, Çağdaş Kur’ân-ı Kerim Tefsiri, Yeni Ufuklar Neşriyat, 1988, 2/574; Kwa maelezo ya kina kuhusu hali ya mwanamke anayefiwa na mume inakuwaje mirathi yake, angalia Hamza Aktan, İslâm Miras Hukuku İşaret Yay., İstanbul, 1991.
11. Kwa maelezo zaidi kuhusu matumizi ya mwanamke na majukumu yake, angalia İslâm’da Kadın Hakları (Diwani) 2/178-283 Rehber Baş. Yay. 1. Baskı. Ankara, 1993.
12. Kwa maelezo zaidi, angalia Ruhi Özcan, İslâm Hukuku’nda Hısımlık Nafakası uk. 68-84, Çağlayan Yayınları İzmir, 1996.
13. Nursi, Badiuzzaman Said, Mektubat uk. 37, Envar Neşriyat, İstanbul, 1997; angalia pia Sözler uk. 381.
14. angalia Kasani, Alauddin Abu Bakr Ibn Masud, Badaiu’s–Sanai’ 4/28. Misri, 1328; Sarakhsi, Muhammad b. Ahmad, al-Mabsut 5/187. Misri, 1324; Ibn Rushd’il–Hafid, Muhammad Ibn Ahmad, Bidayatu’l–Mujtahid 2/55, Misri, 1379.
15. Mathalani, ikiwa mume ni masikini na mke ni tajiri, mume anawajibika. Mwanamke hawezi kuwajibishwa kwa ajili ya matumizi ya mumewe. Amri hiyo hiyo inafaa kwa mume asiyeweza kupata na kumpa matumizi mkewe kwa sababu kadhaa kama vile kuwa mlemavu. Katika hali hii, matumizi ya mwanamume hutolewa na ndugu wa mumewe, si mkewe. Mwanamke husaidiwa na nduguze. Matumizi ya ndoa ambayo mwanamke hupokea kutoka kwa mumewe ni deni lisiloondoka kutokana na maagizo. Hata kama mwanamke atatumia mali yake, anaweza kuchukua mali hiyo kutoka kwa mumewe. Angalia Özcan, Ruhi, Hısımlık Nafakası uk. 71.
16. Kwa matumizi ya wanandugu, angalia Ruhi Özcan, sawa na rejea ya hapo juu uk. 89-154.
17. Nursi, Badiüzzaman Said, Mektubat 37; Sözler uk. 381.
18. Kwa hifadhi ya kijamii ya mwanamke katika Uislamu, angalia Faruk Beşer, Kadının Çalışması Sosyal Güvenliği ve İslâm p.165-180, Nun Yay. İst. 1995; Bayraktar Bayraklı anasema, “Ikiwa baba katika familia ni mzee na ikiwa watoto wa kiume na binti wanafanya kazi kwa pamoja na kupata mali kwa pamoja, mafungu yao katika mirathi ni sawa.” Anatumia  aya 32 ya sura an-Nisa kama ushahidi. Hata hivyo, aya hiyo haiwezi kuwa ushahidi kwa ajili ya suala hilo kwa sababu aya hiyo inaeleza kuwa mwanamke, aliyenyimwa mirathi katika enzi za Jahiliyyah, anahitajika apewe fungu lake kutoka katika mirathi. Fungu la mwanamke kutoka katika mirathi hutegemeana na hali mbalimbali zilizoelezwa zilizoamuliwa na aya na hadithi. Pia ni muhimu kusema kuwa kipato cha mtoto wa kike katika familia ya namna hiyo ni cha msichana tu. Hahitajiki kutumia mali yake katika matumizi ya familia. Ni mali yake binafsi. Angalia Bayraktar Bayraklı, Kadın, Sevgi ve Temel Hakları uk. 64, İşaret Yay. İstanbul, 2000.
19. Kuhusu kanuni za tabaka la kati na kanuni za Kiislamu, angalia İzzet Er, Sosyal Gelişme ve İslâm uk. 94-115, Rağbet Yayınları, İstanbul, 1999.

3 Je wanawake wamepuuzwa katika sheria ya Kiislamu?

Katika Uislamu, wanawake wamepata nafasi na thamani wanayostahiki na wamepata amani na furaha kamili waliyoitamani mara nyingi katika historia yote. Sheria ya Kiislamu imekomesha vitendo vya kukithirisha na kupuuzia na imeweka urari na utangamano baina ya jinsia mbili.

Kwa mujibu wa Uislamu, wanawake na wanaume wako sawa kwa upande wa kuwa waja aliowaumba Allah. (al-Hujurat, 13; an-Nisa 1) Kama Mtume Muhammad anavyolieleza hilo, “Wanadamu wote wanaume au mwanamke wako sawa kama meno ya kitana.” (Bilmen, Ömer, Nasuhi, Hukuk-u İslâmiye ve İstilahat-ı Fıkhiye Kamusu, II. 73-74).

Wanawake na wanaume ni nusu mbili za tufaha. Aya hii inalieleza hilo vizuri zaidi:

“Wao ni vazi kwenu, na nyinyi ni vazi kwao.” (Al-Baqarah, 2:187) Kama mavazi yanavyositiri sehemu za siri, kukukingeni dhidi ya joto na baridi, basi pia msitiriane na mrekebishane kasoro zenu.

Basi mjadala ‘kama wanaume au wanawake ndio walio bora’ haufai. Tena, kwa mujibu wa maelezo katika Qur’an, wanaume wana baadhi ya sifa na fadhila, wasizokuwa nazo wanawake; halikadhalika, wanawake wana baadhi ya sifa na fadhila wasizokuwa nazo wanaume. Kwa hiyo, jinsia zote mbili zinahitajiana katika sura mbalimbali; na kwa hivyo, jinsia zote mbili zina fadhila zinazotofautiana kimaumbile. Kulinganisha nukta zinazolingana kutatufanya tufikie kwenye majibu yasiyo sahihi. (An-Nisa, 4:34)

Kwa mujibu wa Quran, mwanadamu ana sifa moja tu pasi na kujalisha jinsia. Wanawake na wanaume wanawajibishwa kwenye sifa zinazolingana za kimaadili. Kinachozingatiwa mbele ya Allah ni maadili ya kidini na taqwa. Allah anatueleza ukweli huu katika Quran kama ifuatavyo:

Hakika aliye mtukufu zaidi kati yenu kwa Mwenyezi Mungu ni huyo aliye mchamngu zaidi katika nyinyi.” (al-Hujurat, 13)

Kama inavyoonekana, kwa mujibu wa Quran, kwa Allah undugu hautegemei jinsia, rangi au mbari ya mtu bali juu ya “maadili bora ya Kiislamu” yaliyoelezwa na Allah. Kiukweli, Allah anaeleza kuwa muumini mwanamume au mwanamke anayefuata maadili atalipwa mema duniani na ahera:

“Mwenye kutenda mema, mwanamume au mwanamke, naye akawa ni Muumini, tutamhuisha maisha mema; na tutawapa ujira wao kwa bora ya waliyo kuwa wakiyatenda.” (an-Nahl, 97)

Baada ya utangulizi huo mfupi, hebu tuangalie kwa ukaribu baadhi ya mila zilizofutwa na Uislamu kwa manufaa ya wanawake na haki ambazo Uislamu unawapa wanawake.

Baadhi ya Mila Zilizobatilishwa na Uislamu kwa manufaa ya Wanawake: Uislamu umekataa dhana kuwa wanawake wamelaaniwa, ambazo ni imani ya Wakristo na Wayahudi. Uislamu umekataza kwa nguvu desturi ya kuwazika watoto wa kike wakiwa hai, ambazo zilikuwa mila za enzi za kabla ya Uislamu Uarabuni. Mtume Muhammad (S.A.W) alitangaza kuwa hakukuwa na ndege mbaya katika chochote na kuvunja imani ya kuwaona wanawake kuwa ni nuksi. Aliwaamuru wanaume wawe na huruma sana, mapenzi na kuwajali wanawake. Aliitweza chuki dhidi ya watoto wa kike na akawasifu kwa kusema, “kuweni waadilifu wakati wa kuwapa zawadi watoto wenu; kama ningekuwa mwenye kupendelea, basi ningewapendelea watoto wa kike.” Katika kumjibu mmoja kati ya Masahaba zake aliyeuliza kuhusu nani alistahiki zaidi kuheshimiwa, alisema “Mama yako” mara tatu, katika mara ya nne alisema “Baba yako.”

2. Haki Zinazotambulika za Wanawake: Haki na wajibu ni maneno mawili pacha. Ikiwa kuna haki, lazima kuwe na wajibu pia. Sheria ya Kiislamu, ilitambua haki na uhuru wa wanawake kutoka mwanzoni kabisa na imetweza jambo la kuwadharau, umeweka majukumu juu yao. Kabla ya kuzitaja, tutakumbuka kanuni alizozitaja katika Hotuba ya Mwisho mbele ya watu 130.000:

“Enyi Watu! Ni kweli mnazo haki kwa wanawake wenu lakini nao pia wana haki juu yenu. Kumbukeni kuwa mmewachukua wawe wake zenu chini ya dhamana ya Allah na idhini yake tu. Kama watashikamana na haki zenu basi na wao wana haki ya kulishwa na kuvalishwa kwa ukarimu. Watendeeni wema na ukarimu kwani wao ni wenzenu na wasaidizi wenye kujitolea nafsi. Na pia ni haki yenu kuwa wasifanye urafiki na yeyote msiyemkubali, pia wasifanye machafu.

Katika hadithi nyingine, anasema tena, “Mcheni Allah kuhusu kutimiza haki za wanawake. Kuweni na hadhari ya kukiuka haki na uhuru wao. Kwani mmedhaminiwa hayo.” (Ajluni, Kashfu’l-Khafa, Beirut, 1351, I.36)

Baada ya majumui haya, hebu tuangalie kwa kifupi haki zinazotambuliwa za wanawake katika sheria ya Kiislamu:

Haki ya Masurufu (Nafaqa) kwa wanawake: Mume amewajibishwa kumpa masurufu mkewe na watoto aliomzalia. Yaani, wanawake wanaweza kudai masurufu kutoka kwa waume wao. Katika sheria ya Kiislamu, mume anatakiwa akidhi matumizi ya mkewe ya chakula, mavazi, makazi, na mtumishi. Wanawake wasishurutishwe kugawana uchangiaji matumizi: ni wajibu juu ya mume kuleta matumizi ya mke na watoto...

Haki ya wanawake ya kutenda: Katika sheria ya Kiislamu, wanawake wana haki ya kutenda. Wana uhuru juu ya mali zao wenyewe. Wanaweza kujipatia au kujichukulia wenyewe haki yoyote ya kiraia.

Zaidi ya hayo, uleaji watoto hupewa wanawake, kwa watoto wa kiume mpaka umri wa miaka saba, na kwa watoto wa kike mpaka waolewe.

Haki ya Mirathi: Kinyume na mifumo yote ya sheria za mila-desturia (isipokuwa Sheria za Kirumi) katika kipindi ulipoingia Uislamu, sheria ya Kiislamu ilitambua haki za wanawake katika mirathi. Desturi hii imezingatia usawa isipokuwa kwa kuwapa mafungu mawili makaka na fungu moja kwa madada miongoni mwa ndugu wa baba mmoja na mama mmoja. Mantiki ya desturi hiyo ya (fungu) moja kwa mawili imeelezwa kwa kiasi cha kutosha katika Qur’an na katika hadithi. Suala la wanawake kupunjwa katika mirathi si jambo la hakika.

Haki ya Kujifunza na Elimu kwa Wanawake: Kujifunza na elimu imekuwa na dhima kubwa katika jamii ya Kiislamu. Mwanamke ni mwalimu wa uhakika. Ni mwanamke ndiye kwa sehemu kubwa huwalea na kuwafundisha watoto. Haiingii akilini kuwa wanawake wanyimwe elimu. Mtume Muhammad (S.A.W) kila mara aliwahimiza na kuwaamrisha wanawake wajifunze kuandika na kusoma. Kulitokea idadi kubwa ya wanawake wasimulizi wa hadithi, wanafasihi wa kike, na la muhimu zaidi wanasheria wa kike katika historia ya Kiislamu.

Haki ya kufanya kazi: Wanawake wanaweza kuwa na taaluma yoyote, ambayo si kinyume na dini na maadili.

Haki nyingine ambazo Wanawake wanaweza kudai kutoka kwa Waume wao: Mwanamke anaweza kutaka mahari (mahr) yake anayostahiki kutoka kwa mumewe. Mbali na hayo, mume anatakiwa akae vyema na mkewe. Mwanamke anaweza kuzuru familia yake baada ya kumjulisha mumewe wakati wowote anapotaka kufanya hivyo. Mume ataniane na mkewe na kumruhusu kupata starehe za halali. Mume asimfanyie ukatili mkewe kwa sababu yoyote ile. Mume asifichue siri za mkewe.

Hebu tuoneshe kuwa ingawa wanawake wana haki hizo, mkuu wa familia ni mume. Hata hivyo, hiyo ni kanuni iliyochukuliwa kutoka katika mfumo wa sheria za Wayunani na Warumi. Kuafikiana na kanuni hizi hakumaanishi, kama wanavyodai baadhi ya wanasheria, kuwa zipo tofauti baina ya wanawake na wanaume. Aya inayoeleza ukweli huu kuwa mume ni mkuu wa familia pia inayakanusha madai hayo. Qur’an Tukufu inatangaza:

Wanaume ni wasimamizi wa wanawake, kwa kufadhiliwa na Mwenyezi Mungu baadhi yao juu ya baadhi, na kwa mali yao wanayo yatoa.(an-Nisa, 4:34)

4 Kwanini wanawake katika Uislamu wana nusu ya haki ya wanaume katika kutoa ushahidi?

Mambo ya lazima yanayounda misingi ya sheria ya Kiislamu yanategemea ufunuo (wa Allah). Yameorodheshwa katika Qur’an. Kwa maneno mengine, mambo ya lazima yamewekwa na kuamrishwa na Muumbaji wa Ulimwengu. Zama, angahewa na mazingira yoyote mtu anamoishi, mambo hayo ya muhimu ndio chanzo cha amani na njia ya kupata faraja. Hii ni kwa sababu ya amri hizo ndio zenye kufaa zaidi kwa uumbwaji wa mwanadamu. Amri na mamlaka za kisheria katika Qur’an zinapotafitiwa, nukta inayosalia nki kwamba kuwepo kwa mwanadamu kimwili na kiroho huzingatiwa.

Katika mambo ya kutoa ushahidi, inawezekana kuliangalia hilo, pia. Tafsiri ya aya inayohusu kutoa ushahidi ni kama ifuatavyo:

“…Na mshuhudishe mashahidi wawili katika wanaume wenu. Ikiwa hapana wanaume wawili, basi mwanamume mmoja na wanawake wawili katika mnao waridhia kuwa mashahidi. Ili ikiwa mmoja wao akipotea, mmoja wao amkumbushe mwengine…” (1)

Kwa hivyo, hapa, jambo la msingi linahusiana moja kwa moja na uumbwaji wa wanawake. Hili ni sharti la sura yao ya kisaikolojia. Msingi wa silika ya mwanamke ni kusisimka na yeye anaishi kwa misisimko yake. Kwa hiyo, dhana hujikita moyoni mwake zaidi kuliko akilini mwake na kuleta athari kwa njia hiyo. Kwa hakika hawezi kutokuwa na upendeleo mbele ya matukio. Yeye huliendea jambo akiwa na welewa unaoendana na jinsi inavyotawala dhamiri na huruma yake.

Kwa sababu ya sifa yao hiyo, Qur’an inasema: “Wanawake wanaweza kusahau, kwa hiyo wanatakiwa wapewe wasaidizi katika ushahidi.” Hayo yamesemwa na Allah aliyemuumba mwanamke. Kwa hivyo, ni kanuni isiyobadilika. Je hakuna wanawake wasiosahau kirahisi na wenye kumbukumbu kali kuliko wanaume? Ndiyo, wapo, lakini kwa ujumla, hali hiyo ya kisaikolojia (kusahau) huonekana mara nyingi zaidi kwa wanawake. Ni jambo la kimaumbie tu kwamba hawezi kutunza kumbukumbu kwa muda mrefu.

Kwa upande mwingine, mwanamke ni mndani sana. Ana dunia ya kwake mwenyewe. Yeye ameshughulishwa sana na kazi za nyumbani kutwa nzima. Anawatunza watoto na kuwalea. Wanawake wachache sana huvutiwa na kazi, biashara, na siasa. Mwanamke ambaye yuko mbali sana na dunia ya nje anawezaje kujua matukio yanayotokea huko, atayajuaje na kuyahifadhi akilini mwake na kwa kiasi gani ataweza kutoa ushahidi?

Kwa kupokea ushahidi wa wanawake wawili sawa na wa mwanamume mmoja, na kwa hivyo kutokumtwisha mzigo mwanamke kwa kumpa wajibu ule wa mwanamume katika mambo ya kuutoa ushahidi, Uislamu hauharibu haki yake, kinyume chake, unamuhifadhi na kumzuia asitende dhambi. Hayo ni kwa sababu kutoa ushahidi ni jukumu zito lenye majukumu makubwa.

Katika aya ya Qur’an, yanaelezwa yafuatayo:

“…Wala msifiche ushahidi. Na atakaye ficha basi hakika moyo wake ni wenye kutenda dhambi. Na Mwenyezi Mungu ni Mjuzi wa mnayo yatenda.” (2)

Katika hadithi (maneno ya Mtume) yameonesha kuwa kutoa ushahidi kuna majukumu makubwa na kuwa ushahidi wa uongo unahesabiwa ni miongoni mwa madhambi makubwa mno.

Kwa hakika, Uislamu unamhifadhi mwanamke dhidi ya madhambi makubwa na kumzuia kutenda dhambi ya ushahidi wa uongo, kwa kuhadaiwa na baadhi ya udhaifu wake kupitia msisimko au kupitia hali ya kuwa na jazba. Uislamu umechukua tahadhari dhidi ya hilo kwa kumteulia mwanamke msaidizi kando yake. Kwa sababu hii tu, katika baadhi ya mambo ya ushahidi, wanawake wawili huchukua nafasi ya mwanamume mmoja.

Wakati mwingine wanawake wanaweza kuwa na wivu katika mambo watakayoyatolea ushahidi na hisia za ushindani zinaweza kutawala. Kwa hiyo, wanaweza kuwa na dosari ya kutambua haki kwa kuficha baadhi ya vipengele vya jambo hilo. Hata hivyo, ikiwa wanawake wawili watatoa ushahidi, mashaka yatafutwa pale mmoja wao atakapofafanua nukta atakayoificha mwingine.

Kwa upande mwingine, kuwa ushahidi wa wanawake wawili huchukulika kuwa sawa na ushahidi wa mwanamume mmoja hakuna namna ya kumaanisha kuwa mwanamke ana thamani ya nusu ya mwanamume. Hili ni dalili tu kuwa umuhimu mkubwa kwa kuwepo namna zote za uhakikisho katika ushahidi. Katika madai yapi mwanamke hutoa ushahidi, ni katika madai gani hayumo, na katika yapi ushahidi wake ni nusu ya ule wa mwanamume?

Sheria ya Kiislamu imemtoa mwanamke katika ushahidi wa makosa yanayohukumiwa adhabu inayoitwa ‘had’ kama vile uzinifu, pombe na wizi na katika adhabu za ‘qisas’ (kisasi) na ushahidi wake katika hayo haupokelewi. Katika madai hayo, adhabu ya uzinifu inahitaji ushahidi wa wanaume wanne na hayo mengine ni wanaume wawili. Katika madai yanayohusiana na mambo kama ya biashara, kuuza na kununua, ndoa na talaka, yaliyomo katika kundi la mahusiano na miamala, ikiwa hakuna wanaume wawili, basi ushahidi wa mwanamume mmoja na wanawake wawili hutakiwa. Hata hivyo, katika mambo ambayo wanaume si mahiri kama vile kujua ubikira, hali za wakati wa uzazi kuhusu mama na mwana, na kuanzisha undugu wa kunyonya, ushahidi wa mwanamke mmoja unatosha. Zaidi ya hayo, Umar Ibn Al-Khattab (Allah awe radhi naye) aliona ushahidi wa mwanamke mmoja kuwa unatosha hata katika mambo ya talaka. Hayo ni kwa sababu kusudio halisi katika ushahidi ni kuhifadhi haki mbalimbali, kuendeleza haki na kuutambua ukweli. Hekima mojawapo ya kutokutumia ushahidi wa mwanamke katika adhabu za ‘had’ na katika qisas (kisasi) ni kiwango cha hisi ili kuzuia shaka hata ndogo sana katika mambo hayo. Hayo ni kwasababu katika madai ya qisas kwa kauli zisizo kamilifu, haki ingeweza kukiukwa au mtu angeweza kulipiziwa kisasi kimakosa. Mwelekeo kama vile wa usahaulivu na kuelemewa na jazba kuhusu wanawake kunaweza kulitoa jambo hilo maanani.

(1) Al-Baqarah, 282.
(2) Al-Baqarah, 283.