Ni upi uhalisia wa Imani?
Share
The Answer
Dear Brother / Sister,
Imani ni baraka kubwa na ni neema ya Allah kwa wanaadamu. Allah huwapa waja wake awatakao. Hata hivyo, haiwezi kudaiwa kuwa mja hana mchango wowote katika kuipata Imani.
Kinyume chake, mja anapaswa kutumia upendeleo na utashi wake kwanza na kuwa na nia ya kuamini na kuongoka. Allah atampa Imani na mwongozo kwa matakwa yake. Hivyo, baadhi ya wanachuoni wa Kiislamu na mawalii wameieleza Imani kuwa, “Ni nuru ambayo Allah mtukufu huiweka katika moyo wa mtu amtakaye baada ya huyo mtu kutumia sehemu yake ya utashi na upendeleo katika njia hiyo.”
Maswali juu ya Uislamu
