Ni nini faida za ibada kwa mtu mmoja mmoja na kwa jamii?

The Answer

Dear Brother / Sister,

1. Moja kati ya faida za ibada ni kwamba, ibada huweka hukumu zinazohusiana na itikadi na imani kutulia katika moyo na nafsi na kutengamaa.

Kama inavyojulikana, elimu huongezeka, hukua na kumakinika kutokana na matendo na uzoefu. Ni vigumu kuihifadhi elimu ambayo haifanyiwi kazi na kutumiwa; haitokuwa na maana yoyote kwa mwanadamu. Jambo hilo ni sahihi pia kwa elimu na hukumu za Imani na itikadi. Hutulia katika moyo wa mwanadamu tu kupitia ibada, kwa sababu ibada, ambayo maana yake ni kutekeleza maamrisho ya Allah na kuacha makatazo yake, ni kama kutenda na kuifanyia kazi Imani.  

Kuacha ibada husababisha taathira chanya ya Imani katika tabia ya mwanadamu kudhoofika na kufutika kabisa kwa kadri muda unavyoenda. Kwa kadri ambavyo taathira chanya ya tabia ya mwanadamu hudhoofika tabia mbaya na matamanio yenye madhara hutawala katika ulimwengu wake wa hisia na kumsukuma mwanadamu kutenda madhambi mbalimbali na matendo maovu. Kwa mantiki hiyo, Imani na ibada vina uhusiano wa karibu sana. Kama tutaifananisha Imani na taa, basi ibada ni kama glasi ya taa hiyo ambayo huizuia kuharibiwa na upepo na hivyo kuongeza mwanga wake. Katika kuonesha kazi ya ibada kuilinda Imani, Mtume (rehma na amani ziwe juu yake) amesema, “Imani ni mwili ulio uchi; nguo yake ni ucha Mungu.” Kama inavyojulikana, ucha Mungu ni kuacha makatazo ya Allah na kujitenga mbali sana na mambo yote ya haramu na dhambi; tuliyoyaorodhesha juu ndio maana ya ibada.

2. Ibada hufanya kazi muhimu ya kupangilia mfumo wa maisha wa mtu kwasababu ibada hugeuza fikra zote kwa Allah Mtukufu na kuuweka utukufu na ukubwa wa Allah katika akili za watu. Jambo hili humfanya mtu kufukiria kupata radhi za Allah katika kila jambo analofanya na kutii maagizo ya Kiungu na kuacha makatazo yote.

Hivyo, maisha ya mtu binafsi yanapangiliwa kwa kufuata maelekezo ya dini na huwekwa katika nidhamu maalumu kivitu na kiroho.

3. Ibada hufanya kazi muhimu sana ya kuunganisha watu na kuhakikisha Amani na upendo katika jamii vile vile. Kuabudu kwa kuelekea Qibla kimoja huanzisha uaminifu usiovunjika na uhusiano usio na ukomo baina ya Waislamu. Uaminifu na uhusiano huu huleta umoja imara, mapenzi ya dhati na urafiki wa kweli.

Hivyo, maisha kwenye jamii yanakuwa ya Amani na upendo; maendeleo ya vitu na kiroho hudumishwa.

4. Kwa ajili ya kuleta athari za ibada kwenye ulimwengu wa kitabia na kiroho wa mwanadamu:  

Muumini anaetekeleza ibada zake hupata Amani na utulivu. Huwa madhubuti kiroho. Huishi kwenye amani na furaha kwenye maisha yake yote pamoja na utulivu wa kisaikolojia wa mtu anaetekeleza majukumu yake.

Hatohisi kuchanganyikiwa, kuchoshwa au kukata tamaa. Hatohisi huzuni na kukosa matumaini wakati anapokabiliwa na changamoto, mazito na yasiyowezekana; hatopoteza msimamo na kujiamini kwake. Ulimwengu wa ndani wa mtu anaetekeleza ibada huwa na utulivu uliotengamaa. Kimbunga cha kisaikolojia, mikanganyiko na migogoro haitochukua nafasi katika maisha yake.

5. Ibada ndio njia kubwa kufikia ukamilifu wa mtu na kufikia ukomavu.

Kama inavyojulikana, mwanadamu ni kiumbe kidogo na dhaifu kwa kiwiliwili chake. Ingawa, anamiliki nafsi madhubuti na vipawa vikubwa vya akili. Fikra zake na matakwa yake hayana ukomo; fikra zake hazikuwekewa mipaka wakati alipoumbwa. 

Kitu kinachonyanyua na kukuza nafsi ya mwanadamu, ambae atakuwa na asili hiyo, ni ibada.

Kitu kinachokuza uwezo wake na akili zake ni ibada.

Kitu kinachonyanyua hisia na matamanio ni ibada. 

Kitu kinachomtambulisha malengo yake na kuyafanya upya matumaini yake ni ibada.

Kitu kinachohakikisha mawazo sahihi na hoja za msingi kwa kuziwekea kanuni za nidhamu fikra zake ni ibada.

Kitu kinachodhibiti hisia na mihemko, ambacho kinamlinda mtu asivuke mipaka na kuvuka kiwango katika utendaji wa mambo ni ibada.

Kwa ujumla, ibada ni kitu kinachomfanya mwanadamu kupata ukamilifu, Ukomavu wa kitabia na kiroho.

Maswali juu ya Uislamu

Author:
Maswali juu ya Uislamu
Subject Categories:
Read 902 times
In order to make a comment, please login or register
MASWALI YENYE KUFANANA