Kama Uislamu ni dini ya kweli, kwa nini ni kuna watu wengi wanaoukataa na ambao ni watu wa dini zingine duniani? Nani anayewazuia watu kuwa Waislamu?

The Answer

Dear Brother / Sister,

Awali ya yote, tusisahau kuwa huenda idadi ya Waislamu ni ya kwanza kwa wingi au angalau ya pili. Kama ingekuwa dini ya kweli inategemea idadi ya wafuasi wake, dini za Ukristo na Uislamu ni za kweli. Mmoja kati ya watu watatu duniani ni Muislamu kwa sasa. Wingi huu wa idadi ni dalili ya ukweli muhimu.

Katika historia nzima, hakuna dini iliyoweza kuwafanya watu wote duniani waifuate. Kama nukta hii itapozingatiwa, italazimu kuamini kuwa hakuna dini ya kweli. Fikra hii si sahihi hata kidogo.

Wale wasiokubali dini ya Uislamu wamegawanyika katika makundi matatu:

Kundi la kwanza: Hawaukubali Uislamu bila ya ushahidi wowote wenye kuupinga. Huko kunaitwa kukataa bila ya kukubali. Yaani, hao ni watu wasiojihangaisha kutaka kujua kama Uislamu ni sahihi au laa, wanaopendelea starehe zao tu, wasiotaka kuukataa Uislamu kwa kuegemea ushahidi wowote au wasiofikiria kutumia juhudi zozote za kukubali Uislamu kwa ushahidi wowote.  Watu wengi wasioukubali Uislamu ni kama hao. Hawataki kuacha starehe zao kwa kuukubali Uislamu, unaolenga kuadabisha maisha ya watu kwa kuwabebesha mizigo na majukumu. Kundi hili, lililotofautiana na Uislamu, likokatika ujinga kabisa.

Kundi la pili: Ni watu wenye mzio wa kuuchukia Uislamu bila ya sababu, wasiosikia ushahidi wowote unaoupendelea Uislamu na wanaozingatia kila dalili dhaifu kuwa ni ushahidi ulio kinyume na Uislamu. Hao ni wachache na hawakumudu na kamwe hawataweza kuukataa ukweli wa Uislamu kupitia ushahidi wa kisayansi au wa kimantiki bila ya chuki. Kinyume chake, wengi wasio Waislamu wameukubali Uislamu kupitia sayansi na mantiki katika historia yote. Hata leo, maelfu ya watu, miongoni mwa ambao kuna mamia ya wanasayansi na wahudumu a kanisa, ambao waliuwa Wakristo, ambayo ni dini inayodai kuwa ya wote, wamesilimu na kuendelea kusilimu.

Kwa mujibu wa Nursi, kuna vizuizi vinavyozuia Uislamu, ambayo dini ya wote na inayofanya masuala yake yote yakubaliwe na Akili, dhidi ya kuenea duniani kote. Orodha yake ni kama ifuatavyo:

1. Ujinga wa wageni/wasio-Waislamu. Hata watu wa Kitabu hawakuweza kutofautisha kati ya rangi nyeupe na nyeusi kwa sababu walikuwa wajinga sana.

2. Wanaishi maisha yasiyo ya ustaarabu. Kwa hivyo, walishindwa kabisa kufahamu uzuri wa ustaarabu wa Kiislamu.

3. Hususani watu wa Kitabu, walionekana kung’ang’ania sana dini yao. Ung’ang’anizi huo kiliwazuia kuuona ukweli wa Uislamu.    

4. Utawala na udikteta wa wahudumu wa kanisa na viongozi wa kidini. Udikteta huu haukuwaruhusu watu kuwa na uhuru wa kuhoji na kufanya uamuzi.

5. Watu waliwatii na kuwafuata wahudumu wa kanisa na viongozi wa kidini bila ufahamu. Ukweli kuwa Akili za watu zilinyakuliwa na hazikuwaruhusu watu kufikri uwezekano kuwa ukweli ungeweza kuwa mwingine.

6. Mtu mmoja mmoja na utawala wa kijamii na mamlaka waliyo nayo Waislamu. Udikteta huu umeharibu mazuri ya Uislamu na ustaarabu wa Quran kimamlaka na kusababisha mandhari yaliyoonekana kutowafurahisha wageni.

7. Maovu mengi miongoni mwa Waislamu yaliyoanzia kwenye vitendo vilivyokuwa kinyume na Uislamu. Maovu haya yasiyo ya Uislamu yaliharibu mvuto wa jua la Uislamu na kuzuia jua hilo angavu kama mawingu mazito lisizifikie Akili. Vizuizi hivyo viwili vilianza kupotea kwa kuibuka fikra ya uhuru miongoni mwa wanadamu, na Matakwa ya kutafuta ukweli.

8. Kizuizi cha nane kilikuwa kuwepo kwa hadaa kuwa kulikuwa na mabishano katika baadhi ya masuala katika Quran na yaliyothibitishwa na sayansi. Kutokana na hadaa hii, wanasayansi wengi walijitenga na Uislamu, wakifanya kosa kubwa sana.

Kwa mujibu wa Nursi, kikwazo cha kwanza, cha pili na cha tatu vimevunjwa kwa neema ya elimu na ustaarabu, na vimeanza kupotea.

Kikwazo cha nne na cha tano vimeanza kutoweka kwa kuwa fikra ya uhuru na hali ya kutafiti na kutafuta ukweli imejitokeza miongoni mwa watu. 

Kikwazo cha sita na cha saba vitatoweka kama udikteta utaondoshwa na upande mbaya wa uovu utaonekana. Ukweli kuwa nguvu ya kimamlaka inayoshikiliwa na mtu mmoja mmoja imeanza kuporomoka inaashiria kuwa udikteta wa kutisha wa makundi makubwa katika jamii na wa kamati pia utaporomoka katika kipindi cha miaka thelathini au arobaini. Na ghadhabu kubwa katika bidii ya Kiislamu, pamoja ma ukweli wa matokeo mabaya ya uovu unadhihirika wazi kuwa vikwazo hivyo viwili vinakaribia kuporomoka; kwa kiasi, vimeanza kuwa hivyo. Inshaallah, vitatoweka kabisa hapo baadaye.

Kikwazo cha nane kinaelekea kwenye kutokomea kwani inadhihirika kuwa hakuna ubishani kati ya ukweli wa Quran uliofahamika kwa usahihi na uvumbuzi uliofahamika vyema wa kisayansi. Hapo nyuma, wanasayansi na wanafalsafa waliupinga Uislamu kwa sababu hawakujua vyema kuhusu uhakika wa Uislamu. Hali hiyo imebadilika kabisa kwa sasa.

“Katika Muhtasari wa Miujiza ya Quran, Risale-i Nur inaonesha nuru za hali ya kimiujiza ya miujiza iliyopo chini ya aya zote zinazoshambuliwa na sayansi, na inadhihirisha ukweli mtukufu, usioweza kufikiwa na sayansi, katika sentensi hizo na ibara za Quran tukufu kuwa lengo la wanasayansi wanalodhani kuwa linaonesha ukosoaji; inamlazimisha hata mwanafalsafa mbishi sana kujisalimisha. Ni ushahidi unaojidhihirisha wenyewe, yeyote anayetaka anaweza kuona.”

“Wakati ujao utakuwa mzuri kwa Uislamu peke yake. Na mtawalawake atakuwa mambo ya kweli ya Quran na imani… Sisi, Waislamu, ambao ni wanafunzi wa Quran, tunafuata ushahidi; tunaendea mambo ya ukweli wa imani kwa njia yay mantiki, ingawa, na nyoyoni mwetu. Hatuachi ushahidi unaopendelea utii usio na fikra na uigaji wa mhudumu wa kansa kama wanavyofanya baadhi ya wafuasi wa dini zingine. Kwa hivyo, siku za baadaye, pindi akili, sayansi na teknolojia itakapoenea, kwa hakika, huo utakuwa wakati Qur'an itakapopanda juu, inayoegemea shuhuda za kimantiki na kuiachia akili ithibitishe.” [Hutbe-i Şamiye (Hotuba ya Damaskas)]

Maswali juu ya Uislamu

Author:
Maswali juu ya Uislamu
Subject Categories:
Read 1.118 times
In order to make a comment, please login or register
MASWALI YENYE KUFANANA
THE MOST ASKED QUESTIONS