Ni zipi nguzo za Uislamu?

Submitted by on Wed, 08/08/2018 - 11:49
Dear Brother / Sister,
Dini ya Uislamu imejengwa juu ya nguzo tano. Nazo ni: saumu, salah (kuswali), Hajj (kuhiji Makka), Zakat (Kutoa zaka), kushuhudia Upweke (tauhidi ya) wa Allah na utume wa Mtume Muhammad (Shahadah).
Nguzo mojawapo ya Uislamu ni kufunga katika Mwezi wa Ramadhani. Kwa njia ya saumu, Waislamu wanajikinga dhidi ya kutawaliwa na nafsi yenye uovu kwa kuitia nidhamu na kuitakasa. Na hapo inakuja hisia ya kuwahurumia masikini katika nyoyo zao kwa kuhisi maumivu yao ya kuwa na njaa.
Nguzo nyingine ya Uislamu ni kuswali. Inamaanisha kusimama mbele ya Allah mara tano kwa siku kwa mtu kujifahamu udhaifu wake na upungufu kwa kuinama na kusujudu na kuonesha utumwa Kwake. Swala za faradhi ni ibada ya wote na shukrani ya wote. Kila Muislamu ni lazima atekeleze. Mtume Muhammad (s.a.w) aliamuru: Swala ni nguzo ya dini (Tirmidhi, Iman-8)
Nguzo nyingine ya Uislamu ni Hajj (Kwenda Hija katika mji mtakatifu wa Makka). Wameamrishwa Waislamu wenye uwezo wa mali na wa kiafya kulingana na sheria ya Kiislamu, kwenda Hajj angalau mara moja maishani katika msimu mahususi uliopangwa na sheria (Shariah) ya Kiislamu. Mojawapo ya hekima za ibada hii, ambayo ni ya lazima, ni Waislamu wa dunia nzimakuweza kukutana na kudhihirisha kuwa watu wote wako sawa mbele ya Allah (SWT) pasi na kujali utaifa, lugha, rangi ya ngozi, na hadhi ya kijamii.
Nguzo nyingine ya Uislamu ni kutoa zaka (Zakah), ambayo ni nguzo ya mwisho ya Uislamu. Allah Mtukuka amewafaradhishia Waislamu matajiri, kwa ajili ya Allah, kwa kuwapa, Waislamu masikini kiasi (2.5 %) katika mali zao, kilichopangwa na Uislamu. Mali hii, ambayo tajiri humpa masikini, huitwa Zakah. Kwa mujibu wa sheria ya Kiislamu, hii ni haki ya maskini. Uislamu unawahimiza Waislamu kuwasaidia masikini hata kwa njia isiyokuwa ya Zakah pia. Nazo huitwa sadaqah (sadaka).
Ili kuweza kuwa Muislamu, ni lazima mtu atamke kalima ash-shahada. Maana ya kalima ash-shahada ni kama ifuatavyo "Ninashuhudia kuwa hakuna mwenye haki ya kuabudiwa isipokuwa Allah na kwamba Nabii Muhammad ni mja Wake na mjumbe Wake."
Sehemu ya kwanza ya shahada inaeleza kuwepo kwa Allah na upweke (tauhidi Wake na kuwa Hana washirika au washindani. Sehemu ya pili inaeleza kuwa Nabii Muhammad (s.a.w) ni mja wa Allah na kwamba aliteuliwa na Allah kuwafikishia watu Misingi ya imani na nguzo za Uislamu.
Maswali juu ya Uislamu