Kwa nini Uchaguliwe Uislamu?

Submitted by on Wed, 08/08/2018 - 11:56
Dear Brother / Sister,
Dini zote zina kanuni kuu za namna moja na zinasisitiza mambo ya namna moja. Kila Mtume aliyetumwa na Allah alikuja kuendeleza na kutimiza yale ya mtume aliyemtangulia, alikariri ujumbe wa mtangulizi/watangulizi wake, aliutimiza kulingana na hali na mazingira, alifafanua masuala yaliyohitaji ufafanuzi, alifanya upya mambo yaliyohitajika kufanywa upya na kuunganishwa na mambo yenye kufanana nayo katika upande wa nidhamu - katika kukubaliana na mazingira ya kipindi hicho na mahitaji ya kipindi hicho. Masuala haya ya upwekeshaji, utume, kufufuliwa baada ya mauti na ibada yalikuwa mambo ya msingi kwa mitume wote. Ndiyo, kanuni zilizotajwa hapo juu ziliunda msingi wa ujumbe wa mitume wote huku kukiwa na tofauti ndogondogo katika mtindo, maneno na mitazamo.
Ujumbe wa Quran ni muendelezo wa ufunuo ulioanzia kwa Nabii Adam (as), mtu wa kwanza na mtume wa kwanza. Hivyo, msingi wa dini zote hizo mbele ya Allah ni mmoja: Uislamu.
“Bila ya shaka Dini mbele ya Mwenyezi Mungu ni Uislamu (utii kwa Matakwa yake). ” (Aal-i Imran, 3/19)
Mitume waliotumwa katika enzi na mahali tofauti hawakupingana; Nabii Muhammad (s.a.w) pia, hakumkana yeyote katika wao.
“Mtume ameamini yaliyo teremshwa kwake kutoka kwa Mola Mlezi wake, na Waumini vile vile. Wote wamemuamini Mwenyezi Mungu, na Malaika wake, na Vitabu vyake na Mitume wake. Hatutafautishi baina ya yeyote katika Mitume wake, na (Waumini) husema: Tumesikia na tumet'ii. Tunakutaka maghfira Mola Mlezi wetu! Na marejeo ni kwako.." (al-Baqara, 2/285)
“Sema: Tumemuamini Mwenyezi Mungu, na tuliyo teremshiwa sisi, na aliyo teremshiwa Ibrahim, na Ismail, na Is-haak na Yaakub na wajukuu zao, na aliyo pewa Musa na Isa na Manabii wengine kutoka kwa Mola wao Mlezi. Hatubagui baina yao hata mmoja, na sisi ni wenye kusilimu kwake." (Aal-i Imran, 3/84)
Kwa upande wake, Nabii Muhammad (s.a.w) ni kama muendelezo na ukamilishaji wa mitume wote waliotangulia. Hata hivyo, kuna tofauti; yeye ni mtume wa mwisho; hakuna mtume atakayekuja baada yake; kwa hivyo, yeye ndiye aliyeleta Ujumbe wa Kiungu kwa wote.
Allah, aliyemuumba mwanadamu, anayemjua kwa kina na ndiye anayempa mahitaji yake, alipeleka ujumbe kwa watu katika kila enzi na kuishia kwa Nabii Muhammad (s.a.w). Hivyo, hakutakuwa na mitume baada yake; hakutakuwa na mabadiliko katika ufunuo; na watu watafuata ufunuo wa misho.
“…Leo nimekukamiliishieni Dini yenu, na nimekutimizieni neema yangu, na nimekupendeleeni UISLAMU uwe ndiyo Dini...” (al-Maida, 5/3)
“Na anaye tafuta dini isiyo kuwa Uislamu haitakubaliwa kwake. Naye Akhera atakuwa katika wenye kukhasiri…” (Aal-i Imran, 3/85)
“Muhammad si baba wa yeyote katika wanaume wenu, bali ni Mtume wa Mwenyezi Mungu na Mwisho wa Manabii, na Mwenyezi Mungu ni Mjuzi wa kila kitu.” (al-Ahzab, 33/40)
Dini ya Uislamu ina kanuni zote zinazomkamilisha mwanadamu kimwili na kiroho na zinazohakikisha furaha yake na uokovu. Uislamu humwongoza mtu na jamii wenye kuifuata kwenda kwenye furaha, kutoka katika uzuri na kwenye ukamilifu kutoka katika furaha. Uislamu unaipa umuhimu hifadhi ya maisha. Unawaadhibu vikali wale wanaojaribu kuvuruga amani katika jamii. Huamuru umoja, kusaidiana na mshikamano. Unalinda uhai wa kijamii dhidi ya vurugu na kitisho.
Dini ya Uislamu ina kanuni zote zinazomkamilisha mwanadamu kimwili na kiroho na zinazohakikisha furaha yake na uokovu. Uislamu humwongoza mtu na jamii wenye kuifuata kwenda kwenye furaha, kutoka katika uzuri na kwenye ukamilifu kutoka katika furaha. Uislamu unaipa umuhimu hifadhi ya maisha. Unawaadhibu vikali wale wanaojaribu kuvuruga amani katika jamii. Huamuru umoja, vipawa na mshikamano. Unalinda uhai wa kijamii life dhidi ya vurugu na hofu.
Uislamu unawapa watu maadili makubwa watu na huwanufaisha katika vipengele vyote. Masuala yake yote yana manufaa mengi sana, na huponya maradhi ya kimwili na kiroho. Dini ya Uislamu inazingatia elimu na busara; Hivyo, unawaelekeza watu wenye akili kwenye matendo mema na furaha kwa kuwafanya watumie utashi wao wenyewe. Huutazama ujinga kuwa ni adui mkubwa; huwapeleka watu kwenye tafakuri. Ni lazima kuzingatia hali ya dunia kabla na baada ya Enzi za Upeo wa Furaha ili kufahamu namna dini ya Uislamu ilivyokuwa ni rehema kubwa kwa utu.
Kabla ya Uislamu, dunia nzima ilikuwa katika ujinga na upotovu, kitisho na vurugu. Ushenzi huu na hofu iliyoathiri sana dunia pia iliikumba Rasi ya Uarabuni. Watu walikuwa wakijivuna kwa kuwazika mabinti zao. Waliamini ushirikina, waliabudu masanamu waliyoyatengeneza kwa mikono yao na kuyaomba msaada.
Katika kipindi cha giza, nuru ya Quran iliibuka kama jua kutoka katika pembe ya Rasi ya Uarabuni. Ilivunjavunja matabaka ya ukafiri na ukandamizaji. Iling’aza macho kwa ufunuo wa juu, ilisafisha roho kwa rehema na uongofu, ilichangamsha Akili na kuziongoza dhamiri. Iliondoa ushirikina na kuweka upweke (wa Allah) nyoyoni. Ilondoa uonevu na kuweka haki. Iliondoa chuki na uadui kutoka nyoyoni na kuweka mapenzi, huruma na upole nyoyoni.
Athari hii ya Quran sio finyu kwa kuishia katika Enzi za Upeo wa Furaha pekee. Taifa lolote lililopokea Uislamu na kuutekeleza baada ya hapo lilipata maendeleo katika sayansi, biashara, na kuwa ni mifano ya kuigwa na mataifa mengine. Mfano mzuri zaidi ni maendeleo ya ustaarabu wa Andalusia, wa-Seljuki na wa-Ottoman.
Maswali juu ya Uislamu