Je, kuna kanuni kama vile "Hakuna kuulizana katika dini" katika Uislamu? Kama ipo, inamaanisha nini?

Submitted by on Wed, 08/08/2018 - 15:19
Dear Brother / Sister,
Kuna namna mbili za amri za shari'ah:
1. Amri na makatazo yanayokuja moja kwa moja kutoka kwa Allah; tunaziita “taabbudi”, yaani, sababu (hekima) zake hazijulikani.
2. Sehemu ambayo sababu (hekima) zake zinapatikana katika amri za Allah na makatazo ya Allah; tunaziita “maqul al-mana”.
Tunaweza kuangalia swali lako katika sura tofauti. "Kwa nini swala ya asubuhi iwe na rak'ah nne na si kumi au ishirini?" (Rakaa nne ni mjumuiko wa rakaa mbili za faradhi, na mbili za sunna ) Jibu ni "kwasababu Allah ametuamrisha kufanya hivyo."
Swala ya adhuhuri ilipangwa na Allah iwe ya rak'ah 10 (Nne za faradhi na sita za sunna kabliya na baadiya). Kutafuta hekima yake hakutafanikiwa. Jawabu sahihi la swali hilo ni kwa sababu Allah ameamrisha hivyo. Hata hivyo, baadhi ya kanuni za shari'ah zinaweza kufafanuliwa kwa hekima, lakini hizo si sababu halisi. Sababu za uhakika ni amri za Allah na makatazo.
Mathalani, "Kwa nini Allah ameamrisha salah (swala)?" Mtu anaweza kuorodhesha hekima na madhumuni ya jambo hilo katika vitabu vikubwa-vikubwa. Mtu anaweza kujibu kwa nini tunafunga saumu kwa kutafuta hekima na sababu zake. Hata hivyo, sababu (hekima) na manufaa hayawezi kushika nafasi ya Amri za Allah. Mathalani, sababu mojawapo ya kufunga ni kuhisi namna watu wanavyoumizwa na njaa na kuwaendea kwa huruma.
Hivyo, mtu anaweza kusema “Ninaweza kuhisi njaa zaidi na kuzidisha huruma yangu na ninaweza kumsaidia masikini zaidi na zaidi.” Ingawa wakati wa imsak (muda wa kuanza kufunga) ni saa kumi alfajiri, kama mtu anakusudia kufunga saa tano usiku, lakini kama atafungua dakika 5 kabla ya iftar (kufuturu wakati wa magharibi), je, funga yake itakubaliwa? Hapana kwa hakika. Kuna wakati maalumu uliopangwa wa kufuturu. Na ingawa mtu anabakia na njaa kwa muda mrefu zaidi, funga yake haikubaliki. Hiyo inamaanisha kuwa, hekima ya kufunga inayotakiwa imetumika (kwa kubakia na njaa), lakini kwa sababu ya kufungua katika wakati asiouruhusu Allah, funga yake haikubaliwi.
Hivyo, tuziangalie amri zote na makatazo yote kwa namna hiyo. Hiyo inamaanisha kuwa, tunaitekeleza kwa sababu Allah ametuamrisha tufanye hivyo. Kwa hakika, zinaweza kuwepo sababu (hekima) zake, pia. Na sababu hizi zinaweza kutafutwa. Hiyo pia ni elimu na ibada. Hata hivyo, hekima na manufaa kwa hakika si sababu halisi, bali ni ufafanuzi.
Maswali juu ya Uislamu