Tawhid (Umoja wa Mwenyezi Mungu) ina maana gani?
Submitted by on Fri, 01/03/2019 - 15:12
Dear Brother / Sister,
Umoja wa Mwenyezi Mungu maana yake ni: kuamini kutokuwepo kwa mungu yoyote isipokuwa Allah , kwa “kusema maneno laailah illah - Hakuna Mola ila Allah.”
Papo hapo umoja unatukumbusha kuhusu tamko laaillah ilaallah . Hili huitwa neno la upwekesho na maana yake ni kwamba hakuna mola wa kweli wa kuabudiwa isipokuwa Allah.
Malinganisho kadhaa yamefanywa kuhusu uwepo wa ulimwengu huu. Moja kati ya hayo ni kasri la ulimwengu. Kwa hivyo, umoja ni kumjua mfalme wa kasri hili kwamba ni mmoja na kutomshirikisha na yoyote.
Juu na chini ya kasri ya ulimwengu hakuwezi kumilikiwa na dhati tofauti. Taa, na vitu vingine vya ndani ya kasri haviwezi vikawa vimeletwa kutoka dunia nyengine na kuwachwa hapa. Kila kitu katika kasri na muhimu kuliko vyote, kila mgeni, anazaliwa katika kasri hii. Hebu tuangalie ua: kutokea katika dunia hadi katika jua, kila kitu kina mchango ndani yake. Na hebu tuuangalie mwili wa mwanadamu sehemu zake ambazo ni mawe ya msingi katika kasri hili, yapo ndani yake pia.
Milima huanzishwa juu ya tambarare kama viti vya kuegemeza mikono, kwa kutoletwa kutoka sehemu nyengine, bali huchomoza kutokea sehemu tambarare. Matunda yameambatana na matawi, kwa kutotokea kutoka katika nchi nyengine, bali yamekuja kutoka katika mti.
Mtoto huwa juu ya mapaja ya mama yake, hakuletwa kutoka katika nchi nyengine anakuwa katika fuko lake la uzazi. Jua ni taa ya kasri hili; halikununuliwa kutoka sehemu nyengine bali limeumbwa pamoja na mbingu.
Katika dunia hii, viumbe visivyo hisabika huungana na baina yao mchanganyiko hutokea na dunia hii ya viumbe hupewa muundo wa kasri. Watu wanaoakisi njia hii husoma neno la umoja na kufahamu kwamba kasri hili ni mali na kiumbe cha Allah pekee.
Wakati neno la umoja likiwa na maana ya kwamba hakuna mola wa kweli wa kuabudiwa isipokuwa Allah, jina la Allah linakusanya majina yote ya kiungu kwa hivyo, hubeba maana kama hakuna anayetoa maisha isipokuwa Allah hakuna muumbaji isipokuwa Allah hakuna isipokuwa Allah. Na kama hivi ndani ya umoja kuna wingi wa umoja kwa idadi ya majina ya kiungu.
Baadhi ya wanachuoni huugawa umoja katika sehemu mbili umoja unaogemea katika elimu na umoja unaegemea katika matendo. Kwa mujibu wa mgawanyo huu, kujua kwamba Allah ni mmoja na kwamba vitu vyote vilivyokua katika hali ya umoja ulimwenguni vinaonesha umoja wake ni umoja unaoegemea katika elimu. Umoja unaoegemea katika matendo ni umiliki wa imani hii ya umoja kwa ukamilifu ndani ya ulimwengu wa matendo wa mwanadamu.
Aya, “Iyyaka na’budu wa iyyaka nastain” Wewe tu ndie tunakuabudu, na Wewe tu ndie tunayekuomba msaada. Ya sura al-fatiha inatufundisha umoja unaoegemea katika matendo. Tunaelekea upande ambao wewe unataka tunasimama kwa heshima ya uwepo wako tu; tunainama na kukusujudia Wewe tu. Tunafikiria kuhusu mambo unayoyaridhia na tunawapenda wale tu unaowaridhia.
Mtu anayemuabudu Allah pekee anakua amewekwa huru kutokana na udhalili wa kuabudia miungu wa uongo; mtu anayetafuta msaada wa Allah pekee huwa huru na kuabudia sababu na huwa huru pia na kua mtumwa wa matukio. Huomba msaada kutoka kwa mola hali ya kuwa akiwa na utegemezi kamili hii ni yote mawili furaha na nguvu ya ushindi.
Kwa kuongezea, njia ya kuwa muumini kamili ni kwa kupitia ukamilifu katika umoja unaoegemea elimu na umoja unaoegemea matendo.
Umoja hauishii katika mambo hayo tu. Umoja wa sifa, majina na matendo pia upo. Aina hizo zinaweza kufupishwa kama ifuatavyo:
Umoja wa matendo: “Kujua kwamba sababu hazina taathira katika uumbaji wa vitu na katika kuviongoza”, “kuamini kwamba wa pekee ni Allah pekee.”
Umoja wa matendo: “Kufahamu kwamba sifa kama elimu, nguvu, utashi ambazo zinaambatana na viumbe nazo pia ni viumbe wa Allah na sio kuzipa dhati ya kujitegemea.
Umoja wa dhati: “Kufahamu kwamba viumbe vyote havina uwepo unapovilinganisha na dhati yake na uwepo wake.”
Kuhuisha na kufisha, kuponya, kuongoza katika njia sahihi, kutoa chakula kila moja ni kitendo tofauti. Matendo haya yasiyo na ukomo hutegemea sifa hizo hizo. Sifa hizo ni uhai, elimu, nguvu, kusikia, kuona utashi, kuongea na kuumba. Hivyo umoja wa matendo ni kufahamu kwamba matendo yote ya tangu ambayo yanafanya kazi katika ulimwengu wa uumbaji huja kutokana na sifa hizi za kiungu na kuzirejesha sifa hizi kwa dhati moja peke yake ni umoja wa dhati.
Maswali juu ya Uislamu