Imani imegawika sehemu ngapi?
Dear Brother / Sister,
Imani imegawika sehemu mbili:
- Imani ya jumla.
- Imani ya kuhakiki.
Imani ya jumla ina maana gani?
Ina maana kuamini kiujumla yote ambayo Mtume wetu ametufikishia kutoka kwa Allah.
Ikiwa mtu atasema:
“La ilaha illallah muhammadun rasulullah” kwa kutambua maana yake na kukubali, basi atakuwa ameamini kwa ujumla.
Sentensi hii inaitwa tawhid. Maana yake ni kama ifuatavyo:
La ilaha illallah: Hakuna Mola ila Allah.
Muhammadun rasulullah: Muhammad ni mjumbe wake.
Imani ya kuhakiki ina maana gani?
Ni kujua kwa kina na kwa ushahidi aliyotueleza mtume wetu kutoka kwa Allah. Kwa maana nyingine, ni kusoma na kukubali elimu ya lazima kuhusu dini kwa kina.
Ni elimu gani ya lazima ya dini ambayo inahitajika kusomwa?
Elimu ya lazima ya dini ambayo inahitajika kusomwa ni nguzo sita za Imani zilizokusanyika katika Amantu, ibada ya wajibu kama sala, funga, hija, zaka na matendo kama kuua mtu, kunywa kilevi, na zinaa, ambayo ni haramu katika dini.
Ni wajibu kwa kila muislamu kuyafahamu kwa kina na kuyaamini.
Maswali juu ya Uislamu
