Nini kifanyike ili kuujua na kuutekeleza vyema Uislamu?

Submitted by on Wed, 08/08/2018 - 15:43
Dear Brother / Sister,
Mtu anapaswa ategemeze maisha yake ya kidini juu ya Sunnah ya Mtume, si katika akili yake na mantiki. Maana yake, anapaswa ajue namna Mtume alivyotekeleza dini na alichounasihi ummah wake.
Je Uislamu ni dini ya kinadharia tu bila ya kutekelezwa kivitendo? Inapaswa utafute majibu ya maswali haya hapo juu na ujaribu kuutekeleza Uislamu kwa kujisalimisha kwa Allah. Kunaweza kuwepo tofauti kadhaa katika maisha ya mtu katika hatua fulani za maisha kutokana na athari za umri wake.
Tunapotaja Uislamu, jambo la kwanza linalokuja akilini ni Quran na maisha ya Mtume. Allah alishusha kitabu chenye amri na makatazo na Mtume aliyetekeleza yaliyomo ndani ya kitabu hicho. Basi, njia ya kuwa Muislamu mzuri ni kutii Quran na Mtume (s.a.w). Kumfanya Mtume, ambaye ni Quran hai, kama mfano ni jambo analolipenda sana Allah. Kwa hakika, Allah anaeleza yafuatayo katika Quran: “Sema: Ikiwa nyinyi mnampenda Mwenyezi Mungu basi nifuateni mimi, Mwenyezi Mungu atakupendeni na atakufutieni madhambi yenu.'” (Aal-i Imran, 31)
Katika hadithi iliyosimuliwa na Abu Dawud, Mtume amesema, “Tahadhari! Katika wakati mfupi ujao, baadhi ya watu watasema Quran inatutosha. Hata hivyo, nimepewa elimu kiasi au mara mbili ya kiasi cha Quran.” Hivyo, akaeleza kuwa Quran haiwezi kufahamika kikamilifu bila ya Mtume.
Ama kuhusu amri ambazo wanazuoni wa Kiislamu wamezitoa kutoka katika Quran, tuna aya ifuatayo, ambayo iko waziwazi, kuhusu jambo hilo: “…Na lau kuwa wangelilipeleka kwa Mtume au kwa wenye mamlaka kati yao, wale wanao chunguza wangelilijua...” (an-Nisa, 83)
Kama inavyoweza kuonekana, tumeombwa tuwaendee wale waliopewa mamlaka baada ya Mtume. Kuwepo kwa madhhab manne ndio ufafanuzi wa aya hiyo.
Kwa kuhitimisha, njia ya kujifunza vyema Uislamu na kuutekeleza ni kulingana na Quran, Sunnah na hukumu zilizotolewa na wanazuoni wa Kiislamu kutokana na vyanzo hivyo viwili.
Ama kuhusu kutafiti dini zingine na rai zilizo kinyume na Uislamu, ni muhimu kwetu kujifunza sana dini yetu na kwa usahihi kwanza. Inafaa kutafiti vitu vizuri jaani katika maeneo ya jirani nasi kabla hatujajenga misingi na kuta za jengo letu kwa uimara?
Msinielewe vibaya; sitaki kusema kuwa hakuna jema huko bali kama tunataka kupita katika chumba chenye sumu, tunahitajika kuvaa kichuja hewa madhubuti. Vinginevyo, tutadhurika na sumu. Kama tunataka kutafiti baadhi ya mambo yanayodhuru dini na yenye sumu, tunahitaji kichuja hewa kizuri kitakachozuia gesi za namna zote, maana yake, tunahitaji imani nzuri na ya kweli ya kidini ili rai hizo zisitudhuru.
Ndiyo, njia pekee ya kumpata Allah na ukweli ni kuiamini Quran na kutenda kulingana nayo kwa sababu Quran ni kitabu kitukufu kilichoteremshwa na Allah ili kuwaongoza wanadamu kwenye kheri na ukweli. Quran ndiyo itakayomwonesha mwanadamu furaha kamili ya kidunia na ya ulimwengu mwengine na itakayoitengeneza hulka ya mwanadamu. Inamwita mwanadamu kwenye imani na upwekeshaji, ibada na utumishi, undugu na upendo. Inaweka vigezo bora kabisa kuhusu imani na amali njema. Uislamu umejengwa kwa kuegemea juu ya vigezo vya Quran. Hakuna ukweli nje ya kanuni imara na adhimu za Uislamu na hakuna haja ya kutafuta. Chochote ambacho Quran inakiona chema na kukisadikisha ni kweli; chochote inachokiona kibaya na kukikataa ni batili. Uislamu, uliowekwa na Quran, unazikataa imani potofu za zamani, ushirikina, fedheha na umalaya. Kisha, Waislamu wote wanahitajika kutathmini mambo halisi matukufu yanayohusiana na itikadi, ibada, maadili, halali, haramu, kumtaja Allah, fikra na upendo unaotegemea Quran.
Aya za Quran zina nguvu ya kutosha kumshawishi kila mmoja. Watu wa kawaida wanapenda uwazi wa mtindo wake; wasomi na wanasayansi wanavutiwa na ufasaha wake na balagha yake. “Bila ya shaka, katika kumkumbuka Allah nyoyo hupata kuridhika.” Watu wenye fikra nyingi wa ngazi zote hutosheleza haja yao kwa ajili ya imani kwa Quran na wanakomaa kwa kuifuata.
Quran imemhimiza mwanadamu atafakari na imempa vigezo kwa ajili ya hili. Watu wameweza kusoma kitabu cha ulimwengu kupitia vigezo ilivyofundisha, wamevumbua ukweli mwingi uliojificha ndani mwake na wamempata Muumbaji na Mola wao. Ni nuru ya Allah iliyowekwa akilini ili kumulika gizani na katika njia za maisha zenye dhoruba. Jua linaangazia dunia yakinifu na Quran imeteremshwa ili kuangazia dunia ya kiroho.
Yafuatayo yameelezwa katika Quran: “Hakika hii Qur'ani inaongoa kwenye ya yaliyo nyooka kabisa.” (al-Isra, 9)
Ni muhimu kufuata sheria za sayansi ili kufanikiwa katika sayansi hiyo; halikadhalika, ni muhimu kukubali kanuni za Quran na Sunnah ili kuupata ukweli.
Ndiyo, mwanadamu anaweza kujua nafsi na sifa za Allah Mtukuka kwa njia ya uongofu wa Quran na Sunnah tu. Anaweza kufahamu anapotoka na anapokwenda, ana jukumu gani duniani, maumbile na uhalisi wa dunia nyengine, na kitakachokubaliwa na kukataliwa huko kwa kupitia njia hizo mbili. Atajifunza aina ya amali, vitendo na mitazamo itakayovutia radhi za Allah Mtukuka na amali zipi, vitendo na mitazamo itakayovutia ghadhabu Zake, kipi ni kweli na kipi si sahihi, kipi ni kosa na kipi ni sawa kutoka katika kitabu cha Allah na Mtume Wake. Kila Muislamu ana wajibu wa kutambua dunia yake ya imani na kuabudu chini ya uongofu wa viwili hivyo halisi.
Pia atajifundisha kutokana na misingi hiyo miwili, Quran na Sunnah, jinsi atakavyoingia katika wigo wa Uislamu na kuamini kanuni mahususi na jinsi atakavyodumu katika wigo wa Uislamu (kwa kutenda amali fulani na kuacha amali fulani). Kwa kuwa vigezo vya Waislamu wote ni Quran na Sunnah, Muislamu anatakiwa kutathmini rai zote za kibinadamu, madai, imani na itikadi zinazoegemea juu ya Quran na hadithi, ambazo ni tafsiri ya Quran.
Mosi, Quran inatufundisha kanuni za imani, "kumwamini Allah, kadhalika na kuwaamini malaika, vitabu vya kiungu, mitume, akhera, qadar (kwamba Allah ameumba kila kitu, iwe kheri au shari). Mtu anakuwa muumini pindi tu anapoamini ukweli wa imani kama ulivyoelezwa katika Quran.
Quran imefundisha Uislamu ambao una maamrisho na makatazo yote ya Allah, kwa waumini. Muumini anapotii hayo mamrisho na makatazo, anakuwa ni Muislamu kamili.
Maswali juu ya Uislamu