Imani humfanya mtu apate nini?
Submitted by on Thu, 28/02/2019 - 10:56
Dear Brother / Sister,
Mwanadamu hufika kilele cha juu kabisa kwa nuru ya Imani na kupata thamani ya kumfanya astahiki pepo. Hushuka chini kabisa ya vilivyo chini kwa giza la ukafiri na kufikia hali ya kustahiki moto. Imani ni mahusiano. Ni uhusiano unaomuunganisha mwanadamu na Allah. Kujenga uhusiano na Allah inawezekana tu kupitia Imani. Thamani ya kweli ya mtu inategemea uhusiano na ukaribu wake na Allah. Heshima na hadhi ya mtu huongezeka kwa mujibu wa ukaribu wake na Mfalme; vivyo hivyo thamani ya mtu huongezeka kwa mujibu wa ukaribu wake na Allah.
Katika ulimwengu huu, kama mtu ataungana na Allah, na kuwa chini ya hifadhi yake, hapo anaweza kuwa kiongozi wa Allah ardhini, afisa wake, mgeni wake au hata rafiki yake shukrani kwa Imani. Uhusiano huu wa urafiki na Allah unaweza kufahamika kwa nuru ya imani tu. Imani ni nuru ambayo mtu huona ukweli wa kila kitu shukrani kwa nuru hiyo. Huona sababu na maana zilizojificha za viumbe na kufahamu kwamba havikuumbwa bure.
Hisia nzuri zaidi kwa mwanaadamu ni upendo. Kama Imani isingekuwepo, upendo huu ungelimuweka mtu katika matatizo na hiyo ni kwa wingi wa sehemu zake. Kwa mfano mama ambaye mtoto wake mzuri na wa pekee anapofariki atahisi adhabu hii ya kiroho yote kama hatakuwa mwenye kuamini ahera.
Moja kati ya hisia muhimu za mwanadamu ni mapenzi. Mapenzi yaliyopata nuru ya Imani hufanya viumbe vyote kuwa ni marafiki wa mwanaadamu. Uhusiano wa mapenzi kisha huanzishwa kati ya mwanaadamu na mazingira yake. Hisia za kuwa pamoja na watu awapendao milele humfanya awe na furaha. Kwa mfano, mtoto anapokaribia kufariki na daktari kumpa baadhi ya dawa na hatimaye mtoto kupona, mama atakuwa na furaha sana na mwenye faraja.
Vivyo hivyo, mamilioni ya watu tuwapendao na ambao tunawajali kama mtoto huyo tunatenganishwa nao na umauti. Kama tutaliangalia jambo kwa nuru ya Imani, tutafahamu kwamba hawapotei moja kwa moja. Hivyo adhabu na huzuni hugeuka kuwa furaha isiyo na mpaka na faraja.
Kama mwanadamu atazuiwa kuamini, wasiwasi wa kutenganishwa na awapendao milele humpa adhabu kama moto. Kwa mfano kitu cha thamani zaidi kwa mwanaadamu ni akili yake. Kama akili itadondoka katika shirki na ukafiri, hupeleka maumivu na adhabu zinazokuja kutoka wakati uliopita na ambazo zimesababishwa na kupotea kwa milele kwa watu awapendao moyoni mwake. Kwa kuongezea, wasiwasi kuhusu kupotea kwake katika wakati ujao hubadilisha akili kuwa ni kifaa cha adhabu. Kwa hivyo, mtu mwenye dhambi kiujumla hujiingiza katika matumizi ya pombe au burudani ili aweze kukimbia adhabu ambazo hupewa na akili yake.
Kama akili itapata nuru ya Imani, mawazo ya kuwa pamoja na jamaa zake na marafiki zake peponi hutawala katika dunia yake. Humfanya apende maisha na viumbe. Upendo wake kwa mola wake, ambaye atakayefanya iwezekane kwake kuungana tena na awapendao na ambaye atampa yeye na wao furaha isiyo na mwisho, utaongezeka. Akili huwa akili hasa na hupata thamani yake halisi kwa nuru ya Imani.
Kama jicho la mwanadamu litapata nuru ya Imani, huona ulimwengu wote kama pepo iliyopambwa kwa maua. Huona kazi za sanaa, baraka na msaada wa Allah katika kila kiumbe akionacho. Hutazama kwa kutafakari na kupata masomo. Hufahamu ushahidi unaoonesha kuwepo na umoja wa Allah katika kila kitu na kujifunza ili aimarishe Imani yake. Ulimwengu unakuwa kama kitabu kikubwa machoni mwake. Huzisoma maana zilizojificha katika kitabu hiki cha ulimwengu.
Masikio yanapopata nuru ya Imani, husikia sauti za kiroho zinazokuja kutoka ulimwenguni. Hufahamu kutukuzwa kwa Allah kunakofanywa katika lugha ya hali. Husikia nyimbo za upepo, vilio vya mawingu na sauti nzuri za mawimbi ya bahari shukrani kwa nuru ya Imani. Husikia maneno ya kiungu na kutukuzwa kwa Allah kutoka katika kila kiumbe kama sauti ya matone ya mvua, sauti za ndege na maongezi ya wadudu. Ulimwengu huwa kama mkusanyiko wa muziki wa kiungu. Roho na moyo wa mwanaadamu kama huyu vimejawa na ladha nzuri na raha.
Hata hivyo, masikio yanapozibwa na ukafiri, yanazuiwa kusikia sauti hizo tamu za kiroho. Sauti zenye kutoa raha hubadilishwa kuwa sauti za kilio. Maana nzuri na zenye hadhi katika moyo hubadilishwa kuwa huzuni. Sauti zinazokuja kutokana na hali ya kuwa mpweke milele zilizosababishwa na kushindwa kupata marafiki wa kweli hutawala dunia yake. Husikia sauti za huzuni na machungu zilizosababishwa na hali ya kuhisi kutokuwa na umiliki na kutolindwa. Hali hii humfanya aishi maisha ya adhabu sana.
Hivyo, Imani humfanya mtu apate furaha kubwa, baraka, ladha, raha na daraja ya heshima ambayo haiwezi kuelezeka. Fikra ya muumini kuhusu ulimwengu ni chanya. Huona kila kitu kizuri, ana fikra njema na hupata raha ya maisha. Huona viumbe vyote ulimwenguni kuwa ni marafiki zake na nduguze. Hana ugeni na kitu chochote. Kila kitu kina uhusiano na kingine kwa vifungo vya umoja kwa wingi wa majina ya Allah. Dunia ni kama sehemu ya undugu kwake.
Nuru ya Imani huangaza ulimwengu wa mwanaadamu na kuangazia ulimwenguni. Huokoa wakati uliopita na ujao kutoka katika giza. Humpa heshima mwanaadamu na huleta ukamilifu katika kiini cha ulimwengu. Huongeza thamani juu ya thamani yake. Viumbe vyote ulimwenguni hupata maana shukrani kwa Imani. Yanayojiri husimama kuwa ya bahati. Kila kitu kitaonekana kuwa huwepo kwa mpango na programu ya Allah.
Muumini huona athari ya kiini na sura ya rehema ya Allah ndani ya yote yaonekanayo kuwa upuuzi shukrani kwa fikra nzuri na chanya aliyoipata kupitia nuru ya Imani. Kwa mfano huangalia mambo mabaya kama maradhi kwa upande chanya. Hufikiri kuwa yatapelekea kusamehewa dhambi zake, huifunza roho yake, humfanya afanye matendo mazuri na kuzidisha daraja yake, na hatimaye kuifariji nafsi yake.
Kafiri huuangalia ulimwengu na yanayojiri kwa upande hasi na kwa mashaka. Ukafiri ni kama glasi nyeusi huonesha kila kitu kuwa ni kibaya na giza. Ukafiri huona viumbe kuwa ni matokeo ya bahati na bila ya sababu. Kwa fikra ya kafiri kila kitu ni upuuzi kisichokuwa na lengo. Viumbe vyote ni wageni na ni maadui wao kwa wao. Hudhani kuwa viumbe vyote huenda kwa kasi kwenye ulimwengu wa kutokuwepo. Hofu na wasiwasi wa kuwa yeye pia atadondokea katika giza la milele hufanya ulimwengu kuwa gereza kwake. Dunia yake imejawa na giza na shida. Roho yake imezungukwa na giza la hasadi, chuki, uasi badala ya nuru ya mapenzi na upendo. Mtu kama huyo anaishi maisha ya motoni kabla ya kuingia motoni.
Maswali juu ya Uislamu