Ni upi umuhimu wa Quran; unaweza kutoa maelezo gani kuhusu Quran?

The Answer

Dear Brother / Sister,

Quran ni kitabu kitukufu cha mwisho ambacho Allah aliwateremshia watu. Quran iliteremshwa kwa Mtume Muhammad (s.a.w) kupitia kwa Jibril na ikafika leo kwa njia ya kuandikwa na kusimuliwa.

Quran ni mwongozo wa kiyakinifu na kiroho kwa mtu mmoja mmoja na jumuia, matabaka yote ya watu wanaoishi mahali popote au wakati wowote na kwa maisha yote ya mwanadamu. Kila mtu, kuanzia rais mpaka mtu wa mtaani, anapata yanayowahusu wao katika Quran. Wanachukua elimu na mafunzo yaliyo muhimu kwa ajili ya amani na utulivu duniani na ahera. 

Ubora na sifa za Quran zimeelezwa kama ifuatavyo katika aya nyingi na hadithi:

* “Na hichi ni Kitabu tulicho kiteremsha, kilicho barikiwa. Basi kifuateni, na mcheni mungu, ili mrehemewe." (Al-Anam, 6/155).

* " Na hiki ni Kitabu tulicho kiteremsha, kilicho barikiwa, chenye kuhakikisha yaliyo tangulia, na ili uuwonye Mama wa Miji na walio pembezoni mwake. Na wenye kuamini Akhera wanakiamini hichi, nao wanazihifadhi Sala zao." (Al-Anam, 6/92).

* “Hebu hawaizingatii hii Qur'ani? Na lau kuwa imetoka kwa asiye kuwa Mwenyezi Mungu bila ya shaka wangeli kuta ndani yake khitilafu nyingi." (An-Nisa, 4/82).

* “Qur’ani kuwa ni uwongofu kwa watu, na hoja zilizo wazi za uwongofu na upambanuzi...." (Al-Baqara, 2/185).

* "(Qur’an) ni uwongofu na bishara njema kwa Waumini." (Al-Baqara, 2/97).

* “Na hiki Kitabu, tumekuteremshia wewe, kimebarikiwa, ili wazizingatie Aya zake, na wawaidhike wenye akili." (Sad, 38/29).

* Masimulizi yafuatayo yamesimuliwa kutoka kwa Harith bin Awar: Wakati fulani, Swahaba Ali alisema:

"Nilimsikia Mjumbe wa Allah akisema:

' Tazama! Utatokea mfarakano.' Kwa sababu hiyo, nilimuuliza,

 ‘Ewe Mjumbe wa Allah! Ni ipi namna ya kuondokana nao?' Alisema,

'Ni kutii kitabu kitukufu cha Allah.' (Kisha Mtume akaeleza sifa bainifu za Quran kama ifuatavyo:

'Ina maelezo yote kuhusu kilichowakuta jamii za kabla yenu, habari za mifarakano na misukosuko itakayokutokeeni na dalili za Siku ya Kiama. Ni kipambanuzi baina ya ukweli na uwongo. Kama yeyote anatafuta uongofu mahali pengine Allah atamwacha apotee. Ni kamba imara ya Allah. Ni ukumbusho wenye hekima, na njia iliyonyooka. Inazilinda nyoyo zinazoitii dhidi ya kuvurugwa na kupotoshwa na ndimi zenye kuisoma dhidi ya utata.

Wanazuoni wa Qur’an daima huwa wana shauku nayo. Kuisoma tena na tena kamwe hakumchoshi mwenye kuisoma; wala msomaji hapotezi ladha yoyote kwa kukariri kuisoma. Mastaajabu yake makubwa yaliyowashangaza watu hayataisha kamwe, " wakasema: Hakika sisi tumeisikia Qur'ani ya ajabu!" (Al-Jinn 1). Mwenye kuitamka, husema ukweli. Mwenye kutenda kulingana nayo, atalipwa. Mwenye kuhukumu kulingana nayo, atakuwa mwadilifu. Mwenye kuwaita watu kwenye Qur’an, atawaongoza kwenye njia iliyonyooka.'" (Tirmidhi, Thawabu"l-Qur'an 14, 2908)

* "Quran ni nuru ya waziwazi, dhikr yenye hekima na njia ya kweli."

* "Quran ni kamba ya Allah iliyorefushwa mpaka ardhini kutoka mbinguni."

* "Ubora wa Quran juu ya maneno mengine ni kama ubora wa ar-Rahman juu ya viumbe Wake."

* "Ikiwa mtu atasoma aya moja katika kitabu kitukufu cha Allah, itakuwa ni nuru inayomwangazia katika Siku ya Kiama."

* "Zitieni nuru nyumba zenu kwa kuswali na kusoma Quran."

Quran ilitremshwa moyoni mwa Mtume (s.a.w) kwa hali zote, maana na maneno yake pia. Hiyo ndiyo sababu, Quran inaitwa wahy al-matluww (ufunuo unaosomwa). Kwa hiyo, Quran si maana yake tu, bali ni pamoja na maneno pia. Quran haikuteremshwa yote kwa Mtume (s.a.w) kwa mara moja; ilikuwa ikiteremshwa aya baada ya aya na sura baada ya sura.

Muujiza wa Quran

Quran ina namna zote za kanuni za imani, amali na maadili yatakayomfanya mwanadamu apate furaha kamili ya halisi. Ni muujiza mkubwa wa kifasihi kwa upande wa maneno na maana. Mtume (s.a.w) amesema yafuatayo kuhusu jambo hilo:

"Kila Mtume alipewa miujiza iliyowafanya watu waamini, lakini nilichopewa mimi, ni Msukumo wa Kiungu alionifunulia Allah. Kwa hivyo ninatumaini kuwa idadi ya wafuasi wangu itawazidi wafuasi wa Mitume wengine katika Siku ya Kufufuliwa." (Bukhari, Fadhailu'l-Qur'an, 1)

Kwa hakika, miujiza ya mitume wengine iliisha baada ya kuisha muda wao. Muujiza wa Quran utaendelea kuwepo mpaka Siku ya Kiama. Katika aya kadhaa za Quran, kumeelezwa kwa msisitizo kuwa Quran ni muujiza:

“Sema: Wangeli kusanyika watu na majini ili walete mfano wa hii Qur'ani basi hawaleti mfano wake, hata wakisaidiana wao kwa wao...." (al-Isra, 17/88).

Kwa hakika, hakuna aliyeweza wala atakayeweza kuleta aya moja inayofanana na aya za Quran kwa mtindo na ufasaha. Quran ni muujiza kwa kulingana maneno yake na maana yake. Mtume (s.a.w) hakuwa mwenye kusoma na kuandika. Hakujifundisha chochote kutoka kwa yeyote. Kwa hiyo, alizingatiwa kuwa asiyejua kusoma na kuandika. Hata hivyo, kitabu kitukufu alichokuja nacho kilikuwa na ukweli wa hali ya juu na kilifahamisha mengi ya ukweli wa kisayansi ambayo sayansi na uzoefu viliweza kuyapata katika miaka elfu moja na mia nne iliyopita. Hili linathibitisha kuwa Quran ni neno la Allah moja kwa moja. Mathalani, ukweli kuwa jua linazunguka lenyewe na linakwenda katika kituo maalumu kilichopangwa pamoja na sayari zingine zinazolitegemea, kufunguka mapiramidi na miili ya maiti za Mafarao zilizohifadhiwa kwa dawa zimegunduliwa katika karne iliyopita.

Hata hivyo, Quran ilitueleza kuhusu hayo na mengine kama hayo katika karne nyingi zilizopita. Haijalishi sayansi inaendeleaje, haiwezi kuipinga Quran. Hata hivyo, maendeleo ya sayansi yataleta urahisi kwa Quran kufasiriwa na kuelezwa. Kama Badiuzzaman Said Nursi anavyoliweka wazi hilo,

"Kadiri muda unavyozidi kusogea, Quran inazidi upya; ukweli mwingi iliyo nao unadhihirika zaidi."

Kipengele kingine cha kimiujiza cha Quran ni kuwa imebashiri matukio mengi yaliyotokea baadaye. Chochote ilichobashiri kilitokea sawa na kilivyobashiriwa.

Baadhi ya fafanuzi na maelezo ya Quran ni kama ifuatavyo:

- Qur'an Yenye Hekima Nyingi, inayomfahamisha kwetu Mwenye kuturuzuku, ni mfasiri wa milele wa Kitabu kikuu cha ulimwengu... 

Ulimwengu umelinganishwa na kitabu kikuu kilichoandikwa kwa kalamu ya uwezo. Katika kitabu kidogo, ibara inayosema ishara za uumbwaji (ayat at-takwiniyya) imetumika kwa ajili ya viumbe duniani. Ishara ya uumbwaji inamaanisha kilichoumbwa kutokana na amri "kuwa" (kun), inayoonesha uwepo, upweke, majina na sifa za Allah na kinachokuwa ushahidi juu ya hayo. Aya (ishara) zilizo katika Quran zinatokana na sifa za Allah zinazoitwa kauli na ishara za ulimwenguni zinatokana na sifa Zake zinazoitwa uwezo (qudrah). 

Kitabu hiki cha ulimwengu hufanya Allah atambulike pamoja na ishara zake zote lakini wanadamu hawajaweza kukisoma na kukitathmini kwa usahihi. Yaani, hawakufahamu lugha ya kitabu kitukufu. Quran Yenye Hekima Nyingi imekitafsiri kitabu kitukufu cha ulimwengu, imewajulisha wanadamu kuhusu kitabu hicho na kueleza sifa za Mola wetu Mlezi, ambaye ndiye mwandishi wa kitabu hicho, kwetu. Kimetueleza kuhusu sifa Zake, majina na amali.

- kidhihirisho cha hazina za Majina ya Kiungu zilizofichwa katika kurasa za ardhi na mbingu...

Maana zilizofichwa, zimesitiriwa, ambazo zimekuwa hazionekani na hazijulikani. Tunaishukuru Quran, kwa kutafsiri kitabu kitukufu cha ulimwengu, udhihirishaji wa majina ya Allah yaliyokuwa yamefichikana duniani na mbinguni yameanza kuweza kusomwa. Katika sentensi hii, majina ya Allah yamefananishwa na hazina. Mathalani, jina al-Khaliq (Mumbaji) ni a hazina; viumbe wote ni kama vito vya hazina hiyo. Jina al-Muhyi (Mwenye Kuhuisha) ni hazina nyingine; uhai wote unatoka kwenye hazina hiyo.

- ufunguo wa kuyaendea ya kweli yaliyofichikana upo chini ya mistari hiyo ya matukio...

Katika kitabu hiki cha ulimwengu, kila jambo, kama vile kila kiumbe, ni kama neno au mstari. Ni muhimu kuyasoma kwa usahihi. Ukweli uliofichikana chini ya mambo unaweza kusomwa kwa usahihi kwa kutumia uongofu na maelekezo ya Quran tu.

Usiku na mchana, afya na maradhi, furaha na huzuni, uzee na umauti ni katika ya kweli iliyoandikwa katika kitabu hicho. Miongoni mwa matukio muhimu zaidi kwa watu ni kifo. Wanaozingatia kifo kuwa ni "kuto-kuwa, kuto-kuwepo, kuingia kaburini na kupotea hawawezi kufahamu ukweli wa kifo na kutathmini vibaya tukio hilo. Ukweli wa kifo unafahamika kwa uongofu wa Quran. Maana ya kuzaliwa ni kuja duniani kutokea katika jeraha; halikadhalika, kifo kinamaanisha kwenda katika ulimwengu wa barzakh kutoka duniani. Kisha, kuzaliwa kwingine kunakoitwa ba'th kutafuatia; watu watakwenda katika mahali pa Kukusanywa kutoka katika ulimwengu wa kaburi kupitia humo.

Kuna maelezo ya kina zaidi kuhusu ukweli wa kifo katika Mkusanyiko wa Risale-i Nur. Hebu tukumbuke baadhi yake: Kifo ni “kubadilisha makazi, kupumzika kutoka katika wajibu, roho kupewa uhuru”. Kaburi ni “mlango wa kuingia katika ulimwengu ulio bora zaidi ya dunia hii.”

- hazina ya fadhila za Mwingi wa Rehema na hotuba za milele, zinazotoka katika Dunia ya Ghaibu nyuma ya pazia la Dunia Bayana...

Ibara inayosema dunia ya ghaibu iliyotajwa hapo juu inaweza kufahamika kuwa ni kiti kikubwa cha enzi ambapo ulimwengu huu wenye kuonekana unadhibitiwa na kutawaliwa, kama ulimwengu wa tashbihi ambapo hupigwa mifano ya kila kitu, na kama ulimwengu usiojulikana kama Ubao Uliohifadhiwa (Lawh al-Mahfudh) ambapo kila kitu kimeandikwa na kuhifadhiwa.

Maneno fadhila na hotuba yanakamilishana yenyewe na kuashiria kwenye lengo lile lile moja. Kuhutubiwa na Allah Mtukufu ni fadhila kubwa kwa waja Wake. Kujulishwa kuhusu amri Zake na makatazo Yake, kupata radhi Zake, na kuoneshwa njia za kwenda Peponi ni rehema kubwa na zawadi ya Allah.

- jua, msingi, na mpango wa dunia ya kiroho ya Uislamu...

Chanzo cha mazuri yote, fadhila, manufaa na maadili ya juu, imani ya kimsingi, ni jua la Quran. Msingi wa dini yetu ni ukweli mwingi wa Quran. Jengo la uongofu na uthabiti litakaoendelea daima limejengwa na hadithi, ambazo ndizo fasiri za mwanzo za Quran, juu ya msingi huu.   

Neno mpango linaweza kutafsiriwa kuwa ni ijtihad na fatwa zilizotokana na nuru ya Quran na hadithi ili kujibu mahitaji mapya yanayoibuka katika jengo linalokua la Uislamu.

- na ramani ya dunia za ahera...

Katika Quran, ramani ya barabara ya maisha ya ahera inayonzia katika Mahali pa Kukusanywa na kuendelea kama vile “kusimama, mizani (Mizan), daraja (Sirat) na Pepo au Jahanamu" umechorwa; sura nzuri za Peponi na adhabu za Jahanamu pia zimeoneshwa kwa mwanadamu kama picha.

- kifasili cha kipekee, ufafanuzi halali, ushahidi wa kueleweka, na mfasiri dhahiri wa Dhati ya Kiungu, sifa, na amali...

Chanzo pekee cha maelezo mazuri kuhusu dhati, sifa, na amali za Allah ni Quran. Akili na fikra za kibinadamu haziwezi kufanya chochote kuhusu ukweli huo mwingi usiojulikana na wa milele. Kwa kuwa Allah anajitambulisha Mwenyewe katika Quran, Hakuna haja ya ukisiaji usio na msingi maalumu wa mwanadamu na fikra zisizofaa.  

Tunajifundisha kutokana na aya za Quran na wanazuoni wetu walioidhinishwa ukweli ufuatao na yaliyo kama hayo: “Kuwepo kwa Allah ni lazima; Yeye hana mwanzo wala Hana mwisho; Hahitaji wakati wala nafasi; Ana sifa zisizo na ukomo; hakuna mabadiliko wala upungufu utakaojitokeza katika sifa hizo bila ya kujalisha idadi ya viumbe Anaowaumba; Kuwepo Kwake na sifa, rehema Zake na ghadhabu, neema zake na wivu na matendo Yake mengine yote hayawezi kulinganishwa na hali na uwezo wa viumbe Wake.

Viumbe wa ulimwenguni wanatangaza kuwepo kwa Allah na sifa Zake kwa hali zao lakini watu kwa ujumla hupuuza misemo hiyo ya kiroho au kutokuifahamu. Kwa hiyo, burhan an-natiq (ushahidi wenye kueleweka) ni muhimu.  (Pindi ibara burhan an-natiq inapotumika kwa ajili ya Mjumbe wa Allah (s.a.w), inamaanisha anayefikisha ujumbe wa Quran kwa watu.)   

Ibara inayosema mfasiri dhahiri inamaanisha Quran inawatafsiria watu maneno ya kitabu kitukufu cha ulimwengu yale wasiyoyafahamu; ina maana inayolingana na ibara inayosema ushahidi wenye kueleweka.

mwalimu, hekima ya kweli, mwelekezaji, na kiongozi wa dunia ya utu...

Quran ilishushwa ili kuzifundisha roho za watu, kuzikamilisha nyoyo zao kwa njia ya imani na akili zao kupitia sayansi na elimu, kuwafundisha hekima ya kweli, kuwatoa watu kutoka katika njia potovu na kuwaonesha njia ya uongofu. Hekima ya kweli, yaani, habari sahihi kuhusu lengo la kuumbwa wanadamu na viumbe wengine na majukumu yao linaweza kufundishwa kutoka katika Quran kwa sababu aya za Quran ni maneno ya Muumbaji aliyewaumba viumbe hao. 

Kama inavyojulikana, neno "hekima" pia hutumika kwa ajili hekima. Kivumishi "-a kweli" kilichotumika hapa kinaashiria kuwa falsafa si hekima ya kweli. 

Hekima ina fafanuzi kadhaa. Mojawapo ni "amali pamoja na elimu" (mtu kufanya anayoyajua na anayojifundisha) Yaani, kama fikra inayomfanya mtu afanye amali njema, ina hekima. Fikra zinazozungumzwa tu lakini hazifanywi kwa vitendo ni fikra binafsi; haziwezi kuwa njia ya uongofu kwa ajili ya watu. 

ni kitabu cha yote mawili hekima na sheria, na kitabu cha swala na ibada, na kitabu cha amri na mawaidha, na kitabu cha maombi na elimu ya Kiungu - ni kitabu kwa ajili ya mahitaji yote ya kiroho; nacho ni maktaba tukufu inayotoa vitabu vinavyofaa katika njia za watawa wote na wasema kweli, watakatifu na wanazuoni, ambao njia zao zote ni tofauti...

Quran ni kitabu cha hekima kwa sababu kinamfundisha mwanadamu lengo na mambo ya wajibu kwa viumbe wote; ni kitabu cha shari'ah (sheria) kwa sababu kinamjulisha mwanadamu kuhusu amri na makatazo kuhusu maisha ya mtu mmoja mmoja na ya kijamii.

Pia ina "swala, ibada, amri na miito", ambayo ni misingi ya shrai'ah, pamoja na vipengele vyote.

Quran ni kitabu cha dhikr inayomfanya mwanadamu apate angalau thawabu kumi kwa herufi yake moja anapoisoma; pia ni kitabu cha elimu ambapo kinamtambulisha Allah pamoja na majina Yake na sifa Zake.

Misingi ya njia zote za kweli ipo katika Quran. Kila mti wa matunda unatambua matunda mbalimbali kwa kuzingatia maumbo yao ulimwenguni; halikadhalika, kila mwanazuoni wa tafsiri hutambua maana mbalimbali katika Quran, anapata milango ya elimu mbalimbali, anafunuliwa udhihirisho wa majina tofauti ya Allah na inaleta njia tofauti ya uongofu. Kwa kipengele hiki, Quran inakuwa kama maktaba ingawa ni kitabu kimoja. (angalia Badiuzzaman Said Nursi, Sözler (Maneno) , Yirmi Beşinci Söz (Neno la Ishirini na Tano).

Maswali juu ya Uislamu

Author:
Maswali juu ya Uislamu
Subject Categories:
Read 1.805 times
In order to make a comment, please login or register
MASWALI YENYE KUFANANA