Je, Uislamu ni dini ya hofu?

The Answer

Dear Brother / Sister,

Kunaweza kuwepo baadhi ya dini potovu zinazoegemea hofu lakini si sahihi kusema kuwa msingi wa dini zote ni hofu. Hususani wanaoitizama dini ya Uislamu kuwa ni dini ya hofu, hawako sahihi. Quran inatoa habari njema na maonyo. Maonyo hayalengi katika kuwatisha watu; bali badala yake, yanalenga katika kuwalinda watu dhidi ya kufanya makosa. Kuwajulisha watu kuhusu hatari wanazoweza kuzikabili na yanalenga katika kuwaonya dhidi ya kuchukua hatua; hayalengi katika kuwatisha. 

Uislamu hautaji Jahannamu tu, bali pia Pepo. Kabla ya kuja Uislamu, watu walikuwa wakiishi bila ya kuamini imani ya ufufuo; walikuwa wakiamini kuwa wangepotea baada ya kufa. Uislamu uliondosha imani hii na ukawapa waumini habari njema kuwa watakwenda Peponi. Kwa hakika, hadithi ifuatayo ya Mtume (s.a.w) ni mfano mzuri wa hayo:

"Rahisisheni, msifanye ugumu; toeni habari njema, msiifanye ngeni." (Bukhari, 3/72.)

Dini ya Uislamu ni msaada wa Muumbaji kwa wanadamu na elimu ya kuujua ukweli unaolenga katika kuwafanya wawe na furaha duniani na kupata wokovu katika akhera. Tunamjua Muumbaji wetu na sisi wenyewe tunashukuru kwa Uislamu; pia tunafahamu lengo la msingi la kuwepo na kupata amani na utulivu katika dunia yetu ya ndani na ya nje tunashukuru kwa hilo. Mitume wote tokea Nabii Adam mpaka Nabii Nuh, tokea Nabii Ibrahim mpaka Nabii Musa, tangu Nabii Isa mpaka Nabii Muhammad (s.a.w) walikuwa wajumbe na viongozi wa wito huu wa amani, mapenzi na wokovu.

Maswali juu ya Uislamu

Author:
Maswali juu ya Uislamu
Subject Categories:
Read 45 times
In order to make a comment, please login or register
MASWALI YENYE KUFANANA
THE MOST ASKED QUESTIONS