Nini maana ya Hajj? Ni zipi hekima za hajj na mantiki zake?

The Answer

Dear Brother / Sister,

Hajj ni aina ya ibada inayojumuisha matendo yote yanayowakilishwa.

Wakati wa hajj, mahujaji wanavaa nguo isiyoshonwa inayofanana na shuka linaloitwa ihram. Tendo hili linawakilisha kufariki na kuachana na mahusiano yote ya kidunia.

Waqfa kwenye Arafat ni mfano mdogo wa Siku ya Kukusanywa.

Mahujaji, wanaokwenda Muzdalifa huku wanatamka takbir baada ya Arafat, wanabakia huko usiku kabla ya sikukuu. Wanaanza safari ya kwenda Mina katika siku hiyo ya sikukuu ili kumrushia mawe Shetani. Kumrushia mawe Shetani ni alama na ushahidi wa kuvichukia vitimbi vyake na udanganyifu wa Shetani. Pia inamaanisha kuifwta sunnah ya kurusha mawe ya Nabii Ibrahim (a.s.).

Baada ya kuonesha kuchukizwa na shetani na kwamba watataabika dhidi ya shetani kwa kufanya kadiri wawezavyo kumrushia mawe Shetani kwa ishara, ambaye ni alama ya maovu, mahujaji wanachinja wanyama ili kuonesha kwamba wako tayari kuyatoa muhanga maisha yao katika njia ya Allah. Wanapitia kusalimu amri kwa tendo la kutolewa kafara katika njia ya Allah kama ilivyooneshwa na Nabii Ismail.

Hata kama kisingizio kitakuwa ni sahihi, hakiwezi kuwa ndio cha juu zaidi bila ya kuwa na watetezi na wafuasi walio tayari kuyatoa muhanga maisha yao. Hivyo, kwa kuwachinja wanyama, mahujaji wanaonesha kwa ishara kwamba watayatoa kafara maisha yao kwa ajili ya Allah ikilazimika.

Kutufu, yaani, kuzunguka Kaaba, ni ibada iliyotokana na mfumo wa ulimwengu. Ulimwenguni, sayari huzunguka jua, elektroni zilizo pembezoni mwa kiini na wadudu nondo wakiwa pembezoni mwa moto; kutokana na mzunguko huu, wanaonesha utiifu wao na upendo kwenye kitovu. Katika hali hii, kuzunguka Kaaba, ambayo ni ishara ya upwekeshaji, kunaashiria upendo na utiifu kwa dini.

Kila uzungukaji Kaaba unaashiria kwenda juu hadi mbingu ya 7 kwa kupitia awamu moja katika kila mzunguko, kwenda juu mpaka kwenye ngazi ya juu ya nafsi, ambayo ina ngazi ya 7, kuanzia ngazi ya chini zaidi katika ulimwengu wetu wa duniani, kufikia lengo la maisha ya binadamu na kuyafikia maisha ya kiroho.

Hekima na Manufaa ya Hajj

Hajj ina hekima nyingi, na manufaa ya kimwili na kiroho. Hebu tuorodheshe baadhi yake:

* Waumini wanakutana pamoja kwa lengo moja na imani shukurani kwa hajj. Umati mkubwa usiionekana pengine popote duniani unarudi kwa Muumbaji wa ulimwengu pamoja na umakini na msisimko wa ibada na kumsihi Yeye, kumwomba msamaha na kusali kwa ajili yake ili kuishi na kufa katika imani. Kwa furaha ya kiroho wanayoipata, wanaachana na tabia zao mbaya. Wanapata shauku ya kushikamana na maamrisho ya Allah.

* Wakiwa miguu chini bila ya viatu na vichwa wazi, mahujaji wakiwa wote wamevaa nguo nyeupe inaashiria Siku ya Mkusanyiko. Hivyo, nyoyo zitalainika, uangazaji macho utabadilika, misisimko itaonekana waziwazi na kutapitiwa na namna ya sikukuu ya kiroho.

* Mahujaji, wanaotambua utukufu wa Allah, aliyewajaalia mamilioni ya watu kukimbilia ardhi Tukufu kwa amri moja kwa karne 14, kwa misisimko yao yote, wanaona, kwa macho yao wenyewe, mamilioni ya watu wanaoamini mambo hayo hayo; hivyo, hawautilii maanani wasiwasi na udanganyifu wa Shetani. Imani yao inaimarika.

* Mahujaji wanapotembelea ardhi tukufu ilikotokea dini yao na kuenea duniani, ambapo watu wanaishindania, wameyatoa muhanga maisha yao na kumwaga damu zao, na wanapotembelea makaburi ya mashujaa wa kuheshimika watafundisha matamanio na shauku ya kuutekeleza na kuuhudumia Uisilamu. Watawaeleza kiukweli mujahidina hao na kusema, “tunaahidi kuyatunza mabaki matakatifu mliyotuachia na kuyahamisha kwa vizazi vijavyo baada yetu.”

* Mateso na shida zinazopitiwa wakati wa safari zinamfanya binadamu aheshimu baraka walizonazo na kumshukuru Mungu. Mtu kuwa mbali na mali yake, jamaa, na marafiki na asiweze kupumzika kutamkumbusha binaadamu matatizo ya masikini na kumfanya awaonee huruma na kuwasaidia.

* Hajj ina malipo ya jihad kwa sababu wakati wa hajj, mtu anasafiri, anapambana dhidi ya nafsi yake na kuvumilia matatizo na uchovu.

Mbali na mambo ya ulimwengu mwingine na manufaa ya kiroho yaliyotajwa hapo juu, hajj pia ina manufaa ya kimwili na kijamii.

* Hajj ni kama mkutano mkuu wa ulimwengu wa Kiislamu unaofanyika kila mwaka. Katika msimu wa hajj, Nchi za Kiislamu zina fursa ya kukubaliana masuala yao ya ndani na ya nje na kuwa kitu kimoja dhidi ya dunia. Pia zina fursa ya kujuana na kubadilishana mawazo yao kuhusu utamaduni, sayansi na sanaa.

* Katika msimu wa hajj, ambao ni kama maonesho ya kimataifa ya Nchi za Kiislamu, kila nchi inaweza kuonesha uwepo wake wa kimwili na kiroho. Watakuwa na Nchi za Kiislamu zisizoendelea na kuzisaidia ili zipate maendeleo.

Maswali juu ya Uislamu

Author:
Maswali juu ya Uislamu
Subject Categories:
Read 478 times
In order to make a comment, please login or register
MASWALI YENYE KUFANANA