Je, Uislamu ni dini ya kimantiki?

The Answer

Dear Brother / Sister,

Hukumu na kanuni za dini ya Uislamu zinafaa kwa umbo la mwanadamu na mantiki yake. Tathmini hii ni sahihi. Isipokuwa kwa sehemu ndogo ya kanuni ambazo ni “ta'abbudi” (zinahitaji utii bila ya kuhitaji kujua mantiki yake), kanuni zote katika Uislamu ni "ma'qul al-mana" (zinafahamika kiakili na kimantiki).

Ukweli kuwa amri na makatazo ya Uislamu yanawafaa watu waliobaleghe na wenye akili timamu na hawawajibishwi watu wasio na akili timamu unaonesha kuwa Uislamu huipa umuhimu akili na kuiambia akili na pia inaonesha kuwa Uislamu ni “dini ya mantiki”. 

Kwa mfano, desturi ya zaka katika Uislamu ni mpango uliowekwa kwa matajiri kuwasaidia masikini na kuweka usawa wa kijamii, kuzuia migogoro baina ya masikini na matajiri na kuigeuza migogoro hiyo kuwa suluhu, mapenzi-heshima na huondoa dhuluma inayochochea chuki baina ya matabaka katika jamii. Kazi hii ya zaka inaweza kufahamika kirahisi na pia ni ya kiakili sana.

Kwa kuongezea, sharti la kwanza katika kusilimu ni kumwamini Allah na kuamini mitume Wake. Imani iko moyoni. Moyo una nafasi ya kutosha ya kuwa na hisia, msukumo, hadithi na akili kuhusu Allah. Ni ishara dhahiri ya ukweli huu kuwa mtu asiye na akili timamu hawajibiki kuwa na imani.

Mtindo wa Qur’an umejaa shuhuda za kimantiki zinazotakiwa kwa ajili ya kuthibitishwa na akili ya mtu. Humo kila mara   kuna shuhuda na mifano ya kimantiki inapoeleza kuwepo kwa Allah, kwamba Nabii Muhammad (s.a.w) ni mtume wa kweli, kwamba Qur’an ni neno la Allah, na kuhusu kuwepo kwa ufufuo baada ya kufa.

Kwa kweli, kama amri au adhabu yoyote ya Allah haitoshelezi mantiki ya mwanadamu, basi haitaweza kusemwa kuwa hapa lipo jaribio lisilo na upendeleo. Kama mtu anamwajibisha mwanafunzi wa shule ya awali kwa maswali ya sayansi yanayofaa kwa ajili ya shahada za chuo kikuu au za udaktari wa falsafa, basi mtu huyo atakuwa ameonewa. Ndio sababu, mara zote akili na fikra za kibinadamu zinatiliwa mkazo katika Qur’an na kuna maneno kama ifuatavyo: “Je hamfahamu? Je hamfikiri?”  

Pili, maneno “Uislamu ni dini ya mantiki” hutilia mkazo falsafa ya mtu anayeziegemeza fikra zake kwenye sababu na mantiki yake yeye mwenyewe. Hayo si sahihi. Kwa mujibu wa mtu huyo, “Fikra za akili zilizo bora hufanana”, kwa hivyo mambo asiyoweza kuyafahamu hayako sahihi. Kwa hiyo, kile ambacho Uislamu unacho na kile unachokipinga katika mtazamo wake kinakuwa si sahihi.

Ni kwasababu Uislamu ni dini ya mantiki. Kisichokuwa na mantiki hakina nafasi katika dini.

Watu wa namna hii wenye falsafa kama hii hawawezi kufahamu dhana ya “mantiki” kwa sababu mantiki yenyewe peke yake haiwezi kushika kila kitu bila ya hali za nje; kinyume chake, inajaribu kwenda katika mwelekeo wa elimu na fikra alizopewa hapo kabla. Ni uthibitisho bora kabisa wa ukweli huu kuwa mtu mwenye akili ya juu sana lakini ambaye si lazima awe msomi hawezi kufahamu na kufanya mambo anayoyafanya mhandisi, daktari au mufti ambaye si hodari.

Nukta muhimu zaidi ya kuitaja hapa ni hii: Haifai kwa baadhi ya watu wasiofahamu jambo fulani kusema jambo hilo “halina mantiki.” Wengi wetu hatujui kuhusu fizikia, kemia, unajimu, hisabati, n.k. na hatuyafahamu hayo lakini hakuna anayesema kuwa hayo hayana mantiki kwasababu watu wengine hawayafahamu. Akili peke yake haiwezi kugundua kila kitu. Kama ingewezekana, kusingekuwa na haja ya mitume. Kila jambo lina uwanja wa kitaaluma unaoweza kufahamika kwa wataalamu peke yao. Wataalamu hao wanaweza kufahamu kwa urahisi  masuala ambayo watu wengine hawawezi kuyafahamu. Halikadhalika, ukweli kuwa baadhi ya watu hawawezi kufahamu ukweli wa Quran haimaanishi kuwa ukweli huo si wa kiakili na usio na mantiki. 

Nukta nyingine muhimu ni hii: Kuwepo kwa baadhi ya mambo yanayoitwa ta’abbudi na kwamba hayawezi kufahamika kwa akili kunahusu kujaribiwa mwanadamu. Kanuni za imani ni za kisayansi na zimeegemea mantiki. Kanuni chache za Uislamu zipo ili kuijaribu imani na kujisalimisha sio kuiridhisha akili. Kuna haja ya kuwepo baadhi ya mambo ambayo akili haiwezi kuyafahamu kwa urahisi ili idhihirike kama mtu anaamini akilini mwake tu au anaamini na anajisalimisha kwenye Uislamu.

Kwa kuhitimisha, mtu anayesema, “Kwa kuwa Quran ni neno la Allah, kila kilichomo ndani mwake ni sahihi – hata kama akili yangu haiwezi kufahamu “anafaulu jaribio. Anayesitasita na huku akisema, “Jambo kadha katika Quran halina mantiki; akili yangu haiwezi kulifahamu” anafeli jaribio kwa sababu ama si mnyoofu au ni mjinga sana.

Mathalani, ukweli kuwa swala ya subuhi ina rak'ah mbili lakini swala ya adhuhuri ina rak'ah nne haihusiani na akili. Hata hivyo, masuala kama vile kuharamishwa kwa nyama ya nguruwe na ulevi kunaweza kuelezwa na sayansi na mantiki. Mambo ya kimantiki ni zaidi kuliko mambo ya ta’abbudi.

Maswali juu ya Uislamu

Author:
Maswali juu ya Uislamu
Subject Categories:
Read 163 times
In order to make a comment, please login or register
MASWALI YENYE KUFANANA
THE MOST ASKED QUESTIONS