Nini maana ya Allah kuwa huru na mbali kutokana na wakati na sehemu? Je, unaweza kuelezea kupitia mifano?

The Answer

Dear Brother / Sister,

Dhati ya Allah na sifa zake ni za tangu… dhati na sifa zetu ziliumbwa baadaye… bila ya shaka, hatuwezi kujua dhati yake au sifa zake vya kutosha; hatuwezi kufahamu kuwa kwake wa tangu na kuwa kwake huru kutokana na wakati… Vipi tutaweza kufahamu hayo? Hatuwezi hata kufahamu wakati ni kitu gani!..

Wakati ni nini? Ni kitu cha aina gani? Kitu chenye kutembea katika mto mmoja katika wakati mmoja, lakini kwa nini unaathiri vitu kwa tofauti? Huwafanya watoto wawe viana, watu wa makamo kuwa vizee na vizee kuelekea katika umauti. Je, mto huu unatembea kuelekea chini au juu?

Shairi lina uliza kwa uadilifu:

Wakati ni nini, ni nini?

Ni maji au ndege?

Wakati ni nini, ni nini?

Chini ya mlima au juu ya mlima?

Tumewekewa mpaka na wakati. Tuna jana na kesho. Ni awamu za muda wote wa maisha. Hata hivyo, awamu zote hizo ni zenye mahusiano; zimepewa majina kwa uhusiano. Leo iliitwa jana masaa ishirini au thelathini yaliyopita. Asubuhi, tutaiita jana. Muda uliyopita na ujao hauna tofauti na jana na leo. Kila siku, kila saa, hata kila wakati ni dunia yenye kujitegemea… Yote yanayojiri katika ulimwengu katika wakati fulani huleta michoro tofauti ukilinganisha na wakati mmoja kabla yake na wakati mmoja baada yake. Hivyo, mchoro tofauti unadhihirishwa katika dunia hii kila wakati.

Wakati unasomwa kupitia michoro hiyo iliyopangiliwa katika mistari, au michoro hiyo imezamishwa ndani ya wakati. Maneno mengi yamesemwa kuhusu wakati. Bila ya kujali asili yake halisi ni kitu gani, wakati, ambapo ni dhana inayohusiana na vitendo, harakati, kutulia na kuondoka kwa viumbe, hauwezi kuwa tendaji kwa Mola na Muumba wa limwengu zote. Anajua kila kitu ambacho kiliumbwa na kitakachoumbwa kupitia elimu yake ya azali.

Aya ifuatayo inaeleza vizuri sana:

Asijue aliye umba, naye ndiye Mjua siri, Mwenye khabari? (al-Mulk, 14 )

Mtu anayetazama kitabu lazima afikiri kwamba kila neno, mstari, na herufi ndani ya kitabu hiki imeandikwa. Hivyo, yule aliyeandika hayo lazima atakuwa tofauti na maandiko na kuwa huru na kufanana na herufi na maneno!..

Ulimwengu, wanadamu wote, wanyama, mimea wanatiririka katika mto wa wakati kwa kuendelea… wanaelekea upande wa umauti na akhera. Anayefanya mto huo utiririke bila ya shaka yupo huru na wakati. Hiyo ni kusema, hajafungwa au kudhibitiwa na wakati. Na hakuna kati ya hao wanaotiririka katika mto huo awezaye kufahamu kuwa huru kutokana na wakati vya kutosha.

Allah yupo huru na mbali kutokana na sehemu, pia. Tunaweza kutoa mwanga wa jua kama mfano: Upo katika vitu vyote vyenye kung’ara ulimwenguni kupitia rangi zake saba; Lipo na linaonekana katika kila kitu kwenye mfumo wa mwanga, joto na rangi saba, ambazo ni kama sifa zake; hata hivyo, halipo lenyewe dhati yake katika kila kitu linachokimulika na kukiangazia. Hiyo ni, jua lipo katika vitu vyote vyenye kung’ara ulimwenguni kupitia sifa zake lakini halipo katika kitu chochote kiupande wa ukubwa na umbo lake.

Sifa na asili ya Allah ambaye analipa jua sifa hizi, ni kamilifu sana kufahamika na akili zetu. Allah amekizunguka kila kitu kupitia sifa zake, hiyo ni kusema, kupitia nguvu zake, elimu na utashi. Hata hivyo, hayupo katika kitu chochote kwa dhati yake. Hiyo ni kusema, Yeye yupo kila mahali kwa sifa zake. Na hayupo sehemu yoyote kwa dhati yake. Kwakuwa Yeye ndiye aliyeumba sehemu; hahitajii sehemu.

Maswali juu ya Uislamu

Author:
Maswali juu ya Uislamu
Subject Categories:
Read 969 times
In order to make a comment, please login or register
MASWALI YENYE KUFANANA