Je, njia fanisi zaidi ya kueneza Uislamu ni vita au tabligh (kulingania)?

Submitted by on Wed, 08/08/2018 - 15:26
Dear Brother / Sister,
Ni muhimu kujibu maswali "Mtume ni nani?", "Wajibu wake ni upi?" Ili kuweza kutathmini dhana ya jihad kwa usahihi. Huku akiwafanya watu wote waende katika ulimwengu wa ahera, Allah Mtukuka aliwatuma mitume ili wawaongoze watu katika safari yao ya kuwapeleka Peponi au Motoni. Wajibu mkuu wa wajumbe hao wa Allah ni kuwafanya watu wamjue Allah, kuwafundisha ibada, halali na haramu, na kuwafundisha namna ya kumshukuru Allah kwa neema Zake zisizo na ukomo.
Mtume Muhammad (s.a.w), ambaye ni Mtume wa zama za mwisho, alitimiza wajibu huu kikamilifu; aliwajulisha watu kuhusu Allah huko Makkah, aliwafundisha amri Zake na makatazo na aliwaambia kuwa kuabudu masanamu ni kumshirikisha Allah. Alivumilia namna zote za mateso na ukatili wa watu waliopinga ujumbe wake kwa miaka kumi na mitatu na kisha alihamia Madinah kwa kufuata amri na idhini ya Allah; aliendelea na wajibu wake huko. Washirikina waliotaka kumzuia asitekeleze wajibu huu wa juu kabisa waliendelea kumsumbua huko Madinah pia lakini hawakuweza kuuzuia Uislamu kufuatwa na watu wa huko.
Kitu muhimu sana cha Mtume (s.a.w) wa zama za mwisho kilichotajwa katika vitabu vyote vya mbinguni ni kwamba yeye ni “sahib-us sayf” (mmiliki wa upanga); yaani, pamoja na uongofu wa kiroho, anaruhisiwa kupigana (anapozuiwa kufikisha ujumbe wake). Baadhi ya mitume waliotangulia, kama vile Nabii Dawud na Nabii Suleiman, waliendesha jihad zao kwa mapanga pindi ilipolazimu.
Historia inapochunguzwa bila upendeleo, itaonekana kuwa jambo kubwa lililofanya Uislamu uvutie nyoyo na ari halikuwa vita bali kufikisha ujumbe, yaani, kuwaambia watu kuhusu uhalisia wa Uislamu na kuwaonesha mazuri ya Uislamu. Wanahistoria wanakubali kuwa makundi mawili ya watu yalikuwa na mchango mkubwa zaidi katika kuenea kwa Uislamu. La kwanza ni wanazuoni na walimu waliojitolea maisha yao kwa kufundisha Uislamu na wakahamia nchi za mbali sana ili kufanya hivyo. Kundi la pili ni wafanyabiashara waliokwenda katika baadhi ya nchi ili kufanya biashara na wakawaonesha watu wa huko mazuri ya Uislamu.
Aya zifuatazo zinaonesha waziwazi kuwa Uislamu umeenea kwa njia ya kufikisha ujumbe na wito wala si kwa njia ya upanga:
“Hapana kulazimisha katika Dini. Kwani Uwongofu umekwisha pambanuka na upotofu.” (surat al-Baqara, 256)
“Basi kumbusha! Hakika wewe ni Mkumbushaji. Wewe si mwenye kuwatawalia.” (al-Ghashiya, 21-22)
Kuna shuhuda nyingi zinazoonesha kuwa Uislamu umeenea kwa njia ya kufikisha ujumbe wake. Tutataja baadhi yake: Mtume (s.a.w) alipoanza kufikisha ujumbe wa Uislamu katika mji wa Makkah, hakuwa na mali au nguvu. Ingawa washirikina wote wa hapo walimfanyia uadui, alizishinda nyoyo za watu kwa kufikisha ujumbe na ushawishi. Watu wengi, kuanzia Abubakr mpaka Umar, walisilimu kama hivyo na wakamtamkia kila mmoja kuwa Uislamu ulikuwa ni nguvu isiyoshindika. Kama Maswahaba wangetaka, wangewaua washirikina wote wa Quraysh, wa kwanza Abu Jahl, kwa ghafla moja. Hata hivyo, hawakufanya hayo. Waliendelea kufikisha ujumbe wa Uislamu kwa kustahamili mateso na taabu za aina zote; hawakutumia kitisho na vurugu.
Waislamu waliohamia Madinah kabla ya Mtume waliwaingiza watu wengi katika Uislamu huko kwa kufikisha ujumbe wa Uislamu na kuwalingania Uislamu. Hivyo, misingi ya Uislamu iliwekwa kwa njia ya kufikisha ujumbe kote Makkah na Madinah.
Katika miaka iliyofuata, Uislamu uliimarika Madinah. Washirikina wa Makka waliwakubali Waisilamu kuwa wana nguvu na wakasaini nao mkataba huko Hudaybiya. Kipindi cha mkataba kilikuwa ni miaka kumi lakini kilidumu kwa miaka miwili na kikavunjwa na washirikina wa Makka. Hata hivyo, idadi ya watu waliosilimu katika kipindi cha miaka hiyo miwili ilikuwa ni zaidi ya idadi ya watu walioufuata Uislamu katika kipindi cha miaka ishirini tangu Uislamu ulipoibuka.
Katika karne zilizofuatia, Wa-Mogul waliumaliza ukhalifa wa ukoo wa Abbas; wakachoma na kuharibu rasilimali za Kiislamu. Hata hivyo, baada ya muda, walianza kusilimu kwa hiari yao wenyewe. Ni ukweli wa kihistoria kuwa panga halikuwa na lolote katika kusilimu kwa Wa-Mogul.
Kuenea kwa Uislamu katika maeneo ya Indonesia, Malaysia na Africa kulifanyika kwa njia ya ufikishaji ujumbe na si kwa njia ya upanga.
Baada ya kuiangalia historia hiyo kwa kifupi, hebu tuangalie hali ya leo: Waislamu wamepoteza uwezo wao wa kimali katika karne iliyopita lakini Uislamu umeendelea kuenea na kuendelea kiroho. Watu wengi waliosilimu katika nchi za Ulaya kwa kuanzia na Ujerumani na Uingereza, na katika Amerika ni wanasayansi; wengi wao wamesilimu baada ya kuuchunguza tu, bila ya hata kufikishiwa ujumbe wa Uislamu.
Maswali juu ya Uislamu