Muumini ni nani? Ni zipi sifa za muumini?

The Answer

Dear Brother / Sister,

Muumini ni mtu anayemwamini Allah, ahera  na misingi ya Imani. Kama mtu atasema yeye ni muislamu atazingatiwa kuwa ni muislamu.

Tunaweza kuorodhesha sifa kuu za muislamu ambazo Allah amezitaja katika Qur’an kama ifuatavyo:

Waumini humuamini Allah pekee. Hakuna dhati nyengine isipokuwa yeye wanayoiabudu akilini mwao. (al-Fatiha, 1/1-7; an-Nisa, 4/36)

Wanamuogopa Allah. Huepuka kufanya mambo ambayo yamekatazwa na Allah au yaliyo kinyume na radhi zake. (Aal-i Imran, 3/102; Yasin, 36/11; at-Taghabun, 64/15-16; az-Zumar, 39/23)

Wanamuamini Allah pekee. (al-Baqara, 2/249; at-Tawba, 9/25-26)

Hawamuogopi yeyote ila Allah. (al-Ahzab, 33/39)

Wanamshukuru Allah. Kwa hivyo, kuwa na matatizo ya kiuchumi au kuwa katika hali nzuri haiwafanyi wasikitike au kujivuna. (al-Baqara, 2/172; al-Isra, 17/3; Ibrahim, 14/7)

Wameamini kutokana na elimu ya hakika. Hawana mawazo ya kurudi bila ya kupata radhi za Allah. Wanaendelea kuhudumia dini yao kwa ari kila siku. (al-Hujurat, 49/15; al-Baqara, 2/4)

Wanashikamana na Qur’an. Hupangilia matendo yao yote kwa mujibu wa Qur’an. Ni wenye kuacha mara moja kufanya jambo pale wanapogundua ni lenye kukinzana na Qur;an. (al-Araf, 7/170; al-Maida, 5/49; al-Baqara, 2/121)

Wanamtaja Allah daima. Wanajua kuwa Allah huona na kusikia kila kitu; Ni wenye kuweka akilini mwao daima kuwa nguvu za Allah hazina ukomo. (Aal-i Imran, 3/191; ar-Rad, 13/28; an-Nur, 24/37; al-Araf, 7/205; al-Ankabut, 29/45)

Ni wenye kufahamu udhaifu wao mbele ya Allah. Ni wapole. Hata hivyo haina maana ya kuonekana dhaifu mbele ya watu wengine na kuwa wanyonge. (al-Baqara, 2/286; al-Araf, 7/188)

Ni wenye kufahamu kuwa kila kitu hutoka kwa Allah. Kwa hivyo, hawapatwi na fazaa wanapokutwa na jambo; huwa na subira na kuegemea kwa Allah. (at-Tawba, 9/51; at-Taghabun, 64/11; Yunus, 10/49; al-Hadid, 57/22)

 

Ni wenye kutazamia maisha ya ahera; wameamua kuwa ahera ndiyo lengo lao kuu. Hata hivyo, hufaidika na neema za duniani; Ni wenye kujaribu kutengeneza mazingira ambayo ni kama pepo hapa duniani. (an-Nisa, 4/74; Sad, 38/46; al-Araf, 7/31-32)

Ni wenye kuwafanya waumini peke yao kuwa ndiyo marafiki zao na wanaowaamini. (al-Maida, 5/55-56; al-Mujadala, 58/22)

Ni wenye akili. Daima wapo makini, kwa sababu wana ufahamu wa ibada zao. Daima huwahudumia waumini na dini kwa kutumia akili. (al-Mumin, 40/54; az-Zumar, 39/18)

Ni wenye kupambana kiakili kwa nguvu dhidi ya wakanushaji kwa ajili ya Allah. Hususan wakanushaji wakubwa. Huendelea na mapambano yao bila ya hofu wala uvivu. (al-Anfal, 8/39; al-Hajj, 22/78; al-Hujurat, 49/15; at-Tawba, 9/12)

Hawana woga wa kusema ukweli. Hawana hofu ya kuuweka wazi ukweli kwa kuhofia watu. Hawaogopi wakisemacho wakanushaji dhidi yao; hawapuuzi mashambulizi na dhihaka zao; Hawaogopi kukosolewa na wale wenye kuwalaumu. (al-Maida, 5/54, 67; al-Araf, 7/2)

Kufikisha dini ya Allah kwa watu. Ni wenye kuwaita watu katika dini ya Allah kwa kutumia njia tofauti. (Nuh, 71/5-9)

Si madhalimu. Ni wenye huruma na huathirika na shida za wengine. (an-Nahl, 16/125; at-Tawba, 9/128; Hud, 11/75)

Ni wenye kujizuia na hasira; ni wenye uvumilivu na kusamehe. (Aal-i Imran, 3/134; al-Araf, 7/199; ash-Shura, 42/40-43)

Ni waaminifu. Huonyesha utu wenye nguvu na husifika kwa kujiamini. (ad-Duhan, 44/17-18; at-Takwir, 81/19-21; al-Maida, 5/12; an-Nahl, 16/120)

Wanaumizwa na ukandamizaji na ukatili. (ash-Shuara, 26/49, 167; al-Ankabut, 29/24; Yasin, 36/18; Ibrahim, 14/6; an-Naml, 27/49, 56; Hud, 11/91)

Ni wenye kuvumilia shida. (al-Ankabut, 29/2-3; al-Baqara, 2/156, 214; Aal-i Imran, 3/142, 146, 195; al-Ahzab, 33/48; Muhammad, 47/31; al-Anam, 6/34)

Hawana hofu na dhulma pamoja na umauti. (at-Tawba, 9/111; Aal-i Imran, 3/156-158, 169-171, 173; ash-Shuara, 26/49-50; as-Saffat, 37/97-99; an-Nisa, 4/74)

Ni wenye kupambana na mashambulizi na vitimbi ya wakanushaji. (al-Baqara, 2/14, 212)

Wapo chini ya himaya ya Allah. Vitimbi vyote dhidi yao hushindwa. Allah huwafanya washindi kwa kuwahami dhidi ya uzushi wote na vitimbi. (Aal-i Imran, 3/110-111, 120; Ibrahim, 14/46; al-Anfal, 8/30; an-Nahl, 16/26; Yusuf, 12/34; al-Hajj, 22/38; al-Maida, 5/42, 105; an-Nisa, 4/141)

Ni wenye umakini mkubwa dhidi ya wakanushaji. (an-Nisa, 4/71, 102; Yusuf, 12/67)

Ni wenye kuwafanya maadui shetani na wafuasi wake. (Fatir, 35/6; az-Zukhruf, 43/62; al-Mumtahina, 60/1; an-Nisa, 4/101; al-Maida, 5/82)

Ni wenye kupambana na wanafiki; hawautumii muda wao pamaja nao. (at-Tawba, 9/83, 95, 123)

Ni wenye kujikinga na udhalimu wa wakanushaji. (al-Ahzab, 33/60-62; al-Hashr, 59/6; at-Tawba, 9/14-15, 52)

Ni wenye kufanya mambo yao kwa kushauriana. (ash-Shura, 42/38)

Hawana wivu au kuiga maisha ya kifahari ya makafiri. (al-Kahf, 18/28; at-Tawba, 9/55; Taha, 20/131)

Hawaathiriki na utajiri na cheo. (al-Hajj, 22/41; al-Qasas, 28/79-80; an-Nahl, 16/123)

Ni wenye uangalifu na umakini kuhusu ibada; wanatekeleza sala, funga na ibada kwa uangalifu. (al-Baqara, 2/238; al-Anfal, 8/3; al-Muminun, 23/1-2)

Hawafuati wingi bali vipimo vilivyowekwa na Allah. (al-Anam, 6/116)

Ni wenye kupambana kwa nguvu ili kufika kwa Allah na kuwa waumini wa kupigiwa mfano. (al-Maida, 5/35; Fatir, 35/32; al-Waqia, 56/10-14; al-Furqan, 25/74)

Si wenye kutenda kwa kuegemea ushawishi wa shetani. (al-Araf, 7/201; al-Hijr, 15/39-42; an-Nahl, 16/98-99)

Hawawafuati wazee wao kwa upofu. Wanatenda kwa mujibu wa Qur’an. (Ibrahim, 14/10; Hud, 11/62, 109)

Hawapotei kwa israfu. (al-Anam, 6/141; al-Furqan, 25/67)

Wanajihifadhi kutokana na zinaa na huoa kwa njia ambayo Mwenyezi Mungu anataka. (al-Muminun, 23/5-6; an-Nur, 24/3, 26, 30; al-Baqara, 2/221; al-Maida, 5/5; al-Mumtahina, 60/10)

Hawana kupita kiasi katika dini. (al-Baqara, 2/143; an-Nisa, 4/171)

Sio wabinafsi (al-Insan, 76/8; Aal-i Imran, 3/92, 134; at-Tawba, 9/92)

Wanatilia umuhimu usafi. (al-Baqara, 2/125, 168; Muddaththir, 74/1-5)

Hawachunguzani. (al-Hujurat, 49/12)

Wanaepuka uchoyo. (an-Nisa, 4/128)

Wanaomba msamaha kwa Allah. (al-Baqara, 2/286; Aal-i Imran, 3/16-17, 147, 193; al-Hashr, 59/10; Nuh, 71/28)

Maswali juu ya Uislamu

Author:
Maswali juu ya Uislamu
Subject Categories:
Read 2.102 times
In order to make a comment, please login or register
MASWALI YENYE KUFANANA