Je inawezekana kwetu kumuona Allah na kufahamu asili yake halisi?

The Answer

Dear Brother / Sister,

Haiwezekani kwa mwanadamu kumuona Allah katika dunia hii na kufahamu asili yake halisi.

Ni kwa sababu akili na hisia za mwanadamu zina ukomo. Havitoshi kufahamu asili halisi ya Allah. Hata hivyo, mwanadamu anaweza kufahamu uwepo wake na umoja wake kwa kuangalia viumbe na kufahamu nguvu yake isiyokuwa na ukomo, na sifa zake nyingine pamoja na majina yake.

Kwa hivyo, Allah ametukataza kufikiria kuhusu dhati yake na asili yake halisi; ametuamuru kufahamu kuwepo kwake na umoja wake na kufahamu sifa zake na majina yake.

Hayo yameelezwa katika hadithi:

“Angalia mbingu na ardhi na jiangalie wewe mwenyewe ili uweze kufahamu kuwepo na umoja wa Allah; na fikiri kuhusu uzuri katika maumbile ambao hushangaza akili na kwamba haviwezi vikawepo wenyewe. Kwa sababu, hizo ni dalili zenye kuonesha kuwepo na umoja wa Allah.

Hata hivyo, usifikiri kuhusu dhati na asili halisi ya Allah. Usianze kufikiri ‘Je, Allah ni kama hivi au kama vile?’ Vipi Allah huona na kusikia? Nguvu yako haitatosha katika hilo. Hata ukijaribu vipi, huwezi kujua na kufahamu vizuri. Utachanganyikiwa. Vipimo vyako vya elimu na uzoefu havitatosheleza.

Ikiwa tutafikiri japo kidogo, tunaweza kufahamu kupitia akili zetu kwamba ni muhali kufahamu asili halisi ya Allah. Kifaranga ndani ya yai hatarajiwi kufahamu dunia iliyo nje ya yai. Akili ya mwanadamu haitofautiani na kifaranga ndani ya yai kuhusu suala la kujua ulimwengu wa kushangaza na Nyanja za ulimwengu ambazo Allah ameziumba. Hivyo, haiwezekani kwa akili ambayo imewekewa uwezo wa kufahamu wenye ukomo kufahamu asili halisi ya aliyeumba ulimwengu pale mtu anapofikiri kuhusiana na hilo kupitia akili yake.

Mehmed Kırkıncı anafafanua kuhusiana na jambo hilo kama ifuatavyo:

 “Jaalia kwamba kuna mtu ameishi ndani ya pango na kwamba hakuwahi kuona mwanga wowote na kwamba alitolewa nje ya pango mapema asubuhi kabla ya jua kuchomoza. Pale mtu huyo ambaye amepata kizunguzungu kwa mwanga ambao umekuja kutoka kila sehemu alipo ambiwa kwamba mwanga umetoka katika jua, angelishangazwa na jua hilo na angelijaribu kujua kuhusiana na jua hilo.

Ni wazi kwamba, vyovyote alivyolifikiria jua katika mawazo yake, asingeweza kulifahamu jua na angelifikiria vitu tofauti kila mara atakayojaribu kulijengea picha jua hilo. Angelilifananisha jua hilo na vitu alivyoviona;  kila mfanano ungelikuwa si sahihi.

Ikiwa kuamini juu ya jua ingelikuwa msingi wa Imani kwa mtu huyo, vyovyote angelifikiria jua angefanya shirki. Kitu pekee angeliweza kufanya ingelikuwa ni kufahamu kwamba mwanga umetoka katika jua lakini asingeliweza kujua asili halisi ya jua hilo. Kwa hakika, Imani inayotarajiwa kutoka kwake ni hiyo tu.

Kama ilivyokuwa mtu huyo katika mfano hawezi kulifahamu jua, mwanadamu hawezi kufahamu asili halisi ya mfalme aitwaye roho ambaye anatawala katika nchi ya mwili wake. Japo kuwa tunajua kwamba miili yetu hufanya kazi pamoja na roho, na kwamba mwili utashindwa kufanya kazi pale roho itakapouacha mwili huo, kwamba mfalme anautazama ulimwengu huu kupitia dirisha la jicho, anafahamu ulimwengu wa sauti kupitia sikio, na anaonja kila kitu kupitia mizani ya ulimi, sisi hatufahamu asili  halisi ya roho. Vyovyote tusemavyo kuhusiana na asili yake halisi, itakuwa ni kinyume na ukweli; vyovyote tuifikiriavyo dhati ya roho, tutafanya makosa kuhusiana na hilo.

Mwanadamu, ambaye ni dhaifu kuelewa au kufahamu dhati ya jua ambayo hakuwahi kuiona kabla na ambaye ni mjinga mno kufahamu  asili halisi ya roho yake, hawezi kumfahamu, kwa namna yoyote, muumbaji mtukufu na mmiliki wa kweli wa limwengu zote. Ambaye yupo huru kutokana na wakati pamoja na mahali; itakuwa ni kosa kubwa na uendawazimu kujaribu kuifahamu dhati yake na ni fikra isiyo ya kawaida ambayo itamfanya mwanadamu adondoke katika shirki.” .” (Hikmet Pırıltıları: Glitters of Wisdom)

Maswali juu ya Uislamu

Author:
Maswali juu ya Uislamu
Subject Categories:
Read 311 times
In order to make a comment, please login or register
MASWALI YENYE KUFANANA