Kuna tofauti gani kati ya Qur’an na vitabu vingine vya kiungu?
Dear Brother / Sister,
Katika vitabu vya kiungu kwa sasa hakuna kilicho katika katika nakala ya asili ile waliyoteremshiwa Mitume wa Allah, isipokuwa Qur’an iliyo. Nakala za asili za vitabu hivyo zimepotea katika nyakati balimbali na zikaandikwa upya na wanadamu. Hivyo, vipengele vya ushirikina viliingizwa. Mathalani, Taurati haikuweza kuhifadhiwa na Wayahudi kwa sababu walikamatwa mateka na wakaishi uhamishoni kwa muda mrefu baada ya Nabii Musa (AS) na hata walifuata upagani kwa kupoteza imani yao; na pamoja na ukweli huo wa kihistoria, nakala iliyopo sasa ya Taurati iliandikwa na baadhi ya watu wa dini kwa muda mrefu baada ya Nabii Musa na kikakubalika kuwa ni kitabu cha kidini kama ilivyokuwa nakala ya mwanzo. Ni dhahiri kuwa Taurati haiwezi kuwa nakala ile ile aliyoteremshiwa Nabii Musa (AS) baada ya kipindi hicho kirefu chenye utata. Kwa hivyo, ina baadhi ya madai na kashfa zisizoweza kusemwa na mitume na kuna hukumu zilizo kinyume na dini ya upwekeshaji.
Zaburi ya Nabii Dawud pia ilipatwa na yale yale yaliyopatwa na Taurati.
Ama kuhusu Biblia, Nabii Isa (Yesu) hakutoa mwanya wa kuandikwa wahyi. Kwa kuwa, alipata utume alipokuwa na umri wa miaka thelathini na kazi ya utume iliisha alipofikisha umri wa miaka thelathini na tatu. Alijitahidi kuonesha njia ya kweli kwa muda mfupi sana wa miaka mitatu kwa kwenda kijiji hadi kijiji kingine na mji mmoja hadi mwingine. Kuelekea mwishoni, kila mara alikuwa akifukuzwa na watawala wa Kirumi kutokana na uchochezi wa Wayahudi. Kwa hivyo, hakuweza kupata muda au fursa ya kuandikwa Biblia. Kwa hivyo, Biblia zilizopo leo zimeitwa kwa majina ya watu walioziandika na zina hotuba, mafunzo na uongofu wa Yesu (AS) na zinaonekana kama tawasifu yake. Licha ya hivyo, hazikuandikwa na wafuasi wa mwanzo wa Yesu (AS) na waumini wake bali watu waliowaona wafuasi wa Yesu (AS); kwa hivyo walikuwa ni wasikilizaji.
Zipo tofauti baina ya Biblia zilizopo, kwa upande wa maudhui na usimulizi. Kwa hakika, Biblia hizo zilikubaliwa na baraza la kiroho lililokutana mnamo mwaka 325 BK huko Nicaea. Baraza hilo lilichunguza mamia ya Biblia na kukubali Biblia nne, zilizotamka fikra ya kipengele cha uungu wa Yesu, kwa muwafaka wa wajumbe 318 kwa kuziharibu Biblia zingine zilizosalia.
Kama ilivyoonekana, hekima ya dhana ya Yesu ya kuwa mwana wa Mungu ilikubaliwa na baraza baada ya Yesu kuondoka.
Kwa hakika, baadhi ya makanisa ya Kikristo hayakukubaliana na uamuzi huu. Hivyo, haiwezekani kusema kuwa Biblia nne zilizopo sasa zinalingana na Biblia aliyoteremshiwa Yesu (AS).
Maswali juu ya Uislamu
