Ni nini Haram?
Dear Brother / Sister,
Ni vitu vyote ambavyo vimekatazwa na dini yetu kutendwa, kutumia, kula, au kunywa basi hivyo ni haramu; kwa mfano, kunywa vilevi, kamari, kufanya uzinzi, kuua mtu, kusengenya, kuzua… Ikiwa kitu au kitendo kimefanywa kuwa haramu kutokana na madhara, uovu na uchafu ambao unapatikana katika kitu au kitendo hicho, kinajulikana kama haramu kwa hali yake (haram liaynihi ) au kwa dhati yake (kilivyo) [haram lidhatihi]; kwa mfano, nyama ya nguruwe na pombe. Ikiwa kitu kitaitwa haramu si kwa sababu ya kilivyo au hali yake lakini ni kwasababu zilizo nje ya kitu au kitendo hicho kama vile njia ya kukipata, basi hujulikana kama haramu kwa kinyume chake (haram lighayrihi); kwa mfano, mkate ulioibwa, fedha iliyoporwa …
Maswali juu ya Uislamu

