Vipi tunaweza kuimarisha Imani yetu?

Submitted by on Fri, 01/03/2019 - 11:56
Dear Brother / Sister,
Imani ni nuru, baraka kutoka kwa Allah. Hata hivyo, Imani ni elimu wakati huo huo, ambayo ni lazima isomwe. Kuna njia mbili za kuimarisha Imani yetu:
Njia ya kwanza na ya msingi ni kanuni za Sunnah na kuchunguza kwa mujibu wa Qur’an na Hadithi, kama inavyohitajika katika wakati wetu.
Njia ya pili ni kupanda daraja katika mambo ya kiroho kupitia kutekeleza matendo mema, kuutakasa moyo na roho kwa kuepuka dhambi.
Hata hivyo, hali ya karne hii inaifanya njia ya pili kuwa ngumu kuifuata. Kwa sababu hii, ni muhimu sana kusoma vitabu vinavyofunza Imani ya kuchunguza. Pia imekuwa muhimu kusoma sayansi kama sifa ya karne yetu, ukiachia mbali kusoma masomo ya dini. Hii ni kwa sababu nuru ya akili ni sayansi kama ilivyo nuru ya moyo ni masomo ya kidini. Tunaweza kusema kuwa moja kati ya vitabu muhimu vyenye kufundisha yote mawili ni mkusanyiko wa Risale-i Nur. Kwa kuongezea, mtu anaweza kufaidika sana na vitabu vya watu maarufu kama imamu Al-Ghazali, Imamu Al-Rabbani, Imamu Mawardi na Imamu Qushairi.
Kuilinda na kuiimarisha Imani ni jambo muhimu zaidi kwa muislamu. Ni muhimu kuipa umuhimu Taqwa (Kumcha Allah) ili kuilinda Imani. Imani inaweza tu kulindwa ndani ya ngome ya Taqwa. Bila ya Taqwa, Imani hushuka. Ni muhimu kusoma na kufanya utafiti katika vitabu vinavyohusu Imani sana ili kuiimarisha Imani. Mambo ya Imani yanayotokana na elimu hayana taathira katika hisia za mtu labda yanapochujwa kupitia hoja. Kwanza, akili lazima iridhike.
Kutafakari ni muhimu sana. Ukweli wa mtume Ibrahim kumtambua Mola wake kwa kuangalia mwezi na nyota na kutafakari umeelezwa katika Qur’an. Imani huboreka kwa tafakuri. Kwa sababu hiyo, imeelezwa katika Qur’an kuwa
“Kutafakari kwa muda wa saa moja ni bora kuliko sala za sunna za mwaka mzima.”
Mazingira yana taathira kubwa kwa wanadamu. Dhambi hushauri watu ukafiri. Shauri lina taathira kubwa kwa wanaadamu. Linaingiza ukafiri ndani ya sehemu ya kutojitambua ya mtu bila ya watu kutambua. Kwa sababu hiyo, mtu anapaswa kuwa mbali na sehemu za dhambi kwa kadiri itakavyowezekana. Dhambi zinazotendwa bila ya mazingatio hushawishi watu kuwa hakuna akhera wala kuadhibiwa. Ili kulindwa na taathira hasi za mashauri kama hayo, mtu anapaswa kuwa mbali na sehemu za dhambi kadri awezavyo na kujaribu kuwashauri watu kuhusu wema na kuwakinga na shari kadri awezavyo. Mtu anapaswa kusoma mambo kuhusu Imani sana na kuwa makini na ujumbe unaotolewa ili kufidia uharibifu wa mashauri hasi aliyopewa. Ni muhimu kukutana na watu ambao wanajali kuhusu matendo mema na wanaishi kwa mujibu wa Taqwa. Katika hali kama hiyo, umuhimu wa jamii unadhihirika zaidi. Kama ilivyo dhambi kuwa inashauri hiana, matendo mema yanashauri Imani.
Maswali juu ya Uislamu