Je, jeni zina taathira yoyote juu ya kuamini kwa mtu au kutoamini? Je, kadhia hii inaondoa jukumu la mtu?
Submitted by on Thu, 28/02/2019 - 15:45
Dear Brother / Sister,
Kuwa mwenye akili au la hakusababishi mtu kuamini au kukufuru. Ikiwa ni hivyo basi ingelikuwa dhulma. Hivyo, wale wenye akili sana wangeliamini na wasiyo na akili sana wangekufuru.
Kuwa na Imani au la kunaungana moja kwa moja na utashi wa mtu. Watu wenye akili, wawe na akili sana au kidogo. Wanabebeshwa jukumu. Wajibu unahusu kuwa na akili au la. Ni juu ya utashi wa mtu kuamini au la. Mtu hukubali au kukataa Imani kwa utashi wake.
Shetani aliasi japo alikuwa na akili sana na alimfahamu Allah. Uasi hautokani na uendawazimu wa shetani. Sababu ulizozitaja zinaweza kuathiri kuamini kwa mtu au la lakini sababu ya kweli ni utashi wa mtu. Hamna katika sababu hizo zenye kuathiri kuwajibika kwa mtu. Wendawazimu na wale wasiyopata ujumbe wa Uislamu hawa hawawajibiki.
Mfumo wa maumbile hauathiri katika utashi wa mwanaadamu asilimia mia moja. Unaweza tu kuwa moja ya sababu. Kama wajibu wa kujaribiwa, bila ya shaka kutakua na baadhi sababu zenye kuathiri katika Imani ya mtu. Hata hivyo, hakuna kati ya hizo itakayoweza kumuathiri asilimia mia moja. Kama mfumo wa maumbile ungelikuwa unaathiri asilimia mia moja, kila mtu angeliamini kama Hz. Adam (a.s). Mtoto wa Nabii Nuhu aliangamizwa katika gharika kabla ya kumuamini baba yake. Jambo linaloonesha kuwa mfumo wa maumbile hauna taathira katika imani. Mwanaadamu kiasili ana tabia ya kuamini au kutoamini. Hata hivyo, mambo mawili hayo yapo katika ngazi moja.
Kwa mujibu wa Badiuzzaman Said Nursi, “Imani ni mwanga wenye kung’aa unaotolewa na jua la milele (Allah mtukufu) na ni nuru kutoka katika neema isiyo na mwisho.” (Said Nursi, İşârâtü'l-İ'câz)
Maswali juu ya Uislamu