Ikoje Taswira ya Quran kwa watu wa kitabu kitukufu (Wayahudi na Wakristo)?

The Answer

Dear Brother / Sister,

Dini ya Kiislamu haioni kuwa washirikina (wanaomshirikisha Allah) wako sawa na watu wa kitabu kitukufu, ambao ni Wakristo na Wayahudi. Katika Surah Al-Maidah, Allah (SWT) anatangaza, Na chakula cha walio pewa Kitabu ni halali kwenu, na chakula chenu ni halali kwao. (Al-Maidah Surah, 5:5). Kunaweza kuwepo kufungamana nao kiuchumi na kibiashara. Sehemu ifuatayo ya aya inasomeka kuwa baadhi ya Waislamu wanaume wanaweza kuwaoa wanawake mabikra kutoka kwa watu wa kitabu kitukufu. Lakini Muislamu haruhusiwi kumwoa mshirikina.

Tunaona kuwa inafaa kuzionesha aya hizi za Qur’an zinazowahusu watu wa kitabu kitukufu:

Sema: “Enyi Watu wa Kitabu! Njooni kwenye neno lililo sawa baina yetu na nyinyi: Ya kwamba tusimuabudu yeyote ila Mwenyezi Mungu, wala tusimshirikishe na chochote; wala tusifanyane sisi kwa sisi kuwa Waola Walezi badala ya Mwenyezi Mungu.” (Al-i-Imran Surah, 3:64)

Wala msijadiliane na Watu wa Kitabu ila kwa njia iliyo nzuri kabisa, isipo kuwa wale walio dhulumu miongoni mwao. Na semeni: "Tumeyaamini yaliyo teremshwa kwetu na yaliyo teremshwa kwenu. Na Mungu wetu na Mungu wenu ni Mmoja. Na sisi ni wenye kusilimu kwake." (Al-Ankabut Surah, 29:46)

Hakika utawakuta walio shadidi kuliko watu wote katika uadui kwa walio amini ni Mayahudi na washirikina. Na utawakuta walio karibu mno kwa mapenzi ni wale wanao sema: “Sisi ni Manasara.” (Al-Maidah Surah, 5:82)

Maswali juu ya Uislamu

Author:
Maswali juu ya Uislamu
Subject Categories:
Read 237 times
In order to make a comment, please login or register
MASWALI YENYE KUFANANA