Je Uislamu, uliokuja miaka 1400 iliyopita, unajibu maswali ya zama zetu na kutosheleza haja zake?

The Answer

Dear Brother / Sister,

Lengo la Qur’an katika Mkusanyiko wa Risale-i Nur limejadiliwa katika nyanja mbili:

Kufundisha ukweli wa Uwanja wa Kimamlaka na maadili ya Uwanja wa utumishi (ibada). Tunaposema Uwanja wa Kimamlaka, tunamaanisha mtu, sifa, vitendo, na majina ya Allah (SWT). Qur’an imemtambulisha Allah (SWT) kwa wanadamu katika njia hii na ikawalinda dhidi ya kila namna ya ushirikina (imani potovu). Inapokuja kwenye uwanja wa utumishi, inamaanisha majukumu ya wanadamu kwa Allah (SWT). Alichoamrisha Allah (SWT) na kukataza ni nini? Vitendo gani na amali gani zinazomvutia radhi Zake na kinachosababisha ghadhabu Zake? Majibu ya maswali haya yamejibiwa vizuri sana katika Qur’an.

Katika nyanja zote mbili, akili ya binadamu haina hata neno moja la kusema. Katika nyanja zote mbili hakutakuwa na athari ya muda. Allah (SWT) bado ana nafsi Yake na sifa kama zilivyokuwa hapo tangu. Mkondo wa kibinadamu aliouweka Allah (SWT) unathibitisha yaleyale kama ilivyokuwa hapo tangu na tangu.

Hapa ni kweli kuwa katika zama za mitume waliotangulia, katika karne mbalimbali, kulifanyika njia tofauti kwenye mitazamo. Na mabadliko haya yamefikia kikomo pale mwanadamu anapokuwa amefikia mahali ambapo kila mmoja anaweza kujifunza kutoka kwa mtume mmoja na akapata nidhamu kutokana na Kitabu kimoja.

Mijadala au upingaji wa namna hii hufanyika zaidi kwenye njia zinazohusu mitazamo na maadili, bado kinyume cha njia hizo hakiwezi kupatikana. Pingamizi huletwa na watu waliozoea uharibifu; na kuona kuwa njia za Qur’an hazitafaa katika jamii yenye ufisadi wa namna hii, wanajaribu kuleta madai ya aina hii.

Ukweli haubadiliki kwa kufuata idadi ya watu. Ukweli uko pale pale. Umma unapaswa uutafute na kuufuata, sio kuuweka ukweli uwategemee wao.

Hebu tutoe mifano miwili. Qur’an imekataza pombe na riba. Si mwingine bali wenye waraibu ndio wanaoweza kudai kuwa mambo hayo ni mazuri na yana manufaa. Katika nchi au katika karne, kama watu wengi wanakunywa pombe au wanajihusisha na riba, hii isingemaanisha kuwa Qur’an haikusudii kuiambia nchi hiyo au karne hiyo. Badala yake, hiyo itamaanisha kuwa wao wako nje ya wanaoambiwa na Qur’an, kwamba wako nyuma sana na kwamba wamepotoka.

Njia nyingine ziko kama hivyo.

Maswali juu ya Uislamu

Author:
Maswali juu ya Uislamu
Subject Categories:
Read 36 times
In order to make a comment, please login or register
MASWALI YENYE KUFANANA
THE MOST ASKED QUESTIONS