Ni nini zakah (zaka)? Zaka ina umuhimu gani kwa mtu anayeitoa na anayeipokea?

The Answer

Dear Brother / Sister,

Nini zakah?

Kilugha, zakah ni, kuongezeka, kusafika, wingi, maadili mema na kusifu; kama ilivyo istilahi ya kidini, inamaanisha kutoa sehemu ya mali kwa watu maalumu ili kumridhisha Allah.

Zakah, ambayo ni moja ya ibada za kifedha, ni moja ya nguzo tano za Uisilamu; iliwajibishwa katika mji wa Madina katika mwaka wa pili wa Hijria. Yafuatayo yameelezwa katika Quran:

“Na shikeni Sala, na toeni Zaka…” (al-Baqara, 2/43, 110; al-Hajj, 22/78; an-Nur, 24/56; al-Mujadala, 58/13; al-Muzzammil, 73/20);

Chukua sadaka katika mali zao, uwasafishe na uwatakase kwazo, na uwaombee rehema. Hakika maombi yako ni utulivu kwao. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kusikia Mwenye kujua.” (at-Tawbah, 9/103).

Umuhimu wa zakah (zaka) kwa mtu anayeipokea

* Zakah humuhifadhi mtu anayeipokea dhidi ya kuwa mtumwa wa mahitaji yake makuu. Hakuna kinachodhalilisha zaidi kama mtu kudharaulika na kutaabika na kuwahitaji wengine kwa sababu ya kutoweza kupata mahitaji yake ya lazima. Kwa hivyo, Mjumbe wa Allah (s.a.w.) ameeleza yafuatayo katika moja ya dua zake: Ewe Allah! Nakuomba taqwa, stara na neema kutoka kwako.”

* Zakah inamfanya masikini afanye kazi. Yafuatayo yanaelezwa katika hadithi: “Mkono unaotoa ni bora kuliko mkono unaopokea.” “Muumini mwenye nguvu ni bora kuliko muumini dhaifu.” Masikini atajaribu kuwa ni mkono unaotoa na sio mkono unaopokea; atajaribu kuwa mkakamavu na sio kuwa dhaifu. Isitoshe, hadithi ifuatayo inawahamasisha waumini kufanya kazi: “Hakuna aliyekula mlo bora zaidi kuliko yule aliyechuma kwa kazi yake.”

* Zakah inafifisha hisia za choyo kwa masikini. Inatokomeza chuki inayowaangukia matajiri. Hivyo, hakutakuwa na ubaguzi kati ya masikini na matajiri katika jumuia.

* Zakah inanyanyua hadhi ya masikini katika jumuia. Kwa kuwa, zakah ni haki ya masikini. Sio msaada wa matajiri. Matajiri hawataachwa bila ya jukumu hili isipokuwa wawatafute masikini na kuwapa zakah. Kwa kuwa masikini wanawaondolea matajiri jukumu la zakah, hadhi ya masikini ni ya juu katika jumuia.

Umuhimu wa zakah (zaka) kwa mtoaji

* Zakah humwokoa mtu dhidi ya kuhusudu kitu. Inavunja msururu wa uchu kwa binaadamu. Inauepusha moyo dhidi ya usugu na nafsi dhidi ya ushenzi.

* Zakah ni ufunguo wa kuwahurumia watu.

* Zakah huidumisha mali ya mtu. Mali iliyotumiwa kwa ajili ya jema la umma katika njia ya Allah haipotei bali hudumu milele.

* Zakah huunda na kutunza uwiano kati ya roho na kiwiwili.

* Zakah ni kielelezo cha shukurani za dhati kwa Allah. Shukurani zinazotamkwa kwa ulimi tu hazitotimiza wajibu wa shukurani za mali. Kushukuru kwa mali hutimizwa kupitia zakah na sadaqah.

* Zakah huitakasa mali. Zakah humsafisha mtu kutokana na ubakhili na sifa ya chuki, choyo, wizi na macho ya hasadi. Hivyo, inaboresha usalama wa mali na maisha ya binadamu.   

* Zakah humkinga mwenye mali dhidi ya kuwa mtumwa wa mali na kumkomboa. Yafuatayo yanaelezwa katika hadith:

 “Wale wanaohusudu dhahabu, fedha (pesa) na mahameli (anasa) wataangamizwa.”

* Zakah huuimarisha mwonekano wa matajiri na kuwaongoza katika heri. Inawaongezea hadhi yao katika jumuia.

* Zakah inaongeza mali. Inasababisha mali ikue na kuwa nyingi. Ipo ahadi iliyotolewa na Allah kuhusiana na suala hili.

Kutoa zakah hakusababishi mali kupungua.

* Zakah inamhimiza mtu mmoja mmoja kuwekeza.

* Zakah ni tiba ya kupenda dunia moyoni.

* Zakah inawakinga Waislamu dhidi ya fitina (majaribu) ya mali. Yanaelezwa yafuatayo katika aya:

“Hakika mali yenu na watoto wenu ni jaribio. Na kwa Mwenyezi Mungu upo ujira mkubwa.” (at-Taghabun, 15).

Yafuatayo yanaelezwa katika hadith:

 “Katika kila ummah kuna fitina (majaribu). Na fitina ya ummah wangu ni mali.”

* Zakah inamfanya Mwislamu kuwa na nidhamu kwa upande wa kipesa.

* Zakah inamkumbusha mtu mmoja mmoja juu ya umuhimu wa uwezo wa kipesa.

Maswali juu ya Uislamu

Author:
Maswali juu ya Uislamu
Subject Categories:
Read 883 times
In order to make a comment, please login or register
MASWALI YENYE KUFANANA