Je inaweza kuthibitishwa kupitia ushahidi wa Quran kuwa Uisilamu sio dini ya ugaidi bali ni kinyume chake inakataza gaidi, vurugu na fitina?

The Answer

Dear Brother / Sister,

Quran imekemea vikali ugaidi na kuzielezea vurugu na fitina kuwa ni mambo maovu mno.

Uisilamu umekataza aina zote za ugaidi, dhuluma, na usaliti na kupinga aina zote za vurugu na tabia mbaya. Uisilamu haujibu uovu kwa uovu. Dini ya Uisilamu imeletwa na Allah Mtukufu ili kusimamisha haki, kuvunja udikteta na dhuluma za kiholela za uovu wa kikatili na kuifanya dhamiri ya mtu kuchemka. Hivyo, Uisilamu uko makini mno kuhusu hilo. Quran unayazingatia mauaji ya mtu asiye na hatia kuwa ni mauaji mabaya kabisa yaliyofanywa dhidi ya watu wote.

Allah Mtukufu anatangaza “… aliye muuwa mtu bila ya yeye kuuwa, au kufanya uchafuzi katika nchi, basi ni kama amewauwa watu wote. Na mwenye kumuokoa mtu na mauti ni kama amewaokoa watu wote… (al-Maidah, 32) Quran pia inalaani aina zote za fitina. Quran inatutanabahisha juu ya vichochezi na kueneza fitina ya wale wanaoanzisha mfarakano, wanaosababisha uhasama katika maisha ya jamii, na kueneza uhasama akiwa katika madaraka, na pia inaonesha bayana kitisho cha kueneza ufisadi, na uzito wa uhasama: “Na anapo tawala hufanya juhudi katika nchi kwa kufisidi humo na kuteketeza mimea na viumbe. Na Mwenyezi Mungu hapendi ufisadi.” (al-Baqarah, 205)

Quran imekataza fitina, katika sura al-Baqarah, 217, Allah Mtukufu anatangaza: “Na fitina ni mbaya zaidi kuliko kuuwa.” (Al-Baqarah, 217)

Ndani ya nafsi ya Mwisilamu, anayezitumia aya hizi za Quran kwa kiwango kikubwa, mnakuwa hamna uadui, chuki na ukatili. Umo undugu fulani hata kati ya adui yake mkubwa. Mwisilamu anaukubali ukweli, ambao, “tunamvumilia kiumbe kwa sababu tu ya Muumbaji.” Mwisilamu ni mtetezi wa upendo. Hana muda wa uhasama. Katika Quran Tukufu, Allah Mtukufu amewazindua waumini wajiepushe na madhara ya sehemu za ibada, kwa kuashiria kuwa sehemu za ibada zimehifadhiwa dhidi ya watu fulani kutokana na uingiliaji kati wa watu wengine: “… Na lau kuwa Mwenyezi Mungu hawakingi watu kwa watu, basi hapana shaka zingeli vunjwa nyumba za wat’awa, na makanisa, na masinagogi, na misikiti, ambamo ndani yake jina la Mwenyezi Mungu linatajwa kwa wingi.” (al-Hajj, 40) 

Mtume Muhammad ni mtume wa huruma na upendo. Katika Quran Tukufu, Allah Mtukufu anaeleza: “Nasi hatukukutuma ila uwe ni Rehema kwa walimwengu wote.” (al-Anbiya, 107) Mtume (S.A.W.) ameonesha maadili yote mema kwa namna bora zaidi katika maisha yake na kuinasihi jumuia yake kujiepusha na fitina. Aliwaamuru kujiweka mbali na fitina kwa uzito usio na kifani na kwa umakini:

Jihadharini na fitina! Kwa kuwa, wakati ule ule, ulimi ni kama pigo la upanga. (Ibn Majah, Fitan, 24)

 “Hapa pana uhakika kuwa kutatokea fitina, mfarakano na mgogoro. Itakapotokea hali hii, nenda Uhud na upanga wako. Upige jiwe kubwa mpaka livunjike vipande vipande. Kisha bakia nyumbani kwako. (Usitoke nje) hadi utakapokufikia mkono wa dhambi au kifo kikufikie nyumbani kwako.” (Ibn Majah, Fitan, 24) Ni kabla ya Siku ya Kiama, kutakuwa na fitina kama vipande vya usiku wa giza. Wakati wa fitina hiyo, mtu ataamka asubuhi hali ya kuwa ni muumini, lakini ataishia kuwa kafiri ifikapo usiku; ikifika usiku atakuwa muumini lakini ikifika asubuhi atakuwa kafiri. Wakati wa fitina hiyo, mwenye kukaa atakuwa bora zaidi ya mwenye kusimama wima. Hivyo vunjeni pinde zenu, vurugeni mishale yenu na mapanga yenu yapigeni kwenye mawe. Kama itaingia ndani ya nyumba ya mmoja wenu, uwe yule mbora zaidi kati ya wana wawili wa Adam (kuwa utakayeuliwa sio muuaji). (Abu Dawud, Fitan 2, Tirmidhi, Fitan 33)

Maswali juu ya Uislamu

Author:
Maswali juu ya Uislamu
Subject Categories:
Read 347 times
In order to make a comment, please login or register
MASWALI YENYE KUFANANA
THE MOST ASKED QUESTIONS