Kwa nini Allah amefanya dini nne za lazima? Je isingekuwa sawa kama ungepelekwa Uislamu tu?

The Answer

Dear Brother / Sister,

Kila kitu ni bora katika mazingira kilipokuwepo. Hata hivyo, kwa ujumla kuna jambo ambalo ni bora zaidi na zuri zaidi ya mambo yote.

Kwa mfano, katika Qur’an tukufu, kumeelezwa kuwa mwanadamu aliumbwa kwa udongo bora mwusi. Kwa ulinganifu, vitu vingine viliumbwa kwa dosari? Hapana. Hivyo pia ni viumbe vizuri sana katika mazingira yao wenyewe.

Kwa mfano, jua ni zuri mno katika mazingira yake lenyewe. Kwa maneno mengine, hakuna watu ambao wangeweza kuishi kama Jua lisingekuwepo. Hata hivyo, mwanadamu ni Mzuri sana kwa ujumla, na Jua ni Zuri sana kwa upande wa kuwepokwake, na kwa upande wa Kazi linayofanya. Tunaweza kutoa mifano mingine zaidi. Kondoo, ardhi, miti ya matunda, malaika, n.k. vyote ni viumbe wazuri sana na wakamilifu kabisa katika mazingira yao wenyewe.

Kwa hali hiyo, ukweli kuwa mwanadamu ni mkamilifu zaidi haimaanishi kuwa viumbe wengine si wakamilifu na kuwa wameumbwa wakiwa na kasoro.

Hakuna kondoo wengine walio wakamilifu kuliko wale kondoo waliopo wanaweza kufikiriwa. Hakuna ngamia wengine zadi walio wazuri zaidi kuliko ngamia hao au hakuna jua zuri zaidi kuliko Jua linavyoweza kufikirika. Kwa namna hiyo hiyo, vitabu vitukufu vilivyoshushwa vilikuwa vikamilifu zaidi vilivyopelekwa katika nyakati hizo.

Kumfundisha mwanafunzi mwanafunzi wa shule ya msingi jedwali la kuzidisha namba si ziada wala upungugufu. Hata hivyo, si jedwali lakuzidisha namba bali mada za masomo ya juu hufundishwa mwanafunzi wa chuo kikuu. Halikadhalika, vitabu vitukufu vilivyotumwa kabla ya Qur’an vilikuwa bora sana katika wakati wao na kuvituma katika wakati huo kulifaa na si upungufu. Kwa mtazamo huo, kila mtume na kila ufunuo waliopelekewa ni bora na ulifaa sana kwa wakati wake.

Hata hivyo, kwa maneno mengine, Qur’an ilishushwa pindi watu wote walipokuwa katika kiwango sawa na cha wanafunzi wa chuo kikuu ambao wanaweza kuchukua masomo yao kutoka katika kitabu kimoja na kutokakwa mtume mmoja.

Kwa kutazama kuwa sayansi nyingi zilizosonga mbali hufundishwa katika vyuo vikuu, je tunaweza kusema sayansi inayofundishwa katika chuo kikuu inapaswa wafundishwe watoto wa shule za msingi? Wanadamu pia kama taasisi ya elimu. Kila kipindi ni kama idara za shule na wahadhiri wa idara hizo ni Mitume.

Kwakuwa tangu wakati wa Adam (amani iwe juu yake), wanadamu wamefikia mpaka katika kiwango cha chuo kikuu na wamepata uwezo wa kuchukua mafunzo kamili ya dini ya Uislamu. Kwa hivyo, dini kamilifu zaidi ilibakishwa kuwa ndio ya mwisho. Umuhimu wa hisabati pia upo hata katika shule ya msingi. Hata hivyo, somo hilo hufundishwa kulingana na kiwango cha wanafunzi wa shule ya msingi na mwalimu hafundishi kila anachokijua bali hufundisha mada wanazoweza kuelewa.

Vivyo hivyo, mitume wengine waliwafundisha watu kulingana na viwango vyao na wakawaelimisha. Mwishowe, walipofikia kiwango cha kuweza kufundishwa katika vipengele vyote, dini ya Uislamu na Mtume mtukufu (s.a.w) aliletwa.

-Kwa nini Allah aliachilia Injili na Taurati kugeuzwa-geuzwa na Akailinda Qur’an? Kwa nini Allah aliachilia maneno Yake kubadilishwa hapo kabla?

1. Kumtegemea Allah juu ya yale tusiyojua sababu (busara) zake kunadhihirisha ukamilifu wa imani yetu na uaminifu wetu kwa dini yetu.

2. Viumbe alivyoviumba Allah duniani havilingani. Yeye huviambatanisha baadhi kwa kuwepo sababu na kuumba baadhi yao bila ya sbabu au maana. Kwa mfano, ingawa kila mtu anatokana na mama na baba, alimuumba Adam (s.a.w) bila ya mama na baba, Isa (s.a.w) bila ya baba na Hawa bila ya mama. Inamaanisha kuwa wakati mwingine huwa Anatenda nje ya sheria za ujumla.

Aidha, kwa mujibu wa sheria, moto huunguza, Mwezi haupasuki katika vipande viwili, miti haitembei na fimbo hazigeuki nyoka. Hata hivyo, kwa amri na utashi wake Allah, Ibrahim (s.a.w) hakuunguzwa na moto, Mwezi ulipasuka vipande viwili, mti ulitembea kwa amri ya Mtume (s.a.w) na fimbo ya Musa (s.a.w) iligeuka nyoka.

Aidha, wakati baadhi ya mitume walikuja na wakauliwa na kaumu walizotumwa kwao, Allah aliwahifadhi baadhi ya mitume Wake kama vile Musa, Ibrahim na Muhammad (s.a.w).

Hali sawa na hiyo inaweza kuwa ilijitokeza kuhusu vitabu. Allah, ambaye aliachilia vitabu vingine vibadilishwe, alizuia Qur’an Tukufu kutobadilishwa kwa ukarimu Wake mahususi. Kwa sababu hiyo, Ameashiria kuwa Qur’an iko chini ya Hifadhi Yake binafsi. Allah, aliyemhifadhi Ibrahim (s.a.w) asiungue katika moto, pia ameihifadhi Qur’an kubadilishwa.

Roho zetu na mashetani haziwezi kuuliza kwa nini Hakuzuia mitume Wake wengine wasiuliwe lakini akamhifadhi Ibrahim; haziwezi kutoa rai zao juu ya jambo hilo, pia.

3. Kama Adam asingetolewa Peponi, watu wengi wasingeongezeka. Mbegu hutoka ghalani na kufika mashambani ili zigeuke kuwa miti; halikadhalika, watu wameshuka katika shamba laDunia kutoka ghala la Pepo ili waweze kuongezeka kama miti.

Halikadhalika, kama vitabu vingine visingebadilishwa, basi, ufunuo wa Qur’an usingekuwepo. Vilipaswa kubadilishwa ili ije fursa ya kuja ufunuo Qur’an. Hata hivyo, wale tu waliovibadilisha ndio wanaowajibika na ubadilishwaji huo.

4. Hadhi ya Mtume (s.a.w) miongoni mwa mitume wengine iko dhahiri. Alitumwa ili iwe rehema kwa ulimwengu wote na utume wake haufungamani na wakati au kipindi fulani isipokuwa ni wa nyakati zote na vipindi vyote. Na ametumwa kwa watu na majini. Mitume wengine hawana sifa hizo.

Kwa hivyo, Kitabu cha mtume (s.a.w) ni cha nyakati zote na sehemu zote. Kama kitabu hicho kisingekuwa na muhuri kuwa hakibadilishiki, watu wangekibadilisha. Muhuri huo umekihifadhi.

5. Hakuna anayweza kufanya chochote tofauti na anavyotaka. Hayo, Ameyaonesha kwa kuiifadhi Qur’an.

Maswali juu ya Uislamu

Author:
Maswali juu ya Uislamu
Subject Categories:
Read 150 times
In order to make a comment, please login or register
MASWALI YENYE KUFANANA
THE MOST ASKED QUESTIONS