Kwa nini kufunga swaumu kumefaradhishwa?

Submitted by on Fri, 10/08/2018 - 11:49
Dear Brother / Sister,
Yafuatayo yanaelezwa katika Quran:
“Enyi mlio amini! Mmeandikiwa Saumu, kama waliyo andikiwa walio kuwa kabla yenu ili mpate kuchamngu.” (al-Baqara, 2/183).
It is known that the Messenger of Allah said,
Inatambulika kuwa Mjumbe wa Allah amesema,
“Kufunga swaumu ni ngao inayomkinga mtu na Moto wa Jahanamu kama ngao inayokukinga na hayo wakati wa vita.” (Nasai, Sawm, IV, 167)
Kufunga swaumu ni aina ya ibada inayomkinga mtu anayefunga kutokana na aina zote za matamanio ya ashiki na inamwongezea unyoofu. Ni muhimu sana kujizuia na njaa, kiu na matamanio mengine ya nafsi. Waumini wanaomwamini Allah na wanaopigana jihad kwa ajili Yake watakuwa na imani thabiti shukurani kwa swaumu.
Ramadhani hutangulia kwa siku kumi au kumi na moja kila mwaka kwa kuwa kalenda ya Hijri inategemea mwandamo wa mwezi. Kwa hivyo, wakati mwingine mtu hufunga katika kipindi cha baridi kali ya wakati wa kipupwe wakati mwingine wakati wa joto kali msimu wa kiangazi. Kwa namna fulani, muumini ananuia: “niko tayari kutimiza amri za Allah hata katika baridi ya kuganda au joto la kubabua.”
Vilevile, ni tukio muhimu sana kwa muumini kuyaacha matamanio ya nafsi yake kwa mwezi mmoja ili apate radhi za Allah.
Unafiki hauna nafasi katika kufunga swaumu. Kwa hakika, asili na sifa za kufunga swaumu na muumini anayefunga zinaelezwa kama ifwatavyo:
“Kinga ni ngao (au stara au hifadhi). Hivyo, mtu anayefunga swaumu anatakiwa ajiepushe kuingiliana na mkewe na anatakiwa asiwe na tabia za kipumbavu na kifidhuli, na kama mtu anatapigana naye au kumtukana, anatakiwa amwambie mara mbili, ‘nimefunga.” Mtume ameongezea kusema, “Naapa kwa Yule Ambaye nafsi yangu iko Mikononi Mwake, harufu inayotoka kinywani mwa aliyefunga ni bora mbele ya Allah kuliko harufu ya uturi. (Allah anasema kuhusu mtu aliyefunga), Ameacha chakula chake, kinywaji chake na matamanio yake kwa ajili Yangu. Swaumu ni Yangu. Hivyo basi nitailipia (kwa aliyefunga) na malipo ya amali njema ni mara kumi.” (Bukhari, Siyam)
Maswali juu ya Uislamu