Je, inawezekana kuona ishara zinazohusu kuwepo kwa Allah kwa kuangalia katika ulimwengu?

The Answer

Dear Brother / Sister,

Ni jambo lenye kupendeza kuwa Allah anaaziita sentensi zake mbili (aya) ndani ya Qurani na kazi zake katika kitabu cha ulimwengu (aya) (ishara). Ndani ya Qurani, moja kati ya ishara zilizotajwa mara nyingi za ulimwengu ni mbingu. Allah mara nyingi huelekeza mazingatio katika mbingu ambayo kila mtu huiona wakati wote na mara nyingi hupendezewa nayo.

 “Je! Hawaangalii mbingu zilizo juu yao! Vipi tulivyozijenga, na tukazipamba…” (Qaf, 50/6) 

Yafuatayo yameelezwa katika aya nyingine:

“Na katika Ishara zake ni kuumba mbingu na ardhi, na kutafautiana ndimi zenu na rangi zenu. Hakikakatika hayo zipo Ishara kwa wajuzi.” (ar-Rum, 30/22)

Aya ya kwanza inatuamrisha kuangalia katika ulimwengu na kutafakari. Aya ya pili inasema kwamba wale wenye kupata elimu ya uumbaji wa mbingu na ardhi na wale wanaotafakari kwa kutumia elimu hiyo wataona shuhuda kuhusu kuwepo kwa Allah. Aya hizi ziliteremshwa zaidi ya karne ya kumi na nne zilizopita. Kumekuwa na maendeleo makubwa kuhusu elimu ya mwanadamu juu ya anga tokea hapo. Tawi jipya linaloitwa elimu ya falaki limeundwa. Hatuwezi kutoa maelezo yote hapa. Tutajaribu kufahamu namna ya kusoma ishara za Allah kwa kutumia maelezo mapya ambayo tumeyapata kuhusu anga kupitia mfano mmoja.

Shuhuda kutoka katika anga juu ya kuwepo kwa Allah.

Tunapoangalia mbingu, inaonekana kama kuba nzuri ni kama iliyopambwa kwa dhahabu katika kasri ya Dunia hii. Katika mtazamo mwengine inaonekana kama bahari ya anga ambayo ndani yake mamilioni ya safina husafiri kwa kasi sana. Na bado katika mtazamo mwengine inaonekana kama mkusanyiko wa ndege ambazo ni kubwa mara mabilioni kuliko ndege zilizotengenezwa na mwanadamu na ambazo ni zenye kutembea kwa kasi zaidi.

Umewahi kufikiri kuna nyota ngapi mbinguni? Kumekuwa na majaribio mengi ya kujibu swali hilo lakini hakuna aliyeweza kupata jibu sahihi. Mnamo mwaka 2003, kundi la watafiti kutoka chuo kikuu cha taifa cha Australia walifanya makadirio kwa kutumuia vifaa vya kisasa vya teknolojia. Namba waliyoipata ilikuwa ni 70.000.000.000.000.000.000.000 (seventy sixtrilion). (1)

Kwa mujibu wa wanasayansi hao hao, idadi ya nyota angani ni nyingi mara kumi zaidi kuliko idadi ya chembe za mchanga ardhini. Tunapoifikiria kwa kipimo cha anga, mapigano ya umiliki wa dunia ni kama mapigano ya watoto kwa chembe moja ya mchanga. Mwisho, hata tukiumiliku ulimwengu wote tutakacho kimiliki hakitakuwa hata sehemu moja ya kumi ya chembe ya mchanga katika kipimo cha anga.

Kitu gani nyota na sayari ambazo idadi zake hatuzifahamu zinatueleza? Allah anatutaka tufikiri kuhusu namna gani zimekuja katika uwepo na namna gani zinatembea kwa mfumo wa kupendeza na kuelekeza mazingatio yetu kwazo. Tunaweza kuziweka idadi za nyota zisizo hesabika chini ya mwanga wa vipawa, elimu, na uzoefu tulionao. Tunaweza kufahamu namna viumbe hivi vya mbinguni vilivyokuja katika uwepo kwa kuvilinganisha na kitu kilicho tengenezwa na wanadamu.

Mwanadamu hajaweza kutengeneza nyota bado; hata hivyo, nchi zote zinajaribu kutengeneza sayari ndogo iitwayo Kituo cha anga cha kimataifa kwa kuunganisha nguvu zao. Kisha, tunaweza kufahamu, kwa kiasi fulani, namna nyota na sayari zilivyokuja katika uwepo kwa kuangalia sayari ndogo iliyotengenezwa na mwanadamu. Ninapotumia neno ndogo, usifikiri kwamba ninadharau moja kati ya kazi nzuri ya mwanadamu. Kwa kweli, najisikia fahari katika jina la ubinadamu kwa kazi hii nzuri, ambayo sitoweza kuifahamu hata nikitumia maisha yangu yote. Nataka kusema kwamba ni ndogo inapolinganishwa na ulimwengu pamoja na sayari nyengine. Ikiwa watu hapa wanajaribu kutengeneza kituo kingine cha anga, hawatoweza kufanya hivyo kwa sababu hatuna mamia, maelfu ya wanasayansi na wahandisi wa kufanya hivyo. Hatuna viwanda vya kuzalisha vifaa vya lazima. Yaani, ni lazima kuwa na elimu na elimu iliyoendelea katika matawi mengi ya sayansi kama fizikia, uhandisi, baiolojia, na hesabati ili kutengeneza sayari ndogo. Nguvu kazi na mashine pia ni lazima ili kuifanyia kazi elimu hiyo. Kwa ufupi sayari ndogo ni kazi ya daraja ya juu ya elimu na nguvu kubwa. Basi, trilioni za nyota na sayari ambazo ni kubwa zaidi na nzuri zaidi kuliko kituo cha anga cha kimataifa, ni kazi ya dhati ambayo ina elimu na nguvu isiyokuwa na mwisho. (2)

Mtu anayeangalia anga kwa umakini anaona kuwa inamuashiria Allah kwa uwazi zaidi kuliko maneno ya kiarabu “laa ilaaha illa llah” (Hakuna mola ila Allah). Kwa kuwa, kama ulimwengu utafananishwa na kasri, mwezi ni taa yetu ya usiku, jua ni jiko na taa yenye mwanga mkali, na nyota nyengine ni zenye kupambwa kwa dhahabu na taa ndogo zilizopambwa. Basi, nani aliyeziumba nyota hizi, jua na mwezi? Quran inajibu swali hili kama ifuatavyo;

“Ameziumba mbingu na ardhi kwa Haki. Ametukuka na wanayo shirikisha.” (an-Nahl, 16/3).

“Na amefanya ukutumikieni usiku na mchana, na jua na mwezi, na nyota zikutumikieni kwa amri yake. Hakika katika hayo zipo ishara kwa watu wenye akili.” (an-Nahl, 16/12).

Haliwi jua kuufikia mwezi, wala usiku kuupita mchana. Na vyote vinaogelea katika njia zao. (Yasin, 36/40).

Na jua linakwenda kwa kiwango chake. Hayo ni makadirio ya Mwenye nguvu, Mwenye kujua. (Yasin, 36/38).

Aya mbili zilizopita zinaashiria mzunguko wa jua. Sayansi ya falaki imegundua kwamba jua lilikuwa likizunguka katika karne ya ishirini tu, lakini ukweli kwamba Hz. Muhammad (s.a.w), ambaye hakuweza kusoma au kuandika ametueleza kuhusiana na hilo karne kumi na nne zilizopita ni ushahidi kamili kwa utume wake.

Kwa mujibu wa elimu ya falaki ya sasa, jua linatembea 225 km kwa sekunde, kilomita 13.500 kwa dakika na kilomita 810.000 kwa saa moja. Tukifikiria kasi ya ndege iyendayo kwa kasi zaidi namna inavyotembea, tunaweza kufahamu kwamba jua linatembea mara 100 kwa kasi zaidi kuliko ndege iendayo kwa kasi zaidi.

Katika ndege ya kigiriki mnamo mwaka 2005, marubani wawili walifariki kutokana na baridi kwa sababu mfumo wa kupooza hewa ulileta hitilafu na ndege ikagonga mlima katika dakika kadhaa. Basi, vipi trilioni za ndege (nyota na sayari) ambazo ni kubwa mara mabilioni na zenye kasi mara maelfu kuliko ndege zetu zinatembea bila ya kugongana na kuanguka ilhali hazina marubani? Tunapolinganisha nyota na sayari na ndege zilizotengenezwa na mwanadamu, tutaona kuwa dhati yenye elimu isiyo na mwisho, nguvu na hekima imeumba nyota hizo na kwamba yeye kwa kuendelea anazihifadhi na kuzidhibiti. Na hiyo ni ni sababu haya yameelezwa katika Quran;

“Hakika Allah ndiye anaye zuilia mbingu na ardhi zisiondoke. Na zikiondoka hapana yeyote wakuzizuia isipo kuwa Yeye.” (Fatir, 35/41)

Japo kuwa tumetengeneza mfumo wa kujihami dhidi ya makombora yaliyotengenezwa na mwanadamu, hatuwezi kufanya kitu bali kuangalia “makombora ya angani” ambayo yanaweza kutuangukia toka angani.

Shuhuda za kuwepo kwa Allah kutoka katika ulimwengu wa mimea.

Sio nyota tu pekee bali kila kitu tukionacha ambacho kimetezunguka kinatueleza kuhusu Mola wetu kupitia ndimi tofauti. Isha nzuri zaidi zenye kutueleza kuhusu Allah katika sayari ya bluu tunayoishi ni mimea na wanyama na wanadamu. “Maisha”, ambayo ni muhuri wa kiungu wanaoshiirikiana wote, unatuonesha Allah katika kila nyanja. Ni Allah ambaye ni Al-hayy (Aliye hai) na Al-Qayyum (Msimamizi), anayetoa uhai na kuuhifadhi. Qurani inaeleza ukweli huu kama ifuatavyo:

“Kwa hayo (maji) Yeye anaizalisha kwa ajili yenu mimea, na mizaituni, na mitende, na mizabibu, na kila namna ya matunda. Hakika katika haya zipo ishara kwa watu wanao fikiri.” (an-Nahl, 16/11).

Aya hii kwa uwazi inaeleza kuwa mimea imeumbwa kutokana na maji na Allah na kwamba kuna mafunzo makubwa ndani yake kwa wale wenye kutafakari. Sayansi inakubali kwamba asili ya uhai kwa sasa ni maji lakini haijaweza kufahamu kwa ukamilifu uhai ni kitu gani. Hata hivyo, kuna wanyama hai na mimea katika kila inchi ya sayari yetu.

Katika mwaka 2014 wanasayansi wa elimu ya mimea wameamua kuwa kuna spishi 350,000 za mimea. Yote hii ni yenye kufanana na yenye kutofautiana. Kwa vile yote imeundwa kutokana na atomu, elementi, molikuli na seli ambazo ni zenye kufanana; Kwa vile zina miundo tofauti na zina DNA tofauti, zinatofautiana.

Usiidharua mimea. Hakuna mwanadamu awezaye kufanya kinachofanywa na mmea mmoja. Kama tutataja kwa mujibu wa kila tendo linalofanywa na jani la kijani, itakuwa inaendana kuliita kila jani “kiwanda cha oksijeni na chakula”. Mwanadamu ameelewa kidogo kile kilichokuwa kinafanywa na jani la kijani kwa muda wa miaka milioni kati kati ya karne iliyopita. Dr. kelvin amepata tuzo ya Nobel kwa sababu alielezea moja ya stadi za jani la kijani. (3) Katika maneno mengine, baada ya kufanya juhudi kwa karne nyingi baadhi tu ya wanadamu wenye akili ndio wamekuja kufahamu kidogo kile kinachofanywa na mimea ya kijani. Hata hivyo, hakuna mwanasayansi anayeweza kufanya kinachofanywa na mimea. Kwa hivyo, tunapomuambia mtu wewe ni mfano wa nyasi huwa tuna msifu na kukashifu nyasi. Pengine anastahiki kuitwa nyasi mtu mwenye akili sana hata kupata zawadi ya nobel.

Mimea ambayo tunaidharua kwa kuita nyasi ni watumishi wetu, ambayo inajitoa muhanga kwa ajili yetu. Inatoa oksijini, ambayo ni hitajio letu kubwa, kwa kufanya kazi kwa kuendelea na hutoa vitamini vya lazima na protini kwa ajili ya miili yetu; inajitoa muhanga maisha yao kwa ajili ya kuendelea kwa maisha yetu. Wanadamu hutumia spishi zaidi ya elfu nne za mimea na wanyama kama chakula. Miti inafanya kazi kama viwanda vikubwa na kutuandalia chakula. Hatushukuru kikamilifu huduma ambayo mimea inatupa kwa sababu hatufikirii kuhusu ilo. Kutokana na pazia la sababu tunarejesha matunda kwa miti na mboga mboga bustanini. Hatuvipi thamani yake halisi. Kama tutajaribu kutengeneza tunda katika kiwanda, tusingeweza kununua tunda moja hata kwa bilioni 1 ya dola. Wingi wa chakula hauoneshi kwamba havina thamani bali huonesha wingi wa rehma. Kwa hakika, oksijini, ambayo ni kirutubisho chenye thamani zaidi kwetu ni bure lakini sio kama haina thamani. (4)

Kila mmea, kila tunda na kila mboga mboga ni neema ya kiungu ya kimaajabu na zawadi nzuri kutoka kwa mola. Jaalia kwamba kampuni imetoa biskuti zenye mbegu na ulipozipanda mbegu za biskuti, ukapata miti ya buskuti; utashangazwa. Itagonga vichwa vya habari na televisheni zitautaja mti huo. Kwa kweli, ni lazima kustaajabishwa na mtu anayestaajabishwa na biskuti kuwa na mbegu lakini kuzingatia maelfu ya matunda na mboga mboga zenye mbegu ni kawaida.

Sayansi ya sekula na falsafa isiyo na dini inaficha kazi ya kiungu ambayo ni miujiza kutoka katika nyanja zote nyuma ya pazia ya asili na sababu, kuzifanya zionekane za kawaida. Wanazifanya kazi za mwanadamu ambaye hubadilisha vitu viliopo katika miundo tofauti zionekane za kimaajabu. Katika kitabu chake cha mwisho alichotuteremshia Allah anatuuliza mara thelathini na moja:

 “Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayoikanusha” (ar-Rahman, 55/13,)

Kama tutatumia akili zetu na kuthamini na kushukuru thamani ya kila neema, hatuwezi kukana yeyote kati ya neema hizo. Hata hivyo, kama tutarejesha neema hizi kwa asili na kwa bahati, tutazikana zote. Mamia ya maelfu ya spishi ambazo zina vitamini na protini ambazo wanyama na wanadamu wanahitajia, na kwamba zinaendana na ladha yao, mdomo, meno, na tumbo ni katika shuhuda za wazi za rehema ya Allah. Mtu mwenye akili anaweza kumtambua mola wake hata kupitia tufaha moja. Muundo wa kimajabu wa tufaha, ambao umeundwa bila ya teknolojia (5) katika daraja la atomu, mulikuli, na seli unaonesha elimu isiyo na mwisho, nguvu na hekima ya mmiliki wake; uhusiano wake na makubaliano na jicho la mwanadamu, jino, ladha na tumbo huoenesha huruma isiyo na mwisho, rehema na msaada.

Mtu anayetumia akili yake vizuri anaweza kumtambua mola wake kwa kutazama tufaha moja. Ndio, mtu anayeweza kufahamu tufaha moja tu anaweza pia kufahamu kuwepo kwa mola wake. Kama nilivyotaja hapo mwanzo, usilidharau tufaha. Ni lazima kuandaa kiwanda kikubwa kama ulimwengu na kupanda mti ambao una seli hai ili kutenegeneza tufaha moja. Mtu asiyeweza kutengeneza seli moja hawezi kutengeneza mti wenye bilioni za seli kwa namna yoyote, jaalia ameweza asingeweza kuwa na taathira kwa jua na asingeweza kuratibu joto lake kuivisha tufaha, tunaweza kuoredhesha maelfu ya hali kama hii ya lazima kwa kutengeneza tufaha.

Badiuzzaman Said Nursi anaelezea kwa ufupi tulichokimaanisha hapo juu kama ifuatavyo:

“Anayeumba tufaha bila shaka lazima awe na uwezo wa kuumba matufaha yote ulimwenguni na kuleta majira ya kuchipua katika uwepo. Kinyume chake, asiyeweza kuumba majira ya kuchipua hawezi kuumba tufaha moja vile vile, kwa kuwa tufaha huundwa kutoka sehemu hiyo hiyo moja. Lakini anayetengeneza tufaha anaweza kutengeneza majira ya kuchipua. Kila tufaha ni mfano wa mti mdogo, hata wa bustani au wa ulimwengu mzima. Mbegu ya tufaha inayobeba ndani yake maisha ya mti mkubwa, kutoka katika mtazamo wa kisanaa, muujiza kama huo, anaye uumba mti na kama hivyo basi anaweza kufanya kila kitu.” (6)

Kwa hivyo, Qurani inatutaka tule kwa kufikiri namna chakula tunachokila huundwa, badala ya kula kwa lengo la kujaza matumbo yetu tu:

“Hebu mtu na atazame chakula chake. Hakika Sisi tumemimina maji kwa nguvu, Tena tukaipasua pasua ardhi kwa nguvu, Kisha tukaotesha humo nafaka, Na zabibu, na mimea ya majani, Na mizaituni, na mitende, Na bustani zenye miti iliyo songana baraabara, Na matunda, na malisho ya wanyama; Kwa manufaa yenu na mifugo yenu.” (Abasa, 80/24-32).

Shuhuda za kuwepo kwa Allah kutoka kwenye ulimwengu wa wanayama.

Tunapowaangalia wanyama kwa kutumia akili zetu na elimu, tunaweza kusema kwamba kila mmoja ni mashine au “kiwanda chenye kutembea”. Mwanadamu amepiga hatua kubwa katika kutengeneza vifaa vya kiteknolojia tokea mapinduzi ya kiviwanda. Vifaa ambavyo havikuwahi kufikiriwa karne moja kabla kama televisheni, simu za mkononi na kompyuta vimekuwa ni sehemu katika maisha ya kila siku. Tunaishai katika zama za maajaabu ya kitejnolijia na kila siku tunaona mapya. Hata sayansi isiyo ya dini huzingatia uwezo wa mwanadamu wa kutengeneza vifaa changamani ili kufikia mahitaji yao na matakwa kama ni elementi ya msingi inayo mtofautisha yeye na wanyama. Ndege, magari, treni za umeme, na majumba marefu, ni matunda ya uwezo huu. Kila mtu anafahamu kupitia uzoefu wake kwamba hata kifaa kidogo zaidi kilicho tengenezwa na mwanadamu ni kazi ya sayansi na nguvu. Vifaa kila vinapokuwa changamani, elimu na sayansi zaidi huwa ni lazima. Kwa mfano, mtoto mweye elimu ndogo na nguvu ndogo anaweza kutengeneza gari ya mbao. Hata hivyo, hata maelfu ya watoto wakikusanyika pamoja, hawawezi kutengeneza hata gari ndogo. Kisha, linganisha wanyama na “maajabu ya kiteknolojia” ambazo ni kazi zetu.

Inaweza ikawa rahisi kwetu kumtambua mola wetu kwa kutafakari katika uumbaji na stadi za wanyama ambazo daima tunaziona katika maisha yetu, bustani za wanyama na maisha halisi ya wanyama katika televisheni. Qurani ina tueleza kupitia aya ifuatayo kuna mifano ya ishara katika wanyama.

“Hakika katika mbingu na ardhi ziko Ishara kwa Waumini. Na katika umbo lenu na katika wanyama aliowatawanya zimo Ishara kwa watu wenye yakini.” (al-Jathiya, 45/3-4).

Kwa kweli, si vigumu kuona ishara za kimifano kwa wanyama zinazotuambia kuhusu Allah kwa kuwaangalia kwa makini. Qur'an inawaelezea wale wasioamini kama vipofu na kusema kwamba hawataweza kuona ishara hizi isipokuwa waamini na kufungua macho yao kuona ukweli. Hebu tujaribu kusoma baadhi ya ishara kwa wanyama kwa kutumia akili zetu.

Wanasayansi waliyotafuta wanyama wameamua kuwa kuna takriban milioni 2 za spishi za wanyama tofauti hadi sasa. Kulingana na makadirio, takwimu hii ni asilimia 20 tu ya wanyama wote. Inakadiriwa kuwa kuna spishi milioni 10 tofauti za wanyama. (7)

Kwa mujibu wa wanasayansi wanaotafuta wanyama wanatuambia, hata mnyama mdogo sana ni ajabu zaidi kuliko bidhaa zetu za teknolojia kubwa katika suala la uendeshaji wake. Kwa maneno mengine, tunapolinganisha "vifaa vya kiteknolojia vya kibinadamu" na "vifaa vya kiteknolojia vya kiungu", tunaona tofauti kubwa kati yao. Katika kitabu alichoteremsha, Allah anatoa changamoto kwa mtu, ambaye anajivunia "vifaa vya teknolojia ya juu", kama ifuatavyo:

“Enyi watu! Unapigwa mfano, basi usikilizeni. Hakika wale mnao waomba badala ya Mwenyezi Mungu, hawatoumba hata nzi ijapo kuwa watajumuika kwa hilo. Na nzi akiwapokonya kitu hawawezi kukipata kwake. Amedhoofika kweli huyo mwenye kutaka na mwenye kutakiwa.” (al-Hajj, 22/73)

Achilia mbali kuzalisha nzi, haijawezekana kuzalisha hata seli ndogo ya nzi hadi sasa. Basi, hebu tuulize kwa maneno ya Quran:

“Au wao wameumbwa pasipo kutokana na kitu chochote, au ni wao ndio waumbaji?” (at-Tur, 52/35).

Mfumo wa mwili wa ajabu wa wanyama unaonyesha kuwepo kwa Allah mara nyingi kama idadi ya aina zao na labda idadi ya wanyama wote; faida na madhara ya wanyama vinashuhudia hekima na rehema ya Allah. Qur’an inaeleza ukweli huu kama ifuatavyo:

“Na hakika katika wanyama mna mazingatio kwa ajili yenu.Tunakunywesheni katika vile viliomo matumboni mwao, vikatoka baina ya mavi na damu, maziwa safi mazuri kwa wanywao.” (an-Nahl, 16/66).

Yaani, hatupaswi kuwadharau wanyama. Hatupaswi kuwaita watu tunaowakasirikia "wanyama" na kudharau wanyama. Ni sahihi zaidi kuwapa wanyama majina kulingana na yale wanayofanya kama ifuatavyo: "kiwanda cha maziwa na nyama" kwa ng'ombe, kondoo na mbuzi, "kiwanda cha yai na nyama nyeupe" kwa kuku, "kiwanda cha hariri" kwa mdudu wa hariri na "kiwanda cha nyuki" kwa nyuki. Kwa kweli, tunapofikiria faida nyingine za wanyama hawa, hata majina kama hayo hayatoshi.

Katika aya ya juu, Allah anasema kuwa kuna masomo katika wanyama wa ndani ikiwa ni pamoja na ng'ombe. Tawi tofauti la sayansi linaloitwa dawa ya mifugo ilianzishwa ili kuelewa hekima hizo. Maelfu ya wanasayansi wamejaribu kuwaelewa lakini hawajaweza kumaliza bado.

Kwa mfano, Dk. Virtanen, ambaye alikuwa akijaribu kuelewa jinsi ng'ombe hutoa maziwa, hakuweza kuzalisha maziwa lakini aligundua jinsi ya kupata maziwa zaidi kutoka kwa ng'ombe. Alipewa Tuzo ya Nobel kwa sababu yake. (8) Sasa, ninawauliza swali hili: Kama tuzo ya Nobel inapewa kwa mtu aliyeelewa kwa kiasi fulani kile ng'ombe alichofanya lakini ambaye hawezi kuzalisha maziwa, ni aina gani ya tuzo tunapaswa kumpa ng'ombe?

Nadhani kila mtu anayeelewa kwa kiasi fulani ni nini ng'ombe wanavyofanya anahitaji kuwaheshimu. Kwa kweli, ninaweza kuelewa kwa nini Wahindus wanaabudu ng'ombe ingawa wanachofanya ni ukafiri. Nadhani kuwona ng'ombe kama viumbe vya kawaida ni ajabu sana kama kuabudu ng'ombe.

Maneno yafuatayo kwa muhtasari ya Badiuzzaman Said Nursi yanafupisha kile tulichosema hadi sasa:

“Kuweka ndani ya chuchu za ng'ombe, ngamia, mbuzi na kondoo, pamoja na mama za kibinadamu, kati ya damu na uchafu lakini bila kuchafuliwa, kitu ambacho ni kinyume kabisa, maziwa meupe, safi, mazuri, ya lishe, na kuchochea huruma katika nyoyo zao kwa watoto wao ambayo ni ya kupendeza zaidi, tamu na yenye thamani zaidi kuliko maziwa - hii inahitaji kiwango cha rehema, hekima, ujuzi, nguvu, utashi na utunzaji ambapo haiwezi kuwa kazi ya bahati changamani, ya mchanganyiko wa vitu, au ya nguvu pofu. " (9)

Ushahidi wa kuwepo kwa Allah kutoka kwa "Mwanadamu"

Ushahidi mwingine, labda muhimu zaidi, kwa kuwa kuwepo kwa Allah kunafanyika katika ulimwengu wetu wa ndani. Kila mtu anaweza kumtambua Mola wake kwa kutafakari juu ya uumbaji wake mwenyewe na neema anayopewa kila siku. Ushahidi ambao mtu anaona katika kila kitu katika ulimwengu huitwa "objective", yaani, "ushahidi wa nje" na ushahidi anao uona na anahisi ndani yake unaitwa "subjective", yaani, "ushahidi wa ndani". Ni rahisi kuelewa ushahidi wa ndani kwa sababu unategemea uzoefu wa kibinafsi. Kwa bahati mbaya, watu wengi wana shida ya kuona ushahidi huo kwa sababu hawafikiri juu ya miili yao wenyewe. Hata hivyo, Quran inaelekeza umakini wetu katika masomo juu ya uumbaji wa mwanadamu:

“Na katika umbo lenu na katika wanyama aliowatawanya zimo Ishara kwa watu wenye yakini.” (al-Jathiya, 45/4).

Katika kipindi ambacho hapakuwa na teknolojia kabisa, uumbaji wa mwanadamu umeelezwa katika Qur'ani kama ilitazamwa kupitia "ultrasound ya Mungu":

“Kisha tukaiumba tone kuwa damu iliyo ganda, na tukaiumba damu kuwa pande la nyama, kisha tukaliumba pande la nyama kuwa mifupa, na mifupa tukaivika nyama. Kisha tukamfanya kiumbe mwengine. Basi ametukuka Allah mbora wa waumbaji.” (al-Muminun, 23/14).

Mwanasayansi ambaye aliona uumbaji wa mwanadamu kutoka kwenye tone la maji katika uzazi wa binadamu kwa mara ya kwanza, alieleza kile alichoona kama "muujiza". Kushangaza kwa kutosha, hata waraka zilizoandaliwa kwa uelewa wa kidunia zilihitajika kuuita "muujiza wa maisha".(10)

Watu wengi wamesahau muujiza huu, ambao wanapata katika safari yao ya maisha, na wanaishi bila ya mazingatio na bila ya kushukuru kama kwamba wametumwa kutoka angani. Aya ifuatayo ya Qur'ani inawahimiza watu wenye akili kuamka kutoka katika kutozingatia na kuona muujiza wao wa uumbaji:

“Kwani mwanaadamu haoni ya kwamba Sisi tumemuumba yeye kutokana na tone la manii? Kisha sasa yeye ndio amekuwa ndiye mgomvi wa dhaahiri?” (Yasin, 36/77).

Kuumbwa kwa mwanadamu kutoka kwenye tone la maji kunaweza tu kuwa kazi ya dhati yenye ujuzi usio na mwisho, nguvu na hekima. Ikiwa mtu anadai kinyume, anaweza kuthibitisha madai yake kwa kumtengeneza mwanadamu au seli moja ya mwanadamu kutoka kwenye tone la maji. Qur'an imetoa wito wa kushindana kwa wasioamini kuhusu suala hilo kwa karne kumi na nne. (11) Hakuna mtu aliyeweza kujibu changamoto hii hadi sasa; hakuna mtu anayesema kuwa wanaweza hata licha ya teknolojia ya hivi karibuni. Hii inathibitisha kuwa Quran ni kitabu cha Allah na Allah ni Muumbaji wa viumbe hai vyote.

Uumbaji wa mwanadamu ni muujiza; Vivyo hivyo, neema ya maziwa ya mama kutoka kwa mama yake ni "muujiza wa rehema" tofauti. Wengi wetu tunaona kama tukio la kawaida. Tuseme kwamba juisi ya machungwa badala ya maziwa imetoka kwenye matiti ya mama zetu; tutafanya nini? Tutastaajabishwa na tutasema kuhusu hilo kwa kila mtu. Ni dhahiri kuwa itakuwa habari ya kwanza kwenye televisheni. Hata hivyo, "juisi ya machungwa" inayotokana na matiti ya mama zetu badala ya "maziwa" ni kitu ambacho ni mara elfu zaidi ya kushangaza na kwamba inahitaji kujiuliza zaidi. Wanasayansi wanashauri wanawake kunyonyesha watoto wao kwakuwa hawajaweza kupata kitu cha kuchukua nafasi ya maziwa kikamilifu. Kama inavyoonekana katika mfano wa maziwa, kila kitu ni ajabu na muujiza lakini huonekana kuwa vya kawaida kwetu kwa sababu sisi daima tunaviona. Wale wanaofungua "jicho la akili" kwa uangalifu wanaweza kuona matendo ya miujiza na mtendaji wao nyuma ya "pazia la kawaida".

Ninataka kutoa mfano mwingine kuhusiana na ushahidi wa ndani. Wakati mtu anafikiria mwili wake mwenyewe, anaweza kuona ishara zinazoonyesha Mola wake. Kila kiungo cha mwili wetu, mpangilio wao bora na utendaji, utaratibu wao na hekima na faida zisizo na hesabu zinatuonyesha sisi dhati yenye ujuzi usio na mwisho, hekima, huruma na nguvu. Ninataka kukuambia juu ya kitu ambacho nimejifunza hivi karibuni na kukiweka wazi kile ninachotaka kumaanisha. Nina meno yaliyofanywa na binadamu na meno ya asili katika kinywa changu. Sikupata mtu wa kawaida kufanya meno yangu. Nilikwenda kwa daktari wa meno mwenye ujuzi ambaye alikuwa amehitimu kutoka katika kitivo cha meno. Kwa nini nilikwenda kwa daktari wa meno na si mtu wa kawaida? Jibu ni rahisi: Kwa sababu sio rahisi sana kupata nyenzo nzuri kwa meno, kuyafanya kwa usawa na meno yangu mengine na kuyaweka katika kinywa changu. Si kila mtu anayeweza kufanya hivyo. Mtu ambaye hana ujuzi wa kutosha wa meno na ambaye hana zana muhimu hawezi kufanya hivyo.

Sasa, hebu tulinganishe "meno yaliyofanywa na binadamu" na "meno mengine". Yepi ni bora zaidi? Ambayo ni salama zaidi? Ambayo ni kamilifu? Bila shaka, ni yale mengine. Mfano wa wazi zaidi ni kwamba hakuna daktari wa meno anasema niruhusu kutoa meno yako na kukuekea meno ya kisasa ya teknolojia badala yake kama meno yako ni mazima.

Sasa, hebu fikiria kwa uangalifu: "meno yaliyofanywa na binadamu" yanaweza kutolewa kupitia teknolojia ya juu na nguvu; basi, inawezekana kwa yale "meno" mengine, ambayo ni bora zaidi kuliko meno yaliyofanywa na wanadamu katika kila kipengele yaweze kujiunda wenyewe au kwa bahati mbaya? Je, yanaweza kuwa kazi ya nguvu ya asili ambayo yamenyimwa ujuzi na ufahamu na ambayo ni jinga na yasio na akili? Basi, kila jino letu ambalo sio lililotengenezwa na mwanadamu linatujulisha kuhusu Allah. Kwa kuwa meno, ambayo ni miongoni mwa sehemu rahisi zaidi za mwili wetu, yanatujulisha kuhusu Mola wetu kama hivyo, narejesha kwa akili yako kufikiri juu ya jinsi mamia mengine ya viungo kama jicho, pua na ubongo vinavyotuambia kuhusu Allah.

Tunaweza kufupisha kile tulichoandika hadi sasa kama ifuatavyo:

Mola wetu amefanya ulimwengu kuwa kitabu kizuri na kutujulisha juu yake mwenyewe kupitia maneno (ishara) ya viumbe hai na viumbe visivyo na uhai ambayo aliandika ndani yake. Alitafsiri kitabu hiki kupitia Qur’an na kutufundisha jinsi ya kusoma kitabu hiki kupitia Hz.Muhammad (s.a.w), ambaye ni mwalimu mkuu. Tunapoondoa glasi nyeusi za bahati na asili na kusoma kitabu cha ulimwengu kupitia glasi za uwazi ambazo Quran inatupa, tunaweza kumwona Mola wetu, kuchunguza shughuli zake na kutafakari juu ya hekima yake katika kila kitu tunachosoma. Tunaweza kumjua kwa njia ya kazi zake zisizo na hesabu na kumpenda kwa njia ya neema zake zisizo na mwisho.

"11 Eylül’e Rağmen Amerika’da Yükselen İslam (Islam Rising in America despite September 11)" Nesil Yayınları 

Maelezo ya chini:

(1) Unaweza kufikia makala iliyotajwa katika maandishi kwa njia ya kiungo kinachofuata:

http://www.cnn.com/2003/TECH/space/07/22/stars.survey/

(2) Yafuatayo yamesemwa katika aya ya Quran: “Na ukiwauliza: Nani aliye ziumba mbingu na ardhi? Bila ya shaka watasema: Mwenyezi Mungu.” (Luqman, 25)

Neno "wao" linatumiwa kwa wasioamini katika aya hii. Aya hii huangazia mambo mawili muhimu: Kwanza, inafaa zaidi kuanzia uumbaji wa mbingu na ardhi, ambazo ni ishara kubwa zaidi, unapowaambia wasioamini kuhusu Allah. Pili, hata wasioamini hawawezi kueleza uumbaji mkubwa na utukufu wa mbingu na ardhi; wakati wanafikiria vizuri, watasema "Allah".

(3) http://nobelprize.org/nobel_prizes/chemistry/laureates/1961/calvin-bio.html

(4) Katika mfumo wa soko huria, bei zimewekwa kulingana na usambazaji na mahitaji, sio thamani ya bidhaa na huduma. Sababu ya kwa nini oksijeni, ambayo ni muhimu kwa mwanadamu, ni bure haionyeshi kwamba haina thamani, lakini ni nyingi; ili, kusiwe na mtu anayelipia fedha kwa ajili yake. Ni kosa kwamba watu hutathmini bidhaa na huduma kulingana na bei ya soko. Kwa kweli, vitu vingi ambavyo haviuzwi na kununuliwa kwenye soko ni vyenye thamani sana.

(5) Kuchunguza suala hilo katika mwelekeo wa atomiki au molekuli na kufunua sifa zake mpya.

(6) "Umekutana na mahitaji yako ya chakula, vinywaji na nguo katika duka la dunia. Ikiwa utalipa pesa kwa ajili ya bidhaa hizi za bure kutoka hazina ya kimungu, ungeweza kununua komamanga moja kwa pesa nyingi na kwa kutumia muda mwingi. Kwa maana, makomamanga hayo yanahusiana na vitu vyote. Inaeleweka kutoka kwa vitu vyema kama kudarizi, nidhamu, sanaa, harufu, ladha na harufu nzuri kwamba komamanga ni kazi ya Muumba anayeumba kwa urahisi, na hahitaji mawasiliano ya kimaada nayo."(Badiuzzaman Said Nursi, Hubab Risalesi, Mesnevi-i Nuriye).

(7) Kuna baadhi ya wanasayansi ambao wanakadiria kuwa idadi ya wanyama ni milioni 100: http://news.bbc.co.uk/2/hi/science/nature/4013719.stm

(8) Dk. Virtanen alipata Tuzo ya Nobel katika Kemia mwaka 1945 kwa kazi zake zinazohusiana na kuongeza uzalishaji wa maziwa wa ng'ombe.

(9) Badiuzzaman Said Nursi, Mwale was aba, Ishara kuu.

(10) Hati iliyoitwa "Muujiza wa Maisha" iliyotengenezwa na NOVA, mmoja wa wazalishaji wa hati nzuri, ni mfano tofauti wa hilo.

(11) Unaweza kusoma jinsi Thomas, mtu asiyeamini Mungu, amenyamazishwa na changamoto ya Quran katika kitabu kinachoitwa Rabbini Arayan Thomas (Thomas akimtafuta Mola wake) na mwandishi aliyechapishwa na Nesil Yayınları (Publications).

Maswali juu ya Uislamu

Author:
Maswali juu ya Uislamu
Subject Categories:
Read 2.124 times
In order to make a comment, please login or register
MASWALI YENYE KUFANANA