Je, Uislamu ni rai au mtindo wa kimaisha?

The Answer

Dear Brother / Sister,

Uislamu ni dini pekee aliyoshusha Allah kwa mwanadamu tangu mwanzo wa uumbaji. Nuh, Ibrahim, Musa na Isa wote walifanya kazi ya kueneza dini hiyo hiyo moja. Mtume wetu, Muhammad (s.a.w), alifikisha ujumbe wa mwisho wa Allah kwa kuwa alikuwa ni mtume wa mwisho.

Uislamu ni dini yenye kutambulika kikamilifu.  Uislamu unawakilisha mfumo wa kimaadili unaomwongoza mtu katika kila hatua yake.

Dini ambayo Allah aliwachagulia wanadamu kuwa inawafaa katika maisha yao ni dini ya Uislamu. Allah aliirahisisha sana dini Yake ili watu waitekeleze kwa vitendo.

Kumtumaini na kumtegemea Allah, ambaye ni mmiliki wa viumbe wote na matukio yote yanayofanyika ulimwenguni, na kumfanya Yeye rafiki, inamaanisha mwisho wa hofu zote za mtu, wasiwasi, matatizo na taabu.  Huu ni urahisi mmojawapo muhimu na katika mazuri yaliyoletwa na dini ya Uislamu kwa anayetekeleza maadili ya Quran kwa vitendo. Kwa kuongezea, Allah aliwajulisha watu kuhusu amri Zake na hukumu Zake zote, zinazowafaa kwa umbile lao na ambazo si ngumu.

Allah anaeleza katika Quran kuwa maadili ya dini ni rahisi na kuwa mambo yatakuwa mepesi kwa wafuasi wa dini ya Allah kama ifuatavyo:

"Na tutakusahilishia yawe mepesi.." (al-A'la, 87/8)

"…Yeye amekuteueni. Wala hakuweka juu yenu mambo mazito katika Dini. Nayo ni mila ya baba yenu Ibrahim..." (al-Hajj 22/78)

Sambamba na aya za hapo juu, Mtume (s.a.w) amesema,  

"Dini ni wepesi." (Bukhari, Iman: 29; Nasai, Iman: 28; Musnad, 5:69)

Hivyo, aliwaita watu kwenye kuitekeleza dini.

Ni kweli kuwa dini ya Uislamu ni namna bora ya maisha kwa ajili ya asili, amani na furaha ya mwanadamu na kuwa maisha yaliyoongozwa na maadili ya Quran ni maisha bora zaidi kwa mwanadamu.

Maswali juu ya Uislamu

Author:
Maswali juu ya Uislamu
Subject Categories:
Read 32 times
In order to make a comment, please login or register
MASWALI YENYE KUFANANA
THE MOST ASKED QUESTIONS