Ni zipi tofauti kati ya Imani juu ya “Mungu “ katika dini tofauti na imani juu ya “Allah” kama ilivyoelezwa na Quran; na ni zipi sifa za Muumba kama zilivyobainishwa na Uislamu?”
Submitted by on Fri, 01/03/2019 - 15:18
Dear Brother / Sister,
Quran inajibu swali hili kwa ufupi katika sura ndogo yenye maana ya kina. Kwa sura hii Allah anataka kusahihisha kosa lililoenea baina ya wanadamu; Pia anawaokoa Waislamu kutokana na kosa ambalo Wakristo wamelifanya. Allah anajibu swali la hapo juu katika sura al-Ikhlas kama ifuatavyo:
Sema: Yeye Mwenyezi Mungu ni wa pekee; Mwenyezi Mungu Mkusudiwa; Hakuzaa wala hakuzaliwa; Wala hana anaye fanana naye hata mmoja. (al-Ikhlas, 112/1-4)
Aya ya mwanzo inakataa namna zote za shirki kwa kusema kuwa Allah ni mmoja na sio zaidi ya mmoja. Aya ya pili inasema kuwa yeye hahitajii chochote lakini kila kitu kinamuhitaji Yeye kila wakati. Aya ya tatu inasema kuwa imani ya utatu ni batili na kwamba kitu kilichozaliwa na kuwa mtoto hakiwezi kuwa Mungu. Aya ya nne inasema kuwa Yeye yupo tofauti na viumbe vyote kama Muumba na haifai kumlinganisha na chochote.
Quran inataja Muumba aliye hai ambaye anaumba wakati wote na anayehifadhi ulimwengu wa kuwepo kwa kuendelea pamoja na kudhihirisha jina lake la al-Qayyum (Mwenye kuwepo kwa kujitegemea). Quran inawajibu ambao wanadai kuwa Mungu ameumba ulimwengu kama kwamba ametengeneza saa na kuiacha peke yake kama ifuatavyo:
“Vinamwomba Yeye vilivyomo katika mbingu na ardhi. Kila siku Yeye yumo katika mambo.” (ar-Rahman, 55/29)
Aya inasema kwamba viumbe wote humwomba Allah ili kufikia mahitaji yao wakati wowote na kwamba Allah anajibu maombi haya. Tunaposoma aya kinyume, tunaweza kupata maana kwamba kama kusingekuwa na uumbaji wa kuendelea dua za viumbe zingelikua hazina maana. Aya zifuatazo zinatujulisha kwamba ulimwengu unahifadhiwa na Muumba kwa kuendelea kwa jina lake la al-Qayyum:
“Mwenyezi Mungu, hakuna mungu ila Yeye - Aliye Hai, Msimamizi wa yote milele.” (al-Baqara, 2/255 and Aal-i Imran, 3/2).
( (1) Kumfananisha Allah na mwanadamu ni kosa la msingi ambalo dini nyingi hulifanya. Ukristo na Uyahudi unaegemeza mtoto kwa Allah wakati ambapo inaaminika katika dini nyingi za kishirikina kuwa Mungu amezaliwa. Nilishangazwa na kauli ya mzungumzaji wa Kihindu katika shirika liitwalo siku ya sala duniani iliyofanywa na The Unity Church wiki ya pili ya mwezi wa Septemba aliposema: Leo ni siku muhimu kwetu kwa sababu “Leo ni siku ya mazazi ya Mungu mkubwa ambaye Wahindu wanamuamini.”
“Maandiko hapo juu yamefupishwa kutoka katika kitabu cha Dr. Furkan Aydıner ambapo ndani yake amekusanya maandishi aliyoandika alipokuwa anaongea na makundi ya wasio na dini.”
Maswali juu ya Uislamu