Je, unaweza kumtathmini mwanaadamu kupitia vioo vya Imani na ukanushaji kwa mujibu wa pande tofauti alizonazo?
Submitted by on Thu, 28/02/2019 - 15:32
Dear Brother / Sister,
Mwanaadamu ana ujamaa na viumbe vyote. Ana namna ya kubadilishana na kila kitu. Analazimika kukutana, kuongea na kuishi karibu na vitu vilivyomzunguka kimaada na kiroho kiasili yake. Kwa namna hiyo, mtu ana pande sita: kulia, kushoto, mbele, nyuma, juu na chini. Kwa kuvaa miwani ya Imani na ukafiri, mtu anaweza kuona viumbe na hali zao katika pande hizi sita.
Upande wa kulia: Upande huu una maana ya wakati uliyopita. Wakati uliyopita unapotazamwa kupitia miwani ya ukafiri, utaonekana kana kwamba ni uwanja wa makaburi. Mtazamo huu utampa mtu hofu kubwa na kukata tamaa.
Hata hivyo, upande huu unapotazamwa kupitia miwani ya Imani, huwaona watu waliotangulia wamehaulishwa kwenda katika ulimwengu bora na wenye nuru. Huona makaburi ni njia za chini kwa chini zilizochimbwa ili kufika katika ulimwengu wenye nuru. Hivyo, Imani humpa mtu furaha kubwa, raha na amani na humfanya aseme “Ahsante Allah”.
Upande wa kushoto: Upande wa kushoto, ambao ni wakati ujao unapotazamwa kwa miwani ya ukafiri utaonekana kama kaburi kubwa baya lenye giza ambalo litatufanya tuharibike na ambalo litatuangamiza kwa kuwafanya nyoka na nge kututafuna.
Hata hivyo, unapotazamwa kwa miwani ya Imani, utaonekana kama meza iliyojaa aina tofauti za vyakula vitamu na vizuri na vinywaji vilivyoandaliwa na Allah, mwenye huruma na ambaye anamuumba mtu kutokana na si kitu. Na itamfanya aseme “ahsante Allah” mara nyingi.
Upande wa juu: Mtu mwenye kuangalia mbinguni kupitia miwani ya ukafiri huona kuwa mamilioni ya nyota na sayari hutembea kwa haraka na kufanya harakati tofauti kama farasi mwenye kukimbia au ndege ya kivita katika anga isiyo na mwisho; kwa vile hafahamu kuna anayevidhibiti, anapata hofu na woga.
Hata hivyo, muumini anapoangalia mbinguni, anafahamu kwamba ndege hizi za ajabu zipo chini ya amri na udhibiti wa mwenye amri. Huona kwamba nyota ambazo hupamba dunia na mbinguni ni taa zinawaangazia wanaadamu. Kwa vile anafahamu kwamba utawala wake upo katika mikono ya Allah, huangalia kwa mapenzi matendo ambayo ni kama farasi wanaokimbia badala ya hofu na woga. Bila ya shaka haitoshi kusema “Ahsante Allah” mara elfu kwa baraka ya Imani yenye kueleza matendo ya anga.
Upande wa chini: Ni ardhi. Mtu anayeangalia dunia kupitia jicho la ukafiri huona dunia ni kama sanamu, mnyama asiyedhibitiwa pembeni mwa jua au jahazi bila ya nahodha na kupata hofu.
Hata hivyo, kama ataangalia kupitia Imani, huiona katika muundo wa meli chini ya amri ya Allah, na vyakula vyote, vinywaji, nguo na watu, yenye kusafiri pembeni mwa jua Na anaanza kusema “Ahsante Allah” mara nyingi kwa baraka kubwa iliyotokana na Imani.
Upande wa mbele: Kafiri anapoangalia upande huu, huona kwamba viumbe hai vyote, wawe wanaadamu au wanyama, wanakwenda upande huo kwa haraka kwa makundi na kupotea. Yaani wanasimama kuwepo. Kwa vile anajua kwamba ataenda huko pia, atakaribia kwenda kuwa mwendawazimu kwa huzuni.
Hata hivyo, kwa muumini anayetazama kupitia jicho la Imani, kutembea na kusafiri kwa watu upande huo siyo kwenda katika ulimwengu wa hakuna kitu bali ni kuhaulishwa kama kuhama kwa mabedui kutoka ardhi kwenda kwenye ardhi nyingine. Ni kuhama kutoka sehemu ya muda kwenda sehemu ya kudumu, kutoka katika shamba la huduma ya kazi kwenda katika ofisi ya malipo, kutoka katika ardhi ya shida kwenda katika ardhi ya neema. Kwa vile anafahamu kuwa kuhama huku si kwa ajili ya kwenda katika ulimwengu wa hakuna kitu, hukabiliana nao kwa furaha.
Hata hivyo, shida zionekanazo kama umauti na kaburi njiani ni matukio ya furaha baadaye kama matokeo. Njia ya kufika katika ulimwengu wa nuru hupita kaburini, na matukio makubwa ya furaha ni matokeo ya mabalaa mabaya. Kwa mfano, Hazrat Yusuf aliufikia ufalme wa Misri baada ya kutupwa katika kisima na ndugu zake na baada ya kuingia jela kama matokeo ya sakata la Zulekha.
Vivyo hivyo mtoto anayekuja duniani kupitia tumbo la mama yake hupata furaha ya kidunia kama matokeo ya shida na maumivu ayapatayo njiani.
Upande wa nyuma: Ikiwa wale wanaokuja nyuma watatazamwa kwa jicho la ukafiri, maswali kama “Wanaelekea wapi na wametokea wapi? Kwanini wamekuja duniani?” Hayawezi kujibiwa na kafiri hubaki katika adhabu ya kusita.
Hata hivyo, kama mtu atatazama kwa jicho la Imani, atafahamu kuwa watu hawa wametumwa na Allah kuona miujiza ya nguvu ya ajabu inayooneshwa katika maonesho ya ulimwenguni. Anafahamu kuwa watu hawa watafikia daraja kwa kufahamu maana ambazo Allah anazitaka zifahamike ulimwenguni kwa mujibu wa kiasi wanachofahamu na kurejea kwa Allah. Atasema “Ahsante Allah” kwa baraka ambazo Imani humfanya apate baraka hii ya ufahamu.
Pande hizi sita za mwanaadamu huangaziwa shukrani kwa Imani; wakati wote na sehemu zote hugeuzwa kuwa ulimwengu mkubwa na wenye raha. Ulimwengu wote takriban huwa kama nyumba yake anayoijua, si ngeni kwake na hujisikia amani ndani yake. Na kama hivyo, anakuwa kama mfalme wa ulimwengu shukrani kwa Imani.
Maswali juu ya Uislamu