1
Ukristo ni nini? Utatoa maelezo kuhusu Ukristo uliotajwa ndani ya Quran?
Ukristo ni dini ambayo kiasili imetegemea ufunuo, yenye kitabu kitukufu na ambayo kiasili ni dini ya kumwamini Mungu mmoja; hata hivyo, iligeuzwa kuwa imani ya utatu hapo baadaye. Kuna dhana ya kidini kama mitume, malaika, ahera na qadar (majaaliwa) katika dini hii lakini hayafahamiki na kufafanuliwa kwa namna sawa kama ilivyo katika Uisilamu.
Kwa uhakika, Ukristo ni dini inayoegemea kwenye imani ya Mungu mmoja. Yapo maelezo yenye kutilia mkazo ukweli huu katika Biblia na vyanzo vyengine. Kumpwekesha Allah kumetajwa (Yohana.V / 44). Hata hivyo, baadhi ya ibara na maelezo ya kuunda katika maandishi hayo hayo yamesababisha kuibuka kwa imani ya utatu. Baadhi ya waandishi wa Biblia na muda kati ya Yesu na muda wa kuandikwa Biblia una mchango mkubwa katika ufahamu huu. Kwa upande mwengine, utatu hauelezewi waziwazi popote pale katika kitabu kitakatifu cha Ukristo. Hata hivyo, baadhi ya maelezo kama “mimi na Baba ni kitu kimoja”, roho ya baba yako”, “roho ya Mungu” kumepelekea kwa baadhi ya tafsiri zinazomzingatia Yesu na roho mtakatifu kuwa ni Mungu pamoja na Mungu.
Mtu wa mwanzo kuanzisha tafsiri hizi alikuwa ni Paul, ndiye aliyeunganisha wanafunzi baadaye. Paul, anaetambulika kuwa ni “mwanathiolojia mkubwa wakati wa zama za Yesu Isa”, anajulikanwa kuwa ndio mwasisi wa Ukristo leo. Kwa mujibu wa wanazuoni wa kisasa, Ukristo wa leo unajumuisha ufasiri wa Paul kuliko mfumo uliotambulishwa na Yesu. Hata pia inaweza kusemwa kuwa karne zilizofuata zimetegemea imani yao ya kidini kwa tafsiri ya Paul kuliko Biblia. Mapendekezo ya Paul yamelenga kwenye Yesu Masiya kuliko Mungu. Kwa mujibu wake, Yesu hakuwa ni mtu tu bali pia alifufuliwa kwa uwezo wa Mungu.
Kama inavyoonekana, Ukristo wa leo umeegemea kwenye tafsiri ya Paul. Mifumo yote miwili ya dini hii ya asili na Biblia, kitabu chao kitakatifu, kimegeuzwageuzwa. Ukristo ni dini iliyogeuzwageuzwa. Hata hivyo, Ukristo uliogeuzwageuzwa na Wakristo wanaoishi leo na ukristo uliotajwa ndani ya Quran ni tofauti kabisa.
Katika Quran, neno “Nasrani” linatumiwa kwa Mkristo na neno “Nasara” kwa Wakristo. . (Aal-i Imran, 3/67; al-Baqara, 2/62, 111, 113, 135, 140; al-Maida, 5/14, 18, 51, 69, 82; at-Tawba, 9/30; al-Hajj, 22/17). Wakristo pia wametajwa na aya zilizokuwemo ibara “Ahl al-Kitab” (Watu wa Kitabu) kama aya ifuatayo:
“Sema: Enyi Watu wa Kitabu! Njooni kwenye neno lilio sawa baina yetu na nyinyi: Ya kwamba tusimuabudu yeyote ila Mwenyezi Mungu, wala tusimshirikishe na chochote.” (Aal-i Imran, 3/64)
Kwa mujibu wa Quran, kama vile Wayahudi, Wakristo hawakutimiza ahadi yao; kwa hivyo, uadui na kinyongo vitawatawala hadi Siku ya Kiama. Bwana Muhammad (s.a.w.) ni mjumbe aliyetumwa kwao, pia. Aliwafafanulia mambo mengi yaliyofichwa na Watu wa Kitabu. Hata hivyo, Wayahudi na Wakristo walisema wao walikuwa ni “watoto wa Allah na vipenzi vyake”; hivyo, walimpinga Bwana Muhammad (s.a.w.). Wayahudi walimzingatia Uzayr na Wakristo walimzingatia Yesu kuwa ni mwana wa Mungu. Wamekuwa ni makafiri tokea walipomfanya binadamu kuwa ni mungu. (al-Maida, 5/12-18; at-Tawba, 9/20) Walitenda kinyume na asili ya dini ya upwekeshaji kwa kuwasifia watoto kuwa ni Mungu. Hata hivyo, yafuatayo yanaelezwa katika Quran:
“Sema: Yeye Mwenyezi Mungu ni wa pekee. Mwenyezi Mungu Mkusudiwa. Hakuzaa wala hakuzaliwa. Wala hana anaye fanana naye hata mmoja.” (al-Ikhlas, 112/1-4).
Quran inaeleza kuwa Yesu ni mja wa Allah na mjumbe na kwamba anafikisha ujumbe wa kumpwekesha Allah. (al-Maida, 5/46-47, 62-69, 72-77). Kwa hali hiyo, Wakristo waliomfanya Yesu kuwa ni mungu wanasema, “Mwenyezi Mungu ni wa tatu wa Utatu.” (al-Maida, 5/73); hivyo, wameikengeuka njia ya kweli na kwenda nje ya mstari wa upwekeshaji. Allah anawaita Wakristo walio nje ya kanuni ya upwekeshaji kuja kwenye uasili wa dini, kuja kumpwekesha Allah na kwenye njia ya Uisilamu. (al-Maida 5/46).
Kama inavyoelezwa hapo juu, Ukristo asili yake ni dini ya kweli. Mtume wake ni Yesu na kitabu chake ni Biblia. Yesu, aliyeunda nukta ya mazingatio ya Ukristo wa leo na misingi ya thiolojia ya Paul, ni mja wa Allah na mjumbe wake. Yesu yeye mwenyewe anaeleza hayo kama ifuatavyo:
“(Mtoto) akasema: Hakika mimi ni mtumwa wa Mwenyezi Mungu. Amenipa Kitabu, na amenifanya Nabii. Na amenijaalia ni mwenye kubarikiwa popote pale niwapo. Na ameniusia Sala na Zaka maadamu ni hai, Na nimtendee wema mama yangu. Wala hakunifanya niwe jeuri, mwovu. Na amani iko juu yangu siku niliyozaliwa, na siku nitakayo kufa, na siku nitakayo fufuliwa kuwa hai.” (Maryam, 19/30-33).
Isitoshe, Wakristo waliomfanya Yesu na mama yake kuwa ni mungu, wanaounda imani ya utatu watakumbana na Yesu Siku ya Kiama; hivyo, uongo uliosemwa na Wakristo utafunuliwa mara moja. Suala hili linaelezwa katika Quran kama ifuatavyo:
“Na pale Mwenyezi Mungu atakapo sema: Ewe Isa bin Maryamu! Ati wewe uliwaambia watu: Nifanyeni mimi na mama yangu kuwa ni miungu badala ya Mwenyezi Mungu? (Na Isa) atasema: Subhanaka, Wewe umetakasika! Hainifalii mimi kusema ambayo si haki yangu. Ikiwa nilisema basi bila ya shaka umekwisha yajua. Wewe unayajua yaliyo ndani ya nafsi yangu, lakini mimi siyajui yaliyo katika nafsi yako. Hakika Wewe ndiye Mjuzi mkubwa wa yaliyo fichikana. Sikuwaambia lolote ila uliyo niamrisha, nayo ni: Muabuduni Mwenyezi Mungu, Mola wangu Mlezi na Mola wenu Mlezi. Na mimi nilikuwa shahidi juu yao nilipokuwa nao. Na ulipo nifisha ukawa Wewe ni shahidi juu ya kila kitu.” (al-Maida, 5/116, 117).
Ukristo katika zama za Mtume (s.a.w.) ulikuwa ushageuzwageuzwa kama ulivyo Ukristo wa leo.
Kisha, Ukristo wa leo sio sawa na Ukristo uliofikishwa na Yesu. Wao wenyewe walitunga sentensi kama vile “Na Wakristo wanasema Masihi ni mwana wa Mungu.” (at-Tawba, 9/30) na “Wamewafanya makuhani wao na wamonaki wao kuwa ni marabi badala ya Mwenyezi Mungu, na pia Masihi bin Maryamu.” (at-Tawba, 9/31).
Vivyo hivyo, Ukristo wa leo hauna uhusiano na Biblia iliyoletwa na Yesu. (al-Maida, 5/68) Kwa kuwa, kama vile wanazuoni wa Kiyahudi, mapadri wa Kikristo walibadilisha maamrisho ya Kitabu walichoteremshiwa na Allah kwa sababu ya manufaa ya kupata kitu. (at-Tawba, 9/34)
2
Ni zipi tofauti kuu kati ya Uisilamu na Ukristo wa leo?
1. Katika Ukristo, ipo imani ya utatu lakini katika Uisilamu, kuna imani ya kumpwekesha Allah.
2. Uisilamu unahusisha dini zote za mbingu na mitume; Ukristo unaikubali Biblia tu kuwa ndio kitabu cha kweli; hauikubali Quran kuwa ndio kitabu kilichotegemea ufunuo.
3. Ukristo unadai kuwa binadamu ni mwenye dhambi ya kuzaliwa nayo na kwa ajili hiyo, lazima abatizwe ili atakaswe; Uisilamu unaeleza kuwa watu wote wanazaliwa wakiwa hawana makosa na kwamba hakuna mtu anayebeba dhambi ya mtu mwengine.
4. Katika Ukristo, mapadri na viongozi wa dini wana mamlaka ya kusamehe makosa ya watu wanapokiri; katika Uisilamu, madhambi husamehewa na Allah pekee.
5. Katika Ukristo, maneno ya Yesu yanazingatiwa kuwa ni maneno ya Mungu; katika Uisilamu, amri za kiungu zinafikishwa kupitia ufunuo na Jibril.
6. Kwa mujibu wa Wakristo, Yesu alisulubiwa. Kwa mujibu wa Uisilamu, alipaishwa mbinguni, kwa Allah.
7. Ingawa Wakristo wa leo wanadai kuwa dini yao ndio dini ya mwisho, dai hilo si halali kwa mujibu wa Uisilamu kwa sababu yafuatayo yanaelezwa katika Quran:
“Bila ya shaka Dini mbele ya Mwenyezi Mungu ni Uisilamu…” (Aal-i Imran, 3/19);
“Na anaye tafuta dini isiyo kuwa Uislamu haitakubaliwa kwake. Naye Akhera atakuwa katika wenye kukhasiri.” (Aal-i Imran, 3/85).
(tazama. Şamil Insaiklopidia ya Uisilamu, Ukristo)
3
Ni ipi dini ya mwisho ya Mwenyezi Mungu?
Wanazuoni wa Kiislamu wanagawanya dini katika makundi makuu mawili:
1. Dini za kweli.
2. Dini potovu.
Dini zenye msingi wa kumwamini Mungu mmoja na kuwaamuru watu kumwabudu na kumtii Yeye tu zinaitwa "dini za kweli". Dini za kweli zilizotoka kwa Allah. Kwa hivyo, pia zinaitwa dini zinazotoka mbinguni. Dini ya kweli pia huitwa "dini ya upwekeshaji" kwasababu zina msingi wa kumpwekesha Allah na kumwabudu Yeye tu.
Dini ambazo hazikuteremshwa na Allah, zilizoundwa na watu na hazina msingi wa kumwamini Mungu mmoja zinaitwa "dini potovu".
Baadhi ya dini za kweli zilipotoshwa na watu baadaye; na ushirikina na imani potovu ambazo hapo mwanzoni hazikuwepo ziliongezwa baadaye. Dini zilizokuwa za kweli hapo mwanzoni lakini baadaye zikabadilishwa zinaitwa "dini zilizogeuzwa"; mathalani, Uyahudi na Ukristo.
Dini ya kwanza kwa wanaadamu ni ya upwekeshaji iliyokuwa na msingi wa kumwamini Mungu mmoja, iliyoteremshwa kwa Adam, mtu wa kwanza na Mtume wa kwanza. Tafiti za kielimujamii zinakubali kuwa dini ya mwanzo ya wanaadamu ilikuwa ya upwekeshaji. Kwa hakika, Schmidt, mtafiti wa historia za dini mbalimbali na mwanaelimujamii, alionesha kwamba Mbilikimo, ambao ni jamii ya kale zaidi duniani, walikuwa na imani ya Mungu mmoja. Uchunguzi wa Schmidt umekanusha madai ya Durkheim kwamba Utambikaji ulikuwa dini ya mwanzo ya wanadamu na akaondosha nadharia hiyo iliyoenea huko Magharibi.
Baada ya Nabii Adam (a.s), baadhi ya watu waliacha kuamini upweke (wa Allah), wakatoka kwenye dini za kweli na kuingiza baadhi ya imani potovu kadiri wakati ulivyosonga mbele kwa kutii nafsi zao na ushawishi wa Shetani. Hivyo, dini potovu zikaibuka. Kadiri watu walivyojitenga na dini ya kweli, Mwenyezi Mungu aliwapelekea mitume wengine na dini ili wawaite kwenye imani ya upwekeshaji. Hata hivyo, baadhi ya watu walikubali wito huo na wengine waling’ang’ania imani zao potovu. Wachilia mbali kuendelea kung’ang’ania imani zao wenyewe, walijaribu kuwazuia wale waliotaka kurejea kwenye dini ya kweli na wakawakandamiza na kuwatesa. Hivyo, mara zote kumekuwa na mapambano baina ya walioamini dini ya kweli na ambao hawakuamini, katika kila karne na enzi. Mapambano haya bado yanaendelea na hayataisha mpaka Siku ya Kiama.
Dini ya Mwisho ni Uislamu.
Leo hakuna hata kimoja katika vitabu vitukufu vilivyoshushwa kabla ya Quran chenye hali yake asili. Kadiri wakati ulivyosonga mbele, uasili wake ulipotea na vikaandikwa upya na watu. Kwa hivyo, ushirikina na imani potovu vikachanganywa ndani mwake. Mathalani, ni ukweli wa kihistoria kuwa Taurati isingeweza kudumishwa na Wayahudi baada ya Nabii Musa, kwani waliishi uhamishoni kama watumwa kwa karne nyingi na walipoteza imani yao na wakaabudu sanamu; pia ni uweli wa kihistoria kuwa Taurati iliyopo sasa iliandikwa na baadhi ya wanazuoni na ikapokelewa kana kwamba ilikuwa ile Taurati ya asili. Ni dhahiri kuwa kitabu kilichoandaliwa baada ya kupita muda huo mrefu uliovurugika hakiwezi kuwa Taurati ileile aliyoshushiwa Nabii Musa. Kwa hivyo, ina baadhi ya madai na kashfa zisizowastahiki mitume na amri zilizo kinyume na dini yenyewe.
Zaburi aliyopelekewa Dawud ilipatwa na hali hiyo hiyo.
Ama kuhusu Injili (Biblia), Nabii Isa (Yesu) hakupokea wahyi wa kimaandishi kwasababu alipata utume alipokuwa na umri wa miaka thelathini na kazi ya utume iliisha alipofikisha umri wa miaka thelathini na tatu. Alikwenda kijiji hadi kijiji kingine na mji mmoja hadi mwingine ili kuwaongoza watu katika kipindi kifupi sana cha miaka mitatu. Katika siku zake za mwisho, kila mara alifuatwa na watawala wa Kirumi kutokana na uchochezi wa Wayahudi. Hakuweza kupata muda au fursa ya kuandikwa Injli. Kwa hakika, Injili zilizopo leo zimeitwa kwa majina ya watu walioziandika na zinaonekana kama wasifu wenye mahubiri, mafunzo na wongozo wa Yesu kwa mitume wake. Kando ya hayo, hazikuandikwa na mitume wake, ambao walikuwa waumini wa mwanzo, bali waliosikiliza maneno ya kiungu aliyopewa Yesu kuwafikishia.
Zipo tofauti baina ya Biblia zilizopo, kwa upande wa maudhui na masimulizi. Kwa hakika, Biblia hizo zilikubaliwa na baraza la mapadri elfu moja mnamo mwaka 325 BK huko Nicaea. Baraza lilichunguza mamia ya Biblia na kukubali Biblia 4 zilizodai kuwa Yesu alikuwa katika uungu kwa muwafaka wa wajumbe 318 na wakaziharibu Biblia zingine kwa kuzichoma moto.
Kama ilvyoonekana, kanuni ya kwamba Yesu alikuwa mwana wa Mungu – Allah atukinge dhidi ya hilo – ilipokelewa na baraza lililokutana miaka mingi baada ya Yesu. Kwa hivyo, ni muhali kusema kuwa Biblia zilizopo leo ni kama Biblia za asili
4
Ahl al-Kitab (Watu wa Kitabu) inamaanisha nini?
Wafuasi wa dini za mbinguni kama vile Uyahudi na Ukristo wanaitwa “Ahl al-Kitabu” (Watu wa Kitabu). Watu wa Kitabu wametajwa kwa wingi ndani ya Quran. Watu wa Kitabu wanazingatiwa kuwa ni “makafiri” kwa sababu hawamkubali Mtume (s.a.w.) lakini sio makafiri kwa upande wa “kumkanusha Allah.”
Quran inatoa kipaumbele kwa watu wa Kitabu kuhusiana na masuala fulani ikilinganishwa na makafiri wengine. Mathalani, inaruhusiwa kuwaoa wasichana na wanawake wa watu wa Kitabu na inaruhusiwa kula nyama ya wanyama waliowachinja. (al-Maida, 5) Kipaumbele hiki wanapewa wao kwa sababu wako karibu na imani ikilinganishwa na makafiri wengine. Quran inawahutubia ifuatavyo:
“Sema: Enyi Watu wa Kitabu! Njooni kwenye neno lilio sawa baina yetu na nyinyi: Ya kwamba tusimuabudu yeyote ila Mwenyezi Mungu, wala tusimshirikishe na chochote; wala tusifanye sisi kwa sisi kuwa Waola Walezi badala ya Mwenyezi Mungu.” (Aal-i Imran, 64) Yaani, tusitambuane kuwa ni Miungu. Hebu tuzitathmini amali zetu kwa kutegemea amri ya Allah na radhi zake. Hebu na tuwe waja wa Allah. Hebu na tujijue kuwa ni waja Wake. Hebu tuheshimiane kwa kutegemea kanuni hii. (1)
Quran inaeleza kuwa Watu wa Kitabu wanawafanya wanazuoni wao na Mapadri wao kuwa ni Miungu. (at-Tawba, 31) Wakati Adiy b. Haram, aliyesilimu kutoka katika Ukristu, alisema, “Ewe Mjumbe wa Allah! Hatuwafanyi kuwa ni Miungu wetu”, Mjumbe wa Allah (s.a.w.) akasema,
“Wanaharamisha alichokihalalisha Allah na kuhalalaisha Allah alichokiharamisha. Hili linamaanisha kuwafanya Miungu wao.” (2)
Kwa kweli, sio lazima kumwita mtu “Mungu” ili kumfanya awe Mungu. (3)
Aya ifuatayo inaeleza njia ya kuifuata wakati wa kutendeana na watu wa Kitabu:
“Wala msijadiliane na Watu wa Kitabu ila kwa njia iliyo nzuri kabisa, isipo kuwa wale waliodhulumu miongoni mwao. Na semeni: Tumeyaamini yaliyo teremshwa kwenu. Na Mungu wetu na Mungu wenu ni Mmoja. Na sisi ni wenye kusilimu kwake.” (al-Ankabut, 46)
Katika aya hiyo, Watu wa Kitabu wanashughulikiwa katika makundi mawili:
1. Kundi la Wajeuri.
2. Kundi la Waadilifu.
Tunaamrisha kutendeana nao kwa njia bora kabisa. Mtazamo huu utawavutia kuja katika Uisilamu na hawatopata tabu kuukubali Uisilamu kwa sababu wakiukubali hawana haja ya kumkataa Musa (Moses) na Isa (Jesus). Hivyo, wataifuata dini ya Mtume wa mwisho na wataokolewa na kuwa ni wafuasi wa dini iliyogeuzwa.
Quran inaeleza kuwa Wakristu wako karibu na Uisilamu kuliko Wayahudi:
“Hakika utawakuta walio shadidi kuliko watu wote katika uadui kwa walio amini ni Mayahudi na Washirikina. Na utawakuta walio karibu mno kwa mapenzi ni wale wanao sema: Sisi ni Manasara. Hayo ni kwa sababu wapo miongoni mwao makasisi na wamonaki, na kwa sababu wao hawafanyi kiburi.” (al-Maida, 82)
Historia inaithibitisha aya ya hapo juu. Idadi ya Wayahudi walioukubali Uisilamu ni ndogo mno. Hata hivyo, Wakristu wengi wameukubali Uisilamu kutokana na utafiti wao. Idadi ya Wakristu walioukubali Uisilamu barani Ulaya ni zaidi ya mamia kwa maelfu. Makanisa mengi yamegeuzwa kuwa misikiti barani Ulaya na yanahudumia kuwa ni vituo vya Kiisilamu kwa sasa.
Matunda mema ya shughuli za Kiisilamu katika nchi za Kikristu ni ukweli; hata hivyo, ni ukweli pia kuwa wakuu wa nchi hizo wana msimamo dhidi ya Uisilamu.
Allah Mtukufu, anaetuamuru tutendeane na kundi adili la Watu wa kitabu kwa njia bora kabisa, anaeleza yafuatayo kuhusu kundi katili:
“Piganeni na wasio muamini Mwenyezi Mungu wala Siku ya Mwisho, wala hawaharimishi alivyo harimisha Mwenyezi Mungu na Mtume, wala hawashiki Dini ya Haki, miongoni mwa walio pewa Kitabu, mpaka watoe kodi kwa khiari yao, hali wamet’ii.” (at-Tawba, 29)
Suala la kuwa ima sifa zilizotajwa katika aya hiyo “zinahusisha Watu wa Kitabu wote au hapana?” ni kitu cha kujadiliwa. (4) Haipaswi kupuuzwa kuwa aya hiyo haisemi kuwa, “piganeni na Watu wa Kitabu wote mpaka walipe Jizyah (Kodi)” lakini inasema, “piganeni na wale miongoni mwa Watu wa Kitabu wenye sifa hizi na zile.” (5) Matendo ya Mjumbe wa Allah (s.a.w.) yalikuwa kama hivyo. Wakati wa zama za Makkah za Uisilamu, Mtume (s.a.w.) aliwatuma baadhi ya Waisilamu kwenda Ethiopia, ambayo ilikuwa ni nchi ya Kikristu, na kusema kuwa watakuwa salama wakiwa huko. Wakati wa zama za Madinah, Mtume aliingia katika mazungumzo na Wayahudi na Wakristu, akiwataarifu kuhusu dini ya Uisilamu na kujaribu kuwashawishi. Baadhi ya Watu wa Kitabu waliukubali Uisilamu kutokana na matendo haya.
Kama inavyoelezwa katika Quran, “Wote hao (watu wa Kitabu) si sawa sawa,” (Aal-i Imran, 113). Ni kinyume na Quran na ukweli wa kihistoria kuwazingatia wote kuwa ni sawasawa katika kundi moja.
Aya ifuatayo haizuii kutoingia katika mazungumzo na wao na kuwa na mahusiano ya kibinadamu pamoja nao. “Enyi mlio amini! Msiwafanye Mayahudi na Wakristo kuwa ni marafiki. Wao ni marafiki wao kwa wao. Na miongoni mwenu mwenye kufanya urafiki nao, basi huyo ni katika wao. Hakika Mwenyezi Mungu hawaongoi watu wenye kudhulumu.” (al-Maida, 51) Kwa kweli, kuwaoa wasichana na wanawake wa Watu wa Kitabu kumeruhusiwa na Quran. (al-Maida, 5)
Hamdi Yazir anaeleza yafuatayo kuhusiana na aya iliyotajwa-hapo-juu: Waumini hawakatazwi kuwafanyia hisani Wayahudi na Wakristu, kuwafanya marafiki na kuwapa usimamizi; wanakatazwa kuwafanya ni marafiki zao wa ndani na wasaidizi wa uovu kwa sababu hawawezi kuwa ni marafiki wa kweli wa waumini. (6)
Inawezekana kufupisha suala hili kama ifuatavyo: Ni jambo la kuwa na mahusiano ya kiutu pamoja nao na ni jambo jengine kuishangaa dini yao, desturi zao na mila; yaliyopita hayakatazwi na Quran lakini ya baadaye ndio yanayokatazwa.
Marejeo:
1. Yazır, II, 1132
2. Razi, XVI, 37
3. Yazır, IV, 2512
4. Riza, X, 333; Qutub, III, 1631-1634
5. Ateş, III, 1133-1134
6. Baydawi, II, 211
5
Ni ipi hali ya watu wa fatrah (kipindi baina ya mitume miwili) ambao hawakujua kuhusu Uislamu? Jee watakwenda motoni kwa vile walikufa bila ya Imani?
Fatrah maana yake ni kusimama na kupitiwa na muda ndani ya kipindi fulani. Kama neno la kidini, linamaanisha kipindi (muda) baina ya mitume wawili.
Katika hadithi iliyosimuliwa na Bukhari, fatrah maana yake ni kipindi (muda) baina ya mtume Issa na mtume Muhammad (rehma na Amani ziwe juu yao). (1)
Inafahamika katika baadhi ya aya kwamba Waarabu kabla ya Uislamu walikuwa na ufahamu mdogo juu ya mitume waliotumwa kwa watu. Katika Qur’an, imetajwa kwamba Waarabu waabudu masanamu walisema: “…Lau angelitaka Mola wetu mlezi (Kututumia mitume kutuonya) bila ya shaka angeli wateremsha malaika”. (2) na hivyo basi inaelezwa jinsi gani walivyokuwa na uelewa mdogo kuhusu Utume na pia kuhusu dini za haki.
Ingawa Waarabu walijua kuwa Mtume Ibarahim alikuwa ni mtume, walijua kuwa utume wake uliishia katika wakati wake, Kutokana na kipindi kirefu cha miaka elfu tatu (3000) baina ya Mtume Ibrahim na Mtume Muhammad (rehma na Amani ziwe juu yao), si wengi waliojua usafi (Hanif) wa dini aliyokuja nayo Mtume Ibrahim.
Wasomi wa Kiislamu wanawajadili watu wa fatrah (wale walioishi kwenye nyakati baina ya mitume wawili) kwa kuwagawa kwenye makundi matatu:
1. Wale waliojiridhisha na kukubali uwepo na umoja wa Allah kwa msaada wa hoja na uwezo wa akili zao kama vile Qus bin Saida na Zayd bin Amr, baba wa Said bin Zayd ambaye alibashiriwa pepo, n.k.
2. Wale walioingilia kwa kuiharibu na wakaibadili Imani ya Mungu mmoja, wakakubali ibada za masanamu pamoja na wale waliovumbua dini kwa matashi yao na wakawakusanya watu waliowazunguka kuwashawishi: akiwemo Amr bin Luhay, ambaye alianzisha ibada za masanamu kwa Waarabu na waabudu masanamu wengine, n.k.
3. Wale ambao hawakujiingiza ima kwenye Imani sahihi au Imani potofu, ambao hawakuwa waumini wala hawakuwa waabudu masanamu, na ambao waliyapitisha maisha yao kwenye ujinga, na ambao hawakuwahi kufikiri kuhusu mambo haya. Kwenye kipindi cha ujinga (kipindi cha ujinga kabla ya ujio wa Mtume) kulikuwa na watu wa aina hiyo pia.
Katika makundi haya matatu, kundi la pili litakwenda motoni kwasababu walikuwa waabudu masanamu. Wale wanaoangukia katika kundi la tatu hawatoingia motoni kwasababu ndio hasa watu wa kipindi cha fatrah. Hii ni kwasababu mtume ambaye angewalingania kwenye dini sahihi na ya kweli hakuwafikia na hawakuonesha ishara za kutokuamini; na kwa hiyo walikuwa miongoni mwa waliosalimika. Wanazuoni wote wa sunnah (Ahl As-Sunnah - kundi lenye wafuasi wengi) wamekubaliana kwenye hili. (3)
Qus bin Saida na Zayd bin Amr waliotajwa kwenye kundi la kwanza, kwa upande mwengine, watafufuliwa na Allah siku ya Kiama kama ni ummah tofauti (jamii), kwa vile wao waliamini uwepo na umoja wa Allah kati ya maelfu ya watu waliokuwepo kipindi hicho, na hawakuwa watu wa mtume yoyote kwasababu hakukuwa na mtume aliyetumwa kwao, na hawakufika kipindi cha Mtume Muhammad (rehma na amani ziwe juu yake). Wao ni watu walionusurukia na wakaokoa maisha yao ya milele kwasababu ya Imani zao. Watakapofufuliwa, watakuwepo uwanja wa makusanyo siku ya hukumu kama “jamii ya mtu mmoja”. Watu hawa ni “wa kipekee” watafunikwa na rehma na huruma za Allah.
Ni Dhahiri kwamba watu wa fatrah hawahusiki na ibada pamoja na amri za kidini. Ingawa, kuna mgongano kati ya madhehebu mawili ya watu wa Sunnah (Ahl as-Sunnah), Maturidi na Ash’ari, kwamba jee walipaswa kuamini au laa. Kwa mujibu wa Imani ya dhehebu la Maturidi, watu hao walipaswa kutumia hoja na uwezo wa akili walioruzukiwa na Allah ili uwafikishe katika kufahamu uwepo wa Allah kwa kutathmini umbile la mbingu na ardhi na kila kilichomo. Kwa mujibu wa Ash’ari, kwa upande mwengine, watu wa fatrah hawalazimishwi kumuamini Allah. Na hii ni kutokana na hali ya kutokuletewa mtume. Allah anasema katika Qur’an: “…Wala Sisi hatuadhibu (mtu au jamii kwa makosa waliyofanya) mpaka tumpeleke Mtume.” (4) Hivyo basi, hawastahili kuadhibiwa kwasababu hawakupelekewa mtume.
Badiuzzaman, mwanachuoni wa Kiislamu ambaye aliishi na kuchapisha kazi kadhaa karne ya ishirini (20), anaileta aya iliyotajwa kama ushahidi na anasema:
“Watu walioishi kipindi baina ya mitume wawili ni miongoni mwa waliosalimika. Imetajwa kwamba hawatoadhibiwa kwa makosa yao kwenye mambo ambayo si ya msingi. Kwa mujibu wa Imam Shafi'i na Imam Ash'ari, wanasema kwamba hata kama si waumini na hawakuamini misingi ya Imani, bado watakuwa ni wenye kusalimika. Wajibu mbele ya Allah huwepo pale anapopeleka mitume, na mitume wakishaletwa, kuwajibika huanza kupitia elimu ya ujumbe wao. Kwavile kutokujali na kupita kwa muda mrefu kuliwafanya wasijue misingi ya dini ya mitume waliotangulia hawakuweza kutoa ushahidi kwa watu wa kipindi hicho. Kama watatii mfumo wa maisha uliotangulia, watapata malipo; na kama hawakufuata, hawatoadhibiwa. Na kwa msingi huo basi, kwa vile mfumo wa maisha ulifichika, hauwezi kuwa uthibitisho.” (5)
Imam Ghazali, Mwanachuoni wa Kiislamu muhimu, anawagawa watu baada u utume wa Mtume Muhammad (rehma na amani ziwe juu yake) katika makundi matatu makubwa:
1. Wale ambao hawakusikia kuhusu ujumbe wa Mtume na hawakupata taarifa kuhusu Mtume. Wale watakaoangukia kwenye kundi hili ni watu waliosalimika na wataingia peopni.
2. Wale ambao walisikia kuhusu ujumbe wa Mtume, na miujiza aliyokuja nayo, tabia zake zilizotukuka, lakini hawakumuamini Mtume. Kundi hili bila shaka yoyote litaangamia na litapata adhabu iumizayo.
3. Wale ambao walilisikia jina la Mtume, lakini hawakusikia chochote zaidi ya propaganda chafu, na hakuna yoyote aliyewaeleza ukweli na kuwatia moyo kwenye Imani thabiti; kwa sababu hizi, wanabaki katikati. Na natumai kwamba nao watakuwa miongoni mwa watu waliosalimika na hivyo basi wataingia peponi.
Mwanachuoni Badiuzzaman, ambaye anaeleza kwamba mwisho wa zama, watatokea pia watu wa fatrah, na anaelezea kwamba aina hiyo ya watu wasio na hatia ambao hufa katika vita vya dunia nao pia watakuwa watu waliosalimika. Badiuzzaman anasema:
“Katika zama za mwisho (akhir zaman), kutaibuka dini na dini ya Muhammad (rehma na Amani ziwe juu yake) itakuwa kama joho fulani tofauti litakalo akisi aina fulani ya fatrah, na katika zama za mwisho kabisa dini sahihi ya Nabii Issa (Yesu) itatawala na kuwa bega kwa bega na Uislamu. Kwa sababu zote hizi, bila shaka majanga waliyoyapata Wakristo ambao walimfuata Nabii Issa (Yesu) ni aina ya mateso kwao.” (6)
Marejeleo
1. Bukhari, Manaqibu'l-Ansar: 53.
2. Qur’an, Fussilat , 14.
3. Tajrid-i Sarih trns, 4:544.
4. Qur’an, Isra, 15.
5. Barua za (Mektubat), 360-361.
6. Kastamonu Lahikası, p. 77.
6
Je Ukristo na Uyahudi ni dini za kweli kwa sasa? Au, hizo sio tena dini za kweli kutokana na mabadiliko yaliyozikumba kadiri wakati ulivyosonga mbele?
Misingi ya Dini ya Kweli na Dini Zilizo Kuu
Dini ya kweli ni sheria ya Allah na huo ni mkusanyiko mtukufu wa baadhi ya ukumu bora. Allah aliituma kama hiba kwa watu kupitia kwa mitume Wake. Sheria hiyo inamwongoza mwanadamu kwenye heri. Kadiri watu wanavyotii amri za sheria ya Allah kupitia utashi na matakwa yao, watakuwa katika njia iliyonyooka na kupata uongofu. Watapata furaha na uokovu duniani na ahera.
Dini zimegawanyika katika sehemu tatu:
Kwanza ni dini za kweli. Ni dini zenye kutangamana na sifa za hapo juu. Ni dini zilizowekwa na Allah na kutumwa kwa watu kupitia kwa mitume. Pia hizo huitwa dini za "kiungu au za kutoka mbinguni".
Dini zote zinazotoka mbinguni kimsingi zinalingana. Hata hivyo, kuna tofauti chache miongoni mwazo ziko katika baadhi ya ibada na kanuni za kisheria.
Dini zote walizofikishiwa watu kupitia mitume tangu Nabii Adam mpaka Nabii Isa kimsingi zilikuwa sawa; ziliegemea katikakumwamini mungu mmoja, Allah; hata hivyo, zilibadilishwa baadaye na asili zake zikapotea. Allah alimtuma mtume wake wa mwisho na mtukufu zaidi, Nabii Muhammad (s.a.w), kuwa ni mtume wa watu wote. Alituma dini ya kweli ya mwisho na kamilifu, Uislamu, kwa watu kupitia kwa Nabii Muhammad (s.a.w). Kwa sasa, dini pekee ya kweli iliyopo na itakayoendelea kuwepo mpaka Siku ya Kiama ni dini ya Uislamu.
Pili ni dini ambazo asili zake zmrvurugwa na kubadilishwa. Kama ilivyoelezwa hapo juu, mwanzo zilikuwa dini ya kweli isipokuwa zilibadilishwa baadaye na kupoteza sifa zake za kiungu; mathalani, Ukristo na Uyahudi. Hizo sio tena dini ya kweli kwa sababu baadhi ya kanuni zake zimebadilshwa.
Tatu ni dini potovu. Hizo ni dini ambazo asili zake haziuniani na dini ya kweli. Ni dini zilizobuniwa na baadhi ya mataifa. Zinaweza kuwa na baadhi ya hukumu zinazofaa isipokuwa hizo si dini za kiungu kwa upande wa asili zao; kwa hivyo, hazina sifa tukufu. Dini za mataifa yanayoabudu moto, nyota na masanamu ni mfano wa dini hizo.
7
Kama Allah angetaka, angepeleka dini moja tu; kwa nini aliachilia ziwe dini tatu tofauti?
Neno Uislamu hutumika katika ufahamu wa namna nyingi. Hata hivyo, jina mahususi la dini aliyotumwa kuileta Mtume Muhammad (s.a.w) pia ni Uislamu. Kwa hivyo, jina la dini alitumwa Mtume wetu na aliyotumwa Ibrahim ni tofauti. Dini hizi zina majina tofauti lakini mambo yake ni ya namna moja. Hata hivyo, kuna tofauti katika yaliyomo.
Mitume wote, tangu Adam mpaka Muhammad (s.a.w), waliwafikishia watu dini ya kweli. Kanuni za imani, ambazo ni misingi ya dini, mara zote zilibakia zilezile a namna moja. Hata hivyo, masuala ya kiibada na mambo ya kidunia, tunayoyaita shari’ah, na baadhi ya hukumu zilibadilika kwa kuzingatia mahitaji muhimu ya kilakipindi na watu kuanzia kwa Adam mpaka kwa Muhammad (s.a.w). Allah Mtukuka alittuma shari’ah tofauti kwa kila ummah kwa kuzingtattia mitindo ya kimaisha na matakwa ya watu wa kila enzi. Yafuatayo yameeleza katika aya ya 48 ya sura al-Maida:
“…Kila mmoja katika nyinyi tumemwekea sharia yake na njia yake...”
Mathalani, Wayahudi waliabudu katika masinagogi tu na Wakristo makanisani tu; hata hivyo, sisi, Waislamu, tunaweza kufanya ibada popote. Shahamu ya ng’ombe na kondoo iliharamishwa katika shari’ah ya Musa lakini ni halali katika dini yetu.
Suala hili limeelezwa kama ifuatavyo katika Mkusanyiko wa Risale-i Nur:
“Sheria takatifu zunabadilika kwa mujibu wa enzi mbalimbali. Kwa hakika, katika enzi moja huenda kukawa na Mitume zaidi ya mmoja, na hayo yalitokea. Kwa kuwa baada ya Muhuri wa Mitume, Shari'a yake tukufu inatosha kwa watu wote katika kila enzi, hakuna haja tena ya kuwa na Sheria tofauti. Hata hivyo, kwa mambo mengine baada ya hapo, haja ya madhehebu imebakia kwa kiasi.” (Sözler (Maneno), uk. 485)
“Mengi katika hayo yana manufaa kwa wakati fulani na kuleta madhara katika wakati mwingine, na dawa nyingi zilimfaa binadamu wakati wa utotoni na zikaacha kumponya katika wakati wa ujana. Hii ndio sababu Qur’an ilifuta baadhi ya matamko yake ya baadaye. Yaani, ilipitishwa hukumu kuwa wakati wake umekwisha na kwamba umewadia wakati wa hukumu zingine.” (İşarât-ül İ’caz (Alama za Kimiujiza), uk. 50)
Hukumu kuu ni zie zile kwa mitume wote; hazibadliki na wala hazifutwi. Mathalani, kanuni za imani ni zilezile kwa dini zote za kimbinguni, na ibada ipokatikazote hizo. Hata hivyo, kuna tofauti chache katika hukumu za upili (undani) za ibada. Kulikuwa na mabadiliko katikahukumu kama muundo na nyakati za swala na mwelekeo wa qiblah.
Kwa kuwa jina la dini ya wafuasi wa vitabu hivyo halikutajwa katika vitabu vya kiungu isipokuwa Quran na kwa kuwa majina ya Uyahudi na Ukristo yalitungwa baadaye na kwa kuwa wafuasi wa mitume hao waliitwa hivyo baadaye, tunadhani kuwa maana ya ibara “dini mbele ya Allah ni Uislamu (kujisalimisha Kwake)” katika Quran inafahamika vyema. Dini ambayo Mtume Muhammad (s.a.w) aliwafikishia watu ina amri za kipekee isipokuwa ukweli unaotiliwa mkazo katika Quran kuwa kitabu hiki pia kinathibitisha walicholeta mitume waliotangulia inaonesha kuwa walichofikisha kwa ujumla kilikuwa katika Uislamu isipokuwa, kutokana na hekima ya kiungu, muundokamilifu wa mafunzo hayo ulipatikana pindi alipotumwa Muhammad (s.a.w) kama mtume. Kisha, njia pekee ya kupata radhi za Allah ni kuamini yote aliyotuletea.
8
Kwanini dini zingine zisizokuwa Uislamu hazizingatiwi kuwa ni halali?
Allah, ambaye aliwatuma mitume na dini tofauti kwa wanaadamu katika enzi mbalimbali katika historia, aliuleta Uislamu uwe dini ya mwisho na Nabii Muhammad (s.a.w) awe mtume wa mwisho. Kwa kuja Uislamu, uhalali wa dini zilizotangulia kama Uyahudi na Ukristo ulifikia tamati.
Hiyo inalingana na hali ifuatayo: sheria mpya inapotungwa, iliyotangulia inakuwa haifai. Dini na sheria ya Allah ilipoletwa, uhalali wa dini na sheria zilizotangulia za Allah umefikia tamati.
Sababu kuu zinazolazimisha dini zingine zizingatiwe kuwa si halali ni kama ifuatavyo:
1- Awali ya yote, dini zilizotangulia ziliwahutubia watu mahususi wa enzi mahususi. Kwa upande mwingine, Uislamu unawahutubia watu wote. Ujumbe wake ni wa jumla na wa wote.
2- Dini zilizotangulia ziliwahutubia watu waliokuwa hai tu katika kipindi zilipoletwa. Sifa za watu waliokuwa wakiishi katika nyakati hizo zilikuwa za kifidhuli na tabia zao zilikuwa za kishenzi. Hawakuwa na maendeleo kwa upande wa sayansi, ustaarabu, fikra na ufahamu. Njia za usafiri na mawasiliano zilikuwa duni sana. Tamaduni, imani na desturi za kila sehemu na sehemu zilitofautiana. Kubadilishana fikra na tamaduni kulikuwa dhaifu sana.
Kwa hiyo, ikawa ni lazima kutuma mitume tofauti na dini tofauti kwenda katika sehemu tofauti. Muda ulivyosonga mbele na wanaadamu kupata maendeleo katika sayansi, fikra, utamaduni na ustaarabu, dini zilizotangulia za wenyeji zilibakia nyuma na zikashindwa kutimiza haja za watu. Kwa sababu hiyo, Mwenyezi Mungu Mtukuka aliuleta Uislamu, dini ya mwisho, kwa wanaadamu.
Dini ya Uislamu ina rasilimali ya kuweza kumwambia kila mmoja, tokea watu wa miaka 1400 iliyopita, mpaka watu wa leo na watu wa baadaye. Kwa hiyo, uhalali wake ni wa kudumu na hautaisha mpaka Siku ya Kiama.
3- Muda ulivyozidi kusonga mbele, imani za kishirikina na potovu zilipenya na kuingia katika dini zilizotangulia. Kanuni ya kuamini u-moja wa Allah, yaani, imani ya tawhid, ilipotea. Uislamu bado unaendelea kuwepo huku ukiwa na upya wake na usafi bila ya badiliko lolote.
Kwa kuhitimisha, tunaweza kusema yafuatayo:
Dini zisizokuwa Uislamu ni kama taa za kandili zinazoangaza mtaa. Uislamu ni kama jua linaloangaza dunia nzima.
Je, kuna haja yoyote ya kuwepo taa ya mtaani linapochomoza jua?
Je, kufaa (uhalali) kwa taa ya mtaani kunaweza kuwepo pindi linapokuwepo jua?