Ni ipi Shule Wake Safi wa Mtume (Azwaj at-Tahirat)?
Dear Brother / Sister,
Kipindi cha Madina kilikuwa ni kipindi ambapo hukumu za Kiisilamu na maamrisho yalikuwa yakiteremshwa kwa wingi na zikifundishwa kwa ummah na Mtume. Maswahaba wanaume wangeweza kumwona Mtume katika Msikiti wa an-Nabawi na kumwuliza maswali yao na matatizo. Wamejifunza kutoka kwake nini, kwa nini na vipi vya kufanya. Hata hivyo, haikuwa rahisi kwa wanawake. Wao pia walikuwa na maswali ya kuuliza. Kwa hivyo, wanawake walimwomba Mtume kutenga siku moja katika wiki kwa ajili yao nyumbani kwake. Mjumbe wa Allah akakubali pendekezo lao. Hivyo, wanawake wakaanza kwenda nyumbani kwa Mtume na kuuliza maswali yao kuhusu dini na kupokea majibu. Wakati wa mkutano huu, tukio la aina yake likatokea. Muda ambao, wanawake wameanza kuzungumza wao kwa wao kwa sauti kubwa. Walikuwa wakipiga soga. Wakati huo huo, Hazrat Umar aliyekuwa akipita alikerwa na wanawake kuzungumza kwa kelele mbele ya Mjumbe wa Allah na kugonga mlango. Alipofungua mlango, wanawake walimwona na kukatiza mazungumzo mara moja. Hazrat Umar alikerwa alipoona mandhari hiyo. Hakujizuia kuwaonya na kusema, “kinamama! Mnaniogopa mimi, lakini hamwogopi kuzungumza kwa kelele mbele ya uwepo wa Mjumbe wa Allah!” Hapo, wanawake walisema kwa utiifu, “Ewe Umar! Wewe una moyo-mgumu na mkali, lakini Mtume hayuko hivyo”
Hazrat Umar, aliyeitoa mali yake yote kwa ajili ya Mjumbe wa Allah, hakufurahishwa na hilo hakuwa kama Mtume. Mjumbe wa Allah akaligundua hilo na kusema,
“Ewe Umar! Kama utatembea njiani na shetani akakuona unakuja, anaweza kubadili njia yake” ili kumtuliza. Nyumba ya Mtume ilikuwa ni kama shule kwa wanawake. Hususani wake wa Mtume walikuwa ndio wanafunzi wa mara kwa mara na kwa namna fulani ni walimu wa shule hii. Profesa Raşit Küçük, wa Chuo Kikuu cha Marmara, Kitivo cha Theolojia, anafafanua suala hili kama ifuatavyo:
“Hukumu na maamrisho ya Uisilamu yanawahusu wote wanaume na wanawake. Hata hivyo, kuna baadhi ya hukumu na maarisho yanayowahusu wanaume tu au wanawake tu. Bwana Mtume hakupata ugumu wowote katika kufundisha hukumu na maamrisho ambayo yamewahusu wote wanaume na wanawake au wanaume watupu kwa sababu wanaume walikuwa ni jinsia moja na yeye. Alilazimika kuwahutubia wanawake kulingana na mafundisho na utekelezaji wa masuala ambayo yanawahusu wanawake na kujibu maswali yao. Wake za Mtume, waliokuwa katika umri tofauti tofauti na waliokuwa na vipaji tofauti, waliigiza kama ni walimu kwa ajili ya wanawake waumini. Mchakato wa kufundisha uliendelea na hata kuongezeka baada ya kifo cha Mtume.” (1993, İzmir, Ebedî Risalet Sempozyumu Tebliği)
Kwa hakika, shule ya Mjumbe wa Allah, iliyokuwa karibu na Msikiti wa an-Nabawi, ilikuwa na sehemu mbili. Moja ya hizo ilikuwa ni Shule ya Ashab as-Suffa, iliyowajumuisha Maswahaba wanaume, na sehemu nyengine ilikuwa ni Shule ya Wake Watakatifu, iliyowakusanya kinamama.
Kwa kweli, vyumba vya Wake Watakatifu vilikuwa kama shule na wakeze Mtume walikuwa namna zote mbili wanafunzi na walimu wa shule hiyo kwa sababu walijifunza hukumu na maamrisho ya Uisilamu moja kwa moja kutoka kwa Mjumbe wa Allah na kuyafundisha kwa ummah. Wajibu huu uliendelea baada ya kifo cha Mtume kama ulivyotajwa hapo juu. Mmoja ya wanafunzi wa kudumu na hodari zaidi wa Shule ya Ashab as-Suffa alikuwa ni Abu Hurayra, ambae alijitolea maisha yake kuhifadhi hadithi za Mtume na ambaye amepata dua ya Mtume kwa ajili ya kuimarisha uhifadhi wake ili kulibeba jukumu hili vyema; kwa upande mwengine, mwanafunzi hodari zaidi wa Shule ya Wake Watakatifu alikuwa ni Bibi Aisha, ambaye alikuwa na uwezo wa hali ya juu kama umahiri, uhifadhi na ufahamu na alikuwa ni mke wa kipekee wa Mtume. Kwa hakika, wa mwanzo katika “Mukthirun” (watu waliosimulia hadithi nyingi zaidi) alikuwa ni Abu Hurayra, aliyekuwa mwanafunzi hodari wa Shule ya Ashab as-Suffa ambaye amesimulia hadithi 5374; Bibi Aisha, aliyekuwa mwanafunzi hodari zaidi wa Shule ya Wake Watakatifu alikuwa ni mtu wa nne mingoni mwa Mukthirun; alisimulia hadithi 2210.
Ndio, Uisilamu umeleta hukumu na maamrisho yanayohusu ngazi zote za maisha pamoja na ngazi mbalimbali za umuhimu kuwa ndio dini ya mwisho na kamilifu. Upambanuzi, ufundishaji na utekelezaji wa hukumu na maamrisho hayo ulikuwa ni wajibu wa msingi na muhimu zaidi kwa Zama za Furaha Kamili kwa sababu mtindo na muundo ambao Allah angeuridhia, ambao ndio dini yenyewe, ulikuwa umechambuliwa katika kila kipindi na hatua ya maisha.
Tukiangalia vyanzo kadhaa ili tufahamu ukweli huu, tunaona hazina ya kuvutia ya hukumu, maamrisho na siri mbalimbali. Na wajibu wa kuwasilisha hazina hii kwa ummah unakuwa dhahiri kama ilivyo kwa lengo lisilo na dosari kwa ndoa hizo.
Tunaweza kusema kuwa kama tutawatoa kinamama hao hususani Bibi Aisha, ambaye ana nafasi maalumu kati yao, basi kiasi cha nusu ya maarisho na hukumu za dini ya Uisilamu zingetoweka!
Maswali juu ya Uislamu

