Ni ipi miujiza ya Qur’an? Unaweza kutupa mifano?

The Answer

Dear Brother / Sister,

Kila aya ya Qur’an ni muujiza. Kwahiyo haiwezekani kuelezea miujiza yote iliyomo katika Qur’an hapa. Baadhi ya miujiza hiyo ni kama ifuatayo:

1- Katika aya “Mwenyezi Mungu ndie aliye ziinua mbingu mnazo ziona bila ya nguzo” (ar-Ra’d, 2) inapinga dhana potofu kwamba mbingu zimeeinuliwa kutokana na uwepo wa milima

2- Uumbaji wa ulimwengu unaelezwa kama ifuatavyo katika Qur’an: “Yeye ndiye Muumbaji wa mbingu na ardhi bila ya ruwaza” (al-An’am, 101). Aya hii inatueleza ukweli juu ya uumbaji wa ulimwengu miaka 1400 iliyopita, kutokana na mapitio ya muda na mahala, ikafanyika dunia kutokana na mripuko unaojulikana kama big bang, ambayo ndiyo nukta ya mwisho iliyofikiwa na Sayansi leo.

3- Ukweli kwamba dunia inatanuka kila uchao ni matokeo ya uvumbuzi kisayansi ambao ulimwengu wa sayansi unakubali sasa. Qur’an inalionesha jambo hilo kwa aya ifuatayo: “Na mbingu tumezifanya kwa nguvu na uwezo na hakika Sisi bila ya shaka ndio wenye uwezo wa kuzitanua.” (adh-Dhariyat, 47)

4- Uvumbuzi mwengine katika karne ya 20 ni kwamba kila nyota na kila kilicho mbinguni kinatembea katika njia yake inayojulikana kama ‘orbit’. Qur’an inalieleza jambo hili kama ifuatavyo: “Na Yeye ndiye aliye umba usiku na mchana na jua na mwezi, vyote katika anga vinaogelea (katika njia zake maalum).” (al-Anbiya, 33) 

5- Zamani, ilifikiriwa kwamba jua halizunguki. Ingawa Qur’an inaeleza kwamba jua halijasimama; kinyume chake, inaeleza kuwa jua ni ni kati ya maumbo ya mbinguni ambalo hutembea kwa kasi maalumu. Sayansi imeyathibitisha yaliyoelezwa na Qur’an baada ya karne nyingi. Aya inayohusiana na hilo ni hii: “Na jua linakwenda kwa kiwango chake. Hayo ni makadirio ya Mwenye nguvu, Mwenye kujua.” (Ya Sin, 38)

Miujiza ya kijiolojia ndani ya Qur’an:

Kupungua kwa kiwango cha ardhi:

Allah anatufahamisha baadhi ya siri zake katika uumbaji ndani ya Qur’an ambayo aliiteremsha karne 14 zilizopita. Siri hizo zinathibitisha yote mawili kuwa Qur’an ni neno la Allah na inatoa mwanga kwa maendeleo ya sayansi za kimaumbile.

“Je! Hawakuona kwamba tunaifikia ardhi tukiipunguza nchani mwake?...” (Ar-Raad, 41)

 “…. Je, hawaoni ya kwamba Sisi tunaifikia ardhi tukiipunguza ncha zake?...” (al-Anbiyaa, 44)

Kutokana na ongezeko la joto duniani ‘global warming’, tabaka la barafu katika ncha za dunia zinayeyuka na kiwango cha bahari kinaongezeka. Kiwango cha maji kinachobaki hufunika eneo la ardhi. Kwa kadri fukwe za bahari zinavyofunikwa na maji, kiwango cha ardhi kinapungua. (Dr. Mazhar U. Kazi, 130 Miujiza dhahiri ndani ya Qur’an, Crescent Publishing House, New York, USA, 1998, s. 115). Inawezekana kabisa maneno yanayosema “Sisi tunaifikia ardhi tukiipunguza ncha zake “ yaliyotajwa katika Qur’an yanataja jinsi fukwe za bahari zinavyofunikwa na maji.

Habari inayohusu hilo iliyochapishwa kwenye gazeti la New York Times iko kama ifuatavyo:

Katika karne iliyopita, kiwango cha hali joto cha dunia kimeongezeka kwa kiwango cha nyuzi joto 1, na kiwango cha joto kimeongezeka kwenye robo ya mwisho ya karne iliyopita. Wanasayansi walilinganisha takwimu kutoka uchunguzi uliofanywa kupitia nyambizi (submarines) kati ya miaka ya 1950 na 60 pamoja na uchunguzi uliofanywa miaka ya 90, unaoonesha kuwa tabaka la theluji (barafu) kwenye ukanda wote wa Arctic umeliwa kwa asilimia 45. Picha za satalaiti zimeonesha kuwa kiwango cha tabaka la barafu kimepungua kwa kasi katika miaka ya hivi karibuni. (www.planetwaves.net/polar_NYT.html; New York Times, 19/08/2000)

Uvumbuzi uliofanywa mwishoni mwa karne ya 20 ulitusaidia kufahamu hekima ya aya ya 44 katika suratu Al-Anbiya na aya ya 41 katika suratu Ar-Rad.

Mgawanyo wa mabara

Dunia inatembea juu ya tabaka linalojulikana kama ‘mantle’, ambalo ni zito zaidi, kama ambavyo imeweza kuhimili dunia kuogelea juu yake. Mwanasayansi wa Kijerumani anaejulikana kwa jina la Alfred Wegener aligundua kwa mara ya kwanza kwamba mwanzoni mwa karne ya 20 mabara yote yalikuwa kitu kimoja mwanzoni kabisa na hatimae yakaparaganyika kwenye uelekeo tofauti na kila moja likamkimbia mwenzake.

Kwa takriban miaka milioni 500 iliyopita, mabara yote yalikuwa yameungana, na ardhi hiyo ilijulikana kwa jina la kitaalamu kama pangea ilipatikana ncha ya Kusini mwa dunia. Kwa takriban miaka 180 iliyopita, pangea ikagawanyika kwenye mapande mawili makubwa. Moja katika mapande hayo makubwa, yaliyogawika mabara mawili makubwa yalielekea sehemu tofauti, na kufanya Afrika Australia, Antarctica na India; na lile bara la pili likazaa, bara Ulaya, Amerika ya Kaskazini na bara la Asia isipokuwa India.

Ilikadiriwa kuwa utembeaji wa mabara ulikuwa ni tabkriban sentimita 1 hadi 5 kwa mwaka. Kwa kadri ambavyo tabaka zikitembea hivyo, kulitokea mabadiliko kwenye jiografia ya dunia. (nyaraka za Carolyn, Robert Gardner, Samuel F. Howe, General Science, Allyn na Bacon Inc.Newton, Massachusetts, 1985, uk. 305)

Allah ametaja utembeaji wa milima kama mpasuko wa mabara ‘drifting’. Neno la Kiingereza ambalo wanasayansi hulitumia kwa utumbeaji huo wa mabara ni “continental drift”

“Na unaiona milima unaidhania imetulia; nayo inakwenda kama mwendo wa mawingu.” (An-Naml, 88)

Ardhi imeundwa kwa tabaka saba:

Baadhi ya taarifa zinazotolewa na Allah katika Qur’an kuhusu dunia ni kwamba dunia ina tabaka saba sawa na mbingu: “Mwenyezi Mungu ni yule ambaye ameziumba mbingu saba, na ardhi kwa mfano wa hizo…” (at-Talaq, 12) Mola wetu ameelezea kwamba ardhi na mbingu zina tabaka saba saba. Ambapo matokeo ya sayansi kupitia tafiti zilizofanywa baada ya karne kadhaa zimegundua vile vile.  

Tabaka za dunia ambazo wanasayansi wameziorodhesha ni: Tabaka maji (Hydrosphere), Lithosphere, Asthenosphere, Mantle ya juu, Mantle ya chini, kiini cha nje (outer core) na kiini cha ndani (Inner Core):

Hysdrosphere inajumisha sehemu za juu za bahari na fukwe za ardhini zinazoathiriwa nazo. Lithosphere ni tabaka la mwamba mgumu ambao hufanya sehemu ya juu ya ardhi. Iikilinganishwa na tabaka zingine, ni jembamba, baridi na gumu zaidi; na kwa mantiki hiyo, hufanya kazi kama jabali la dunia.  

Chini ya Lithosphere, kuna tabaka linaloitwa Asthenopshere. Tabaka hili lina vitu ambavyo vina joto na ugumu wa kati na kati kiasi cha kuweza kuyayuka vinapopata joto kali, na mgandamizo. Inafikiriwa kuwa tabaka hilo gumu la Lithosphere huelea au kutembea juu ya tabaka lijulikano kama Asthenosphere, tabaka ambalo hutembea taratibu sana. Chini ya tabaka hili, kuna tabaka jengine ambalo lina miamba ambayo ina ugumu wa kati na kati na ni joto sana; na lina upana wa kilomita 2.900 ambalo hujulikana kwa jina la kitaaluma kama Mantle. Mantle, ambayo ina madini chuma, magnesium na calcium kuliko tabaka la crust, ni joto zaidi na zito kwasababu hali joto na mgandamizo kwenye ardhi huongezeka kwa kadri ya ongezeko la kina cha urefu.

Katikati ya dunia kuna tabaka jengine lijulikanalo kama Core, ambalo ni zito mara mbili zaidi ya Mantle. Kinachosababisha uzito huu ni ukweli kwamba lina madini chuma aina ya metals (mchanganyiko wa iron-nickel) tofauti na majabali. kiini cha ardhi lijulikanalo kama Core limeundwa na sehemu mbili tofauti. Moja ni sehemu ya nje ya maji maji ijulikanayo kama liquid outer core, yenye upana wa kilomita 2.200; ambapo jengine ni tabaka gumu lijulikanalo kama solid outer core, lenye upana wa kilomita 1.250. Kwa kadri dunia inavyozunguka, sehemu ya maji kuwa sehemu yenye mvutano wa sumaku wa dunia.  

Jambo la muhimu sana katika yote ni kwamba ukweli huu wa kisayansi ambao unaweza kujulikana kwa kutumia teknolojia tu ya karne ya 20 ulishaelezwa ndani ya Qur’an, ambapo ni mifano michache ya miujiza mingi ndani ya Qur’an.

Mpasuko wa ardhi:

“Naapa kwa mbingu yenye marejeo! Na kwa ardhi inayo pasuka!” (At-Tariq, 11-12)

Neno la kiarabu ‘sada’ limetajwa katika aya likimaanisha nyufa, kupasuka, kutengana n.k. Ukweli kwamba Allah anaapa juu ya kupasuka kwa ardhi ni muujiza mwengine ndani ya Qur’an.

Kwa mara ya kwanza wanasayansi mwaka 1945-46 walikwenda kwenye kina kikubwa chini ya bahari ili kutafiti rasilimali. Moja katika nukta za msingi za tafiti ilikuwa ni nyufa na mipasuko kwenye muundo wa ardhi. Tabaka la mwamba mgumu kwenye sura ya dunia ilikuwa na mwelekeo wa kaskazini-kusini na mashariki-magharibi na lilikuwa limefanya nyufa kwenye maeneo mengi kwa masafa ya maelfu ya kilomita. Shukrani kwa nyufa katika muundo wa ardhi, kiwango kikubwa cha joto kinapunguzwa na kiasi kikubwa cha miamba iliyoyeyuka inafanya vijimilima baharini. Lau kama dunia haikuwa na muundo ambao unaruhusu kiwango kikubwa cha joto kutolewa nje, maisha duniani yasingewezekana kwasababu, kwa hali kama hii, joto ambalo lisingepata sehemu nyengine ya kutokea chini ya ukonde wa ardhi ingesababisha kiasi kikukbwa cha athari hasi za nyuklia.

Maswali juu ya Uislamu

Author:
Maswali juu ya Uislamu
Subject Categories:
Read 1.210 times
In order to make a comment, please login or register
MASWALI YENYE KUFANANA