Ni thamani zipi za msingi ambazo dini ya Uislamu inaamuru zihifadhiwe?

The Answer

Dear Brother / Sister,

Kuna haki nyingi ambazo Uislamu unawapa watu. Tunaweza kuorodhesha thamani nyingi zinazozingatiwa kuwa ni haki za msingi kama ifuatavyo: Uhai, dini, akili, mali na kizazi.

1- Haki ya Kuishi:

Dini ya Uislamu unamzingatia mtu kuwa ni kiumbe bora zaidi na unachukulia kuwa kulinda haki za kibinadamu ni katika kanuni za msingi. Imeelezwa katika Quran kuwa kumuua mtu bila ya haki ni kosa kubwa sana kama kuwaua watu wote na kuwa kuhifadhi uhai wa mtu ni kitendo cha thamani ya juu sana kama vile kuwahifadhi watu wote.

Mtume (s.a.w) aliwahutubia Waislamu wote kama ifuatavyo katika Hajj ya Kuaga: "Kama mnavyouchukulia mwezi huu, siku hii, mji huu kuwa ni Tukufu, basi chukulieni kuwa uhai na mali ya kila Muislamu kuwa ni dhamana tukufu " (Bukhari, "Ilm", 37, "Hajj", 132, Muslim, "Hajj, 147), kwa kueleza kuwa haki ya kuishi ya kibinadamu si yenye kuguswa. Katika hadithi nyingine, yameelezwa yafuatayo: "Epukeni mambo saba yenye kuangamiza. Mojawapo ni kumuua mtu, ambako kumeharamishwa na Allah isipokuwa kwasababu za haki." (Bukhari, "Wasaya", 23; "Tib", 48; "Hudud", 44; Muslim, "Iman", 144; Abu Dawud, "Wasaya", 10).

Kuwaua watu kama vile wanawake, watoto, wazee na viongozi wa dini kumeharamishwa hata katika wakati wa vita. Kumuua mtu na hata kujiua kumeharamishwa na kunazingatiwa kuwa ni katika madhambi makubwa.

2- Haki ya dini:

Kila mtu ana uhuru wa kuchagua dini. “Hapana kulazimisha katika dini.” (al-Baqara, 2/256), “Nyinyi mna dini yenu, nami nina Dini yangu...” (al-Kafirun, 109/6). Jambo hili limesisitizwa katika aya hizo hapo juu. Wasio Waislamu wanaoishi katika mamlaka ya dola ya Kiislamu wamepewa haki ya kutekeleza dini zao wenyewe.

3- Akili:

Akili ndio sifa bora zaidi ya mwanadamu kwa sababu dhamana za Allah ni shukurani zinazokubaliwa na akili na mwanadamu anaweza kupata radhi na kuridhika kwa Allah, hilo ni la kushukuru. Chanzo na mzizi wa elimu ni akili. Uhusiano kati ya elimu na akili ni kama uhusiano kati ya tunda na mti, mwangaza na jua, kuona na jicho. Akili ndiyo inayombainisha mwanadamu na viumbe wengine hai na wasio hai ulimwenguni na kumfanya awe bora zaidi.

Maonyo katika Quran yaliyosababisha watu kufikiri kama vile “Fikiri!”, “Je hamfikiri?”, “Je, hawafikiri”, “Angalia!”, “Je, hawaoni?”, “Pateni onyo, Enyi wenye macho!” inaonesha umuhimu unaopewa akili.

Badiuzzaman Said Nursi anaeleza akili kuwa ni muhtasari wa hali ya dhamiri iliyochujwa kutokana na hisia, kitu cha thamani kubwa kwa mwanadamu, hali ya nuru, ufunguo wa kufungulia hazina za ulimwengu, kifaa kinachoangalia majina na sifa za Allah yanayojidhihirisha duniani, mtafiti anayetafutia ufumbuzi mafumbo ulimwenguni, mwongozo wa kiungu unaomwandaa mtu kupata furaha ya maisha ya milele, zawadi ya thamani kubwa inayotenda kazi juu ya ushahidi na kumwonesha mtu malengo makubwa na ya matunda ya kudumu, na kitu cha msingi kilichoachanishwa na mada na kinahusiana na mada katika utendaji wake.

Dini ya Uislamu imeharamisha ulevi, unaolewesha watu, ili kuuhifadhi msingi huo muhimu na umeweka adhabu juu ya wenye kukiuka uharamishwaji huo. Katika sheria ya Kiislamu, vitu vyote vyenye kumduwaza mtu na kumwondolea uwezo wake wa kufikiri na kuwa na mantiki huzingatiwa kuwa ni haramu pamoja na vinywaji vyenye kulewesha.

4- Mali:

Dini ya Uislamu inahakikisha haki ya kupata mali. Uislamu unamtaka mtu aishi maisha yenye kufaa heshima ya binadaamu. Uislamu haupingani na mali. Uislamu hautaki mali kuwa ni nguvu inayomilikiwa na sehemu ya jamii; unataka mali ienee baina ya watu.

Dini yetu inazingatia kuua kuwa ni katika madhambi makubwa; halikadhalika unauzingatia wizi na unyang’anyi kuwa ni dhambi kubwa na unaweka adhabu kali sana kama vile kukatwa mkono wa mwizi katika kesi ya wizi.

5- Kizazi:

Desturi ya ndoa ni lazima kwa ajili ya kudumisha na kuendeleza kizazi cha binadamu. Kudumu na kustawi kwa kizazi cha biadamu kunawezekana tu kupitia kuanzishwa kwa familia, ambayo inaunda jamii ambayo ni muhimu sana katika jamii. Desturi ya ndoa imeegemea juu ya mkataba wa ndoa unaounda msingi wa jumuiya ya Kiislamu.

Katika kulipa umuhimu jambo la kuiimarisha jamii ya Kiislamu, dini ya Uislamu imetumia na imehimiza kuwa na watoto na kuongeza idadi ya watu. Kwa hakika, Mtume Mtukufu (s.a.w) amesema, "Oeni wanawake wapenzi na wenye kuzaa kwa sababu nitajifaharisha kwa wingi wenu katika hadhara ya ummah zingine katika Siku ya Kiama." (Ahmad b. Hanbal, I, 412).

Nabii Zakariyya (s.a.w) alimwomba Allah dua ifuatayo ili kuendeleza kizazi chake: "Na hakika mimi nawakhofia jamaa zangu baada yangu: na mke wangu ni tasa. Basi nipe mrithi kutoka kwako. Atakaye nirithi mimi na aurithi ukoo wa Yaaqub. Ewe Mola wangu Mlezi! Na umjaalie awe mwenye kuridhisha! " (Maryam 19/5-6)

Katika Uislamu, kuwa na watoto na kuendeleza kizazi huzingatiwa kuwa ni ibada. Kutokana na umuhimu wake, kumdhuru mtoto katika mji wa mimba, kuharibu mimba na kutoa mimba huzingatiwa kuwa ni kuua. Kumeharamishwa kuua  kijusi ambacho viungo vyake vimeshadhihirika. Mjumbe wa Allah (s.a.w) alipopokea ahadi ya utii kutoka kwa wanawake, aliamuru “kutowaua watoto wao kwa njia yoyote” kama ni sharti. Sharti hili ni muhimu sana. Mtoto yuko chini ya udhibiti wa mama yake kabla hajazaliwa. Hata hivyo, baada ya kuzaliwa, baba, sio mama, ndiye anayewajibika. Kisha, sharti la “kutowaua watoto wao kwa njia yoyote” linahusiana na kijusi katika mji wa mimba.

"Ewe Nabii! Watakapo kujia wanawake Waumini wanakuahidi ya kwamba hawatamshirikisha Mwenyezi Mungu na chochote, wala hawataiba, wala hawatazini, wala hawatawauwa watoto wao, wala hawataleta uzushi wanao uzua tu wenyewe baina ya mikono yao na miguu yao, wala hawatakuasi katika jambo jema, basi peana nao ahadi, na uwatakie maghfira kwa Mwenyezi Mungu..." (al-Mumtahina, 60/12).

Maswali juu ya Uislamu

Author:
Maswali juu ya Uislamu
Subject Categories:
Read 274 times
In order to make a comment, please login or register
MASWALI YENYE KUFANANA
THE MOST ASKED QUESTIONS