Vipi muumini na kafiri huutazama ulimwengu?
Submitted by on Thu, 28/02/2019 - 11:10
Dear Brother / Sister,
Ulimwengu hutazamwa kupitia vioo viwili Kimoja ni kioo cha Imani na kingine ni kioo cha ukafiri.
Mtu anayeutazama ulimwengu kupitia vioo vya ukanushaji, ambavyo ni vioo vya ukafiri, ambavyo havikubali uwepo wa muumba huona kila kitu ulimwenguni kuwa ni bila ya mpango, bila ya mwenyewe, bila ya makusudio. Hajui na hawezi kufahamu kwa nini viumbe vimeumbwa na ni yepi majukumu yao ni kama mfano wa mtu aliyeachwa mlimani kwenye giza usiku ambaye chochote akionacho hudhani ni nyoka au dubwana na ambaye hafahamu majukumu ya viumbe hawa na wapoje.
Malengo na makusudio yake yote ni maisha ya kidunia. Hatambui maisha mingine yoyote zaidi ya maisha ya duniani. Kwa hivyo, anataka kutosheleza hisia zake zote katika dunia hii.
Hata hivyo, mwanaadamu amepewa hisia kwa mujibu wa ulimwengu wa ahera. Kila hisia ni kunjufu bila ya mpaka. Ni muhali kutosheleza hisia hizi hapa duniani. Kwa mfano, matakwa ya kuishi milele na matakwa ya kuwa na mali nyingi ni kunjufu bila ya mpaka. Hisia kama upendo na huruma hazina mpaka. Hatusemi “Napenda kiasi hiki cha watu. Hakuna nafasi ya kumpenda mtu mwingine moyoni mwangu.” Hata tukimpenda kila mtu, ukubwa wa hisia hii haujai.
Hata kama mtu anayeutazama ulimwengu kupitia vioo vya ukafiri ataona viumbe vingi kuwa ni vyenye maana, hekima na kusudio, hawezi kuvifahamu. Kwa vile kwa mtu kama huyo watu waliyotangulia wamekufa na kupotea. Watu watakaokuja pia watapotea na kuharibika. Kwa hivyo, hujiona baina ya makaburi mawili na kama kiumbe ambaye atakaye haribika na kupotea karibuni. Mtu kama huyo hawezi kupata raha wala ladha yeyote kutoka duniani kwa kuogopa kwake umauti ni kama mtu aliyehukumiwa kifo anasubiri kunyongwa.
Mtu anayeuangalia ulimwengu kupitia vioo vya ukanushaji hutegemea akili yake na kupima kila kitu kwa akili yake kana kwamba akili yake imechaguliwa kuwa ni mhandisi wa ulimwengu; ana utajiri wa tajiri na umasikini wa masikini. Hupinga pale anaponyimwa nafasi nzuri zaidi na wepesi.
Katika Qur’an utajiri wa Karun umeelezwa, ambao utaangazia jambo hilo. Karun alikuwa tajiri kiasi cha kushindwa kubeba funguo za hazina yake mwenyewe. Watu waliuangalia utajiri wake na kusema, “Tunatamani tungelikuwa na utajiri kama huo.” Hata hivyo, Karun hatimizi wajibu wake wa kuwa tajiri na hatoi zaka, ambayo ni haki ya masikini, na halipi mishahara ya wafanya kazi wake kwa ukamilifu. Anadai kuwa ameupata utajiri wake kutokana na elimu yake.
Allah alipomfukia yeye na mali yake chini ya ardhi, watu waliyotaka kuwa kama yeye walisema, “Tunamshukuru Allah kwa kutotupa utajiri kama huo. Hatutaki kuwa katika nafasi ya Karun.”
Mtu anayeichukulia akili yake kuwa ni mhandisi wa kuamua muundo wa ulimwengu na ambaye ana uadui dhidi ya Allah kwa sababu hakupewa vitu fulani hapaswi kupuuza hadithi hizi zilizoelezwa katika Qur’an. Anapaswa kuwa na furaha na sio huzuni kwa sababu hakupewa vitu ambavyo majukumu yake asingeweza kuyatimiza. Kwa kuwa, Allah anatueleza kuwa kila mmoja ataulizwa kwa kila neema aliyonayo, hata maji anayokunywa mtu na hewa anayovuta.
Mtu anayeuangalia ulimwengu kupitia vioo vya Imani huona ulimwengu ni kama nyumba nzuri ya wageni na sehemu iliyopambwa kwa maua ambapo aina zote za neema na chakula hupatikana. Anahisi shukrani kubwa kwa Muumba wake, aliyembadilisha kutoka maumbile kwenda katika maumbile mingine kuanzia wakati ambapo alikuwa katika fuko la uzazi, aliyemuumba mwanaadamu na sio jiwe, mmea, au mnyama, aliyempatia vipawa kama akili, kufikiri, na kumbukumbu na aliyemkabidhi viumbe vyote vilivyo hai na visivyo na uhai ulimwenguni.
Anapoangalia wakati uliopita, anafahamu kuwa safari iliyoanza kwa baba zake Hz. Adam na Hz. Hawa (Eve) itaishia peponi, kwamba atakuwa pamoja na watu wote awapendao na jamaa huko milele na atakuwa mwenye kupewa aina zote za neema na Muumba wake kwa kuendelea. Anafahamu kwamba dunia si kituo kikuu bali ni chumba cha kusubiria na kituo cha mtihani njiani kuelekea ahera.
Anafahamu kwamba misiba kama maradhi na tetemeko la ardhi ni lazima ili kujaribiwa na hushukuru kwa kuonesha subira na kufikiri kuwa shida na matatizo anayokabiliana nayo hapa yatampa malipo kesho ahera.
Anapokabiliwa na matukio ambayo maana yake hasa hawezi kufahamu husema kama Ibarahim Haqqi anayesema,
“Allah huubadilisha ubaya kuwa uzuri, (Yaani, kuna kitu kizuri nyuma ya kila kitu tukionacho ni kibaya au shari. Allah hukifanya tukionacho kibaya kizuri kwa ajili yetu.)
Usifikirie Allah anafanya jambo jingine, (Yaani, kuna wema na uzuri katika kila kitu akiumbacho Allah. Akiumbacho si vingine ila ni kizuri.)
Mtu mwenye akili hukiangalia, (Mwenye akili, yaani, mtu mwenye elimu hukiangalia tu. Hajaribu kupinga vitu ambavyo sababu na maana zake hafahamu.)
Hebu tuangalie atakalolifanya Allah,
Lolote alifanyalo, hulifanya vyema.
Usiseme kwa nini lipo hivi,
Lipo kama linavyotakiwa liwe,
Kuwa na subira na tazama mpaka mwisho,
Hebu tuangalie atakalolifanya Allah,
Lolote alifanyalo, hulifanya vyema.
Hata kama akili yake haiwezi kuelewa, anajua kuwa Allah hufanya jambo katika njia iliyo bora zaidi.
Maswali juu ya Uislamu