Jee Qur’an imetaja uvumbuzi wa zama za sasa? Unaweza kutoa mifano?
Dear Brother / Sister,
Elimu ya falaki (Astronomy)
Haijulikani kabisa jinsi umbo la kwanza la ulimwengu lilivyopatikana. Inaweza isijulikane milele. Ingawa kuna baadhi ya nadharia ambazo zinaweza kuwa na ukweli na misingi fulani ya uhakika. Maelezo kwenye Qur’an kuhusu jambo hili yanaeleweka vyema pamoja na nadharia hizi:
“Je! Hao walio kufuru hawakuona kwamba mbingu na ardhi zilikuwa zimeambatana, kisha Sisi tukazibabandua? Na tukajaalia kwa maji kila kilicho hai? Basi je, hawaamini? “ (al-Anbiya, 21/30)
“Kisha akazielekea mbingu, na zilikuwa moshi…” (Fussilat, 41/11)
Mtazamo wa ujumla ambao upo kwa wataalamu wa fizikia ya kifalaki ni sawa na msingi ulioelezwa kwenye aya hizo.
Kuna dalili mbali mbali kwamba dunia ni duara.
“Ameumba mbingu na ardhi kwa Haki. Hufunika usiku juu ya mchana, na hufunika mchana juu ya usiku…” (az-Zumar, 39/ 5)
Neno takwir (yukawwiru) “kuingiliana” limetajwa katika aya likimaanisha kufunika kitu kilicho katika umbo la duara; kwa mfano kuzungushia kilemba kwenye kichwa.
Kwa mujibu wa Mahmud as-Sawwaf, hakuna ushahidi wa wazi kuhusu ima kuzunguka au kuto kuzunguka kwa dunia kwenye Qur’an au Sunnah. Ingawa, zipo dalili zinazoonesha kwamba dunia inazunguka:
“Na unaiona milima unaidhania imetulia; nayo inakwenda kama mwendo wa mawingu…” (an-Naml, 27/88)
Anazizingatia aya za hapo juu kama ni aya zinazoonesha kuwa dunia inazunguka.
Fizikia (Physics)
Kwa kadri mtu anavyopaa kwenda juu mawinguni, kiwango cha hewa ya oxygen angani kinapungua na mgandamizo wa hewa hushuka kufikia kiwango cha degree moja kila baada ya mita 100; hivyo basi, hupunguza uwezekano wa kupumua, na tatizo la kuona, na kutokea kwa kuzimia. Mtu akipanda juu kwa mita 20 000, hawezi kupumua ikiwa hana kifaa maalumu; na hatimae, atakufa. Qur’an imeutaja ukweli huu kwenye aya ifauatayo:
“Basi yule ambaye Mwenyezi Mungu anataka kumhidi humfungulia kifua chake kwa Uislamu. Na anaye taka apotee hukifanya kifua chake kina dhiki, kimebana, kama kwamba anapanda mbinguni…” (al-An’am 125)
Jiolojia (Geology)
Sayansi ya miamba imethibitisha kwamba milima ina ujazo kwenda chini sawa na ule unaoonekana juu ya ardhi.
“Kwani hatukuifanya ardhi kama tandiko? Na milima kama vigingi?” (an-Naba’, 78/6-7)
Katika aya ya hapo juu, Qur’an imeifananisha milima na vigingi ambavyo nusu yake huchomekwa ardhini. Aya ifuatayo pia imeelezea:
“Na milima akaisimamisha” (an-Naziat, 79/32)
Aya ifuatayo inaonesha kwamba milima, inayoelea kwenye bahari ya atmosphere, inaweka uzani sawa wa dunia:
“(…) na Ameweka katika ardhi milima ili ardhi isikuyumbisheni…” (Luqman, 31/10)
Katika sayansi ya miamba, inafahamika kuwa milima ni jambo muhimu sana katika kanuni ya kuweka usawa ijulikanyo kama isostasy katika karne hii. Kwa mujibu wa geophysics, kuna mapande mazito ya milima takriban 110 yajulikanayo kama “hot spots”. Mapande hayo ni matope mazito makubwa ya mchanganyiko ujulikanao kwa jina la kitaalamu “basalt compound” ambao huituliza ardhi kama vile rivets; yanatoka chini kabisa ya ardhi kwenye tabaka lijulikanalo kama mantle, hupenya ardhini na kuifanya kuwa ngumu sehemu ya nje ya ardhi, ili kuzuia ardhi isitembee. Mnasaba uliopo baina ya kile kinachoelezwa na aya [ndani ya Qur’an] na kile kinachoelezwa na sayansi, ambacho ni kama tafsiri tu ya aya zinazoelezea uumbaji ambapo imetajwa wazi kabisa.
Botany
Sayansi ya mimea
Jambo la mbolea (fertilization) kwenye miti limejulikana kwa muda mrefu ila uhusiano uliopo baina ya upepo na utoaji mbolea (fertilization) haukujulikana hadi siku za hivi karibuni.
“…Na katika kila matunda akafanya dume na jike…” (ar-Ra’d, 13/3)
Baada ya ukweli ulioneshwa kwenye aya hapo juu kugunduliwa na ikaonekana kwamba miti yote ina chembe chembe za kiume na kike na kwahivyo basi matunda huzaliwa kama matokeo ya mbolea (fertilization) kati ya dume na jike, ikafahamika kwamba mbolea (fertilization) pamoja na pollination hufanywa na upepo.
Urithi (Genetics)
“Na pale Mola wako Mlezi alipo waleta katika wanaadamu kutoka migongoni mwao kizazi chao, na akawashuhudisha juu ya nafsi zao, akawaambia: Je, Mimi si Mola Mlezi wenu? Wakasema: Kwani! Tumeshuhudia. Msije mkasema Siku ya Kiyama sisi tulikuwa tumeghafilika na hayo.” (al-A'raf, 7/172)
Wakati anaielezea aya hii, Sayyid Qutb ameandika, “Qur’an inakunjua pazia kwa kuelezea ukweli mzito, ambao ndio unaotaja asili ya mwanadamu. Maelezo haya ya Qur’an yalitolewa karne 14 zilizopita, wakati mwanadamu hakuwa na jicho lolote la kutambua ukweli wa uumbwaji wa mwanadamu, ukiachilia mbali dhana zisizo kuwa na msingi wowote. Sasa baada ya karne zote hizi, wanadamu sasa wametambua baadhi ya ukweli wa jambo hilo. Leo sayansi ya viumbe hai (biological science) inatueleza kuwa chembe hai (genes) zinahifadhi kumbukumbu ya kila mwanadamu, zikionesha sifa au tabia zake hali ya kuwa bado wako tumboni kwa mama zao. Chembe hai (genes) hizi, ambazo zinaweka kumbukumbu si chini ya wanadamu bilioni 3, zinaweza kuwekwa pamoja kwenye eneo ambalo halizidi kipimo cha cubic sentimita moja. Kupitia ukweli huu ulioelezwa kipindi hicho, ungalikumbana na dharau na shaka.
Allah anasema, Allah, who says,
“Tutawaonyesha Ishara zetu katika upeo wa mbali na katika nafsi zao wenyewe mpaka iwabainikie kwamba haya ni kweli. Je! Haikutoshi kwamba Mola wako Mlezi kuwa Yeye ni Shahidi wa kila kitu?” (Fussilat, 41/ 53)
Kwa hakika inaeleza ukweli mtupu
Sayansi ya alama za vidole (Dactyloscopy)
Tawi hili la sayansi linachunguza athari za vidole (fingerprints). Athari za vidole zinatofautiana kati ya binadamu mmoja na mwengine. Qur’an ilipoelezea kwamba mwanadamu atafufuliwa akiwa amekusanyiwa taarifa zake zote, inaashiria jambo hili.
“Anadhani mtu kuwa Sisi hatutaikusanya mifupa yake?. Kwani! Sisi tunaweza hata kuziweka sawa sawa ncha za vidole vyake!” (Qiyama, 75/3-4)
Biolojia (Biology)
Profesa mmoja wa masuala ya tiba, alizichunguza aya za Qur’an zinazohusu masuala ya uzazi, hasa aya ya 5 katika Suratu al-Hajj na aya ya 12 katika Suratu al-Muuminun na kuzilinganisha na taarifa za tafiti za sayansi ya viumbe katika zama zetu leo, na kusema kwamba zilikuwa sawa sawa na yale yanayozungumzwa na Qur’an ambazo hazikujulikana kabla ya karne ya 19 popote ulimwenguni. Akamalizia maneno yake kama ifuatavyo:
“Qur’an inaelezea ukweli kuhusu uzazi wa mwanadamu ambao wanadamu wataugundua kwa mamia ya miaka kwa kutumia njia rahisi sana”
Aya ambazo profesa alizitaja ni kama zifautazo:
“Enyi watu! Ikiwa nyinyi mna shaka ya kufufuliwa basi kwa hakika Sisi tulikuumbeni kutokana na udongo, kisha kutokana na manii, kisha kutokana na kipande cha damu ilio gandana, kisha kutokana na kipande cha nyama chenye umbo na kisicho kuwa na umbo, ili tukubainishieni. Nasi tunakiweka katika matumbo ya uzazi tunacho kitaka mpaka muda ulio wekwa. Kisha tunakutoeni kwa hali ya mtoto mchanga, kisha mfikie kutimia akili. Na wapo katika nyinyi wanao kufa, na wapo katika nyinyi wanao rudishwa kwenye umri wa unyonge kabisa, hata mtu awe hajui kitu baada ya kuwa anakijua. Na unaiona ardhi imetulia kimya, lakini tunapo yateremsha maji juu yake husisimka na kututumka, na kumea kila namna ya mimea mizuri (jike na dume).” (al-Hajj, 22/5)
“Na kwa yakini tumemuumba mtu kutokana na asli ya udongo. Kisha tukamjaalia awe tone ya mbegu ya uzazi katika kalio madhubuti. Kisha tukaiumba tone kuwa damu iliyo ganda, na tukaiumba damu kuwa pande la nyama, kisha tukaliumba pande la nyama kuwa mifupa, na mifupa tukaivika nyama. Kisha tukamfanya kiumbe mwengine. Basi ametukuka Mwenyezi Mungu Mbora wa waumbaji.” (al-Muminun, 23/12-14)
Usafi (Hygiene)
Kupitia maeleo yaliyotolewa katika Nyanja zote, Qur’an inamuwezesha mwanadamu kulinda usafi wa mwili na wa kiroho; na imeeleza sheria kamili za usafi, ambazo zimefahamika karne kadhaa baada ya kushushwa.
Qu’an inataja tasattur (kustiri mwili), ambalo ni jambo muhimu sana katika kanuni za usafi, kuvaa nguo safi, kupumzika vya kutosha, mlo kamili, kujiepusha kula vyakula vilivyooza na vibaya, vilevi, usaha, damu na nyama ya nguruwe na madhara ya zinaa, ambayo ndio chanzo cha magonjwa hatari sana.
Maswali juu ya Uislamu
