Nini umuhimu wa zakah (zaka) kwa jumuia?

The Answer

Dear Brother / Sister,

* Zakah (zaka) ni uwiano wa nguvu katika umiliki. Sio kuitokomeza mali ya mmiliki wake wala kuiacha yote kwa mwenyewe, kuwanyima masikini mali hiyo. Inaigawa mali kati ya masikini na tajiri kwa mujibu wa viwango maalumu.

* Zakah ni namna ya hifadhi ya kijamii na bima. Miongoni mwa malengo ya zakah ni kuwasaidia wahitaji, kuwasaidia watu wanyonge kama masikini, mafukara, wenye madeni na wasafiri wasioweza kufika ukomo wa safari yao. Chochote kinachoipa nguvu hadhi ya mtu ambacho kitamwimarisha kiuchumi na kumwendeleza kimwili na kiroho pia kinaiimarisha jumuia.

* Zakah ni bima inayoyaenea matabaka yote yenye kuhitaji kwa mahitaji yao yote kuanzia ya kimwili, kiroho na kimaadili. Misingi ya mwanzo ya hifadhi ya jamii ya kisasa imewekwa mwaka 1941. Wawakilishi kutoka UK na USA waliitisha mkataba wa Atlantiki wa mwaka 1941 na kuamua kuratibu taasisi ya hifadhi ya kijamii kwa mtu mmoja mmoja. Hata hivyo, Uislamu umeitambulisha taasisi ya zakah tokea karne 14 zilizopita.

* Zakah inaondoa mwanya na tofauti zilizopo kati ya matajiri na masikini katika jamii. Inapunguza masafa kati ya matabaka na kuwezesha kuundwa tabaka la kati.

Kuongezeka kwa idadi ya raia wa tabaka la kati kutaathiri soko kwa namna chanya. Mali husika haitokuwa ni kitu kinachomilikiwa na tabaka moja tu; uwezo wa kununua wa masikini utaongezeka, pia. Sio matajiri peke yao bali sehemu kubwa ya jumuia itaweza kukidhi mahitaji yake na kuishi kwa raha katika jumuia.

Aya ya 7 ya sura al-Hashr inakataza baadhi ya mali kuzungushwa miongoni mwa matajiri peke yao. Hili linaweza kufikiwa kwa njia ya zakah tu.

* Zakah inaziepusha mali kulimbikizwa; inazipelekea mali kuwekezwa. Kwa kuwa, hutolewa kutoka katika mtaji na sio faida; hivyo itapungua ikiwa haikufanyiwa biashara. Mmiliki atawekeza mali ili zisipungue; na atajaribu kuiongeza.

* Zakah huwezesha uwiano wa kijamii. Allah Mtukuka amewaumba watumishi Wake kwa namna tofauti kwa upande wa maumbile na viwango vya maisha. Baadhi yao ni; matajiri na wengine ni masikini na baadhi yao wapo kati na kati.

Yafuatayo yanaelezwa katika aya:

“Na Mwenyezi Mungu amewafadhilisha baadhi yenu kuliko wengine katika riziki.” (an-Nahl, 71)

Ni muhali kwa kila mmoja kuwa na kiwango sawa cha mapato kwa sababu katika jamii kuna majukumu na kazi mbalimbali zinazotofautiana kwa upande wa majukumu na mazingira ya kazi. Baadhi ya wajibu na kazi zikitelekezwa, athari zake zitasababisha madhara yasiyorekebishika katika jamii. Kama aina zote za wajibu zina mshahara sawa, hakuna atakayetaka kufanya kazi ngumu zaidi; kila mmoja angependelea zile nyepesi. Hivyo, kazi ngumu zaidi na zenye majukumu mengi zingeweza kutelekezwa na mfumo wa maisha ungevunjika.

Kwa hivyo, ni muhimu kwa watu kuwa tofauti kwa upande wa kipato na viwango vya maisha. Hata hivyo, daraja ni muhimu ili kuzuia tofauti hii isitengeneze mporomoko. Daraja hili ni zakah.

* Zakah inawashikamanisha watu wa jumuia.

Zakah inawashikamanisha watu pamoja kwa kuwa ni aina ya mshikamano wa kijamii. Matajiri wataendeleza hisia za upendo, na huruma kwa masikini. Masikini wataendeleza hisia za utii, heshima, kufanya kazi kwa umakini kwa matajiri. Hisia za choyo, chuki na kijicho zitatulizwa na hata kutokomezwa. Matajiri hawatowadhulumu masikini na kuwaweka chini ya masharti; masikini hawaendeleza hisia za udhalilishaji, utumwa, kinyongo na husuda kwa matajiri. Yafuatayo yanaelezwa katika hadith: “Moyo humfanya mtu ampende anayemtendea ihsani na kumfanya mtu amchukie anayemtendea uovu.”

* Zakah huwaepusha watu kutokana na kufuga kinyongo na chuki na kutokana na kushirikiana na maadui wa jamii na wachochezi. Kama matajiri hawakidhi mahitaji ya masikini, ulazima na ugumu wa kifedha utawasababishia kujiunga na maadui wa Waislamu au utawasababishia kutenda shari kama kuiba, kupora au kuua.

* Zakah ni mlango wa uwekezaji na ni hatua kubwa ya maendeleo. Zakah ina mitazamo yote miwili ya kijamii na kiuchumi. Kwa hivyo, ni ari ya kuanzisha maendeleo.

* Tofauti kati ya matajiri na masikini mara zote imekuwa ikisababisha mapambano ya matabaka ambayo yamekuwa yakiendelea kufanyika waziwazi au kimya kimya tangu mwanzoni mwa maisha ya kijamii – mapinduzi na ghasia za umwagaji damu zilizoonekana katika historia ni ushahidi wa mapambano hayo ambayo ni mapambano ya “unacho; mimi sina”. Uislamu umezitambulisha taasisi za zakah, sadaqah ili kutuliza mapambano hayo yaliyopo tokea kuanza kwa maisha ya kijumuia; pia inawafundisha wafuasi wake wawe na subira, kutosheka na kuridhika na qadar. Ufahari wa mali wala husuda zinazosababishwa na umasikini hauonekani kuwepo baina ya waumini waliokuwa wakifundishwa kama hivyo.

Maswali juu ya Uislamu

Author:
Maswali juu ya Uislamu
Subject Categories:
Read 214 times
In order to make a comment, please login or register
MASWALI YENYE KUFANANA